Sheikh Ponda, hakuwa na makosa ila hawakujua kusudio la makosa yake

Civilian Coin

JF-Expert Member
Dec 2, 2012
2,305
4,334
Nilipoanza kusikia habari za Uamsho nilisikitika sana, ila nilipoujua ukweli nikagundua wanaonewa kwasababu ya Maudhui yao. Uamsho walikuwa na madai ya msingi sana, kiasi kwamba wangepwa nafasi ya kusikilizwa ingesaidia kwenye mambo mengine ya msingi kwa Nchi, kumkandamiza Sheikh Ponda ilikuwa ni sawa na upotevu wa rasilimali fedha kwenye Bunge la Katiba zilizo chumwa na kuliwa bila faida yoyote kwa Taifa.

Msingi wa kujua mwongozaji na wenzake wanataka nini, unahitaji hali ya kuvumiliana na kusaidiana kutatua tatizo linalodaiwa bila bughuza, Hekima ya kiongozi inapatikana katika kutatua migogoro na sio kuongoza mazingira kuwa safi. Mimi si msafi ila najua fika tumekuwa tukipotoka sana katika kuamua mambo ya msingi na kujikuta tukiamua kidini au kishabiki au kisiasa na hatuamui kwa maslahi ya Taifa.

Asubuhi njema na Alhamisi njema.

DEOGRATIUS KISANDU,
8 Dec 2016
 
Back
Top Bottom