Shambulio la Lissu: Wajue wasiojulikana watakaojulikana na 'Wasiojulikana' ambao kamwe, hawatajulikana

Iko kazi! Karne ya 21 bado umefumbwa macho na kuzibwa masikio! Kama albadiri ina uwezo wa kimungu si angejufungia chumbani akasoma na mola wetu akamjibu! Nani kasema swala ni mkutano wa hadharani? JF!!!
Nilikuwa nasikia wasukuma wana ukabila kumbe kweli. Wewe siyo great thinker..wewe n mpuuzi tu. Na sitosoma tena makala zako za kipuuzi.
Swali km hawakuhusika kwanini wamemkamata shehe anayataka kusoma all badri
 
Uchunguzi huru wa nchi huru ndani ya nchi nyingine huru?? Sikubaliani na unyama aliofanyiwa lisu lakini sikubaliani zaidi na mawazo mafupi kama haya! Tanzania ni nchi na dola iweje uite Scotland Yard? Ili amchunguze nani na kwa njia ipi? Nisaidieni wajuzi wa jf! Kwamba muingereza njoo uchunguzi serikali yetu tuna Masha ka nayo! That is ignorance of the highest level! Mbona kuna minong'ono ya nani alimuua princess Diana, mbona hatujasikia kelele za tume huru?

Hapo ndipo ukweli ulipolalia Chadema wako tayari kwa uchunguzi huru chini ya FBI au Scotland Yard. Wahusika wa shambulizi hawataki uchunguzi huru ili dhambi zao zisiwekwe hadharani. Zaidi ya wiki polisi hawajasema ni nani mmiliki wa gari ambalo lilikuwa linamfuatilia Lissu na yeye kuweka plate number za gari hiyo hadharani. Hadi hii leo polisi imeamua kuwa kimya kuhusu walinzi wa geti kwenye makazi ya waheshimiwa. Hawataki kusema kama wamehojiwa au la lakini wanalalama kuhusu dreva wa Lissu! Bashite ni mtekaji, mtesaji na muuaji.
 
Naomba kuuliza wakuu. Hivi hii sentensi au msemo wa watu wasiojulikana nyie wenzangu mwauchukulia vp? Najisikia vibaya sana kumsikia msemaji wa mamlaka nyeti akisema watu wasiojulikana bla bla bla.... Huku ni kujishushia heshima. Weledi qenu uko wapi? Intelijensia inafanya kazi kwa msimu? Mbona nyakati fulani ht siki 3 kabla ya tukio mnatuaminisha mko vizuri mmegundua vituvibaya au mipango mibaya? Iweje kwenye issue hot mnakauka km sio nyie na kutuambia wasiojulijana? Mnafanya nn basi msiwajue? Nakerekwa sana na hii misamiati. Tafadhali rejesheni heshima ya kazi. Nachukia mno kusikia eti watu wasiojulikana. This is ridiculous n shame to those responsible.
 
toa unafki hapa, usitake kuunganisha tukio la Hon TL na uchaguzi wa ndani wa CDM, hakuna asojua kwenye awamu hii mtu ambaye anaonekana kwenda kinyume na maneno/matakwa/sera/maoni na mkulu unaonekana msaliti, mchochezi na mwiba mchungu kwa SIRIkali pendwa na unashughulkiwa mara moja (ushahidi na mifano ipo ya kutosha).....
alafu wewe ni mtu mzima sana kiumri sina uhakika na kiakili pia next time jipange, au kwa vile ni verified user utadhani wakubwa wakipita hapa pengine neema ikakuangukia ?
 
P
Kimsingi upo sahihi, ila lipo jambo la kweli kitendo kilichofanywa na hao watu kujaribu kusitisha maisha ya mtanzania mwenzetu, ni ukiukwaji mkubwa wa haki na kila mtu mwenye akili TRIM AMU hawezi kuunga mkono jambo hlo.

Jambo pekee ambalo siwezi kukubaliana na watu(hasa wanaosema kuwa serikali au wale jamaa kuhusiaka)
Hilo jambo kwangu halina mashiko,

Kwanza mheshimiwa lisu hana madhara yoyote kwa serikali, iwe ya maneno au ya vitendo,

Pili hakuna mahali popote pale kulikuwa na viashiria vya vya uhatarishi ambavyo pengine tungesema Ls Anaweza kuvileta

Hvyo waliofanya hayo, ni wahuni tu ambao walitaka kuipaka matope serikali au kunenea mabaya...

Watu wanaojua na wenye akili timama hawawezi kuihusisha serikal kwenye hili...
Niko tayari kukosolewa...

Bonny...
 
Mke wa mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, amesema angependa kuwajua watu waliomshambulia mumewe, aliyewaamuru wafanye shambulio hilo na sababu za kufanya uovu huo.

Na sasa mke huyo wa Lissu na ambaye pia ni wakili, Alicia Magabe anataka kuwajua waliomfyatulia mumewe zaidi ya risasi 30, aliyewatuma na sababu za kuwatuma
Mke wa Lissu anataka kuwajua wasiojulikana, hivyo hii search ya kuwaulizia na kutaka kuwajua au kuwabaini hawa watu wanaoitwa kwa jina maarufu la watu "wasiojulikana", inaendelea, wanazidi kutafutwa na kuuliziwa, hivyo hapa nafanya kukumbushia tuu kuwa kwenye hawa watu wasiojulikana, kuna makundi mawili. Kuna wasiojulikana na 'wasiojulikana'. Wasiojulikana ni wale ambao wakitafutwa kwa bidii kwa kutumia mbinu za kisasa za utafutaji zikihusisha mambo ya ki inteligensia, mwisho wa siku watakuja kujulikana na kufikishwa kunakohusika, lakini kwa hawa 'wasiojulikana', hawa ni wale ambao kamwe hawatakuja kujulikana!.

Paskali
 
Mke wa Lissu anataka kuwajua wasiojulikana, hivyo hii search ya kuwaulizia wasiojulikana, inaendelea, wanazidi kuuliziwa, hivyo nakumbushia tuu huwa wasiojulikana ambao watakuja kujulikana na wasiojulikana ambao kamwe hawatakuja kujulikana!.

Paskali

pascal
Hapa mke wa lisu asilete drama ,,, Mr wake kasema anawajua maana yeye na dreva wake waliwaona wanavyosema kila siku wao wenyewe kwa vinywa vyao kuwa wanawafahamu.

Kwa nini sasa, asimuulizie lisu huko room/ hospital amwambie ili aje atuambie badala ya kutupotezea muda kuleta tena maswali kwa jamii ili hali majibu yapo kwa mume wake!?
 
Wanabodi,
Tangu kutokea kwa shambulizi kwa Tundu Lissu, ambalo mpaka sasa linaelezewa kufanywa na watu wasiojulikana, kumeibuka shauku kubwa ya kuwabaini hawa watu wanaoitwa kuwa ni watu wasiojulikana huku zikijengwa dhana mbalimbali kuhusiana na wasiojulikana hawa, hadi kufikia kuwanyooshea vidole baadhi ya watu, wakiwemo wale "jamaa" zetu.

Kufuatia taarifa nyingi za watu wasiojulikana kuhusika kwenye baadhi ya matukio na Jeshi letu la polisi ndio mamlaka rasmi ya kufanya uchunguzi na mara zote hutoa taarifa kuhusu kuhusika kwa wasiojulikana ambao mwisho wa siku hubakia hivyo hivyo kuwa wahusika wa tukio fulani ni watu wasiojulikana, kumbe sometimes sii kweli kuwa wahusika ni watu wasiojulikana, sometimes wahusika wa matukio hayo sio watu wasiojulikana bali ni watu 'wasiojulikana'.

Hivyo hili ni bandiko la kuwahusu watu wasiojulikana ambao mwisho wa siku baada ya uchunguzi wa kipolisi, watajulikana, lakini pia kuna mashambulio yanayofanywa na watu 'wasiojulikana', ambao kamwe hawatajulikana!.
Haswa pale ambapo 'wasiojulikana' ni wale "Jamaa Zetu"!.

Hebu fuatilia jinsi hawa ,"Jamaa zetu" 'wasiojulikana', wanavyotekeleza mashambulizi mbalimbali na sometimes hadi na mauaji in a very clean job and professional way hivyo kamwe hawawezi kuja kujulikana, hivyo kubaki ni watu 'wasiojulikana', daima.

1. Kuna kiongozi mmoja mkubwa serikalini anayesemekana alikufa kwa ajali ya gari, ila mwili wake ulikutwa na majeraha ya kitu fulani, inasemekana ni wale "jamaazetu"
Kifo cha Sokoine: Tujiondoe jela ya kifikra | JamiiForums | The ...

2. Aliyekuwa Waziri wa Fedha wa Mwinyi, Kighoma Malima alipo defect kutoka CCM na kujiunga na NRA, aliugua ghafla na kupoteza maisha. Inasemekana ni wale "jamaa zeta".
Ukweli wa kifo cha Kighoma Ally Malima ni upi? | JamiiForums | The ...

3. Horace Kolimba akiwa CCM high ranking oficer, aliposema CCM imepoteza Dira na Haina Mwelekeo, alipoteza maisha kwa kuugua ghafla. Ikasemekana niwale "jamaa zetu"
Kabla ya kutoka ccm jiulize mara mbili;horace kolimba,gen kombe ...
Wananchi wakitaka kujua nani alimuua nani? | JamiiForums | The ...
Vifo vya viongozi vyenye utata | JamiiForums | The Home of Great ...


4. Kiongozi mwingine mkubwa wa serikali alifariki ghafla baada ya tuu ya kukamilisha ziara ya kutembelea maonyesho ya Saba Saba, mmoja wa hao "jamaa" akajiunga jf na kutueleza kila kitu kuhusu madudu yao humu na kutueleza humu hiyo ni kazi, ya wale "jamaa zetu".
Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa ...
5. Tukio la kutekwa kwa Dr. Ulimboka, Absolom Kibanda, Roma Mkatoliki, Mwandishi wa habari wa DW, Salma Said, na kupotea kwa mwana jf maarufu Ben Saanane, pia kukihusishwa na wale "Jamaa zetu" 'wasiojulikana'.

6. Tukio la Uvamizi wa Kituo cha TV cha Clouds TV kilichofanywa na wale makirikiri wenye silaha wanasemekana ni wale ""jamaa zetu" na walitumia Nissan Patrol Nyeupe!.

7. Yule mpuuzi aliyemnyooshea Nape bastola, anajulikana kwa sura katika media zote, na alikuja kwa kutumia gari aina ya Nissan Patrol Nyeupe, naye licha ya picha yake na sura yake kuenea kote kuanzia kwenye mainstream media hadi kwenye social media, lakini na yeye a anaelezewa kuwa ni mtu 'asiyejulikana'!. Taarifa za chini chini zinaeleza huyu jamaa ni miongoni mwa wale jamaa "jamaa zetu".

8. Huyu Blogger wa Kenya amesema haya kwenye mitandao ya kijamii, hadi akataja majina ya wahusika na magari yaliyohusika ikiwemo hiyo Nissan Patrol Nyeupe na sijasikia yoyote akikanusha taarifa ya blogger huyu!, hata serikali yetu kukanusha. Hivyo sometimes silence ni admission of guilt, kwa vile ni 'wasiojulikana", hawana sababu ya kujibu lolote wasije wakajulikana!.
Hii inapelekea mimi kujiuliza maswali haya.
  1. Kama wahusika wa Tukio la shambulio la Tundu Lissu, ni wale "jamaa zetu", kwa vile wale ni ma pro, and they have never missed a target, kama ni kweli ni wao, how could they missed a target?. Hawa watakuwa sio wale!, na kama ni wale, saa hizi tungekuwa tunazungumza mengine!. Unless wamejifanya to miss the target makusudically ili kupiga maboya kwa kupoteza lengo ionekane ni amateurs.
  2. Kama they have 100 ways to do elimination in a good clean way, on natural death look like, accidents, or any clean job that nobody would've suspected anything, why did they do such a dirty job?!.
  3. Was Tundu Lissu such a threat to status quo ya yule boss wao?, kama kuna defectors very high rankings wame cross na wamejizolea kura nyingi kuliko zilizomuingiza Kikwete madarakani ile 2010, hawa ndio the real threat!, kwa nini hawa wasiwe targeted?. Why Lissu?.
  4. What if ni kutokana na issue nyingine yoyote na sio siasa?.
  5. Kama kuna chama viongozi wake waliwahi kutuhumiwa kupanga vitendo vya ugaidi na utekaji na video zikaletwa humu, hawawezi kuwa ndio wao waliopanga mpango huo?, kwa kufanya timing ya Dodoma ili wadhaniwe ni "wale jamaa?".
  6. Kama Wangwe alipotaka kugombea uenyekiti alikufa kwa ajali yenye utata mpaka kesho, na huu ni mwaka wa uchaguzi wa ndani, haiwezekani ikawa ni inside job ya friendly fires?.
  7. Kama Zitto alipotaka kugombea alifanyiwa life atempt kwa sumu, lakini kwa vile ameaga kwao, akasalimika, haiwezekani na Lissu pia kwao ameaga na ndio maana amesalimika?.
  8. Kama Mlinzi wa Dr. Slaa, alihudumiwa hivi,watu wanaoweza kushughulikia hivi binadamu wenzao, they are capable of doing anything, then haiwezekani hii sasa ndio the advanced methods za kudeal na the internal threats zao?.
Conclusion Kuwahusu hawa Watu Wasiojulikana na 'wasiojulikana', acording to the motive behind the shooting.
1. Kama the motive behind the shooting ya Lissu ni kwa sababu he is jvery vocal hivyo kuonekana ni mwiba, then hawa wanaoitwa ni wasiojulikana, kiukweli sio wasiojulikana, hawa watakuwa ni 'wasiojulikana' ambao ni wale "jamaa zetu", kama ni wale "jamaa zetu", then hawa sio watu wasiojulikana, hawa ni watu 'wasiojulikana', kama yule mpuuzi aliyemshikia Nape bastola ni mtu 'asiyejulikana' na mpaka leo hajulikani na kamwe hatajulikana, and if this being the case, then watu hawa hawatajulikana kabisa, hata yule aliyetajwa na blogger wa Kenya, pia ni mtu 'asiyejulikana'. Ila hukumu ya karma itawahusu wahusika wote.

2. Kama the motive behind the shooting ya wasiojulikana hawa ni partly politics ya siasa za ndani na run of kuelekea 2020, then polisi wetu waendelee na uchunguzi, soon watasalitiana na tutawabaini na watu wa tabaki midomo wazi kwa kutoamini.

3. Lakini kama the motive behind wasiojulikana hawa ni hawa wezi wa rasilimali zetu na lengo lao ni kutufarakanisha sisi na serikali yetu kwa kutuhamisha kwenye hoja ya rasilimali zetu, ili tusahau makinikia, Tanzanite, Dhahabu, Almasi na Gesi, then, hawa, sisi as sisi, hatuna uwezo wa kuwabaini bila msaada wa Scotland Yard, ila, kwa vile tayari, tumeisha wastukia nia yao ovu, hatuta farakana, tutasimama firm as one, and under th e united front. Kama lengo ni ili tufarakane, tuichukie serikali yetu kuwa ni ya kidikiteta, na kuanza kufanya vurugu, tukifarakana, tutakuwa tumewapa walichokitaka, tusikubali kufarakana, kwa kufakaranishwa na wafakaranishaji hawa, lets stand together as one, tupendane, tuheshimiane, tuvumiliane, tustahimiliane, tubishane bila kupigana, tukubaliane kwenye maslahi ya taifa na ikishindikana tukashindwa kukubaliana, then tukubaliane kutokubaliana lakini mwisho wa siku, wasiojulikana wajulikane lakini 'wasiojulikana', sijui.

We Wish TL To Get Well Soon.

Paskali
Ulianza vizuri ila umeharibu mwishoni nyie watu mnao taka kuingia makumbusho mna shida sana ...
Ngoja nimalize mfungo nitakuja nikujibu
 
Kwa utamaduni wetu mwenzetu akipatwa na tatizo huwa tunautaratibu wa kuonyesha kuguswa kwetu na tukio husika.Lakini pale itakapoonekana jamaa hafati ule utaratibu wa kuonyesha kuwa ameguswa na tukio,basi huwa tunamwita kuwa ni mchawi wa tukio.But to every action there is an equal and opposite reaction.
 
Rudi sh
pascal
Hapa mke wa lisu asilete drama ,,, Mr wake kasema anawajua maana yeye na dreva wake waliwaona wanavyosema kila siku wao wenyewe kwa vinywa vyao kuwa wanawafahamu.

Kwa nini sasa, asimuulizie lisu huko room/ hospital amwambie ili aje atuambie badala ya kutupotezea muda kuleta tena maswali kwa jamii ili hali majibu yapo kwa mume wake!?
Rudi shule ukasome fasihi.
 
Mke wa Lissu anataka kuwajua wasiojulikana, hivyo hii search ya kuwaulizia wasiojulikana, inaendelea, wanazidi kuuliziwa, hivyo nakumbushia tuu huwa wasiojulikana ambao watakuja kujulikana na wasiojulikana ambao kamwe hawatakuja kujulikana!.

Paskali
Ishakuwa zilipendwa, nayy ana maswali ya kujibu maana michango mil 400+ katafuna na m/kiti Mbowe.
 
Watu wasiojulikana hawapo,isipokuwa anayewatafuta anakuwa na mfumo usiojulikana.Kila mtu anajulikana endapo anayemtafuta ana IQ kubwa na hana chembe ya upumbavu,pia awe amesoma kwa kiwango cha juu kuhusu kitu kiitwacho telepathy.Ni watu wachache sana ambao wamefuzu namna ya kutumia telepathy, maana telepathy ni kama jicho la tatu lililopo katika ubongo.
 
Mke wa Lissu anataka kuwajua wasiojulikana, hivyo hii search ya kuwaulizia wasiojulikana, inaendelea, wanazidi kuuliziwa, hivyo nakumbushia tuu huwa wasiojulikana ambao watakuja kujulikana na wasiojulikana ambao kamwe hawatakuja kujulikana!.

Paskali
Wasiojulikana watajulikana na watu wenye IQ kubwa na waliobobea katika kutumia telepathy.
 
pascal
Hapa mke wa lisu asilete drama ,,, Mr wake kasema anawajua maana yeye na dreva wake waliwaona wanavyosema kila siku wao wenyewe kwa vinywa vyao kuwa wanawafahamu.

Kwa nini sasa, asimuulizie lisu huko room/ hospital amwambie ili aje atuambie badala ya kutupotezea muda kuleta tena maswali kwa jamii ili hali majibu yapo kwa mume wake!?
Si kila unachokisoma unatakiwa kukitafsiri kama unavokisoma, ndo maana hata madarasani wanafundisha aina na dhana za aina kadhaa za ufahamu.
Wewe umekurupuka, hicho ulichokisoma kina dhana ya lugha ya picha ambayo kwa tukio husika ni lugha ya kisheria zaidi.
Si kila penye pazia ni mgahawa pengine panakuwa ni choo
 
Tuseme ukweli hivi Lissu wakati anamdhihaki mpakwa mafuta wa bwana askofu kilaini kuwa kahongwa na Rugemalira alitegemea kusomewa misa gani?

Halafu badala ya kutubu munataka kumsomea albadir? Tangu lini misa za majini zitawapata wakatoliki waliojitoa nadhiri kwa bwana?

Yeye aende bukoba akatubu hamna njia nyingine ya kusalimika.
 
Back
Top Bottom