Shairi: Toto Tundu limekuwa ni spika

Emc2

JF-Expert Member
Sep 26, 2011
16,808
16,834
Tulikupeleka shule, Elimu ukaipata
Tulijinyima tusile, Huduma ukaipata
Ulifanya tusilale, Matunzo kuyatafuta
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Hutaki maendeleo, Unapiga makelele
Huna hata mwelekeo, Nchi wataka ilale
Twataka maendeleo, Si maneno hayo tele
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Uzalendo wako nini, Hebu nieleze sasa
Vipi huko kijijini? Wanacheza kwasakwasa?
Huvipendi vya nyumbani, Ni nini ulichokosa?
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Kila kitu unabeza, Umegeuka uchungu
Wajifanya mangimeza, Kuwatetea wazungu
Vijana wawapoteza, Badilika ndugu yangu
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Wewe kipaza sauti, cha wanyonyaji wa kale
Zawadi yako ni suti, na wezi ni wale wale
Unapewa matikiti, Ili upige kelele
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Wale sio ndugu zako, Ka jojo wakutumia
Sisi ndio ndugu zako, Ukitemwa kufikia
Wale huko ni koboko, kung’ata wamezoea
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Elimu uliyopata, Tumia kujenga nchi
Acha kuwa ni robota, la kubebea kabichi
Huo ni ujinga futa, Simama tujenge nchi
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Chungu ni wadogo sana, Lakini wako pamoja
Kwanini wapenda sana, Kuvunja wetu umoja?
Sifa umepata sana, Sasa wafanya vioja
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Tamati nimefikia, Maelezo nimeyatoa
Ujumbe kuwafikia, Sina haja kokotoa
Ndugu yetu kasikia, Aachane kukodoa
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika
 
LOWASSA: SIASA ANAZOFANYA LISSU ZILIPITWA NA WAKATI....

“Lissu ni kijana wangu ninayempenda sana, ni mwasheria mzuri sana na mtu anayejiamini vizuri. Siasa anazozifanya za kila siku kupambana na vyombo vya dola kwasababu zisizo na msingi zilipitwa na wakati, Ni lazima tubadilike tuache siasa za kiharakati na tufanye siasa za kimaendeleo. Kila siku Mh. Mbowe anaongea, mimi naongea, Ndugu yangu Sumaye anaongea ila mbona hatukamatwi mara kwa mara. Sikatai Jeshi letu la polisi kuna wakati linapoteza mwelekeo, ila unapokamatwa kila siku unaonekana wewe ndo una matatizo” Edward Lowassa.
 
Mda mwingi sana mnatumia kufanya uongo kuwa kweli nawapongeza ni jambo njema kwa imani yenu.... Sasa basi nae tundu atapeleka mbuzi kwa Magu wamalizane.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tulikupeleka shule, Elimu ukaipata
Tulijinyima tusile, Huduma ukaipata
Ulifanya tusilale, Matunzo kuyatafuta
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Hutaki maendeleo, Unapiga makelele
Huna hata mwelekeo, Nchi wataka ilale
Twataka maendeleo, Si maneno hayo tele
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Uzalendo wako nini, Hebu nieleze sasa
Vipi huko kijijini? Wanacheza kwasakwasa?
Huvipendi vya nyumbani, Ni nini ulichokosa?
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Kila kitu unabeza, Umegeuka uchungu
Wajifanya mangimeza, Kuwatetea wazungu
Vijana wawapoteza, Badilika ndugu yangu
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Wewe kipaza sauti, cha wanyonyaji wa kale
Zawadi yako ni suti, na wezi ni wale wale
Unapewa matikiti, Ili upige kelele
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Wale sio ndugu zako, Ka jojo wakutumia
Sisi ndio ndugu zako, Ukitemwa kufikia
Wale huko ni koboko, kung’ata wamezoea
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Elimu uliyopata, Tumia kujenga nchi
Acha kuwa ni robota, la kubebea kabichi
Huo ni ujinga futa, Simama tujenge nchi
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Chungu ni wadogo sana, Lakini wako pamoja
Kwanini wapenda sana, Kuvunja wetu umoja?
Sifa umepata sana, Sasa wafanya vioja
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Tamati nimefikia, Maelezo nimeyatoa
Ujumbe kuwafikia, Sina haja kokotoa
Ndugu yetu kasikia, Aachane kukodoa
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika
Lissu,mzalendo wa kweli!
 
Huku vijijini tunatamani kumuona huyu lisu ni mrefu au ni mfupi inawezekana ni mkweli na shuja na msema kweli ni mpenzi wa Mungu.
 
Shairi bovu ni takataka Magu fool anakosa usingizi sababu ya Lissu ww unatuletea vioja
 
Tulikupeleka shule, Elimu ukaipata
Tulijinyima tusile, Huduma ukaipata
Ulifanya tusilale, Matunzo kuyatafuta
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Hutaki maendeleo, Unapiga makelele
Huna hata mwelekeo, Nchi wataka ilale
Twataka maendeleo, Si maneno hayo tele
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Uzalendo wako nini, Hebu nieleze sasa
Vipi huko kijijini? Wanacheza kwasakwasa?
Huvipendi vya nyumbani, Ni nini ulichokosa?
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Kila kitu unabeza, Umegeuka uchungu
Wajifanya mangimeza, Kuwatetea wazungu
Vijana wawapoteza, Badilika ndugu yangu
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Wewe kipaza sauti, cha wanyonyaji wa kale
Zawadi yako ni suti, na wezi ni wale wale
Unapewa matikiti, Ili upige kelele
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Wale sio ndugu zako, Ka jojo wakutumia
Sisi ndio ndugu zako, Ukitemwa kufikia
Wale huko ni koboko, kung’ata wamezoea
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Elimu uliyopata, Tumia kujenga nchi
Acha kuwa ni robota, la kubebea kabichi
Huo ni ujinga futa, Simama tujenge nchi
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Chungu ni wadogo sana, Lakini wako pamoja
Kwanini wapenda sana, Kuvunja wetu umoja?
Sifa umepata sana, Sasa wafanya vioja
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika

Tamati nimefikia, Maelezo nimeyatoa
Ujumbe kuwafikia, Sina haja kokotoa
Ndugu yetu kasikia, Aachane kukodoa
Toto letu hili tundu, Limekuwa ni sipika
Dada Anna una sauti nzuri kama ya lady jayed
 
LOWASSA: SIASA ANAZOFANYA LISSU ZILIPITWA NA WAKATI....

“Lissu ni kijana wangu ninayempenda sana, ni mwasheria mzuri sana na mtu anayejiamini vizuri. Siasa anazozifanya za kila siku kupambana na vyombo vya dola kwasababu zisizo na msingi zilipitwa na wakati, Ni lazima tubadilike tuache siasa za kiharakati na tufanye siasa za kimaendeleo. Kila siku Mh. Mbowe anaongea, mimi naongea, Ndugu yangu Sumaye anaongea ila mbona hatukamatwi mara kwa mara. Sikatai Jeshi letu la polisi kuna wakati linapoteza mwelekeo, ila unapokamatwa kila siku unaonekana wewe ndo una matatizo” Edward Lowassa.
Source..??
 
LOWASSA: SIASA ANAZOFANYA LISSU ZILIPITWA NA WAKATI....

“Lissu ni kijana wangu ninayempenda sana, ni mwasheria mzuri sana na mtu anayejiamini vizuri. Siasa anazozifanya za kila siku kupambana na vyombo vya dola kwasababu zisizo na msingi zilipitwa na wakati, Ni lazima tubadilike tuache siasa za kiharakati na tufanye siasa za kimaendeleo. Kila siku Mh. Mbowe anaongea, mimi naongea, Ndugu yangu Sumaye anaongea ila mbona hatukamatwi mara kwa mara. Sikatai Jeshi letu la polisi kuna wakati linapoteza mwelekeo, ila unapokamatwa kila siku unaonekana wewe ndo una matatizo” Edward Lowassa.

Haya ni maono ya mtu aliyeserve as president wa USA miaka ya 1900!

Patriotism means to stand by the country. It does not mean to stand by the president or any other public official, save exactly to the degree in which he himself stands by the country. It is patriotic to support him insofar as he efficiently serves the country. It is unpatriotic not to oppose him to the exact extent that by inefficiency or otherwise he fails in his duty to stand by the country. In either event, it is unpatriotic not to tell the truth, whether about the president or anyone else.
Theodore Roosevelt

Kwa taarifa fupi ya mtu huyu,soma hapa:
An American statesman, author, explorer, soldier, naturalist, and reformer who served as the 26th President of the United States from 1901 to 1909. He also served as the 25th Vice President of the United States and as the 33rd Governor of New York. As a leader of the Republican Partyduring this time, he became a driving force for the Progressive Era in the United States in the early 20th century. His face is depicted on Mount Rushmore, alongside those of George Washington, Thomas Jefferson, and Abraham Lincoln.
 
LOWASSA: SIASA ANAZOFANYA LISSU ZILIPITWA NA WAKATI....

“Lissu ni kijana wangu ninayempenda sana, ni mwasheria mzuri sana na mtu anayejiamini vizuri. Siasa anazozifanya za kila siku kupambana na vyombo vya dola kwasababu zisizo na msingi zilipitwa na wakati, Ni lazima tubadilike tuache siasa za kiharakati na tufanye siasa za kimaendeleo. Kila siku Mh. Mbowe anaongea, mimi naongea, Ndugu yangu Sumaye anaongea ila mbona hatukamatwi mara kwa mara. Sikatai Jeshi letu la polisi kuna wakati linapoteza mwelekeo, ila unapokamatwa kila siku unaonekana wewe ndo una matatizo” Edward Lowassa.
Kabla ya kupost chochote inabidi upimwe akili kwanza maana kwa uongo huu inaonesha una matatizo makubwa sana ya afya ya akili
 
Tanzania Imejaa mafala na watu wapumbavu sans.
Nini Tundu alofanya zaidi ya kuonya dhidi ya udikteta uchwara unaovunja sheria kila kukicha
We kaa ukimshangiliaHuyo anayejiita mtetezi wa wanyonge huku ukitafakari amekutetea nini wewe na ukoo wako
I diot
 
Back
Top Bottom