Sheikh Ponda amehukumu kama alivyohukumu Don Veto Corleone

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,847
30,185
Binadamu anapokata tamaa ya kupata Haki, Kisa cha Anerigo Bonasera na Don Veto Corleone. Mfano wa Sheikh Ponda.

Katika kitabu cha "The Godfather," kuna watu wawili muhimu katika kueleza nini binadamu hufanya anapodhulumiwa na jamii na watoa haki wakamdhulumu pia.

Amerigo Bonasera kazi yake ni "undertaker," yaani kutayarisha maiti kwa ajili ya maziko.

Kazi hii ilimpa maisha mazuri katika mji wa New York ya baada ya vita ya pili ya Dunia.

Amerigo Bonasera alikuwa na mtoto mmoja binti aliyempenda sana.

Huyu binti akachukuliwa na vijana wenzake wa kiume kwa matembezi kumbe ndani ya nafsi zao walikuwa na lao jambo.

Wakamlewesha kwa nia ya kumbaka.

Huyu binti alikuwa bikra na hakukubali kuvunjiwa heshima yake na wale wahuni washenzi.

Akapambana na washenzi wale na kuishinda azma yao lakini walimuacha uso wake uliokuwa mzuri umevurugika kwa kuumizwa vibaya sana.

Kesi ikaenda mahakamani.

Hawa vijana ni kutoka familia kubwa zenye satwa baba zao wakazungumza na hakimu wale vijana mahakama ikawatia hatiani lakini hukumu ikawa "suspended," yaani hawatatumikia kifungo kama sheria inavyotaka.

Amerigo Bonasera na mkewe wakatoka mahakamani vichwa wameinamisha wanabubujikwa na machozi kwa dhulma waliyofanyiwa na mahakama.

Wale washenzi na wazazi wao wakiwa wamesimama nje ya jengo la mahakama wakawa wanamtazama Amerigo Bonasera na mkewe huku wanacheka wamefurahishwa na hukumu aliyotoa hakimu.

Amerigo Bonasera akamwambia mkewe, "Twende kwa Godfather tukatafute haki yetu."

Godfather Don Veto Corleone akaisikiliza kesi ya Amerigo Bonasera kisha akamuuliza, "Umekwenda polisi na haki yako umepewa."

Hapa kuna mengi baina ya watu hawa wawili sitayaeleza.

Godfather akamwambia Amerigo Bonasera aitue roho yake yeye atampa haki yake aliyonyimwa na mahakama ya serikali.

Amerigo Bonasera alimuomba Godfather awaue wale vijana wote.

Godfather yeye mpenda haki akamkatalia akamwambia, "Hapana wewe mwanao yu hai."

Naam.

Godfather alihukumu kesi ile kwa uadilifu.

Siku ya pili wale washenzi wote walikuwa vitandani hospitali nyuso zao hazitamaniki taya zao zimeungwa kwa waya na nyuso zimepitishiwa nyuzi kadhaa, vijana waliokuwa na sura jamil wametiwa ulemavu wa maisha kama walivyomsababishia binti Bonasera.

Ujumbe ulikuwa umewafikia wazazi wa watoto wale sawia.

Amerigo Bonasera akawa anakunywa kahawa nyumbani kwake na mkewe roho zimewatua kwani haki yao waliyodhulumiwa mahakamani imepatikana nje ya mahakama.

Mpenzi msomaji mitandaoni kumejaa maneno makali dhidi ya masheikh wanaompinga Sheikh Ponda kwa kuwataka Waislam kumpigia kura Tundu Lisu.

Masheikh hawa kwa kukosa kujua hali ilivyo nje ya duru lao kuwa Sheikh Ponda anaungwa mkono na Waislam wengi wamefanya kosa lile lile lililofanywa na hakimu aliyedhulumu haki ya Amerigo Bonasera.

Waislam kwa miaka mingi walishaipeleka kesi yao kwa Sheikh Ponda kutafuta haki yao nje ya watoa haki rasmi kama alivyofanya Amerigo Bonasera.

Sheikh Ponda kama alivyofanya Godfather Don Veto Corleone ametoa hukumu ya haki.

Sheikh Ponda amewaonyesha Waislam njia ya kupita.

Katika kisa cha Amerigo Bonasera kuna mazingatio makubwa kwa hawa masheikh na pia kwa serikali ya CCM.

Ujumbe wa Sheikh Ponda ni mzito na kama ulivyokuwa ujumbe wa Don Veto Corleone umefika na kueleweka sawia.
 
Mzee wa historia na fasihi mara hii ushamuunganisha Godfather na Sheikh Ponda?

Kama Sheikh Ponda ni Don Vito Corleone, basi Tundu Lissu ni Luca Brassi!

Or is it the other way around?

Ila kuhusu ma Sheikh wa uamsho, mahakama ilishamuamuru DPP alete ushahidi mahakamani, kesi isikilizwe.

Au, akishindwa kuleta ushahidi, watuhumiwa waachiwe.

Maana kumfunga mtu miaka sita kwa kisingizio cha "uchunguzi unaendelea" si haki. Miaka sita jela ni hukumu tayari, kabla kesi haijaanza.

Mahakama ilimpa DPP mwezi mmoja kukamilisha uchunguzi. Hiyo ilikuwa September 14 2019. Baada ya hapo sijui nini kimeendelea. Labda kuna amri kutoka juu imepita kuingilia uhuru wa mahakama.

Mpaka sasa kesi inapigwa danadana.

Hivyo Tundu Lissu kusema atawaachia huru ma Sheikh wa uamsho anakuwa anaenda sawa na kauli ya mahakama ya September 14 2019.
 
Mzee wa historia na fasihi mara hii ushamuunganisha Godfather na Sheikh Ponda?

Kama Sheikh Ponda ni Don Vito Corleone, basi Tundu Lissu ni Luca Brassi!

Or is it the other way around?

Ila kuhusu ma Sheikh wa uamsho, mahakama ilishamuamuru DPP alete ushahidi mahakamani, kesi isikilizwe.

Au, akishindwa kuleta ushahidi, watuhumiwa waachiwe.

Maana kumfunga mtu miaka sita kwa kisingizio cha "uchunguzi unaendelea" si haki. Miaka sita jela ni hukumu tayari, kabla kesi haijaanza.

Mahakama ilimpa DPP mwezi mmoja kukamilisha uchunguzi. Hiyo ilikuwa September 14 2019. Baada ya hapo sijui nini kimeendelea. Labda kuna amri kutoka juu imepita kuingilia uhuru wa mahakama.

Mpaka sasa kesi inapigwa danadana.

Hivyo Tundu Lissu kusema atawaachia huru ma Sheikh wa uamsho anakuwa anaenda sawa na kauli ya mahakama ya September 14 2019.
Kiranga,
Tom Hagen ni Tundu Lissu kwani wote wanasheria.
Luca Brassi ile ni ngoma nyingine kabisa kwani staili zake ni za ''watu wasiojulikana.''
 
You are missing a point. TL has never, and will never be Capi dei Capi or Capi Di Tutti. Shekhe Ponda has capitalized in one of the promising bets in the world. TL promised, all those who are kept behind the bars without their cases being ruled, under his presidency, they will be freed.

Can you explain why JK's regime had put them behind the bars? Do you think the issues related to security and terrorism can be easily decided by one chap, because he is the president? What if the same guys go out and kill any foreign dignitary? who is going to bear the consequences?

The better way of doing it, is to stop promulgating the religious division. There is no way one religion can decide the future of a country like Tanzania.

By the way, even Saudi Kingdom, which has been supporting Sunni Wahhabis and salafism to spread the religious extremism, show the sign of giving up. It messes everything. They hate Iran for no reason. They cause massacres in Yemen for no reason. Syria has been ruined for the same reasons.

And you guys think that is what we want for our country!! This time somebody has done a serious error of judgment. Muda utaongea. Naam, this is the beginning of the end.
 
You are missing a point. TL has never, and will never be Capi dei Capi or Capi Di Tutti. Shekhe Ponda has capitalized in one of the promising bets in the world. TL promised, all those who are kept behind the bars without their cases being ruled, under his presidency, they will be freed.

Can you explain why JK's regime had put them behind the bars? Do you think the issues related to security and terrorism can be easily decided by one chap, because he is the president? What if the same guys go out and kill any foreign dignitary? who is going to bear the consequences?

The better way of doing it, is to stop promulgating the religious division. There is no way one religion can decide the future of a country like Tanzania.

By the way, even Saudi Kingdom, which has been supporting Sunni Wahhabis and salafism to spread the religious extremism, show the sign of giving up. It messes everything. They hate Iran for no reason. They cause massacres in Yemen for no reason. Syria has been ruined for the same reasons.

And you guys think that is what we want for our country!! This time somebody has done a serious error of judgment. Muda utaongea. Naam, this is the beginning of the end.
If these guys are all that they are cracked up to be, why is it so difficult for the DPP to build a strong case and nail them?

Surely the DPP isn't that incompetent now, or is he?
 
If these guys are all that they are cracked up to be, why is it so difficult for the DPP to build a strong case and nail them?

Surely the DPP isn't that incompetent now, or is he?

I don't have a straight answer, because I don't know what actually is facing them. The only thing am certain about, when the criminal sheets come from one of the western powers, normally, with our dependence diseases, it may take ages before something eventually happens.
TL knows some of the promises of that kind, are hard to deliver.
 
I don't have a straight answer, because I don't know what actually is facing them. The only thing am certain about, when the criminal sheets come from one of the western powers, normally, with our dependence diseases, it may take ages before something eventually happens.
TL knows some of the promises of that kind, are hard to deliver.
Don't you think that you are pre-judging the case without having the facts?
 
You are missing a point. TL has never, and will never be Capi dei Capi or Capi Di Tutti. Shekhe Ponda has capitalized in one of the promising bets in the world. TL promised, all those who are kept behind the bars without their cases being ruled, under his presidency, they will be freed.

Can you explain why JK's regime had put them behind the bars? Do you think the issues related to security and terrorism can be easily decided by one chap, because he is the president? What if the same guys go out and kill any foreign dignarity? who is going to bear the consequences?

The better way of doing it, is to stop promulgating the religious division. There is no way one religion can decide the future of a country like Tanzania.

By the way, even Saudi Kingdom, which has been supporting Sunni Wahhabis and salafism to spread the religious extremism, show the sign of giving up. It messes everything. They hate Iran for no reason. They cause massacres in Yemen for no reason. Syria has been ruined for the same reasons.

And you guys think that is what we want for our country!! This time somebody has done a serious error of judgment. Muda utaongea. Naam, this is the beginning of the end.
You are trying to create illusions on the things which need actual facts.
Why did the government retain those sheikhs without preceding the case?
Who is above the laws?

We need the DPP to prove those accusations before the court and not media propaganda. Let firstly free those sheikhs. The are innocent up to this moment.
 
Mzee wa historia na fasihi mara hii ushamuunganisha Godfather na Sheikh Ponda?

Kama Sheikh Ponda ni Don Vito Corleone, basi Tundu Lissu ni Luca Brassi!

Or is it the other way around?

Ila kuhusu ma Sheikh wa uamsho, mahakama ilishamuamuru DPP alete ushahidi mahakamani, kesi isikilizwe.

Au, akishindwa kuleta ushahidi, watuhumiwa waachiwe.

Maana kumfunga mtu miaka sita kwa kisingizio cha "uchunguzi unaendelea" si haki. Miaka sita jela ni hukumu tayari, kabla kesi haijaanza.

Mahakama ilimpa DPP mwezi mmoja kukamilisha uchunguzi. Hiyo ilikuwa September 14 2019. Baada ya hapo sijui nini kimeendelea. Labda kuna amri kutoka juu imepita kuingilia uhuru wa mahakama.

Mpaka sasa kesi inapigwa danadana.

Hivyo Tundu Lissu kusema atawaachia huru ma Sheikh wa uamsho anakuwa anaenda sawa na kauli ya mahakama ya September 14 2019.

Sollozo anamsubiri Luca Brasi 😂😂😂😂😂
 
Sheikh ilunga hakua sheikh sheikh kama wakina ponda ilunga alikuwa sheikh mwenywe misimamo migumu sn sn uwezi mfananisha na ponda, ilunga alikuwa anafanana na sheikh aboud rogo wa mombasa , ilunga hakuamini ktk demokrasia ata siku moja. ilunga misimamo yake ccm Chadema wote wapo kwenye batili ndio maana ata kifo cha huyu mwamba kulikua cha utata sn kutokana na kuisemea haqq.tafuta clip zake akiwa azungumzia mauaji ya sheikh rogo
Mohamed Said umenikumbusha harakati za marehemu Ostaz H. ilunga Allah amrehemu alikuwa anamsimulia Sana huyu Amerigo bunasera
 
BINADAMU ANAPOKATA TAMAA YA KUPATA HAKI: KISA CHA AMERIGO BONASERA NA DON VETO CORLEONE MFANO WA SHEIKH PONDA.

Katika kitabu cha "The Godfather," kuna watu wawili muhimu katika kueleza nini binadamu hufanya anapodhulumiwa na jamii na watoa haki wakamdhulumu pia.

Amerigo Bonasera kazi yake ni "undertaker," yaani kutayarisha maiti kwa ajili ya maziko.

Kazi hii ilimpa maisha mazuri katika mji wa New York ya baada ya Vita Vya Pili Vya Dunia.

Amerigo Bonasera alikuwa na mtoto mmoja binti aliyempenda sana.

Huyu bint akachukuliwa na vijana wenzake wa kiume kwa matembezi kumbe ndani ya nafsi zao walikuwa na lao jambo.

Wakamlewesha kwa nia ya kumbaka.

Huyu binti alikuwa bikra na hakukubali kuvunjiwa heshima yake na wale wahuni washenzi.

Akapambana na washenzi wale na kuishinda azma yao lakini walimuacha uso wake uliokuwa mzuri umevurugika kwa kuumizwa vibaya sana.

Kesi ikaenda mahakamani.

Hawa vijana ni kutoka familia kubwa zenye satwa baba zao wakazungumza na hakimu wale vijana mahakama ikawatia hatiani lakini hukumu ikawa "suspended," yaani hawatatumikia kifungo kama sheria inavyotaka.

Amerigo Bonasera na mkewe wakatoka mahakamani vichwa wameinamisha wanabubujikwa na machozi kwa dhulma waliyofanyiwa na mahakama.

Wale washenzi na wazazi wao wakiwa wamesimama nje ya jengo la mahakama wakawa wanamtazama Amerigo Bonasera na mkewe huku wanacheka wamefurahishwa na hukumu aliyotoa hakimu.

Amerigo Bonasera akamwambia mkewe, "Twende kwa Godfather tukatafute haki yetu."

Godfather Don Veto Corleone akaisikiliza kesi ya Amerigo Bonasera kisha akamuuliza, "Umekwenda polisi na haki yako umepewa."

Hapa kuna mengi baina ya watu hawa wawili sitayaeleza.

Godfather akamwambia Amerigo Bonasera aitue roho yake yeye atampa haki yake aliyonyimwa na mahakama ya serikali.

Amerigo Bonasera alimuomba Godfather awaue wale vijana wote.

Godfather yeye mpenda haki akamkatalia akamwambia, "Hapana wewe mwanao yu hai."

Naam.

Godfather alihukumu kesi ile kwa uadilifu.

Siku ya pili wale washenzi wote walikuwa vitandani hospitali nyuso zao hazitamaniki taya zao zimeungwa kwa waya na nyuso zimepitishiwa nyuzi kadhaa, vijana waliokuwa na sura jamil wametiwa ulemavu wa maisha kama walivyomsababishia binti Bonasera.

Ujumbe ulikuwa umewafikia wazazi wa watoto wale sawia.

Amerigo Bonasera akawa anakunywa kahawa nyumbani kwake na mkewe roho zimewatua kwani haki yao waliyodhulumiwa mahakamani imepatikana nje ya mahakama.

Mpenzi msomaji mitandaoni kumejaa maneno makali dhidi ya masheikh wanaompinga Sheikh Ponda kwa kuwataka Waislam kumpigia kura Tundu Lisu.

Masheikh hawa kwa kukosa kujua hali ilivyo nje ya duru lao kuwa Sheikh Ponda anaungwa mkono na Waislam wengi wamefanya kosa lile lile lililofanywa na hakimu aliyedhulumu haki ya Amerigo Bonasera.

Waislam kwa miaka mingi walishaipeleka kesi yao kwa Sheikh Ponda kutafuta haki yao nje ya watoa haki rasmi kama alivyofanya Amerigo Bonasera.

Sheikh Ponda kama alivyofanya Godfather Don Veto Corleone ametoa hukumu ya haki.

Sheikh Ponda amewaonyesha Waislam njia ya kupita.

Katika kisa cha Amerigo Bonasera kuna mazingatio makubwa kwa hawa masheikh na pia kwa serikali ya CCM.

Ujumbe wa Sheikh Ponda ni mzito na kama ulivyokuwa ujumbe wa Don Veto Corleone umefika na kueleweka sawia.
Hovyoooooooo, pumbvuuuuuuuuuuuuuuu
 
Sheikh ilunga hakua sheikh sheikh kama wakina ponda ilunga alikuwa sheikh mwenywe misimamo migumu sn sn uwezi mfananisha na ponda, ilunga alikuwa anafanana na sheikh aboud rogo wa mombasa , ilunga hakuamini ktk demokrasia ata siku moja. ilunga misimamo yake ccm Chadema wote wapo kwenye batili ndio maana ata kifo cha huyu mwamba kulikua cha utata sn kutokana na kuisemea haqq.tafuta clip zake akiwa azungumzia mauaji ya sheikh rogo
Ostaz ilunga nilianza kumfuatilia Muda mrefu Sana alikuwa anamisimamo migumu sana
Ndiyo maana nasema afadhali Shekh Issa Ponda kuliko hao mashekh ubwabwa wabakwata

Waislamu tutamkumbuka milele Allah ampe makazi mema
 
Asante sana mleta mada. Hii habari ya Brassi nilikuwa sijaipata inagwa niliwahi kusikia habari za Filamu ya 'Godfather'!
Nimechakura mtandaoni na nimekutana na nukuu hii.
===
"There are men in this world who go about demanding to be killed. They argue in gambling games; they jump out of their cars in a rage if someone so much as scratches their fender. These people wander through the streets calling out "Kill me, kill me." Luca Brasi was such a man. And since he wasn't scared of death, and in fact, looked for it... I made him my weapon. Because I was the only person in the world that he truly hoped would not kill him. "―Vito Corleone
 
Amin
Ostaz ilunga nilianza kumfuatilia Muda mrefu Sana alikuwa anamisimamo migumu sana
Ndiyo maana nasema afadhali Shekh Issa Ponda kuliko hao mashekh ubwabwa wabakwata

Waislamu tutamkumbuka milele Allah ampe makazi mema
 
You are missing a point. TL has never, and will never be Capi dei Capi or Capi Di Tutti. Shekhe Ponda has capitalized in one of the promising bets in the world. TL promised, all those who are kept behind the bars without their cases being ruled, under his presidency, they will be freed.

Can you explain why JK's regime had put them behind the bars? Do you think the issues related to security and terrorism can be easily decided by one chap, because he is the president? What if the same guys go out and kill any foreign dignarity? who is going to bear the consequences?

The better way of doing it, is to stop promulgating the religious division. There is no way one religion can decide the future of a country like Tanzania.

By the way, even Saudi Kingdom, which has been supporting Sunni Wahhabis and salafism to spread the religious extremism, show the sign of giving up. It messes everything. They hate Iran for no reason. They cause massacres in Yemen for no reason. Syria has been ruined for the same reasons.

And you guys think that is what we want for our country!! This time somebody has done a serious error of judgment. Muda utaongea. Naam, this is the beginning of the end.
Silence might have been your good response to this article! Since, as a nation, we decided and agreed on the rule of law then let's all stick to that!

Those purported "culprits" have denied their rights to be heard, movement, representation and worse, they are "serving" sentences without court conviction!

So pathetic!
 
Back
Top Bottom