Shamim Mwasha, mumewe mbaroni Dar kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya


Mamlaka ya Kupambana na Kuzuia Dawa za Kulevya Tanzania (DCEA) imemkamata mfanyabiashara, Abdul Nsembo maarufu Abdukandida na mkewe, Shamim Mwasha kwa tuhuma ya kukutwa na dawa za kulevya aina ya heroin.

Wanandoa hao wanadaiwa kukutwa na dawa hizo zenye uzito wa zaidi ya gramu 400 nyumbani kwao Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam.

Kamishna wa operesheni wa DCEA, Luteni Kanali Fredrick Milanzi amelieleza Mwananchi kuwa, watuhumiwa hao walikamatwa Mei Mosi mwaka huu.

Amesema kukamatwa kwa Nsebo na mkewe kumekuja baada ya kukamatwa kwa mtandao mkubwa wa dawa hizo hivi karibuni.

Amesema maofisa wa DCEA baada ya kupata taarifa walienda nyumbani kwa watuhumiwa hao na kufanya upekuzi na kubaini mfuko ukiwa na dawa hizo za kulevya na nyingine zilikutwa katika siti ya nyuma ya gari.

"Tulifanya upekuzi kuanzia saa 8:00 usiku hadi saa 1:00 asubuhi na tulizibaini dawa hizo zikiwa zimefichwa na matokeo ya awali kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali yameonyesha ni dawa za kulevya aina ya heroin.”

“Vitu vingine tulivyomkuta navyo ni simu tano, kadi za benki, hati ya kusafiria pamoja na nyaraka mbalimbali ambavyo vyote tumevichukua,” amesema Luteni Kanali Milanzi

Amesema watuhumiwa hao wana mtandao mkubwa wa kimataifa na kwamba wana majina ya watu wanaoshirikiana nao kutoka nchi mbalimbali ikiwamo Brazil.

Amesema wawili hao bado wanashikiliwa na upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani.
Ilikuwa wakati wa Rais hatari wa wala ngada. Magu alimanisha. Mungu ampumzishe kwa Amani.
 
Ilikuwa wakati wa Rais hatari wa wala ngada. Magu alimanisha. Mungu ampumzishe kwa Amani.

sijaelewa kidogo.

Nakumbuka hata awamu ya nne ya JK wa Msoga iliwakamata matycoon kama Shibuka na Abdallah Chonji wa pale Migomigo.

Kwenye tasnia ya madawa TZ Shikuba na Chonji unaongelea watu hatari kabisa kwenye network pana kabisa.
Nakumbuka kipindi hicho wauza unga walimuogopa sana mtu aliteitwa Kamanda Nzowa na aliwatight sana akiwemo Mama Reila Mkenya na washirika wa Tanzania.

Hiko hiko kipindi cha Magu wapo watu walikuwa bado wanatamba uraiani na hawakugushwa na bado waliendelea kushusha maboom in connect na Bosi wa Dar es salaam.
 
Doing Life.

Double Standard.

Mtoto wa Liyumba alivunja rekodi ya kukamatwa na magunia ya sembe ila kashatoka ila Shamim amekamatwa na nusu kilo wamempa maisha.


Mtoto wa Lyiuma alikuwa punda tu wa Shikuba na inawezekana hata alichomeshwa tu maana hizo dili kupigwa bwege mtozeni kawaida sana ili ufanikishe mambo ya watu.
 
Mtoto wa Lyiuma alikuwa punda tu wa Shikuba na inawezekana hata alichomeshwa tu maana hizo dili kupigwa bwege mtozeni kawaida sana ili ufanikishe mambo ya watu.

Sasa mbona skuba mwenyewe alifungwa miaka 7 tu? Unajua aliyekamatwa na ngozi ndiye aliyeiba ng'ombe? Mtoto wa Liyumba na Skuba washatoka jela inagwa walikamata na mizigo ya hatari 209Kg,why mwenye 0.5Kg afungwe maisha?
 
Sasa mbona skuba mwenyewe alifungwa miaka 7 tu? Unajua aliyekamatwa na ngozi ndiye aliyeiba ng'ombe? Mtoto wa Liyumba na Skuba washatoka jela inagwa walikamata na mizigo ya hatari 209Kg,why mwenye 0.5Kg afungwe maisha?

Shikuba yuko jela USA, alikuwa na kimeo kingine huko sina uhakika kama katoka au la, ila kijana wake Tikotiko alitumikia akatoka.

Issue ya Abdul na huyu dada ni tofauti kidogo na Shikuba, Abdul aliingia kwenye mikono ya serikali wakati ambao serikali iliamua kudeal na wauza unga ili kuitokomeza biashara, lengo ilikuwa kumtarget na kumtia nyavuni haijalishi ana mzigo au hana maana habari zake tayari Serikali ilikuwa nazo kama ilivyokuwa kwa Chonji wa Magomeni naye, alitaitiwa baada ya awamu ya nne kumchoka na matukio yake, mamlaka ziamua kumlalia kinomanoma haijalishi ana mzigo au hana ni order ilitoka na ndio mpaka leo Chonji yuko mahabusu hajahukumiwa bado nafikiri.
 
Sasa mbona skuba mwenyewe alifungwa miaka 7 tu? Unajua aliyekamatwa na ngozi ndiye aliyeiba ng'ombe? Mtoto wa Liyumba na Skuba washatoka jela inagwa walikamata na mizigo ya hatari 209Kg,why mwenye 0.5Kg afungwe maisha?

kuna wakati mamlaka zinajua kila mtu na njia zake issue inayosubiliwa inakuwa ni order tu kutoka utaitiwe, Abdul mamlaka zilimuhitaji haijalishi kuna ushahidi au hamna, mdada naye akajikuta yuko kwenye 18 na mme wake ikawa haina jinsi lazima wote waishe.
 
Shikuba yuko jela USA, alikuwa na kimeo kingine huko sina uhakika kama katoka au la, ila kijana wake Tikotiko alitumikia akatoka.

Issue ya Abdul na huyu dada ni tofauti kidogo na Shikuba, Abdul aliingia kwenye mikono ya serikali wakati ambao serikali iliamua kudeal na wauza unga ili kuitokomeza biashara, lengo ilikuwa kumtarget na kumtia nyavuni haijalishi ana mzigo au hana maana habari zake tayari Serikali ilikuwa nazo kama ilivyokuwa kwa Chonji wa Magomeni naye, alitaitiwa baada ya awamu ya nne kumchoka na matukio yake, mamlaka ziamua kumlalia kinomanoma haijalishi ana mzigo au hana ni order ilitoka na ndio mpaka leo Chonji yuko mahabusu hajahukumiwa bado nafikiri.

Hata kama lazima kuwe na ushahidi na sheria zifuatwe ,mbona wengi tu wanafanya uhalifu sema tu wanajificha bila kuwajua hivyo wanapeta tu ,Kufungwa kwa hao watu kuna pia beef kati yao na wakuu(wa enzi hizo)!
 
Doing Life.

Double Standard.

Mtoto wa Liyumba alivunja rekodi ya kukamatwa na magunia ya sembe ila kashatoka ila Shamim amekamatwa na nusu kilo wamempa maisha.

Ila bado bwana wake othman yuko ndani
Mtoto wa lyumba ile kesi ilikuwa lazima achomoke,maana hakuhusika moja kwa moja

Ova
 
Back
Top Bottom