Shaka Hamdu Shaka: Tanzania haiko kwenye mapambano ya demokrasia

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,886
938
SHAKA HAMDU SHAKA: TANZANIA HAIKO KWENYE MAPAMBANO YA DEMOKRASIA.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi.

Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.

Chama Cha Mapinduzi(CCM) kimesema Tanzania hakuna mapambano ya demokrasia kwani mageuzi na mabadiliko toka mfumo wa chama kimoja na kuingia mfumo wa vyama vingi yalifanyika kwa ridhaa na kwa mujibu wa sheria na kuifanya Tanzania kuwa nchi inayosimamia misingi ya kidemokrasia kinyume na madai yaliyotolewa na katibu mkuu wa chadema John Mnyika.

Pia kimesema madai ya Mnyika sikweli kama Mwenyekiti wa Chadema Freeman mbowe ametekwa na polisi wakati polisi si watekaji bali ni walinzi wa amani, usalama wa raia na mali zao wajibu wanaoutekeleza ni kwa mujibu wa katiba na sheria. Hata walipomkamata Mbowe walitoa taarifa kwa umma hivyo waache siasa za kutafuta huruma.

Hayo yamesemwa leo na katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndugu Shaka Hamdu alipotakwa kutolea ufafanuzi juu ya kauli iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chadema John Mnyika kuwa Tanzania iko katika mapambano ya demokrasia ambapo alisema si ajabu na wala si kosa kwa polisi kumkamata kiongozi yeyote wa kisiasa au wa kiserikali ikiwa wataona kuna haja ya kufanya hivyo.

Shaka alisema kinachofanywa na chadema ni kutapatapa, na kuuhadaa umma wa watanzania na jumuiya za kimataifa ilhali masuala ya ndani ya nchi kwa mujibu wa sheria hufanyika pale inapobidi na mamlaka za utawala hazihitaji kibali toka jumuiya zozote za nje au za ndani.

Alisema jumuiya za kimataifa zikiwemo taasisi zinazoshughulikia haki za binadamu, demokrasia na utawala bora zina taratibu na mipaka zinapotaka kujua yanayoendelea au kujiri katika taifa fulani hivyo hazina haki ya kuziamuru mamlaka zilizopo kisheria ili zifuate matakwa yao.

"Polisi wamethibitisha kumkamata Mbowe na wala hajatekwa kama Mnyika na chadema wanavyodai. Matamshi yao yamelenga kujenga chuki na kuchafua taswira ya nchi yetu kwenye Jumuiya ya kimataifa jambo ambalo halikubaliki na hawatafanikiwa maana Tanzania ni nchi huru inayoongozwa kwa misingi ya utawala wa sheria. "Alisema shaka.

Katibu huyo Mwenezi wa CCM alisema si kweli kwa mujibu wa matamshi ya Mnyika kudai Tanzania iko katika mapambano ya demokrasia wakati demokrasia ipo kisheria na kikatiba zaidi Tanzania ni nchi ya kupigiwa mfano katika kuzingatia ustawi wa haki za binadamu na maendeleo ya demokrasia.

Shaka alimtaka Mnyika awe na uwezo wa kutofautisha nini maana ya ukandamizaji wa demokrasia na uhuru wa demokrasia kutumika isivyo na kusababisha uvunjaji na ukiukaji wa sheria za nchi.

"Kutumia kivuli cha demokrasia kuvunja sheria huko ni kuinajisi demokrasia kwani moja ya misingi muhimu ya demokrasia ni utawala wa sheria. Hivyo haya wanayoendelea nayo ni upotoshaji na propaganda za kitoto. Vyama vyote vya vya siasa vimesajiliwa kwa mujibu wa sheria hivyo vina wajibu wa lazima kuwa mfano kwa kutii na kutekeleza sheria za Nchi." Alisema shaka kwa msisitizo

Aliwataka viongozi wa chadema kukaa na kutafakari kwa busara, hekima na uwazi kwanini Mbowe amepewa mashtaka hayo na kupitia wanasheria wao wakajiridhisha juu ya hatua sahihi za kuchukua badala ya kueneza proganda ambazo hazitamsaidia au kuzuia taratibu za kisheria kuendelea dhidi yake. Haya wanayoyafanya ni muendelezo wao wa kutokupenda kuheshimu na kufuata utaratibu.

"Ikiwa hati ya mashitaka iliyowasilishwa mahakamani iko kinyume na sheria mwenye uhalali wa kisheria kueleza vinginevyo ni mahakama tu si yeyote. Sasa kama wao wanahisi kuna jambo halipo sawa, wafuate taratibu za kisheria kupata tafsiri wanayoona wanaistahili badala ya kutaka kulazimisha uvunjwaji wa katiba na sheria za Nchi.

Katika hili niwakumbushe Chadema, moja ya misingi muhimu ya demokrasia ya kweli ni pamoja na kuheshimu na kutekeleza kwa usawa utawala wa sheria. Ikiwa wanaiishi demokrasia na wanaitaka ionekane ikiishi ni vyema wakaheshimu utawala wa sheria ambao hakuna mtu yupo juu ya sheria.

Kukamatwa kwa kiongozi yeyote aidha wa Chama tawala au wa upinzani si shambulio dhidi ya demokrasia kama anavyodai Mnyika huku akijaribu kumshinikiza Rais Samia Suluhu Hassan amuamuru mwendesha mashitaka amuachie huru mbowe kitu ambacho ni kinyume kabisa na matakwa ya kisheria.

Shaka alisema ni kituko kukisikia chama kinachohubiri kufuata misingi ya utawala bora wa sheria huku kikishindwa kuheshimu mgawanyo wa madaraka na kutaka kuingilia uhuru wa mahakama.

"Mnataka demokrasia, utawala wa sheria na haki, halafu muda huo huo mnamtaka Rais aingilie mahakama akiuke katiba na Sheria za Nchi kwa Maslahi yenu! hili halikubaliki kabisa. Serikali ya Rais Samia itasimamia katiba, sheria, haki na usawa wakati wote bila aibu wala kuyumbishwa, kufanya hivyo ndio chachu ya amani na utulivu nchini." Alisema Shaka

Mwisho

IMG-20210731-WA0098.jpg


IMG-20210731-WA0099.jpg


IMG-20210731-WA0100.jpg


IMG-20210731-WA0101.jpg


IMG-20210731-WA0102.jpg


IMG-20210731-WA0103.jpg


IMG-20210731-WA0104.jpg


IMG-20210731-WA0105.jpg


IMG-20210731-WA0106.jpg


IMG-20210731-WA0107.jpg


IMG-20210731-WA0108.jpg


IMG-20210731-WA0109.jpg


IMG-20210731-WA0110.jpg


IMG-20210731-WA0111.jpg
 
Chama kimeshamjibu akwaambie waliomtuma kuwa chadema wamedhamiria walichokifanya hawabahatishi,,,Kwa katiba hiyo mbovu rais anamamlaka ya kuingilia Kati mashitaka ya kubambikiwa kama yalivyofanyaka Kwa mashekh na walisikika hadharani wakimshukuru rais kuwatoa gerezani Kwa kuwa hawana hatia
 
SHAKA HAMDU SHAKA: TANZANIA HAIKO KWENYE MAPAMBANO YA DEMOKRASIA.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi.

Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.

Chama Cha Mapinduzi(CCM) kimesema Tanzania hakuna mapambano ya demokrasia kwani mageuzi na mabadiliko toka mfumo wa chama kimoja na kuingia mfumo wa vyama vingi yalifanyika kwa ridhaa na kwa mujibu wa sheria na kuifanya Tanzania kuwa nchi inayosimamia misingi ya kidemokrasia kinyume na madai yaliyotolewa na katibu mkuu wa chadema John Mnyika.

Pia kimesema madai ya Mnyika sikweli kama Mwenyekiti wa Chadema Freeman mbowe ametekwa na polisi wakati polisi si watekaji bali ni walinzi wa amani, usalama wa raia na mali zao wajibu wanaoutekeleza ni kwa mujibu wa katiba na sheria. Hata walipomkamata Mbowe walitoa taarifa kwa umma hivyo waache siasa za kutafuta huruma.

Hayo yamesemwa leo na katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndugu Shaka Hamdu alipotakwa kutolea ufafanuzi juu ya kauli iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chadema John Mnyika kuwa Tanzania iko katika mapambano ya demokrasia ambapo alisema si ajabu na wala si kosa kwa polisi kumkamata kiongozi yeyote wa kisiasa au wa kiserikali ikiwa wataona kuna haja ya kufanya hivyo.

Shaka alisema kinachofanywa na chadema ni kutapatapa, na kuuhadaa umma wa watanzania na jumuiya za kimataifa ilhali masuala ya ndani ya nchi kwa mujibu wa sheria hufanyika pale inapobidi na mamlaka za utawala hazihitaji kibali toka jumuiya zozote za nje au za ndani.

Alisema jumuiya za kimataifa zikiwemo taasisi zinazoshughulikia haki za binadamu, demokrasia na utawala bora zina taratibu na mipaka zinapotaka kujua yanayoendelea au kujiri katika taifa fulani hivyo hazina haki ya kuziamuru mamlaka zilizopo kisheria ili zifuate matakwa yao.

"Polisi wamethibitisha kumkamata Mbowe na wala hajatekwa kama Mnyika na chadema wanavyodai. Matamshi yao yamelenga kujenga chuki na kuchafua taswira ya nchi yetu kwenye Jumuiya ya kimataifa jambo ambalo halikubaliki na hawatafanikiwa maana Tanzania ni nchi huru inayoongozwa kwa misingi ya utawala wa sheria. "Alisema shaka.

Katibu huyo Mwenezi wa CCM alisema si kweli kwa mujibu wa matamshi ya Mnyika kudai Tanzania iko katika mapambano ya demokrasia wakati demokrasia ipo kisheria na kikatiba zaidi Tanzania ni nchi ya kupigiwa mfano katika kuzingatia ustawi wa haki za binadamu na maendeleo ya demokrasia.

Shaka alimtaka Mnyika awe na uwezo wa kutofautisha nini maana ya ukandamizaji wa demokrasia na uhuru wa demokrasia kutumika isivyo na kusababisha uvunjaji na ukiukaji wa sheria za nchi.

"Kutumia kivuli cha demokrasia kuvunja sheria huko ni kuinajisi demokrasia kwani moja ya misingi muhimu ya demokrasia ni utawala wa sheria. Hivyo haya wanayoendelea nayo ni upotoshaji na propaganda za kitoto. Vyama vyote vya vya siasa vimesajiliwa kwa mujibu wa sheria hivyo vina wajibu wa lazima kuwa mfano kwa kutii na kutekeleza sheria za Nchi." Alisema shaka kwa msisitizo

Aliwataka viongozi wa chadema kukaa na kutafakari kwa busara, hekima na uwazi kwanini Mbowe amepewa mashtaka hayo na kupitia wanasheria wao wakajiridhisha juu ya hatua sahihi za kuchukua badala ya kueneza proganda ambazo hazitamsaidia au kuzuia taratibu za kisheria kuendelea dhidi yake. Haya wanayoyafanya ni muendelezo wao wa kutokupenda kuheshimu na kufuata utaratibu.

"Ikiwa hati ya mashitaka iliyowasilishwa mahakamani iko kinyume na sheria mwenye uhalali wa kisheria kueleza vinginevyo ni mahakama tu si yeyote. Sasa kama wao wanahisi kuna jambo halipo sawa, wafuate taratibu za kisheria kupata tafsiri wanayoona wanaistahili badala ya kutaka kulazimisha uvunjwaji wa katiba na sheria za Nchi.

Katika hili niwakumbushe Chadema, moja ya misingi muhimu ya demokrasia ya kweli ni pamoja na kuheshimu na kutekeleza kwa usawa utawala wa sheria. Ikiwa wanaiishi demokrasia na wanaitaka ionekane ikiishi ni vyema wakaheshimu utawala wa sheria ambao hakuna mtu yupo juu ya sheria.

Kukamatwa kwa kiongozi yeyote aidha wa Chama tawala au wa upinzani si shambulio dhidi ya demokrasia kama anavyodai Mnyika huku akijaribu kumshinikiza Rais Samia Suluhu Hassan amuamuru mwendesha mashitaka amuachie huru mbowe kitu ambacho ni kinyume kabisa na matakwa ya kisheria.

Shaka alisema ni kituko kukisikia chama kinachohubiri kufuata misingi ya utawala bora wa sheria huku kikishindwa kuheshimu mgawanyo wa madaraka na kutaka kuingilia uhuru wa mahakama.

"Mnataka demokrasia, utawala wa sheria na haki, halafu muda huo huo mnamtaka Rais aingilie mahakama akiuke katiba na Sheria za Nchi kwa Maslahi yenu! hili halikubaliki kabisa. Serikali ya Rais Samia itasimamia katiba, sheria, haki na usawa wakati wote bila aibu wala kuyumbishwa, kufanya hivyo ndio chachu ya amani na utulivu nchini." Alisema Shaka

Mwisho

View attachment 1875727

View attachment 1875728

View attachment 1875729

View attachment 1875730

View attachment 1875731

View attachment 1875732

View attachment 1875733

View attachment 1875734

View attachment 1875735

View attachment 1875736

View attachment 1875738

View attachment 1875739

View attachment 1875740

View attachment 1875741
Shaka rudi kwenu Zanzibar, we don’t need zanzibaris in the mainland
 
..Mbowe amekamatwa KIHUNI, usiku wa manane, kwa kuvamiwa na watu walioficha sura zao, waliovalia nguo za kiraia wakidai wao ni Polisi.
 
Ukiona wameanza kuongea ujue ujumbe umewaingia vizuri ,kesho atakuja mwingi na lugha tofauti wakipishana wenyewe.

Mnyika kasema ukweli wakawadanganye wajinga wenzao
 
SHAKA HAMDU SHAKA: TANZANIA HAIKO KWENYE MAPAMBANO YA DEMOKRASIA.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi.

Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.

Chama Cha Mapinduzi(CCM) kimesema Tanzania hakuna mapambano ya demokrasia kwani mageuzi na mabadiliko toka mfumo wa chama kimoja na kuingia mfumo wa vyama vingi yalifanyika kwa ridhaa na kwa mujibu wa sheria na kuifanya Tanzania kuwa nchi inayosimamia misingi ya kidemokrasia kinyume na madai yaliyotolewa na katibu mkuu wa chadema John Mnyika.

Pia kimesema madai ya Mnyika sikweli kama Mwenyekiti wa Chadema Freeman mbowe ametekwa na polisi wakati polisi si watekaji bali ni walinzi wa amani, usalama wa raia na mali zao wajibu wanaoutekeleza ni kwa mujibu wa katiba na sheria. Hata walipomkamata Mbowe walitoa taarifa kwa umma hivyo waache siasa za kutafuta huruma.

Hayo yamesemwa leo na katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndugu Shaka Hamdu alipotakwa kutolea ufafanuzi juu ya kauli iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chadema John Mnyika kuwa Tanzania iko katika mapambano ya demokrasia ambapo alisema si ajabu na wala si kosa kwa polisi kumkamata kiongozi yeyote wa kisiasa au wa kiserikali ikiwa wataona kuna haja ya kufanya hivyo.

Shaka alisema kinachofanywa na chadema ni kutapatapa, na kuuhadaa umma wa watanzania na jumuiya za kimataifa ilhali masuala ya ndani ya nchi kwa mujibu wa sheria hufanyika pale inapobidi na mamlaka za utawala hazihitaji kibali toka jumuiya zozote za nje au za ndani.

Alisema jumuiya za kimataifa zikiwemo taasisi zinazoshughulikia haki za binadamu, demokrasia na utawala bora zina taratibu na mipaka zinapotaka kujua yanayoendelea au kujiri katika taifa fulani hivyo hazina haki ya kuziamuru mamlaka zilizopo kisheria ili zifuate matakwa yao.

"Polisi wamethibitisha kumkamata Mbowe na wala hajatekwa kama Mnyika na chadema wanavyodai. Matamshi yao yamelenga kujenga chuki na kuchafua taswira ya nchi yetu kwenye Jumuiya ya kimataifa jambo ambalo halikubaliki na hawatafanikiwa maana Tanzania ni nchi huru inayoongozwa kwa misingi ya utawala wa sheria. "Alisema shaka.

Katibu huyo Mwenezi wa CCM alisema si kweli kwa mujibu wa matamshi ya Mnyika kudai Tanzania iko katika mapambano ya demokrasia wakati demokrasia ipo kisheria na kikatiba zaidi Tanzania ni nchi ya kupigiwa mfano katika kuzingatia ustawi wa haki za binadamu na maendeleo ya demokrasia.

Shaka alimtaka Mnyika awe na uwezo wa kutofautisha nini maana ya ukandamizaji wa demokrasia na uhuru wa demokrasia kutumika isivyo na kusababisha uvunjaji na ukiukaji wa sheria za nchi.

"Kutumia kivuli cha demokrasia kuvunja sheria huko ni kuinajisi demokrasia kwani moja ya misingi muhimu ya demokrasia ni utawala wa sheria. Hivyo haya wanayoendelea nayo ni upotoshaji na propaganda za kitoto. Vyama vyote vya vya siasa vimesajiliwa kwa mujibu wa sheria hivyo vina wajibu wa lazima kuwa mfano kwa kutii na kutekeleza sheria za Nchi." Alisema shaka kwa msisitizo

Aliwataka viongozi wa chadema kukaa na kutafakari kwa busara, hekima na uwazi kwanini Mbowe amepewa mashtaka hayo na kupitia wanasheria wao wakajiridhisha juu ya hatua sahihi za kuchukua badala ya kueneza proganda ambazo hazitamsaidia au kuzuia taratibu za kisheria kuendelea dhidi yake. Haya wanayoyafanya ni muendelezo wao wa kutokupenda kuheshimu na kufuata utaratibu.

"Ikiwa hati ya mashitaka iliyowasilishwa mahakamani iko kinyume na sheria mwenye uhalali wa kisheria kueleza vinginevyo ni mahakama tu si yeyote. Sasa kama wao wanahisi kuna jambo halipo sawa, wafuate taratibu za kisheria kupata tafsiri wanayoona wanaistahili badala ya kutaka kulazimisha uvunjwaji wa katiba na sheria za Nchi.

Katika hili niwakumbushe Chadema, moja ya misingi muhimu ya demokrasia ya kweli ni pamoja na kuheshimu na kutekeleza kwa usawa utawala wa sheria. Ikiwa wanaiishi demokrasia na wanaitaka ionekane ikiishi ni vyema wakaheshimu utawala wa sheria ambao hakuna mtu yupo juu ya sheria.

Kukamatwa kwa kiongozi yeyote aidha wa Chama tawala au wa upinzani si shambulio dhidi ya demokrasia kama anavyodai Mnyika huku akijaribu kumshinikiza Rais Samia Suluhu Hassan amuamuru mwendesha mashitaka amuachie huru mbowe kitu ambacho ni kinyume kabisa na matakwa ya kisheria.

Shaka alisema ni kituko kukisikia chama kinachohubiri kufuata misingi ya utawala bora wa sheria huku kikishindwa kuheshimu mgawanyo wa madaraka na kutaka kuingilia uhuru wa mahakama.

"Mnataka demokrasia, utawala wa sheria na haki, halafu muda huo huo mnamtaka Rais aingilie mahakama akiuke katiba na Sheria za Nchi kwa Maslahi yenu! hili halikubaliki kabisa. Serikali ya Rais Samia itasimamia katiba, sheria, haki na usawa wakati wote bila aibu wala kuyumbishwa, kufanya hivyo ndio chachu ya amani na utulivu nchini." Alisema Shaka

Mwisho

View attachment 1875727

View attachment 1875728

View attachment 1875729

View attachment 1875730

View attachment 1875731

View attachment 1875732

View attachment 1875733

View attachment 1875734

View attachment 1875735

View attachment 1875736

View attachment 1875738

View attachment 1875739

View attachment 1875740

View attachment 1875741
Huyu wampe likizo aende Mombasa kwa mumewe kwanza
 
Back
Top Bottom