Shaka Zulu alichinja zaidi ya watu 7000 ndani ya mwaka mmoja tu

Robot la Matope, Shaka Zulu nijuavyo mama yake alitengwa hapo kijijini na kwenda ufalme wa jirani siyo kwa sababu Mfalme Senzangakhona alimuoa Nandi ( mama yake Shaka) kuwa kabila tofauti na Wazulu, bali kwa sababu Mfame alimpa ujauzito Nandi kwenye sherehe za mavuno zilizokuwa zinafanyika usiku.

Na kwa mila za Wazulu za wakati huo, mwanamke akibeba mimba kabla ya kuolewa anauawa, kabla ya kuuawa kwanza amtaje aliyempa hiyo mimba naye auawe! Sasa aliyevunja sheria hiyo ni mfalme Senzangankhona mwenywe!

Ili kuepusha aibu hiyo, mfalme aliongea na mfalme mwenzake wa jirani Nandi akatoroka kijijini akamzalia huko Shaka. Lingine, Shaka mwisho wake haukuwa mzuri kutokana na mama yake kumfundisha ushirikina toka akiwa mdogo, ambapo alichanjwa madawa ya ushujaa vitani, madawa ambayo muda wote yalihitaji kuua, yalihitaji damu. Kutokana na hilo, Shaka aliongoza mapambano mengi ya kivita, na furaha yake ilitimia pale anapoua. Falme jirani zote zilikimbia zisikiapo jeshi la Shaka Zulu, Shaka akakosa maadui wa kupigana nao.

Kwa kuwa dawa zake zilikuwa na masharti ya kuua kila wakati, Shaka akaanza kuumwa, kuumwa kwa kukosa wa kuua! Ikafikia sasa Shaka akaanza kuua watu wake, na anapoua kwa mkono wake watu wanne au watano, afya ya mwili wake inarejea bukheri wa afya! Moja ya mbinu aliyoitumia kuua kwa urahisi anapohisi kuumwa kwa kuteswa na madawa ni kuitisha sherehe ya vyakula na pombe ambapo wanakijiji hulewa na kuimba nyimbo, ndipo Shaka huinuka na kuagiza aletewe watu wanaoimba vibaya na hutumia mwanya huo kuwaua, na anapoua afya yake inarejea!

Mwisho Shaka aliuawa na ndugu zake wawili wa mama wengine lakini baba mmoja waliomtembelea na akawaamini kuongea nao kwenye ikulu yake huku walinzi wakiamini mfalme yuko na ndugu zake!
 
JamiiForums ni jamvi ambapo tunajifunza mengi kutokana na hadithi au historia.

Uzi huu una mafunzo mengi ambayo hatupaswi kuyapuuza maana historia huwa na kawaida ya kujirudia.

Ndiyo maana jamii zilizotunza na kuenzi mafundisho kupitia hadithi au historia huweza kujiepusha na mambo mengi mabaya kupitia kumbukizi kama hii ya Shaka Zulu.
 
Huyu jamaa alikuwa na uwezo mkubwa sana wa kurusha mkuki wake na kwenda masafa marefu
Na ndo mana ingawa alikuwa ni mtoto wa njee wa kimada wa chief ambaye ni baba ake alipewa uongoz huo sabb alikuwa na kipaji na nguvu nyingi mnoo
 
Jina lake Anaitwa 'Shaka kaSenzangakhona' Maarufu kwa Jina la 'Shaka Zulu', Alizaliwa Mwaka 1787 Huko Kwazulu-Natal A.Kusini na Kufariki Mwaka 1828 Akiwa na Miaka 41, Alikua Mfalme wa Himaya ya Wazulu Huko Afrika Kusini Kuanzia Mwaka 1816 –1828 Akichukua Ufalme Kutoka kwa Babayake 'Senzangakhona kaJama' Aliyefariki.

Shaka Zulu Alikua Anampenda Sana Sana Mamayake Mzazi 'Nandi kaBhebhe' Kiasi Kwamba Mamayake Huyo Alipofariki October 10, 1827, Shaka Akaanza Kufanya Mauwaji!. .
.
Inaelezwa Kuwa Kila Asubuhi Alipokua Anaamka Alikua Anawachinja Wanawake Waliojifungua Siku za Karibuni Pamoja na Waume Zao, Anawachinja Wanawake Waliokua na Ujauzito, Anawachinja Watu Waliokua Hawaonyeshi Huzuni Juu ya Kifo cha Mama Yake, Hata Ngombe Aliyeonekana Mjamzito au Alitejifungua Hivi Karibuni Alikua Anachinjwa!. .
.
Lengo Kubwa la Kufanya hivyo Lilikua ni Kutaka Pia Watu Wapate Maumivu/Uchungu Aliokuwa Anaupata yeye Kwa Kumpoteza Mama Yake Mzazi.

Zaidi ya Watu 7,000 Waliuwawa kwa Kuchinjwa na Shaka Zulu Ndani ya Mwaka Mmoja tuu, Lakini Licha ya Kuuwa Kiasi hicho, Shaka pia Alipiga Marufuku Mtu Yeyote wa Wazulu Kupanda Zao Lolote Shambani kwa Mwaka Huo.

Mama Yake Alizaliwa Mwaka 1760 na Kufariki 10.10.1827 Kwa Matatizo ya Utumbo na Katika Maisha yake Yote Alimzaa Mtoto Mmoja tuu Ambaye Ndiye Shaka Zulu.

Shaka Zulu Alikua na Uchungu sana Kwa Mamayake Kwasababu Mamayake Alikuwa wa Kabila Lingine la 'Langei' na Baba Yake Alikua Kutoka Katika Kabila la Wazulu.
Baada ya Ujauzito Mamayake Alitoroka na Kwenda Kuishi Milimani Pekeake Kwani Iliamriwa Mtoto Akizaliwa Auwawe Kwasababu Iliaminika kuwa Angekua Mkosi katika Kabila lao Kutokana na Baba Yake Kuwa Kabila Tofauti.

Baadae Jambo Hilo Liliisha kwa Baba Yake Shaka Kulipa Faini ya Mifugo 50.
Shaka Zulu Aliwahi Pewa Amri na Wakoloni Kwamba Aachane na Mila/Tamaduni na Aipokee Dini Vinginevyo Atachomwa Moto Akiwa Hai!, Shaka Akwajibi tuu Kwamba "Huku Kwetu Tunakula Moto". .
.
.Shaka Zulu Nae Aliuwawa Mwaka Mmoja tuu Baada ya Mama yake Kufa, Kwani Tangu Mamayake Afariki Alianza Kufanya Mauwaji Hayo Kila Siku Hadi Siku ya Mwisho Anauwawa Bado Alikua Anachinja Watu tuu.

#tuvituvitu
#Jewajua
#fmfacts
#shakazulu #Afrika
#Ilovefacts

Sent from my Huawei Mate X using Tapatalk
Uongo
 
Jina lake Kamili Anaitwa 'Shaka kaSenzangakhona' Alikua Maarufu kwa Jina la 'Shaka Zulu', Alizaliwa Mwaka 1787 Huko Kwazulu-Natal Afrika Kusini na Kufariki Mwaka 1828 Akiwa na Miaka 41, Alikua Mfalme wa Himaya ya Wazulu Huko Afrika Kusini Kuanzia Mwaka 1816 –1828 Akichukua Ufalme Kutoka kwa Babayake 'Senzangakhona kaJama' Aliyefariki.

Shaka Zulu Alikua Anampenda Sana Sana Mamayake Mzazi 'Nandi kaBhebhe' Kiasi Kwamba Mamayake Huyo Alipofariki October 10, 1827, Shaka Akaanza Kufanya Mauwaji!.

Inaelezwa Kuwa Kila Asubuhi Alipokua Anaamka Alikua Anawachinja Wanawake Waliojifungua Siku za Karibuni Pamoja na Waume Zao, Anawachinja Wanawake Waliokua na Ujauzito, Anawachinja Watu Waliokua Hawaonyeshi Huzunu/Hawasikitiki Juu ya Kifo cha Mama Yake, Hata Ngombe Aliyeonekana Mjamzito au Alitejifungua Hivi Karibuni Alikua Anachinjwa!.

Lengo Kubwa la Kufanya hivyo Lilikua ni Kutaka Pia Watu Wapate Maumivu/Uchungu Aliokuwa Anaupata yeye Kwa Kumpoteza Mama Yake Mzazi.

Zaidi ya Watu 7,000 Waliuwawa kwa Kuchinjwa na Shaka Zulu Ndani ya Mwaka Mmoja tuu, Lakini pia Licha ya Kuuwa Kiasi hicho, Shaka pia Alipiga Marufuku Mtu Yeyote wa Himaya ya Wazulu Kupanda Zao Lolote Shambani kwa Mwaka Huo.

Mama Yake Alizaliwa 1760 na Kufariki October 10, 1827 Kwa Matatizo ya Utumbo na Katika Maisha yake Yote Alimzaa Mtoto Mmoja tuu Ambaye Ndiye Shaka Zulu.

Shaka Zulu Alikua na Uchungu sana Kwa Mamayaje Kwasababu Mamayake Alikuwa wa Kabila Lingine la 'Langei' na Baba Yake Alikua Kutoka Katika Kabila la Wazulu.
Baada ya Ujauzito Mamayake Alitotoka Nyumbani na Kwenda Kuishi Milimani/Porini Pekeake Kwani Iliamriwa Mtoto Akizaliwa Auwawe Kwasababu Iliaminika kuwa Angekua Mkosi katika Kabila lao Kutokana na Baba Yake Kuwa Kabila Tofauti.

Baadae Jambo Hilo Liliisha kwa Baba Yake Shaka Zulu Kulipa Faini ya Mifugo 50.
Shaka Zulu Aliwahi Pewa Amri na Wakoloni Kwamba Aachane na Mila/Tamaduni na Aipokee Dini Vinginevyo Atachomwa Moto Akiwa Hai!, Shaka Akwajibi tuu Kwamba "Huku Kwetu Tunakula Moto".

Shaka Zulu Nae Aliuwawa Mwaka Mmoja tuu Baada ya Mama yake Kufa, Kwasabababu Tangu Mamayake Afariki Alianza Kufanya Mauwaji Hayo Kila Siku Hadi Siku ya Mwisho nae Anauwawa Bado Alikua Anachinja Watu tuu.

Tufollow Instagram @fm_facts


View attachment 1071225

Sent using Jamii Forums mobile app
Umetoa wapi hizi Data Mkuu!!!! Angalia sana mkuu haya mambo mengine ndio yanasababisha Waafrika wajichukie na kutojiamini mpaka leo!!!! Wenye chuki na Waafrika ndio huwa wanapika Data za namna hii wakijua wapo wenye akili ya kushikiwa wanaamini cho chote hata kinachotoka kwa adui yetu!!! Mbona hawamtukuzi Chaka (Shaka) kwa mafanikio yake ya kuweza kuunganisha makabila ya Waafrika kusini ambayo mpaka leo mabaki yake tunayoona ( Kabila la Wazulu ndio kabila kubwa Zaidi kuliko yote Afrika Kusini). Kama angefanikiwa kwenye ndoto yake Chaka ndio angefanikiwa katika juhudi zetu tukuka za kuunganisha Afrika kuwa mmoja. Bila msaada wa mitandao au teknolojia Chaka aliweza kujenga taifa kubwa sana ambalo cheche zake zilifika mpak huku Tanzania!!! Hebu angalia unajua Eswatini ni nchi ya ambayo pia ilikuwa sehemu ya Ufalme wa Wazulu. Zimbambwe kuna Wamatebele ambao pia ni tawi la Wazulu achilia mbali kwetu huku Wangoni!!!!! Niambie kiongozi mwingine Afrika aliefanikiwa kiasi hiki!!!!

Tuamke Waafrika!!!!! Usingizi gani huu tumelala karne na karne…..
 
Siri iliyopo nikuwa shaka zulu aliambiwa na mganga wake kuwa atakapokufa mamayake basi na yeye hana muda mrefu atakufa. Ndo hasira zikaanzia hapo
 
Ni mada iliyokosa ukweli hasa huyu mtawala Shaka alivyoishi,jitahidi uangalie movie yake shaka zulu angalia series zote,jisomee vitabu na kama unauwezo tembelea pale Urundi kupata ukweli wa upande wa pili wa story hii.
 
Akili za Kiafrika zimekaa hovyohovyo tu, kuna mfalme mwingine wa Afrika kusini alikulia katika mazingira ya umasikini basi akaamuru raia wake wote nao pia wawe masikini, na ole wako ujifanye tajiri atahakikisha unaishi kama mashetani.

Maendeleo hayana chama
Mmmmmmmmmh huyo tumewahi kumuona
 
Back
Top Bottom