Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
Romana Mallya
25th February 2011
Mnajimu maarufu Afrika Mashariki na Kati, Sheikh Yahya Hussein
Mnajimu maarufu Afrika Mashariki na Kati, Sheikh Yahya Hussein, ametabiri kuwa serikali ambazo hazitatimiza ahadi kwa wananchi zitaangushwa na kwamba siri nyingi za serikali zitavuja.
Kadhalika, amesema ndani ya miaka saba kuanzia Machi 13, mwaka huu, kutatokea machafuko, maandamano, uasi, maasi na kupinduliwa kwa serikali mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania.
Katika taarifa iliyosomwa jana jijini Dar es Salaam na mtoto wake, Hassan Yahya Hussein kwa niaba yake, ilisema mambo hayo yatatokea kuanzia mwezi huo na yataendelea ndani ya kipindi cha miaka saba.
Sheikh Yahya alisema mambo hayo yatatokea baada ya kuja kwa sayari ya Uranus ambayo itaingia katika nyota ya Punda (Aries).
Alisema sayari hiyo huzizunguka nyota zote kwa miaka 84 na hukaa ndani ya nyota hiyo kwa kipindi cha miaka saba.
Alitaja mambo mengine yatakayojitokeza baada ya kuja kwa sayari hiyo kuwa ni mabadiliko ya ghafla ya kisiasa na kijamii, kuwepo kwa msukumo wa ghafla wa kufanya jambo, kuzinduka kwa watu kifikra na kutaka kujua ukweli na uwazi wa mambo yaliyojificha.
Mengine ni watu kudai haki zao kwa nguvu ambapo wataungana pamoja kupinga serikali na taasisi kubwa ambazo zitakuwa zinawatungia sheria na kanuni na kuwawekea vikwazo.
Alisema hilo litasambaa katika siasa na kwenye midahalo mbalimbali
.
Pia alisema kuanzia Julai, mwaka huu kutatokea mapinduzi ambapo polisi watafumaniwa kwenye maboma yao.
Alisema kutokana na ujio wa sayari hiyo ametabiri mwaka huu kutakuwa na mafanikio katika ugunduzi wa mambo ya afya ambapo wataalamu watavumbua dawa mpya ya kutibu magonjwa mengi.
Alisema wanasayansi watafanikiwa kugundua mbinu mpya za kutibu magonjwa yasiyokuwa na tiba kama Ukimwi na kansa.
Sheikh Yahya alisema kuanzia Januari 23, mwaka huu sayari ya Jupiter imeingia katika nyota ya Punda ambapo utabiri wake unaonyesha kuwa kutasikika habari nyingi kuhusiana na masuala ya michezo na wanamichezo.
Alisema wakati utabiri wake ukimuonyesha kuwa watu hao watapata mafanikio na umaarufu, kutasikika habari za vifo vya wanamichezo, wasanii na waandishi wa habari maarufu hapa nchini.
Alisema sayari ya Jupiter itaingia katika nyota ya ng'ombe Juni 4, mwaka huu ambapo itakaa huko hadi mwishoni mwa mwaka.
Alisema utabiri wake unaonyesha kutakuwa na mafanikio makubwa kwa watu wanaofanya biashara ya kujenga majumba na kuyauza au kuyapangisha kutokana na soko lao kuongezeka.
Sheikh Yahya alisema Aprili 4, mwaka huu sayari ya Neptune itaingia katika nyota ya Samaki ambapo utabiri wake unaonyesha kuwa kutakuwa na mabadiliko mengi ya hali ya hewa sehemu mbalimbali duniani.
Alisema kwa upande wa Tanzania wananchi wategemee kusikia habari za ukame na ukosefu wa maji kuanzia mwezi Aprili hadi Agosti mwaka huu.
25th February 2011
Mnajimu maarufu Afrika Mashariki na Kati, Sheikh Yahya Hussein
Mnajimu maarufu Afrika Mashariki na Kati, Sheikh Yahya Hussein, ametabiri kuwa serikali ambazo hazitatimiza ahadi kwa wananchi zitaangushwa na kwamba siri nyingi za serikali zitavuja.
Kadhalika, amesema ndani ya miaka saba kuanzia Machi 13, mwaka huu, kutatokea machafuko, maandamano, uasi, maasi na kupinduliwa kwa serikali mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania.
Katika taarifa iliyosomwa jana jijini Dar es Salaam na mtoto wake, Hassan Yahya Hussein kwa niaba yake, ilisema mambo hayo yatatokea kuanzia mwezi huo na yataendelea ndani ya kipindi cha miaka saba.
Sheikh Yahya alisema mambo hayo yatatokea baada ya kuja kwa sayari ya Uranus ambayo itaingia katika nyota ya Punda (Aries).
Alisema sayari hiyo huzizunguka nyota zote kwa miaka 84 na hukaa ndani ya nyota hiyo kwa kipindi cha miaka saba.
Alitaja mambo mengine yatakayojitokeza baada ya kuja kwa sayari hiyo kuwa ni mabadiliko ya ghafla ya kisiasa na kijamii, kuwepo kwa msukumo wa ghafla wa kufanya jambo, kuzinduka kwa watu kifikra na kutaka kujua ukweli na uwazi wa mambo yaliyojificha.
Mengine ni watu kudai haki zao kwa nguvu ambapo wataungana pamoja kupinga serikali na taasisi kubwa ambazo zitakuwa zinawatungia sheria na kanuni na kuwawekea vikwazo.
Alisema hilo litasambaa katika siasa na kwenye midahalo mbalimbali
.
Pia alisema kuanzia Julai, mwaka huu kutatokea mapinduzi ambapo polisi watafumaniwa kwenye maboma yao.
Alisema kutokana na ujio wa sayari hiyo ametabiri mwaka huu kutakuwa na mafanikio katika ugunduzi wa mambo ya afya ambapo wataalamu watavumbua dawa mpya ya kutibu magonjwa mengi.
Alisema wanasayansi watafanikiwa kugundua mbinu mpya za kutibu magonjwa yasiyokuwa na tiba kama Ukimwi na kansa.
Sheikh Yahya alisema kuanzia Januari 23, mwaka huu sayari ya Jupiter imeingia katika nyota ya Punda ambapo utabiri wake unaonyesha kuwa kutasikika habari nyingi kuhusiana na masuala ya michezo na wanamichezo.
Alisema wakati utabiri wake ukimuonyesha kuwa watu hao watapata mafanikio na umaarufu, kutasikika habari za vifo vya wanamichezo, wasanii na waandishi wa habari maarufu hapa nchini.
Alisema sayari ya Jupiter itaingia katika nyota ya ng'ombe Juni 4, mwaka huu ambapo itakaa huko hadi mwishoni mwa mwaka.
Alisema utabiri wake unaonyesha kutakuwa na mafanikio makubwa kwa watu wanaofanya biashara ya kujenga majumba na kuyauza au kuyapangisha kutokana na soko lao kuongezeka.
Sheikh Yahya alisema Aprili 4, mwaka huu sayari ya Neptune itaingia katika nyota ya Samaki ambapo utabiri wake unaonyesha kuwa kutakuwa na mabadiliko mengi ya hali ya hewa sehemu mbalimbali duniani.
Alisema kwa upande wa Tanzania wananchi wategemee kusikia habari za ukame na ukosefu wa maji kuanzia mwezi Aprili hadi Agosti mwaka huu.