SautiYaMnyonge
JF-Expert Member
- May 13, 2018
- 439
- 742
Na Mwandishi Wetu,
Dar Es Salaam.
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kuhudhuria kwa maafisa wa kibalozi ,mashirika ya haki za binadamu na Umoja wa Ulaya (EU) zinaweza kuifuatilia kesi yeyote mahakamani ili kujua iwapo mahakama zinatenda haki kwa mujibu wa sheria huku wakiwa hawana haki ya kuingilia uhuru wa mahakama.
Kimesema Tanzania ni Taifa lenye sifa kemkem kutokana na kufuata kwake misingi ya utawala bora, kuheshimu haki za binadamu na kuenzi utii wa matakwa ya katiba na sheria.
Hayo yameelezwa jana na Katibu wa itikadi na Uenezi CCM Taifa Shaka Hamdu Shaka alipoulizwa iwapo anajua lolote huhusu maafisa wa ubalozi wa marekani na Uhamiaji wa ulaya walivyoanza kufuatilia kesi inayomkabili Mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowe mahakamani.
Shaka alisema kwa upande wake hana taarifa za shitaka hilo kufikishwa mahakamani na asingependa kulizumgumzia kwani halijui na hajui chochote hivyo akasema yuko tayari kuzungumzia hatua ya maafisa wa kibalozi kuhudhuria mahakamani.
Alisema maafisa hao wana wajibu wa kufuatilia suala lolote mahakamani baada ya kupewa kibali toka wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa kimataifa aidha wanapotaka kutazama maendeleo ya miradi ya ushirikiano na ya kisekta kama mkakati wa kudumisha mahusiano ya kimataifa.
"Maafisa wa kibalozi wa jumuiya nyingine yakiwemo mashirika ya haki za binadamu na utawala bora toka popote yanaweza kufika mahakamani hakuna cha ajabu. Tanzania nchi mashuhuri kwa sifa ya kuenzi haki za binadamu.
Hivyo uamuzi wao kwenda mahakamani pengine ni kutaka kupata kipimo cha uhuru katika uendeshaji wa kesi mbalimbali katika mahakama zetu"Alisema Shaka.
Aidha alisema Mataifa rafiki kwao yanayoheshimu haki za binadamu, utawala wa sheria, yanayothamini uhuru wa kujieleza, wa maoni na yanayotoa nafasi ya uhuru wa habari hayatapata kitete hadi kuwazuia maafisa wa kibalozi au wa jumuiya za kimataifa zisihudhurie mahakamani.
'Nadhani wana nia ya kusikiliza uendeshaji kesi, utoaji haki na pale mahakama zinapowatia hatiani watuhumiwa na washitakiwa. Nijuavyo mahakama hazifungi watuhumiwa bila kupatikana ushahidi yakinifu. Mahakama ziko huru kwa mujibu wa matakwa ya sheria. Kwa Tanzania hii inaeleweka"Alisisitiza.
Shaka alisema kuwepo kwa maafisa hao au kutokuwepo kwao bado wana uwezo wa kupata taarifa sahihi kupitia vyombo mbalimbali na huo huwa ni mpango wa utakaoionesha dunia kama mahakama za Tanzania ziko na uwazi, zinajiamini kiutendaji na ukweli ikiwemo uhuru wa kisheria bila kuvuka mipaka au kuleta mgongano katika mgawanyo wa madaraka.
Amani, umoja na utulivu tunaojivunia leo na kupigiwa mfano kama kisiwa cha amani ulimwenguni ni pamoja na utoaji haki kwa usawa
unakofanywa na mahakama zetu.
Katibu huyo alisema Tanzania imekuwa ikiwakaribisha hata watazamaji toka mataifa ya nje ili kuja kufuatilia na kutazama uendeshwaji wa michakato ya chaguzi zake kuu toka hatua ya uandikishaji wapiga kura,hatua za uteuzi wa wagombea, upigaji kura, kuhesabu na kutangazwa kwa matokeo hivyo hili la wao kufuatilia kesi mahakamani sio jambo la ajabu.
"Maafisa wanaohudhuria mahakamani husikiliza iwapo mienendo ya kesi kama inafuata taratibu za kisheria. Hawaendi mahakamani. Mambo yote huendeshwa kwa mujibu wa sheria za taifa husika. Hutasikia wakisema hili ni shitaka halisi au ni maonevu. Wapo ili kudumisha mahusiano ya kidipomasia jambo ambalo kama Chama tunapenda kuona yakiimarika zaidi huku uhuru wetu kama Nchi ukiheshimika. "Aleleza Shaka.
Mwisho.
Dar Es Salaam.
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kuhudhuria kwa maafisa wa kibalozi ,mashirika ya haki za binadamu na Umoja wa Ulaya (EU) zinaweza kuifuatilia kesi yeyote mahakamani ili kujua iwapo mahakama zinatenda haki kwa mujibu wa sheria huku wakiwa hawana haki ya kuingilia uhuru wa mahakama.
Kimesema Tanzania ni Taifa lenye sifa kemkem kutokana na kufuata kwake misingi ya utawala bora, kuheshimu haki za binadamu na kuenzi utii wa matakwa ya katiba na sheria.
Hayo yameelezwa jana na Katibu wa itikadi na Uenezi CCM Taifa Shaka Hamdu Shaka alipoulizwa iwapo anajua lolote huhusu maafisa wa ubalozi wa marekani na Uhamiaji wa ulaya walivyoanza kufuatilia kesi inayomkabili Mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowe mahakamani.
Shaka alisema kwa upande wake hana taarifa za shitaka hilo kufikishwa mahakamani na asingependa kulizumgumzia kwani halijui na hajui chochote hivyo akasema yuko tayari kuzungumzia hatua ya maafisa wa kibalozi kuhudhuria mahakamani.
Alisema maafisa hao wana wajibu wa kufuatilia suala lolote mahakamani baada ya kupewa kibali toka wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa kimataifa aidha wanapotaka kutazama maendeleo ya miradi ya ushirikiano na ya kisekta kama mkakati wa kudumisha mahusiano ya kimataifa.
"Maafisa wa kibalozi wa jumuiya nyingine yakiwemo mashirika ya haki za binadamu na utawala bora toka popote yanaweza kufika mahakamani hakuna cha ajabu. Tanzania nchi mashuhuri kwa sifa ya kuenzi haki za binadamu.
Hivyo uamuzi wao kwenda mahakamani pengine ni kutaka kupata kipimo cha uhuru katika uendeshaji wa kesi mbalimbali katika mahakama zetu"Alisema Shaka.
Aidha alisema Mataifa rafiki kwao yanayoheshimu haki za binadamu, utawala wa sheria, yanayothamini uhuru wa kujieleza, wa maoni na yanayotoa nafasi ya uhuru wa habari hayatapata kitete hadi kuwazuia maafisa wa kibalozi au wa jumuiya za kimataifa zisihudhurie mahakamani.
'Nadhani wana nia ya kusikiliza uendeshaji kesi, utoaji haki na pale mahakama zinapowatia hatiani watuhumiwa na washitakiwa. Nijuavyo mahakama hazifungi watuhumiwa bila kupatikana ushahidi yakinifu. Mahakama ziko huru kwa mujibu wa matakwa ya sheria. Kwa Tanzania hii inaeleweka"Alisisitiza.
Shaka alisema kuwepo kwa maafisa hao au kutokuwepo kwao bado wana uwezo wa kupata taarifa sahihi kupitia vyombo mbalimbali na huo huwa ni mpango wa utakaoionesha dunia kama mahakama za Tanzania ziko na uwazi, zinajiamini kiutendaji na ukweli ikiwemo uhuru wa kisheria bila kuvuka mipaka au kuleta mgongano katika mgawanyo wa madaraka.
Amani, umoja na utulivu tunaojivunia leo na kupigiwa mfano kama kisiwa cha amani ulimwenguni ni pamoja na utoaji haki kwa usawa
unakofanywa na mahakama zetu.
Katibu huyo alisema Tanzania imekuwa ikiwakaribisha hata watazamaji toka mataifa ya nje ili kuja kufuatilia na kutazama uendeshwaji wa michakato ya chaguzi zake kuu toka hatua ya uandikishaji wapiga kura,hatua za uteuzi wa wagombea, upigaji kura, kuhesabu na kutangazwa kwa matokeo hivyo hili la wao kufuatilia kesi mahakamani sio jambo la ajabu.
"Maafisa wanaohudhuria mahakamani husikiliza iwapo mienendo ya kesi kama inafuata taratibu za kisheria. Hawaendi mahakamani. Mambo yote huendeshwa kwa mujibu wa sheria za taifa husika. Hutasikia wakisema hili ni shitaka halisi au ni maonevu. Wapo ili kudumisha mahusiano ya kidipomasia jambo ambalo kama Chama tunapenda kuona yakiimarika zaidi huku uhuru wetu kama Nchi ukiheshimika. "Aleleza Shaka.
Mwisho.