19 January 2023
Dar es Salaam, Tanzania
SHEIKH ABUU - HATARI INAKUJA TUSIPOTOA TAHADHARI KWA MADHEHEBU HAYA MAWILI
Sheikh Abuu Iddi ambaye ni Msaidizi wa Mufti wa Tanzania ametoa tahadhari hiyo kwa kuwa inaweza kupelekea amani kuvunjika nchini Tanzania.
Sheikh Abuu Iddi CV (wasifu) yake imesheheni nyadhifa kadha wa kadha ktk utumishi kwa dini na jamii kwani yeye ni imamu mkuu msikiti wa Masjid Mnyamani Buguruni jijini Dar es Salaam. Pia kwa miaka 16 amekuwa akiendesha kipindi ktk kituo cha televisheni cha Channel Ten kutoa daawa na darsa, mratibu Al Risala Foundation, Mratibu wa Kudumisha Amani katika mkoa wa Dar es Salaam, Mwandishi wa kitabu kinachokwenda kwa jina Misingi 15 ya amani, mwandishi wa makala katika gazeti kubwa la Mwananchi pia ni Mshauri wa dini na jamii wa Mufti Mkuu wa Tanzania.
Sheikh Abuu Iddi ameelekeza tahadhari hii hususan kwa madhehebu ya Sunni na Shia yanayo shambuliana kupitia majukwaa mbalimbali ya mitandao ya kijamii wakiongozwa na viongozi wao.
Amewataja Sheikh Mziwanda na Samir wa upande wa Sunni huku upande wa madhehebu ya Shia kupitia Sheikh Hemed Jalala, Sheikh Abdul na wenzie watatu wakijitetea.
Na pande hizi mbili za madhehebu haya yakinukuu kile wanachoamini kwamba ni sawa kwa upande wa madhehebu yao.
Pande hizo zimewekuwa zikirushiana maneno yanayotishia amani za kila aina mfano amani ya viungo, amani ya roho, kuvunjiana heshima n.k huku wote wa pande hizi mbili wakiwa na wafuasi wao hivyo kutishia amani kwa ujumla ya Tanzania maana wafuasi wa pande hizi mbili zinaweza kukabiliana kutetea pande zao na viongozi wao .
Mfumo wa uendeshaji wa mijadala hii imeleta ukakasi mkubwa huku maneno ya kutishiana uhai baina ya pande hizo yakitamkwa asema Sheikh Abuu Iddi kwa masikitiko makubwa.
Sheikh Abuu Iddi anasisitiza kuwa BAKWATA ni ya kwa ajili ya madhehebu yote na hivyo haiwezekeni dhehebu moja kuzuiwa kuja ktk shughuli za BAKWATA kama inavyochagizwa na baadhi ya waumini kuwa viongozi wa madhehebu ya Mashia watengwe......
Dar es Salaam, Tanzania
SHEIKH ABUU - HATARI INAKUJA TUSIPOTOA TAHADHARI KWA MADHEHEBU HAYA MAWILI
Sheikh Abuu Iddi ambaye ni Msaidizi wa Mufti wa Tanzania ametoa tahadhari hiyo kwa kuwa inaweza kupelekea amani kuvunjika nchini Tanzania.
Sheikh Abuu Iddi CV (wasifu) yake imesheheni nyadhifa kadha wa kadha ktk utumishi kwa dini na jamii kwani yeye ni imamu mkuu msikiti wa Masjid Mnyamani Buguruni jijini Dar es Salaam. Pia kwa miaka 16 amekuwa akiendesha kipindi ktk kituo cha televisheni cha Channel Ten kutoa daawa na darsa, mratibu Al Risala Foundation, Mratibu wa Kudumisha Amani katika mkoa wa Dar es Salaam, Mwandishi wa kitabu kinachokwenda kwa jina Misingi 15 ya amani, mwandishi wa makala katika gazeti kubwa la Mwananchi pia ni Mshauri wa dini na jamii wa Mufti Mkuu wa Tanzania.
Sheikh Abuu Iddi ameelekeza tahadhari hii hususan kwa madhehebu ya Sunni na Shia yanayo shambuliana kupitia majukwaa mbalimbali ya mitandao ya kijamii wakiongozwa na viongozi wao.
Amewataja Sheikh Mziwanda na Samir wa upande wa Sunni huku upande wa madhehebu ya Shia kupitia Sheikh Hemed Jalala, Sheikh Abdul na wenzie watatu wakijitetea.
Na pande hizi mbili za madhehebu haya yakinukuu kile wanachoamini kwamba ni sawa kwa upande wa madhehebu yao.
Pande hizo zimewekuwa zikirushiana maneno yanayotishia amani za kila aina mfano amani ya viungo, amani ya roho, kuvunjiana heshima n.k huku wote wa pande hizi mbili wakiwa na wafuasi wao hivyo kutishia amani kwa ujumla ya Tanzania maana wafuasi wa pande hizi mbili zinaweza kukabiliana kutetea pande zao na viongozi wao .
Mfumo wa uendeshaji wa mijadala hii imeleta ukakasi mkubwa huku maneno ya kutishiana uhai baina ya pande hizo yakitamkwa asema Sheikh Abuu Iddi kwa masikitiko makubwa.
Sheikh Abuu Iddi anasisitiza kuwa BAKWATA ni ya kwa ajili ya madhehebu yote na hivyo haiwezekeni dhehebu moja kuzuiwa kuja ktk shughuli za BAKWATA kama inavyochagizwa na baadhi ya waumini kuwa viongozi wa madhehebu ya Mashia watengwe......