Sharif Hamad adondosha chozi...!

Swahilian

JF-Expert Member
Apr 28, 2009
591
66
Nilisikitika hata mie baada ya kutangazwa matokeo yale, japo ndio hivyo ilishatamkwa Dr. Ally M. Shein Ndio Rais Mteule wa Zanzibar.

Hamad alipoitwa alipongeza ushindi huo japo alitamka dhahiri mbinu chafu za baadhi ya watendaji wa tume ya uchaguzi ( ZEC )

Hakika kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwake, aliamua kukaza moyo na kutoa kauli ya mdomoni kuwa Dr. SHEIN ametawazwa kuwa Rais na alisisitiza kwamba ktk uchaguzi huo hakuna mshindi yaani kama ungelikuwa mpira wa miguu ni matokeo ya sare au suluhu baina ya CUF na CCM.

Pembeni ya hapo kwa wale tulomtathimini kwa undani Maalim hasa usoni, alikuwa si yule Maalim mcheshi, mchangamfu na anayejiamini.

Alifanya kila jambo kama amelazimishwa au inambidi afanye hivyo kwani hakukuwa na njia mbadala.

Hisia na Mtazamo halisi wa Hamad (Sharif) umejionesha zaidi ktk machozi yalokuwa yakimtoka kila alipokuwa akizungumza, yalimchuruzika kwa vipindi japo aliweza kujikaza kisabuni asiangue kilio kikubwa.

Pole sana Hamad kwa kuumia, mie niliyaona machozi yako yalonipa ujumbe fulani ktk maisha.
 
Nilisikitika hata mie baada ya kutangazwa matokeo yale, japo ndio hivyo ilishatamkwa Dr. Ally M. Shein Ndio Rais Mteule wa Zanzibar.

Hamad alipoitwa alipongeza ushindi huo japo alitamka dhahiri mbinu chafu za baadhi ya watendaji wa tume ya uchaguzi ( ZEC )

Hakika kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwake, aliamua kukaza moyo na kutoa kauli ya mdomoni kuwa Dr. SHEIN ametawazwa kuwa Rais na alisisitiza kwamba ktk uchaguzi huo hakuna mshindi yaani kama ungelikuwa mpira wa miguu ni matokeo ya sare au suluhu baina ya CUF na CCM.

Pembeni ya hapo kwa wale tulomtathimini kwa undani Maalim hasa usoni, alikuwa si yule Maalim mcheshi, mchangamfu na anayejiamini.

Alifanya kila jambo kama amelazimishwa au inambidi afanye hivyo kwani hakukuwa na njia mbadala.

Hisia na Mtazamo halisi wa Hamad (Sharif) umejionesha zaidi ktk machozi yalokuwa yakimtoka kila alipokuwa akizungumza, yalimchuruzika kwa vipindi japo aliweza kujikaza kisabuni asiangue kilio kikubwa.

Pole sana Hamad kwa kuumia, mie niliyaona machozi yako yalonipa ujumbe fulani ktk maisha.
Nadhani furaha ya ushindi wake wa kishindo ni mwanaume wa shoka ngoma drooo na CCM simchezo
 
Nadhani furaha ya ushindi wake wa kishindo ni mwanaume wa shoka ngoma drooo na CCM simchezo

inawezekana ikawa hivyo lakini machozi yale si ya furaha!
Sijui lakini kila mtu anavyoweza kufasiri hali ile.... What about Pemba's Dream ( One day this Pemba n' Pemba People will never live like so..... The victory will be droven by one or two Son's of the land....)
Unaijua hiyo...?! Na Mengineyo.?!
 
Nilikuwa bored, hata sikupenda kuangalia usanii ule ningeumia roho zaidi...did he cry?
 
Ukweli Hamad ni kifaa CCM wamekubali kuwa kuna vichwa hapa nchini havijafanyiwa repair yaani origino kabisa sio kichwa cha slaa kina viraka kibao UDINI,UKABILA,UBINAFSI NA................Zanzibar ni moja na wazanzibari ni wamoja daima ubabaishaji mwiko.
Nadhani furaha ya ushindi wake wa kishindo ni mwanaume wa shoka ngoma drooo na CCM simchezo
 
hakutokwa na machozi ila aliongea kwa uchungu sana kuilaumu tume ya uchaguzi,hapa alidhihirisha kubali yaishe au kosa vyotevyote au aliye juu mpandie hukohuko
 
Nilikuwa bored, hata sikupenda kuangalia usanii ule ningeumia roho zaidi...did he cry?
alilia mkuu!....

nakumbuka nilikuwa nagugumia kesto laiti kama ya tisa hivi.....!na mimi nikajikuta nalia...INAUMAAAAAA
 
Ni usanii tu wala hakuna jipya. huko visiwani the difference is the same!
 
Nilisikitika hata mie baada ya kutangazwa matokeo yale, japo ndio hivyo ilishatamkwa Dr. Ally M. Shein Ndio Rais Mteule wa Zanzibar.

Hamad alipoitwa alipongeza ushindi huo japo alitamka dhahiri mbinu chafu za baadhi ya watendaji wa tume ya uchaguzi ( ZEC )

Hakika kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwake, aliamua kukaza moyo na kutoa kauli ya mdomoni kuwa Dr. SHEIN ametawazwa kuwa Rais na alisisitiza kwamba ktk uchaguzi huo hakuna mshindi yaani kama ungelikuwa mpira wa miguu ni matokeo ya sare au suluhu baina ya CUF na CCM.

Pembeni ya hapo kwa wale tulomtathimini kwa undani Maalim hasa usoni, alikuwa si yule Maalim mcheshi, mchangamfu na anayejiamini.

Alifanya kila jambo kama amelazimishwa au inambidi afanye hivyo kwani hakukuwa na njia mbadala.

Hisia na Mtazamo halisi wa Hamad (Sharif) umejionesha zaidi ktk machozi yalokuwa yakimtoka kila alipokuwa akizungumza, yalimchuruzika kwa vipindi japo aliweza kujikaza kisabuni asiangue kilio kikubwa.

Pole sana Hamad kwa kuumia, mie niliyaona machozi yako yalonipa ujumbe fulani ktk maisha.

Machozi ya mamba hayo, mwanamapinduzi huwa hakubali kirahisi hivyo, lazima kuna ahadi kapewa ama ni huo u makamu rais. Nataka niwaambie wazanzibari kuwa kwa kukubali kuvunja upinzani mmeiangamiza Zanzibar. Katika maswala ya utawala nilipitia kauli ifuatayo "Where there's no conflict, there's no development." Mahali ambapo hakuna migongano hakuna maendeleo. Kinachotakiwa ni regulate migongano isifike mbali sana na kuleta madhara. Hii serikali ya umoja wa kitaifa itawazidishieni umaskini, maana sasa hakuna wa kumwambia serikali umekosea. Haya shauri yenu.
 
Haukuwa usanii tuliouzoea ilikuwa ni hali halisi Sharrif hajawahi kufanya usanii sasa hukuangalia ulijuaje kuwa ni usanii?any way Zanzibar imeshinda sio CCM wala CUF bali ni wazanzibar CCM 50.1% CUF 49.1% bado huku BARA watu wametupwa kwa mbali bado wanalilia ushindi naanza kupata taswira ya maneno ya LIPUMBA sijui alisema nini vile?
Nilikuwa bored, hata sikupenda kuangalia usanii ule ningeumia roho zaidi...did he cry?
 
Hamad tatizo lake ni uchaguzi ukifika, anakuwa CCM B.

Uchaguzi ukiisha wanamfanya Chambio la CCM na kumtupa.

Kama angelikubali washirikiane na Upinzani wa BARA ili Katiba ibadilishwe, mambo yasingelikuwa hivyo.

Ila utaona Chadema wakienda kumwambia wawabane CCM, yeye atakuja na ya MWAFAKA.

Halafu mtu hapo juu anakuja na kusema Hamad ni KICHWA, kichwa my ***.

Alikubali KULA na sasa ngoja ALIWE KIDOGO.
 
Ukweli Hamad ni kifaa CCM wamekubali kuwa kuna vichwa hapa nchini havijafanyiwa repair yaani origino kabisa sio kichwa cha slaa kina viraka kibao UDINI,UKABILA,UBINAFSI NA................Zanzibar ni moja na wazanzibari ni wamoja daima ubabaishaji mwiko.
Yaa ni kama kichwa cha JK, UFISADI, UNAFIKI,UNDUGU, UFAMILIA Naaaaa.....!
 
Sio kichwa cha slaa kina viraka kibao UDINI,UKABILA,UBINAFSI NA................
Ndugu yangu msema ukweli tumia nguvu ya hoja na siyo kuibuka na unsubstantiated allegations na personal vendetta dhidi ya shujaa Dr Slaa.We unaushaidi wowote kuhusu tuhuma unazozielekeza kwa huyo mzee na mwanamapinduzi wa karne ya 21 kwa Tanzania? Unaruhusiwa kukosoa kwa kutoa maoni yako lakini zingatia kwamba, you must learn to be wise, respect other peoples' views and stance and most important however, unatakiwa kufanyanya utafiti kabla ya kuzungumzia masuala ambayo ni tete na sensitive kwenye jamii.God bless you Msema Ukweli.
 
.... mbona machozi haya mimi sikuyaona ????? na alikuwa Live runingani?

Kwanza sababu kubwa ya Maalimu kukubali ni kuwa Dr. Shein anatoka Pemba (full stop). Inavunja mwiko ambapo Maalimu aliwahi kuambiwa kuwa kamwe Rais hatatokea Pemba. Ukiangalia kwa undani sana inawezekana pia Dr. Shein machoni ni CCM moyoni ni CUF. Unakumbuka Sheikh Abood Jumbe ? who knew will be the opposition within? Pia Hamadi anamheshimu sana Dr. kwa matamshi yake kuwa yuko tayari kuwa Vice-President kama atashindwa.




'.... wao wana pesa, sisi tuna Mungu ... " (Godbless Lema, MB)
 
Hivi jamani mbona wakati ametangazwa mshindi kuwa ni DK shein , kuna watu walitaka kutoka nje ya Hall, pale pale wakaombwa kurudi ndani mara moja, na hapo ndipo Maalim Seif akaamuliwa atoe speech yake( hivi kwa nini vitendo hivyo vilitokea kwa haraka sana?)
 
Hana lolote yalikuwa machozi ya Furaha kuwa at last kapata umakamu wa Rais, kwani mwanaharakati wa kweli hawezi kuwa sehemu ya utawala wa kibeberu, na hivi sasa yeye ni mmoja wao karudi CCM alipotoka
 
Huo ndio ukweli sio kila kitu kinaweza kuwekwa hapa unapotaka shortly ni waraka ambao ninao ukiutaka nitafute huu nimeutoa usikoweza kufika,halafu kuna diwani mmja aliambiwa laivu hatuweki wa.....................kwenye nafasi za ugombea mtasema kweli au kweli iwahukumu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
sio kichwa cha slaa kina viraka kibao udini,ukabila,ubinafsi na................
ndugu yangu msema ukweli tumia nguvu ya hoja na siyo kuibuka na unsubstantiated allegations na personal vendetta dhidi ya shujaa dr slaa.we unaushaidi wowote kuhusu tuhuma unazozielekeza kwa huyo mzee na mwanamapinduzi wa karne ya 21 kwa tanzania? Unaruhusiwa kukosoa kwa kutoa maoni yako lakini zingatia kwamba, you must learn to be wise, respect other peoples' views and stance and most important however, unatakiwa kufanyanya utafiti kabla ya kuzungumzia masuala ambayo ni tete na sensitive kwenye jamii.god bless you msema ukweli.
 
Nimefurahi sana you are advicing people to be wise hivi hao wanaotukana wanatumia hekima gani? kumwita mtu mzinzi lazima aidha awe ametembea na mtu wa nyumbani kwako,ndugu yako au uone tendo lenyewe linafanyika nani ana ushahidi wa hayo kama sio chuki hasama na husda?
Sio kichwa cha slaa kina viraka kibao UDINI,UKABILA,UBINAFSI NA................
Ndugu yangu msema ukweli tumia nguvu ya hoja na siyo kuibuka na unsubstantiated allegations na personal vendetta dhidi ya shujaa Dr Slaa.We unaushaidi wowote kuhusu tuhuma unazozielekeza kwa huyo mzee na mwanamapinduzi wa karne ya 21 kwa Tanzania? Unaruhusiwa kukosoa kwa kutoa maoni yako lakini zingatia kwamba, you must learn to be wise, respect other peoples' views and stance and most important however, unatakiwa kufanyanya utafiti kabla ya kuzungumzia masuala ambayo ni tete na sensitive kwenye jamii.God bless you Msema Ukweli.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom