Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,706
- 155,198
Babu Seya (kulia) akiwaaga watu waliofurika mahakamani kusikiliza kesi yao. Kushoto ni mwanaye Papii Kocha (Mtoto wa Mfalme).
MTABIRI maarufu Afrika Mashariki, Sheikh Yahya Hussein, amesema mwanamuziki maarufu, Nguza Vicking (Baby Seya) atatoka gerezani, kitu ambacho ni habari njema kwa wapenzi wa muziki nchini....
Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake Magomeni jijini Dar es Salaam, Sheikh Yahya alisema alituma ujumbe ulioongozwa na Bw. Hassani Yahya siku ya Jumamosi iliyopita kwenda kumuona Babu Seya gerezani Ukonga na amemuambia mwanamuziki huyo kuwa avute subira kwani elimu ya nambari (Numerology) inaonesha kuwa atatoka gerezani.
Miaka ya nyuma nilitabiri kuwa Nguza atatoka gerezani Februari lakini kumbe kuna Nguza wawili sasa mmoja ametoka pamoja na mdogo wake, sasa bado nasema waliobaki watatoka, alisema Sheikh Yahya.
Alisema alipotabiri kwa waandishi wa habari na kupitia kituo cha televisheni cha Channel Ten kuwa Nguza atatoka Februari wakati ule watu wengi walipuuza lakini sasa imekuwa hivyo.