Sheikh Mselem: Tukiambiwa Hapana, tusishindane na mwenye nguvu

"etween the lines

"Inawezekana tumefanya jambo halali, tumeliombea ruhusa serikalini, tukapewa ruhusa lakini kuna watu wale wasiojulikana, kama wanataka kuharibu kitu au ku-create kitu basi hutengeneza sababu ambayo itatupa sisi dhima kwa hiyo tuwe wavumilivu"

"tutakaporuhusiwa kufanya mijumuiko tutafanya, tukiambiwa hapana basi tusishindane na mwenye nguvu."

Ujumbe wote uko hapo kashasema kila kitu kwa wenye macho makubwa
Hawawezi rudia huu utopolo ila wanatakiwa waweke mtu wa kuwachunguza hawakawi kwenda Iraq kujifunza ugaidi mkubwa
 
Hakuna mahakama iliyosema shutuma zimeshindwa kuthibishwa. Wewe ni mtu mzima na msomi mzuri sana tena mjuvi wa mambo unaelewa kabisa DPP anayo haki na mamlaka kikatiba kuondoa kesi mahakamani pale anapoona hana haja na hiyo kesi tena

Kutokuwa na nia ya kuendelea na kesi haimaanishi makosa hayapo. Kuna Mambo mengi huchangia ikiwemo mwenendo na ushirikiano wa watuhumiwa wenyewe kwa vyombo vinavyohusika

Ikiwa kweli kwa miaka yote hiyo 9 waliwekwa kizuizini kwa kuonewa, hao ni watu wazima na waelewa wa mambo. Naamini wanaouwezo mkubwa kabisa wa kugoma kutoka mahabusu kushinikiza kesi yao isikilizwe na hatimaye hukumu isomwe

Na wafanya hivyo basi tuone Kama kweli mnahisi walionewa

Msiwapambe na kutaka kuwatakatifuza hao watu. Ukweli wa wao kuwekwa huru wanaujua wao na mamlaka zilizowaachia. Nyie wengine mtaendelea kupiga ramli tu

Wakafungue kesi za madai na majina yao yasafishwe basi tuone
Facts
 
Alikosea aliposema tusishindane na mwenye nguvu.

Basi tusingedai himaya ya Mwingereza iondoke Tanganyika maana walikuwa na nguvu ya kutawala dunia.

Shehe Mselem ametoa kituko kikubwa katika historia ya uanaharakati duniani.

Amefungwa kidhalimu kwa kutoa maoni kuhusu Muungano, anatoka anasema ametosheka na furaha ya kutolewa jela, tusishindane na mwenye nguvu. Huko jela atakuwa amelishwa sumu ya kumpumbaza, zombified.
Ulitaka ahamasishe vurugu au mikusanyiko mikubwa ya kuwapokea.....hukuelewa kama alikuwa anaongelea walivyotolewa mmoja mmoja kuangalia upepo huko mtaani kama kutatokea mikusanyiko na sherehe za kuwapokea.
 
Alikosea aliposema tusishindane na mwenye nguvu.

Basi tusingedai himaya ya Mwingereza iondoke Tanganyika maana walikuwa na nguvu ya kutawala dunia.

Shehe Mselem ametoa kituko kikubwa katika historia ya uanaharakati duniani.

Amefungwa kidhalimu kwa kutoa maoni kuhusu Muungano, anatoka anasema ametosheka na furaha ya kutolewa jela, tusishindane na mwenye nguvu. Huko jela atakuwa amelishwa sumu ya kumpumbaza, zombified.
Ni rahisi kuyaandika haya ukiwa na kikombe cha chai pembeni yako huku ukichezea simu yako au laptop kuliko kujiweka katika nafasi ya huyo unayemsema.
 
Hawawezi rudia huu utopolo ila wanatakiwa waweke mtu wa kuwachunguza hawakawi kwenda Iraq kujifunza ugaidi mkubwa
Ukimsikiliza Mselem utaona kabisa hana hamu na harakati tena.

Na anavyosema wameachiwa kwa taratibu za kisheria kwa sharti la kutokufanya kosa tena.

Wakirudia hiyo sheria inaruhusu wakamatwe tena warudishwe mahakama kwa makosa yale yale.

Mselem anasema umri wenyewe umeenda hataki kujiharakishia kifo, haki ataipata Mbinguni🤣😭
 
Ukimsikiliza Mselem utaona kabisa hana hamu na harakati tena.

Na anavyosema wameachiwa kwa taratibu za kisheria kwa sharti la kutokufanya kosa tena.

Wakirudia hiyo sheria inaruhusu wakamatwe tena warudishwe mahakama kwa makosa yale yale.

Mselem anasema umri wenyewe umeenda hataki kujiharakishia kifo, haki ataipata Mbinguni
Hana hamu na ubayani
 
Hana hamu na ubayani
Wale wamekuwa DIS-RADICALISED kabisa.

Kwanza kila mmoja alikuwa anakaa chumba chake na anahojiwa kivyake tena uchi wa mnyama ndani ya chumba kimyaaa. Yaani hapo dunia unaiona wewe kama wewe, mihemko yote ya kushabikiwa na watu hakuna.

Hapo ndio utayaoa maisha kwa mtazamo tofauti. Imagine Masheikh waliokuwa wanaongelea kukata vichwa na kutoa roho mbichi, leo wanahubiri UTU na HESHIMA🤣

Dola ni Shetani kmmmmmake🤣
 
Wale wamekuwa DIS-RADICALISED kabisa.

Kwanza kila mmoja alikuwa anakaa chumba chake na anahojiwa kivyake tena uchi wa mnyama ndani ya chumba kimyaaa. Yaani hapo dunia unaiona wewe kama wewe, mihemko yote ya kushabikiwa na watu hakuna.

Hapo ndio utayaoa maisha kwa mtazamo tofauti. Imagine Masheikh waliokuwa wanaongelea kukata vichwa na kutoa roho mbichi, leo wanahubiri UTU na HESHIMA

Dola ni Shetani kmmmmmake
thats the goverment for you. sometimes ushetani unahitajika ili kuondoa ushetani mwingine
 
Wakati unawakebehi Mashekh hawa kwa kuona madhaifu kwa kile walichokipigania mpaka wakaa gerezani miaka tisa, wenyewe wameona walichokuwa wanakifanya hakikuwa sahihi
Hayo ni ya kwake yeye Mselem. Hatujui kama Shehe Faridi na wenzake wanaamini ni makosa kudai kuvunja Muungano.

Shehe Mselem magerezani amevurugwa psychologically, to say the least.

I mean, sikutegemea Shehe Mselem
atangaze kesho baada ya kuswali Ijumaa tutaanza matembezi huru kuanzia Msikiti wa Mtambani kuelekea msituni.

Lakini pia sikutegemea mwanaharakati aseme furaha ya kuachiwa inanitosha, usishindane na mwenye nguvu, serikali iikishasema hapana basi hapana, itoshe kusema furaha ya uhuru inatosha.

Hell no. Itoshe wewe KUKAA KIMYA!

Shehe Mselem anaingia kwenye vitabu vya rekodi za dunia vya Guiness. Mfungwa wa kwanza wa kisiasa aliyetoka jela la kusema nasalimu amri.

Afrika, the third world, tuna bahati mbaya sana. Hata wapigania haki wetu nao ni third rate, uchwara mtupu.
 
Nimejiuliza sana hili, kama matukio yote yalikuwa wazi kabisa kwa nini imechukua miaka 9 wao bila upelelezi kukamilika!
Lakini pia tujiulize kwanini mara baada ya kuwaweka ndani umwagiaji watu tindikali,na uchomaji wa makanisa ulikoma?
 
Hayo ni ya kwake yeye Mselem. Hatujui kama Shehe Faridi na wenzake wanaamini ni makosa kudai kuvunja Muungano.

Shehe Mselem magerezani amevurugwa psychologically, to say the least.

I mean, sikutegemea Shehe Mselem
atangaze kesho baada ya kuswali Ijumaa tutaanza matembezi huru kuanzia Msikiti wa Mtambani kuelekea msituni.

Lakini pia sikutegemea mwanaharakati aseme furaha ya kuachiwa inanitosha, usishindane na mwenye nguvu, serikali iikishasema hapana basi hapana, itoshe kusema furaha ya uhuru inatosha.

Hell no. Itoshe wewe KUKAA KIMYA!

Shehe Mselem anaingia kwenye vitabu vya rekodi za dunia vya Guiness. Mfungwa wa kwanza wa kisiasa aliyetoka jela la kusema nasalimu amri.

Afrika, the third world, tuna bahati mbaya sana. Hata wapigania haki wetu nao ni third rate, uchwara mtupu.
Mselem kayaona yote. Anakiri kuwa nchi yetu watawala wakitaka sheria haitumiki kabisa na huna cha kufanya.

Hata wanaharakati wengi waliofanikiwa hawakutumia njia ya jino kwa jino. Angalia South Africa, angalia kina Nyerere.

Na unapokuja kwenye nchi kama yetu ambayo watu wanakushangilia lakini, ukikamatwa wanakaa pembeni risks inakuwa kubwa zaidi.
 
Hata wanaharakati wengi waliofanikiwa hawakutumia njia ya jino kwa jino. Angalia South Africa,...

South Africa na Nyerere ?

Umetoa mifano mibaya, mibovu kuliko nchi zote duniani.

Umkontho we Sizwe ya Nelson Mandela walilipua majengo ya serikali dhalimu ya South Africa. Julius Nyerere alitoa safe haven kwa wapiganaji wa ANC.

Na walipotoka gerezani kina Walter Sisulu na Nelson Mandela hawakusema tunafuraha ya kutoka, mwenye nguvu mpishe. Serikali wakisema hapana, hapana.

Sasa wanajipendekeza kwa serikali ?Kama huu si ushehe ubwabwa, ushehe ubwawa ni nini ?

Shehe Mselem is unprincipled.

Hata hajui alikuwa anapigania nini.

I hope and pray Shehe Farid nae hajawa zombified huko magereza manake na yeye ame dissapoint vibaya mno, ametoka jela bila wenzake.
 
Msiende tena mkaanze kuhamasisha kuchoma makinisa na kuwapiga mapadri risasi
Mbona mahakama imeshindwa kuwatia hatiani dhidi ya hayo makosa yako!?
Haki huinua taifa,tuache kutuhumiana pasipo ushahidi.
Chuki za kidini,kikabila,kikanda,kimaisha au kielimu sio za kuziendekeza kabisa.
 
South Africa na Nyerere ?

Umetoa mifano mibaya, mibovu kuliko nchi zote duniani.

Umkontho we Sizwe ya Nelson Mandela walilipua majengo ya serikali dhalimu ya South Africa. Julius Nyerere alitoa safe haven kwa wapiganaji wa ANC.

Na walipotoka gerezani kina Walter Sisulu na Nelson Mandela hawakusema tunafuraha ya kutoka, mwenye nguvu mpishe. Serikali wakisema hapana, hapana.

Sasa wanajipendekeza kwa serikali ?Kama huu si ushehe ubwabwa, ushehe ubwawa ni nini ?

Shehe Mselem is unprincipled.

Hata hajui alikuwa anapigania nini.

I hope and pray Shehe Farid nae hajawa zombified huko magereza manake na yeye ame dissapoint vibaya mno, ametoka jela bila wenzake.
Mandela alipata nini baada ya Uhuru zaidi ya mtu mweusi kukubaliwa kutoa Rais tu ?
 
Osama ni different entity different case.
+ yeye alikuwa ana succession plan? hawa walikuwa nayo au walianzisha harakati juu juu?
Point ni kuwa, kufungwa kwao sio sababu ya kwamba eti hakuna matukio. Hivi ni Shekh Msellem na Faridi ndio waliokwenda kumwagia mtu tindi kali?
 
Mandela alipata nini baada ya Uhuru zaidi ya mtu mweusi kukubaliwa kutoa Rais tu ?
Madai yake manne yote yalipita.

Mandela alikataa kutolewa gerezani mwaka 1984 mpaka:

1. Wafungwa wenzake wote waachiwe

2. ANC isajiliwe tena, iruhusiwe mikutano, iruhusiwe kushiriki chaguzi huru na haki

3. Wanaharakati waliotoroka jela, waliokimbia ujasusi wa kaburu, kutekwa na kuuliwa, watakapotua uwanja wa ndege wanaporudi nyumbani asikamatwe hata mmoja

4. Serikali iseme inafuta udhalimu wa ubaguzi

Alipokataa masharti akapigwa mvua nyingine tano! Baadae YOTE YALITIMIA

Shehe Mselem na Shehe Farid , viongozi waandamizi wa harakati, maskini ya Mungu, wametoka gerezani kabla ya wafuasi wao!

Munyanz Mngu Subhana wa Taala, tuonee huruma na hawa wanaharakati wetu uchwara wa Tanzania
 
Madai yake manne yote yalipita.

Mandela alikataa kutolewa gerezani mwaka 1982 mpaka:

1. Wafungwa wenzake wote waachiwe

2. ANC isajiliwe tena, iruhusiwe mikutano, iruhusiwe kushiriki chaguzi huru na haki

3. Wanaharakati waliokimbia kutekwa, kufungwa na kuuliwa watakapotua uwanja wa ndege wanaporudi asikamatwe hata mmoja.

4. Serikali iseme inafuta udhalimu wa ubaguzi.

YOTE YALITIMIA

Shehe Mselem na Shehe Farid , viongozi waandamizi wa harakati, wametoka gerezani kabla ya wafuasi wao!

Munyanz Mngu Subhana wa Taala, tuonee huruma na hawa wanaharakati wetu uchwara wa Tanzania
Dai kubwa na la msingi, ARDHI halikufutwa. Kila walichokuwa wanamiliki wazungu mpaka leo bado wanamiliki.

Kilichofanyika ni marudhiano tu ya kisiasa ili maisha yaendelee.

Naweza kusema ni sawa na ACT+CCM huko Zanzibar.

Kama ilivyo ngumu wazungu SA kurudisha ardhi ndivyo ilivyo ngumu kuhusu madai ya Mselem.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom