beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Kuelekea Maadhimisho ya Miaka 45 ya CCM, Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka amesema kwa kipindi chote hicho CCM kimeendelea kuwa chama sikivu na makini kinachojali majadiliano kuliko vitisho, kebehi, ubabe au kushurutishwa.
Amesisitiza CCM kipo tayari wakati wote kupokea maoni/ushauri na kutoa rai kwa Vyama vya Siasa Nchini kuendelea Umoja wa Kitaifa, kuthamini na kukuza ustawi wa demokrasia iliyopo akisema yapo Mataifa yanayoitamani Tanzania.
Amesema ndani ya Utawala wa CCM, maendeleo makubwa ya nchi yamepatikana, na yamekuwa msukumo mkubwa wa ujenzi wa amani kwa wananchi.