Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,422
- 911,172
Kwenye Channel Ten Profesa Idrissa Kikula ambaye ni mwendeshaji wa Chuo Kikuu Dodoma alitangazia umma ya kuwa katika uzinduzi wa Chuo hicho ambacho sasa kinatimiza miaka minne seneti ya chuo hicho imeamua kuwaenzi JK na Kawawa kwa mchango mkubwa walioutoa kwa taifa hili.............................Profesa Kikula akielewa joto la siasa lilivyo hivi sasa nchini aliwaomba wananchi wasisome kuwa maamuzi hayo ni ya kisiasa kwa sababu wao ni wataalamu tu.................
Habari hizi pia zimo kwenye gazeti la Habari Leo...la leo...............
Tatizo kwa UDOM hawakutoa vigezo vya maamuzi yao.......na imekuwepo tabia ya vyuo vikuu hapa nchini kuwaenzi wanasiasa ambao ndiyo huwateua viongozi wa vyuo hivyo kwa minajili ya kulinda ajira zao serikalini........................
Kumuenzi JK pengine ndiyo yenye utata mkubwa zaidi kwa sababu zifuatazo:-
a) JK anatuhumiwa kudhulumu taifa hili maamuzi yao ya kikatiba ya kumchagua Raisi wa JMT.......................sidhani kama huu ulikuwa ni wakati mwafaka kumuenzi kiongozi huyu................................
b) JK amekuwa mstari wa mbele katika kusaka PHD za heshima na ikumbukwe tu pale alipoukwaa Uraisi mwaka 2005 alikimbilia USA na kurudi na shahada ya heshima.................na kule Kenya chuo kikuu kimoja kilimuenzi yeye na akina Kibaki na Raila akiwemo Koffi Annan kwa kazi ya usuluhishi ambayo Jk ushiriki wake ulikuwa ni kiduchu.....................................ukizingatia kamati mbili za ODM na PNU ambazo zilifanya kazi usiku na mchana kutafuta ufumbuzi wa mgogoro tajwa hazikuenziwa...........hawa ni akina Martha karua, William Ruto.n.k
c) Mchango wa JK katika utawala wake anahusishwa zaidi na kukua kwa nyufa za kidini na kuporomoka kwa uchumi wa nchi hii sasa sijui UDOM inamuenzi kwa sababu gani.............
d) Sijui sababu za kumuenzi Kawawa na kumuacha shujaa wa taifa hili Hayati Edward Moringe Sokoine......................................
e) Kwa nini UDOM imuenzi kiongozi ambaye yupo madarakani na kuwaacha viongozi wengi ambao hawapo madarakani kwa maana ni wastaafu?
Nao IDM-Mzumbe kumuenzi Nyerere posthumously kama ilivyo kwa Kawawa......lakini kwa Nyerere mchango wake katika ujenzi wa taifa hili kwa kuondoa matabaka ya kimapato na kikabila na kuliunda taifa moja hauna utata...............
Maswali yote haya yanasababishwa na vyuo vikuu vyetu kutokuwa na uwazi na vigezo vyao kuwa ni siri na hivyo kuleta hisia ya kuwa maamuzi ya namna hii ni self-serving tu na hayana masilahi yoyote kwa taifa hili changa duniani...............
Sura nyingine ambayo yaweza kusomwa ni ya udini hasa katika kipindi hiki ambacho udini unatajwa mara kwa mara.......................Prof. Kikula ni muislamu na JK na Kawawa ni waislamu......sas sijui nalo hili la udini limechangia hapa.............
Habari hizi pia zimo kwenye gazeti la Habari Leo...la leo...............
Tatizo kwa UDOM hawakutoa vigezo vya maamuzi yao.......na imekuwepo tabia ya vyuo vikuu hapa nchini kuwaenzi wanasiasa ambao ndiyo huwateua viongozi wa vyuo hivyo kwa minajili ya kulinda ajira zao serikalini........................
Kumuenzi JK pengine ndiyo yenye utata mkubwa zaidi kwa sababu zifuatazo:-
a) JK anatuhumiwa kudhulumu taifa hili maamuzi yao ya kikatiba ya kumchagua Raisi wa JMT.......................sidhani kama huu ulikuwa ni wakati mwafaka kumuenzi kiongozi huyu................................
b) JK amekuwa mstari wa mbele katika kusaka PHD za heshima na ikumbukwe tu pale alipoukwaa Uraisi mwaka 2005 alikimbilia USA na kurudi na shahada ya heshima.................na kule Kenya chuo kikuu kimoja kilimuenzi yeye na akina Kibaki na Raila akiwemo Koffi Annan kwa kazi ya usuluhishi ambayo Jk ushiriki wake ulikuwa ni kiduchu.....................................ukizingatia kamati mbili za ODM na PNU ambazo zilifanya kazi usiku na mchana kutafuta ufumbuzi wa mgogoro tajwa hazikuenziwa...........hawa ni akina Martha karua, William Ruto.n.k
c) Mchango wa JK katika utawala wake anahusishwa zaidi na kukua kwa nyufa za kidini na kuporomoka kwa uchumi wa nchi hii sasa sijui UDOM inamuenzi kwa sababu gani.............
d) Sijui sababu za kumuenzi Kawawa na kumuacha shujaa wa taifa hili Hayati Edward Moringe Sokoine......................................
e) Kwa nini UDOM imuenzi kiongozi ambaye yupo madarakani na kuwaacha viongozi wengi ambao hawapo madarakani kwa maana ni wastaafu?
Nao IDM-Mzumbe kumuenzi Nyerere posthumously kama ilivyo kwa Kawawa......lakini kwa Nyerere mchango wake katika ujenzi wa taifa hili kwa kuondoa matabaka ya kimapato na kikabila na kuliunda taifa moja hauna utata...............
Maswali yote haya yanasababishwa na vyuo vikuu vyetu kutokuwa na uwazi na vigezo vyao kuwa ni siri na hivyo kuleta hisia ya kuwa maamuzi ya namna hii ni self-serving tu na hayana masilahi yoyote kwa taifa hili changa duniani...............
Sura nyingine ambayo yaweza kusomwa ni ya udini hasa katika kipindi hiki ambacho udini unatajwa mara kwa mara.......................Prof. Kikula ni muislamu na JK na Kawawa ni waislamu......sas sijui nalo hili la udini limechangia hapa.............