Shamsa kukabili ufisadi Maliasili bila huruma

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Theopista Nsanzugwanko
Daily News; Friday,February 22, 2008 @06:04


WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga, amewasili katika ofisi yake mpya na kuahidi kutokomeza ufisadi bila kumuonea huruma mfanyakazi ye yote wa wizara hiyo atakayejaribu kuweka doa katika wizara hiyo.

Pia waziri huyo aliwataka wafanyakazi hao kufanya kazi kwa uadilifu na ushirikikiano ili kuhakikisha wanarudisha imani kwa wananchi, na akasema hatamvumilia mtu ye yote mkorofi ambaye atasababisha aibu katika wizara hiyo.

Akizungumza na wafanyakazi wa wizara hiyo katika chuo cha Utalii Dar es Salaam leo, Mwangunga aliwataka wafanyakazi kukabiliana na changamoto za kuhifadhi na kuzifanyia biashara raslimali za taifa ili kukuza uchumi na si kwa nia ya kujinufaisha wao binafsi.

“Nilipoteuliwa kuwa waziri wa wizara hii kuna watu walionipa pole kutokana na unyeti wake huku wakidai kuwa imejaa mafisadi, lakini napenda kuwahakikishia kuwa yote yaliyopita tuyaache na kuanza upya kwa kufanya kazi kwa uadilifu na ushirikiano kwani sitamvumilia mtu yeyote atakayejaribu kuleta ukorofi kwa nia ya kuitia doa wizara,” alisema.

Aliwataka wafanyakazi kufanya kazi zao kwa kuzingatia misingi minne ikiwamo kujitoa mhanga katika kazi, kuipenda kazi na kuwa wabunifu ili kukabiliana na utandawazi, kuwa na bidii ya kazi na uadilifu kutokana unyeti uliopo katika wizara hiyo.

Aliwataka wafanyakazi wa idara ya misitu kubadilika kutokana na malalamiko mengi wanayopata kutoka kwa wananchi kwa kukataa hongo kutoka kwa wafanyabiashara ambazo zinawaondolea heshima pale wanapogundulika kudhulumu raslimali za taifa.

Waziri Mangunga aliwataka wafanyakazi kushirikiana katika idara zote ili kuweza kufanya kzi kwa ufanisi na kukusanya mapato zaidi kitendo kitakachowafanya kuwa kifua mbele kwa Rais hivyo kuongezewa fungu katika bajeti yao.

Awali, Naibu Waziri wa wizara hiyo, Ezekiel Maige, aliwaomba wafanyakazi hao kumpa ushirikiano wa kutosha ili kuweza kukabiliana na changamoto zilizopo za kupambana na ufisadi na kurejesha imani kwa wananachi kwa kuhakikisha rasilimali za taifa zinatumika ipasavyo.
 
Ukweli ni kwamba hawezi kufanya chochote.
Ni mbweko wa mbwa asiye na meno.
Waziri anaweza kumfukuza Mkurugenzi?
Au anaongea juu ya kuwafukuza watunza nyaraka na matarishi?

Rais kikwete mwenyewe tangu aingie kazini amefukuza mtu mmoja tu, yule afande aliyeacha lindo na kwenda kuupaka watu wakashangilia huku wakisema rais hana mchezo.

Kweli rais hana mchezo.?

Hapo Maliasili kuna vigogo ambao wako kwenye timu ya MH Lowassa na nyuma yao MH Kikwete.
Waziri hana ubavu wa kumminya mbavu mtu yeyote, zaidi atanyiminya mbavu mwenyewe.
Hiyo wizara ni ya akina Lowassa mpaka wenyewe tutakapoichukua nchi na kuirudisha mikononi mwa wananchi.
 
Haya anayasema kwa kutaka aandikwe ama ana maana ya kufanya kweli ? Ajue sasa kuna Tanzana mpya we will hold her responsible mwisho wa siku kwa maneno haya haya atayakana kama Sitta ambavyo huwa anayaruka maneno yake .
 
Ukweli ni kwamba hawezi kufanya chochote.
Ni mbweko wa mbwa asiye na meno.
Waziri anaweza kumfukuza Mkurugenzi?
Au anaongea juu ya kuwafukuza watunza nyaraka na matarishi?

Rais kikwete mwenyewe tangu aingie kazini amefukuza mtu mmoja tu, yule afande aliyeacha lindo na kwenda kuupaka watu wakashangilia huku wakisema rais hana mchezo.

Kweli rais hana mchezo.?

Hapo Maliasili kuna vigogo ambao wako kwenye timu ya MH Lowassa na nyuma yao MH Kikwete.
Waziri hana ubavu wa kumminya mbavu mtu yeyote, zaidi atanyiminya mbavu mwenyewe.
Hiyo wizara ni ya akina Lowassa mpaka wenyewe tutakapoichukua nchi na kuirudisha mikononi mwa wananchi.

Mkuu Madela heshima kwako mkuu
ninakuunga mkono kwa kutuelewesha maana halisi ya maneno ya huyo waziri mpya wa majiasili.
Na ni kawaida yao kuingia wizarani kwa mkwara sana halafu wanaishia kujibu uongo bungeni kuwa serikali itafuatilia hiki au serikali ina mpango huu ambavyo tangu adam na eva hakuna kinachofanyika zaidi ya kujipanga kisiasa ili agombee uchaguzi ujao.
 
Hizi ahadi zitaisha lini? Lini wataanza kutoa hesabu za mafanikio yao?

Raha ya Serikalini,,, sio lazima kuwe na deliverables... no performance appraisal... mambo yako yako tu...

Idadi ya ahadi, idadi ya seminar na Washa ndio Key Performance Indicators (KPI)
 
Back
Top Bottom