Gagurito
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 5,600
- 803
Ni mwaka mmoja sasa umepita toka rafiki yangu kipenzi wa tokea primaly, sekondary mpaka chuo alipopata ajira ktk halmashauri fulani (sitaitaja jina) kama Afisa Utumishi. Takribani mwezi wa 6 sasa tangu rafiki yangu huyu anitake ushauri kwani amekua akisisitiziwa na ndugu zake wa pande zote wa upande wa baba na mama yake juu ya kuoa. Anamchumba wa kichaga aliyepo masomoni chuoni dsm mwaka wa 2 sasa akisomea mambo ya habari pale SJMC, Kifupi wanapendana na mimi pia nampenda shemeji yangu huyu kwa mapenzi ya dhati aliyonayo kwa rafiki yangu, siku zote nimekuwa nikiwatakia mema afikie lengo lao la kuishi pamoja(ndoa), majuzi kanipigia simu, kanipa taarifa kua shangazi yake mkubwa amekuja kutoka kijijini na binti ambaye amechaguliwa na ukoo kama mchumba/mke wake, shangazi yake amedai ujio wake ni kutimiza wajibu kama alivyoamuliwa na kikao cha ukoo pia akasema huko kijijini taratibu nyingine za ndoa zinaendelea. Jamaa kachanganyikiwa, ananiomba ushauri juu ya hili jambo, mimi nimeshindwa kumpa jibu coz sijui niegemee upande gani, shemeji yangu wa chuo namkubali, jamaa yangu sipendi agombane na ndugu zake pia.. Nimemwambia anipe muda then nitamjuza nin chakufanya.. Hapa alipo anasubiri ushauri wangu kwani tunaaminiana, tumeshirikiana, kusaidiana na kushauriana ktk mengi. Hapa nilipo nipo dillema ktk kutoa huo ushauri, jamani tusaidiane ktk hili, nini kifanyike hapo? Nimshaurije? Nawategemea sana ktk hili. Asanteni...