kunguni wa ulaya
JF-Expert Member
- Mar 16, 2014
- 4,132
- 6,100
TAARIFA YA MSIBA WA SHEIKH SULEIMAN AMRAN KILEMILE
INNAA LILLAAHI WA INNAA ILAYHI RAAJI'UN
Kwa huzuni na masikitiko makubwa tumepokea taarifa za kufariki dunia Mwanachuoni Mkubwa wa Tanzania na Afrika Mashariki, Sheikh Suleiman Amran Kilemile.
Umauti ulimfikia Sheikh usiku wa Leo Tarehe 06 May 2020, Katika Hospitali ya Sinza Dar es Salaam Baada ya Kuzidiwa na Sukari na baada ya kuwa mgonjwa kwa muda.
Maiti kwa sasa ipo Masjid Thaqafa - Tandika, Kuiandaa kwa ajili ya kuzikwa.
Kifo cha Sheikh Kilemile ambae ni miongoni mwa Masheikh wakubwa na wenye Elimu kubwa ni pigo na pengo jengine kubwa mno katika uwanja wa elimu ya Kiislamu na DA'AWAH sio tu Tanzania, bali Afrika Mashariki na ulimwengu mzima wa Kiislamu kwa kuwa alikuwa mahiri katika kila fani miongoni mwa fani za Kiislamu.
Ameandika na kutafsiri vitabu kadhaa na kutoa mamia kama sio maelfu ya wanafunzi mahiri wengi na Sheikh ni mmoja wa Masheikh wachache waliotoa Darsa muda mrefu katika Msikiti wa Chihota - Tandika miaka ya Themanini.
Tunatoa mkono wa pole kwa Umma wa Kiislamu amma, Waislamu wa Tanzania khaswa, familia, masheikh, maustadh, walimu kwa msiba wa kuondokea na nguzo kubwa katika Uislamu.
Tunamuomba Allaah Taala Amsamehe marehemu, Amrehemu na kumuingiza katika Jannat Firdaws.
Aidha, Tunamuomba Allah Ta'ala awalipe malipo makubwa wafiwa na kuwamakinisha kwa subra na istiqaamah katika kipindi hiki kizito cha Msiba.
Wabillaahi at-Tawfiyq.
MAZISHI YAKE:
INNAA LILLAAHI WA INNAA ILAYHI RAAJI'UN
Kwa huzuni na masikitiko makubwa tumepokea taarifa za kufariki dunia Mwanachuoni Mkubwa wa Tanzania na Afrika Mashariki, Sheikh Suleiman Amran Kilemile.
Umauti ulimfikia Sheikh usiku wa Leo Tarehe 06 May 2020, Katika Hospitali ya Sinza Dar es Salaam Baada ya Kuzidiwa na Sukari na baada ya kuwa mgonjwa kwa muda.
Maiti kwa sasa ipo Masjid Thaqafa - Tandika, Kuiandaa kwa ajili ya kuzikwa.
Kifo cha Sheikh Kilemile ambae ni miongoni mwa Masheikh wakubwa na wenye Elimu kubwa ni pigo na pengo jengine kubwa mno katika uwanja wa elimu ya Kiislamu na DA'AWAH sio tu Tanzania, bali Afrika Mashariki na ulimwengu mzima wa Kiislamu kwa kuwa alikuwa mahiri katika kila fani miongoni mwa fani za Kiislamu.
Ameandika na kutafsiri vitabu kadhaa na kutoa mamia kama sio maelfu ya wanafunzi mahiri wengi na Sheikh ni mmoja wa Masheikh wachache waliotoa Darsa muda mrefu katika Msikiti wa Chihota - Tandika miaka ya Themanini.
Tunatoa mkono wa pole kwa Umma wa Kiislamu amma, Waislamu wa Tanzania khaswa, familia, masheikh, maustadh, walimu kwa msiba wa kuondokea na nguzo kubwa katika Uislamu.
Tunamuomba Allaah Taala Amsamehe marehemu, Amrehemu na kumuingiza katika Jannat Firdaws.
Aidha, Tunamuomba Allah Ta'ala awalipe malipo makubwa wafiwa na kuwamakinisha kwa subra na istiqaamah katika kipindi hiki kizito cha Msiba.
Wabillaahi at-Tawfiyq.
MAZISHI YAKE: