Sheikh yahya awaonyesha njia watoto wa babu seya

eRRy

JF-Expert Member
Jun 12, 2009
1,125
204
1266838421_1.jpg

Sheikh Yahya (aliyeketi katikati) akiwakabidhi Francis (kulia) na Mbangu kitita cha 100,000/= muda mfupi baada ya kuwasili nyumbani kwake.​

Akizungumzia utabiri wake dhidi ya hukumu iliyotolewa hivi karibuni katika Mahakama ya Rufani jijini Dar es Salaam, Shekh Yahya alisema, alijua wazi kwamba tatizo hilo lingetokea lakini alidai kuwa lilitokana na sababu za kimila (za akina Babu Seya).

Alisema, anachokiona yeye ni upuuzwaji wa matambiko, kisomo au dua za kikwao, zilizotakiwa kufanywa na Babu Seya zamani, ndiyo matokeo ya mateso wanayoyapata hivi sasa huko gerezani.

Alitawaka watoto hao kutafakari kwanza maisha ya gerezani huku wakiziacha akili zao zitulie, kabla ya kuingia katika hatua ya pili ya kuhangaikia baba na ndugu yao watoke gerezani.

Alisema, baba yao anatoka katika ukoo wa kifalme ambao hutumia jina la Mbangu, lakini kuna mambo muhimu kufuatana na familia na mila za Kabila lao, ambayo mzee wao (Babu Seya) alitakiwa kuyakamilisha zamani, lakini hakufanya hivyo.

“Hakuna mbaya wa tatizo hili, kuna mambo ambayo mzee wenu aliyapuuza katika ukoo wenu, kwahiyo jambo kubwa kwenu kwasasa ni kumuombea na siyo kumuombea yeye tu bali ni kujiombea wote pamoja.
“Mnapaswa kumfanyia sadaka, msome kisomo kabla hajatoka, kwa mila za kwenu. Msije mkasema labda tatizo ni dansi, maana kama ni dansi mmeanza kuimba miaka mingi kabla, ila tatizo ni hilo la kusahau au kupuuza mila.

“Nimefurahi kuwaona, pumzikeni kwanza, halafu siku zijazo nitawaita na kuwaelekeza vizuri juu ya jambo hilo,” alisema Shekh Yahya.
Aidha mtabiri huyo aliwapatia vijana hao fedha kiasi cha shilingi laki moja kwa ajili ya kuwasaidia katika mahitaji yao.
Juni 25, 2004, Babu Seya na wanaye, walihukumiwa kifungo cha maisha jela, baada ya kukutwa na hatia ya kuwaingilia kimwili watoto wadogo kumi.
 
[ame="http://www.youtube.com/watch?v=axj2tvrENbs"]http://www.youtube.com/watch?v=axj2tvrENbs[/ame]
 
Wizi mtupu.anazidi kuwaongezea majini ya kuwachanganya zaidi.Poleni zenu akina nguza,naona kama mmeingia choo cha kike.
 
badala ya kwenda kanisani kumshukuru Mungu kwa kuwatendea huo muujiza, nyie mnaenda kuyashukuru na kuongea na majini ya shekh yahya, utafuteni uso wa Mungu kwanza oooohooo!
 
vijana mtafuteni mungu acheneni na huyo kizeee atawachanganya na maneno mengi ata hizo hela alizo wapa kueni makini kwani akikupa na mkono wa kulia anachukua na mkono wa kushoto usanii mtupu
 
sheikh yahya hawezi kuonyesha njia kwa mtu yeyote.................sote tunajua kuwa YESU ndio njia ya kweli na uzima na mtu hawezi kumwona mungu bila kupitia kwa yesu....................bora hao watoto waokoke wamjue yesu watafanikiwa
 
sheikh yahya hawezi kuonyesha njia kwa mtu yeyote.................sote tunajua kuwa YESU ndio njia ya kweli na uzima na mtu hawezi kumwona mungu bila kupitia kwa yesu....................bora hao watoto waokoke wamjue yesu watafanikiwa
Jile79 nakubaliana na wewe,but suluhisho si kuokoka tuu,hawa watoto nawashauri wasitetereshwe kiimani,wasimame kwenye imani yao kwani Mungu anasikiliza maombi ya kila amwaminie sio tuu walokole,kuhusu huyu babu nahisi yuko mbioni kufungua dhehebu lake,sababu kila kukicha atataka kuwalisha imani wale wenye imani haba!!
 
Yote ni yote chamsingi wametoka kama ni nani au nani poa ilimradi watoke wote kwa sasa nampa big -up aliweza kuwasaidia hawa madogo kutoka jela wakili nguli mzee marando na wengine wote walioonyesha way foward much respect buddy!
 
mhhhhhhhhh kweli kuacha asili ngumu sana, wasipoangalia watarudi kulekule, masharti ya hawa sangoma ndio yaleyale..............
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom