Kweli mkuu.Yaani ni sawa na...
1.30,000×12=360,000 tsh.
2.40,000×12=480,000 tsh.
NB..Hapa haujapewa kwa mkupuo hapa hujakutana na wapangaji wasumbufu.
Ila ndiyo jamaa amekomalia hao wataweza hata kumfanya ndondocha ama wamtoe roho kabisa.
Hakuna anayekudhulumu, huna mali hapo. Usije ishia kuwa marehemu. Waache na roho zao.Lakini kwanini na wao wagombanie si haki yangu lakini sitaki kuzulumiwa
Mali za urithi ni noma sana ztakuja kukutoa roho ww. Tafuta mali zako 2Nasikitika na kuumia katika maisha yangu sijawahi kulala kituo cha polisi wala kufika kituo cha polisi sababu mimi ni mtu mwema lakini cha ajabu nimelazwa kituo cha polisi siku 4 kwa mara ya kwanza bila ya kosa lolote nimetafunwa na mbu ,watemi manyapara wamenionea kwakuwa nililazwa selo la watukutu nimeumia kwakweli.
Shangazi zangu wakishirikiana na polisi wanataka kunimaliza na kunizulumu mali yangu.Shangazi zangu waliwapa rushwa polisi wanilaze ndani bila ya kosa lolote haki ipo wapi wajameni.
Ni Stori mdefu lakini bibi yangu alizaa watoto 4 ambapo wakike watatu na wa kiume mmoja.Mama yangu ni kati ya hao watoto wanne wa bibi yangu halali kwa uzuri bibi yangu amefariki na ameacha nyumba moja yenye vyumba sita.Siku 5 nyuma nilienda kudai urithi wa bibi yangu nikawataka shangazi zangu wanipe chumba kimoja niwe nachukua kodi kwasababu yule ni bibi yangu na mama yangu hayupo duniani hivyo nichukue haki ya mama na yangu kama mjukuu.
Wale shangazi wakaanza maneno na kukataa katakata na mimi nikawa mbishi iweje haki yangu waninyime ugomvi ukawa mkubwa nikatafuta kufuli nikaenda kufunga kwenye moja ya chumba .
Wale ndugu zangu walitishia kuniloga na walisema wazi wataniloga lakini sikutishika nikang'ang'ania haki yangu mali ya bibi yangu nataka chumba nipewe ili niweze kuyaendesha maisha yangu sasa nitaishi vipi ndipo walipoenda polisi na kuja kunikamata na kunilaza kituoni kwa siku nne na ushahidi ninao .Hii ni haki kulazwa kituoni bila kosa ? Sababu ya kusimamia haki yangu ?
Namshukuru mungu nimetoka ila nimeumia sana polisi kutumika kunikandamiza wakati hao shangazi zangu wanadai wataniloga na wananizulumu haki yangu.
Duniani ukiwa mnyonge utateseka sana na ndugu sio watu kabisa asikuambie mtu .kesi saizi ipo kwa mwenyekit lakini shangazi zangu hawataki kuelewa wana roho mbaya
Mama yako au bibi yako alifariki kwanza?Lakini kwanini na wao wagombanie si haki yangu lakini sitaki kuzulumiwa
Mama yako au bibi yako alifariki kwanza?Lakini kwanini na wao wagombanie si haki yangu lakini sitaki kuzulumiwa
Mahabusu kakaa manji na hela zake
sembuse wewe