Master Race
JF-Expert Member
- Feb 19, 2026
- 823
- 2,004
Hujui unajadili nini, sasa sehemu ya hiyo Ibara si imeongelea Tu Uhuru wa mambo ya imani sasa inahusiana nini na mada yako?, maana ulikuwa unalalamika kuwa Zenji inageuzwa emirate ambapo ukiangalia wao wanafuata katiba yao.Soma ibara ya 19 ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Danganyika sorry Tanzania
Kasome Sheria ya ofisi ya mufti, huoni kuwa unajijibu na kujipinga, nenda kasome katiba ya Zanzibar utaona namna wao Wana Uhuru wa kuamua mambo Yao ikiwemo ya dini, dini (kiislamu ) na serikali Zanzibar zinakaa sehemu moja ndio maana kuna Ofisi ya Mufti ambayo ni ya serikali, mbona hakuna Ofisi ya Catholic, KKT nk iliyo chini ya serikali ya Zanzibar kama kweli serikali haina dini?,
Secular iloyopo (Zanzibar)ni ya kipande kidogo mnooo .....na ndio hoja yangu Inakuja hapo kuwa Zanzibar ni nchi ya kiislamu, Sisi tunawalazimisha tu na tumejichanganya , hujui kuwa mufti (kiongozi wa kiislamu Zanzibar) ni mtumishi wa umma (Serikali)??.... muungano Una missing pieces kibao.