Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,495
- 9,275
Mhubiri wa neno la Mungu Ostadh Mwaipopo ameongea na wanahabari na kutoa maoni yake kuhusu kauli ya Masheikh ya kumuonya Sheikh Ponda aliyetumia neno la Mungu kuwaapisha baadhi ya viongozi wa CHADEMA akiwemo Tundu Lissu kuwa ndio Rais wa Tanzania.
Mwaipopo ameomuomba Rais Magufuli kutofuata maneno ya watu bali afanye kazi kufuata sheria ya Nchi ila amemuomba awaonee huruma Masheikh ambao wapo gerezani ingawa yeye hakuwakamata na Rais Magufuli hajawahi kukamata kiongozi yeyote wa Dini.
“Lissu anatudanganya kuwa atawaachia masheikh waliopo gerezani, wakati wanakamatwa alikuwa bungeni na ni mwanasheria hajawahi kuwatetea hata siku moja bungeni, lakini pia tunatakiwa tumuombe Rais Magufuli awaachie kwa huruma yake kumbukeni aliyewakamata sio Magufuli tena walikamatwa na viongozi wakubwa wote walikuwa Waislamu.
Zitto Kabwe wakati anaondoka CHADEMA na kuanzisha ACT Wazalendo alisema kwa kinywa chake kuwa CHADEMA kuna Udini, Udikteta na Ukabila leo anageuka na kuwaunga mkono walewale aliowakimbia kama sio maslahi binafsi ni nini?
Atueleze kilichomkimbiza CHADEMA ni kipi kwanza na Sheikh Ponda alikuwa anampigia kampeni Lipumba, kwanini sasa hivi amehamia kwa Tundu Lissu tatizo nini kama hatafuti maslahi yake binafsi?
Mwaipopo ameomuomba Rais Magufuli kutofuata maneno ya watu bali afanye kazi kufuata sheria ya Nchi ila amemuomba awaonee huruma Masheikh ambao wapo gerezani ingawa yeye hakuwakamata na Rais Magufuli hajawahi kukamata kiongozi yeyote wa Dini.
“Lissu anatudanganya kuwa atawaachia masheikh waliopo gerezani, wakati wanakamatwa alikuwa bungeni na ni mwanasheria hajawahi kuwatetea hata siku moja bungeni, lakini pia tunatakiwa tumuombe Rais Magufuli awaachie kwa huruma yake kumbukeni aliyewakamata sio Magufuli tena walikamatwa na viongozi wakubwa wote walikuwa Waislamu.
Zitto Kabwe wakati anaondoka CHADEMA na kuanzisha ACT Wazalendo alisema kwa kinywa chake kuwa CHADEMA kuna Udini, Udikteta na Ukabila leo anageuka na kuwaunga mkono walewale aliowakimbia kama sio maslahi binafsi ni nini?
Atueleze kilichomkimbiza CHADEMA ni kipi kwanza na Sheikh Ponda alikuwa anampigia kampeni Lipumba, kwanini sasa hivi amehamia kwa Tundu Lissu tatizo nini kama hatafuti maslahi yake binafsi?