Ni zile zilizo katika mkakati wa maendeleo ambao utekelezaji utawanufaisha wananchi
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeonya yeyote atakayejaribu kufuja au kuzitumia vibaya yakiwemo matumizi binafsa sh. 1.3 zilizotokwna na mkopo wa masharti nafuu, itakula nae sahani moja.
Imesema fedha hizo ni mkopo ambao watanzania wataulipa, hivyo ni lazima zitekeleze miradi iliyokusudiaa ili kuwanufaisha wananchi na kurahisisha upatikanaji wa huduma muhimu.
Hayo yalielezwa jana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka alipozungumza na waandishi wa habari kuipongeza serikali chini ya Rais Samia kuendelea kuaminiwa na jumuia ya Kimataifa na kupatiwa mkopo huo wa masharti nafuu.
"Ikumbukwe Chama Cha Mapinduzi ndicho kilichoshika hatamu zauongozi wa nchi. Hivyo kinawahakikishia Watanzaia kuwa kitahakikisha fedha hizi hazitafunwi na mchwa na atakayethibitika kuhusika na ukwapuzi wa aina yoyote, Chama Cha Mapinduzi hakitasita kuilekeza serikali yake kumfikisha muhusika mbele ya vyombo vya sheria.
"Na kwenye hili tunazielekeza wizara zote
zitakazonufaika na fedha hizi kujipanga vizuri katika usimamizi kama alivyoelekeza Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na Usalama na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia suluhu Hassan, kwa sababu fedha hizi ni mkopo toka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), siyo fedha za sadaka, hivyo ziheshimiwe," alisema.
Alisema Chama kinawasisistiza viongozi na watendaji wenye dhamana kuanzia serikali kuu hadi katika halmashauri za wilaya, wahakikishe fedha hizo zinakwenda kutekeleza miradi iliyokusudiwa, ili kuleta matokeo yaliyolengwa kwa ustawi wa
wananchi.
"Fedha hizi na zingine zote zinazotolewa na serikali kwenda kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo, CCM haitakubali kuona fedha za umma zikitumiwa visivyo na kukibebesha lawama Chama ambacho ndicho kilichopewa dhamana na wananchi ya kuunda na kuongoza serikali.
"Tunatoa wito kwa Watanzania wote kuendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan na serikali yake, kwa kuendeleza na kudumisha umoja, amani na mshikamano uliopo nchini, ili kumpa nafasi na fursa nzuri ya kuijenga nchi yetu. Ndiyo maana mara kadhaa amesikika akitoa wito wa mshikamano na akitoa rai kuwa huu ni muda wa kuijenga Tanzania sio muda wa kuibomoa au kulumbana kwa masuala yasiyo na tija kwa maendeleo ya Watanzania. Kwa pamoja tuipeleke Tanzania katika mwelekeo sahihi wa maendeleo," alisema.
Oktoba 10, mwaka huu, Rais Samia alizindua kampeni kubwa ya Maendeleo kwa ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19 ambayo inagharimu takribani sh. trilioni 1.3 za msaada na mkopo wa masharti nafuu kutoka IMF.
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeonya yeyote atakayejaribu kufuja au kuzitumia vibaya yakiwemo matumizi binafsa sh. 1.3 zilizotokwna na mkopo wa masharti nafuu, itakula nae sahani moja.
Imesema fedha hizo ni mkopo ambao watanzania wataulipa, hivyo ni lazima zitekeleze miradi iliyokusudiaa ili kuwanufaisha wananchi na kurahisisha upatikanaji wa huduma muhimu.
Hayo yalielezwa jana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka alipozungumza na waandishi wa habari kuipongeza serikali chini ya Rais Samia kuendelea kuaminiwa na jumuia ya Kimataifa na kupatiwa mkopo huo wa masharti nafuu.
"Ikumbukwe Chama Cha Mapinduzi ndicho kilichoshika hatamu zauongozi wa nchi. Hivyo kinawahakikishia Watanzaia kuwa kitahakikisha fedha hizi hazitafunwi na mchwa na atakayethibitika kuhusika na ukwapuzi wa aina yoyote, Chama Cha Mapinduzi hakitasita kuilekeza serikali yake kumfikisha muhusika mbele ya vyombo vya sheria.
"Na kwenye hili tunazielekeza wizara zote
zitakazonufaika na fedha hizi kujipanga vizuri katika usimamizi kama alivyoelekeza Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na Usalama na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia suluhu Hassan, kwa sababu fedha hizi ni mkopo toka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), siyo fedha za sadaka, hivyo ziheshimiwe," alisema.
Alisema Chama kinawasisistiza viongozi na watendaji wenye dhamana kuanzia serikali kuu hadi katika halmashauri za wilaya, wahakikishe fedha hizo zinakwenda kutekeleza miradi iliyokusudiwa, ili kuleta matokeo yaliyolengwa kwa ustawi wa
wananchi.
"Fedha hizi na zingine zote zinazotolewa na serikali kwenda kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo, CCM haitakubali kuona fedha za umma zikitumiwa visivyo na kukibebesha lawama Chama ambacho ndicho kilichopewa dhamana na wananchi ya kuunda na kuongoza serikali.
"Tunatoa wito kwa Watanzania wote kuendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan na serikali yake, kwa kuendeleza na kudumisha umoja, amani na mshikamano uliopo nchini, ili kumpa nafasi na fursa nzuri ya kuijenga nchi yetu. Ndiyo maana mara kadhaa amesikika akitoa wito wa mshikamano na akitoa rai kuwa huu ni muda wa kuijenga Tanzania sio muda wa kuibomoa au kulumbana kwa masuala yasiyo na tija kwa maendeleo ya Watanzania. Kwa pamoja tuipeleke Tanzania katika mwelekeo sahihi wa maendeleo," alisema.
Oktoba 10, mwaka huu, Rais Samia alizindua kampeni kubwa ya Maendeleo kwa ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19 ambayo inagharimu takribani sh. trilioni 1.3 za msaada na mkopo wa masharti nafuu kutoka IMF.