Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,371
- 39,186
Sitaupoteza muda, ninalo la kuusia,
Hasa kwenu kina dada, ninyi wa Kitanzania,
Nilisemalo si ada, bali onyo na wosia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Aloupanda jirani, acha kuutamania,
Usijifanye mhuni, ndizi ukajichumia,
Mwenyewe asibaini, kuna mtu aibia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Mgomba huo ni wake, wewe ukauvamia,
Ukazila ndizi zake, bila yeye kujulia,
Kwa kicheko na makeke, ndizi wazifakamia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Utamu wa ndizi hizo, wewe ukazisifia,
Ukasema si mchezo, ndo maana wajilia,
Miye ninakupa funzo, hizo ndizi achilia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Ni ndefu tena ni nene, ndizi wazishangilia,
Katika chani zione, zilivyojipangalia,
Hata ziwe nchi nane, wewe wazitamania,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Wazishika mkononi, wazimenya kwa hisia,
Asubuhi na jioni, shamba lake waingia,
Wewe wala huna soni, ndizi wajitungulia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Ewe binti wa kibongo, miye ninakuusia,
Uache yako maringo, jirani wamuudhia,
Ufanye wako mpango, ndizizo kujilimia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Kilo chako ukishike, cha jirani kuachia,
Sifa yako mwanamke, vya kwako kushikilia,
Utampiga mateke, mwingine akivamia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Nimefikia kikomo, beti nakuandikia,
Kwako hili liwe somo, hekima kukupatia,
Bila kuleta mgomo, ndizi hizo achilia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
M.M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)
Hasa kwenu kina dada, ninyi wa Kitanzania,
Nilisemalo si ada, bali onyo na wosia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Aloupanda jirani, acha kuutamania,
Usijifanye mhuni, ndizi ukajichumia,
Mwenyewe asibaini, kuna mtu aibia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Mgomba huo ni wake, wewe ukauvamia,
Ukazila ndizi zake, bila yeye kujulia,
Kwa kicheko na makeke, ndizi wazifakamia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Utamu wa ndizi hizo, wewe ukazisifia,
Ukasema si mchezo, ndo maana wajilia,
Miye ninakupa funzo, hizo ndizi achilia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Ni ndefu tena ni nene, ndizi wazishangilia,
Katika chani zione, zilivyojipangalia,
Hata ziwe nchi nane, wewe wazitamania,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Wazishika mkononi, wazimenya kwa hisia,
Asubuhi na jioni, shamba lake waingia,
Wewe wala huna soni, ndizi wajitungulia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Ewe binti wa kibongo, miye ninakuusia,
Uache yako maringo, jirani wamuudhia,
Ufanye wako mpango, ndizizo kujilimia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Kilo chako ukishike, cha jirani kuachia,
Sifa yako mwanamke, vya kwako kushikilia,
Utampiga mateke, mwingine akivamia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
Nimefikia kikomo, beti nakuandikia,
Kwako hili liwe somo, hekima kukupatia,
Bila kuleta mgomo, ndizi hizo achilia,
Mgomba huo si wako, acha kula ndizi zake.
M.M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)