SHANGWE : Afisa elimu Iringa awapagawisha wanaCCM, atabiriwa kula shavu kubwa wizarani

nzagambadume

JF-Expert Member
Apr 9, 2018
2,430
5,769
Naam ,baada ya yule mkuu bora kabisa wa mkoa kule mbeya ,kipenzi cha wana ccm bwana chalamila ambaye break ya kwanza baada ya kupewa dhamana ya kumuwakilisha Rais jijini mbeya alisema kipaumbele chake ni kumujondoa sugu kusema ya kwamba WANAOMPINGA MAGUFULI WATAPIGWA SINDANO ZA UKICHAA ,jamaa mwingine toka kanda hiyo ambaye ni afisa elimu naye ametoa kauli ya kishujaa iliyopokelewa vyema na wana ccm mtandaoni huku wengi wakimuomba muheshimiwa Rais ampe cheo wizarani ikibidi hata awe katibu wa wizara ya elimu

Mwanaharakati huyo wa kujitegemea na mzalendo toka iringa alisema....ANAYETOKA NA TAULO CHUMBANI KWA MAMA YAKO NDIYE BABA YAKO,HAIWEZEKANI WALIMU MLIPWE MSHAHARA NA SERIKALI YA CCM HALAFU MSHABIKIE UPINZANI,TUKIKUBAINI TUNAKUTAFUTIA HATA KESI YA UBAKAJI AU UHUJUMU UCHUMI UKAFIE GEREZANI

Ikumbukwe hata Rais Magufuli alishawahi kuwashangaa wakurugenzi wa wilaya na mikoa kwamba inakuwaje kwenye uchaguzi wanatangaza mpinzani kashinda wakati yeye ndiye anawapa mshahara na magari,ikumbukwe pia RPC wa Arusha aliwahakikishia CCM ushindi akwapigia na saluti na kuwasihi wasiwe na wasiwasi,HUO NDIYO UZALENDO TUNAOTAKA.
afisa elimu.jpg

Ni mwendo wa kubatizana kwa moto kama hauchomwi sindano ya ukichaa basi utapewa hata kesi ya uhujumu uchumi
 
Kama afisa elimu anakuwa mpumbavu na mjinga kiasi hicho basi hata elimu yetu huko ni hatari sana

Maana haelewi mashahara wanao lipwa watumishi unatokana na nini

Huenda anadhan mshahara wa watumishi unatoka kwenye kapu la CCM ni ujinga mkubwa kufanywa na ofisa elimu tena msomi.
 
Hv mabeberu wanasubiri nini kuja kututwanga jmn? Niko tayari kutoa shamba langu ili madege yao yatue wakati yanatutwanga mpaka tuchakae
 
Zimesikika nyingi sana mpaka hatuelewi ukweli ni UPI na uongo ni upi, so cha muhimu ni hyo video tu vinginevyo hii itakuwa mbwembwe
video ukiona itasaidia nini,mbona hiyo kauli cha mchumba tu?hukuona RPC arusha kwenye kikao cha ccm anapiga masaluti na kuwahakikishia wasiwe na wasiwasi?
 
Kuna jamaa yangu ni mwalimu tena ni mchapa kazi kweli, wakubwa zake wamemwambia anaweza kupewa ukuu wa shule lakini ni lazima pia achukue kadi ya CCM, hivi ninavyoandika kadi ipo mkononi anasubiri nafasi!
 
Back
Top Bottom