Shaffih Dauda uko vizuri ila jitahidi sana ' uimarishe ' Kiingereza chako kwani ndicho Kinakuangusha na Kukufanya uchoreke

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,052
107,535
Napenda sana Kazi yako, bidii yako na Ubunifu wako ambao hauna mfano ila Kiingereza chako kinakuharibia na sijui ni kwanini hutaki Kukiboresha wakati Uwezo huo unao na ikijulikana kwamba sasa upo vizuri Kimaisha na Pesa Kwako siyo tatizo tena.

Kwa mara ya Tatu mfululizo nimekuwa nikikusikia hasa ukiwa hewani Clouds fm ukiwa unapata ' taabu ' sana Kuzungumza Lugha ya Kiingereza hasa pale unapokuwa unamfanyia Usaili Mgeni ambaye hazungumzi Kiswahili na mara zote Shukuru Mungu kikiwa Kinakushinda kwa haraka sana huwa ' Unaokolewa ' na Watangazaji wenzako akina Jeff Lea na Nicatius Kotinyo ambao hiyo Lugha ya Kiingereza ni kama vile wamezaliwa nayo kwani wanaizungumza Kiufasaha kabisa.

Na Kinachonishangaza zaidi Kwako Big Boss Shaffih Dauda ni kwamba kila Siku unaonekana Ukichanja tu Mbuga Kutembelea nchi Kubwa mbalimbali duniani lakini nasikitika bado Kiingereza chako ni hiki hiki cha ' Kubabia babia ' kama alichonacho An Eagle ( Mimi ) wakati nilitegemea au nilijua ya kwamba kadri unavyosafiri sana Ng'ambo / Ulaya basi hadi hivi sasa ungekuwa unakizungumza vizuri kabisa.

Hebu nakuomba jitahidi uwe unatenga muda kidogo utafute Chuo Kizuri ili ukajifunze vyema kabisa Kuzungumza na pengine hata Kuandika Kiingereza ili basi usiwe ' unajichoresha ' pale ukiwa unakizungumza ' Mubashara ' katika Kituo chako cha Clouds fm. Kwa Big Boss kama Wewe Kuongeza Kiingereza ' Kibovu ' na cha Kukitafuta kama An Eagle Mimi kunakuharibia CV yako na hata kuwapa Watu wengine Mashaka na Uwezo wako.

Halafu si lazima pia kama unajua kabisa kuwa Kiingereza Kwako ni tatizo kama kilivyo Kwangu Mimi An Eagle basi uwe unang'ang'ania tu Kukizungumza Redioni bali unaweza tu ukawa unawaachia wale wanaokijua vyema kama akina Lea na Kutinyo wazungumze na Wewe Bosi Wao ukawa tu unawasilisha Maswali yako ya Kiswahili Kwao na Wao wanayawasilisha kwa Lugha hiyo ya Kiingereza ambayo wanaijua kweli kweli.

Usikasirike na wala usinikasirikie bali yapokee haya niliyokuambia hapa na yafanyie Kazi upesi. Nakukubali Kinoma ' Baharia ' wangu.
 
Jamaa anastahili pongezi. Anajitoa sana kwenye soka, binafsi sijawahi kumsikia akichapa ngeli, labda nigekuwa na maoni tofauti

Km ni kweli akubali kubadilika. Kuhusu ushabiki naona siku hizi kapunguza
 
Jamaa anastahili pongezi. Anajitoa sana kwenye soka, binafsi sijawahi kumsikia akichapa ngeli, labda nigekuwa na maoni tofauti

Km ni kweli akubali kubadilika. Kuhusu ushabiki naona siku hizi kapunguza

Hata Mimi namkubali na ndiyo maana nimempa Sifa zake za Kiutendaji na Kiubunifu ila nimemsema kidogo ili ajijue na ayafanyie Kazi niliyomwambia japo anaweza pia akaachana nayo vile vile kama ataona hayana maana Kwake.
 
Hata Mimi namkubali na ndiyo maana nimempa Sifa zake za Kiutendaji na Kiubunifu ila nimemsema kidogo ili ajijue na ayafanyie Kazi niliyomwambia japo anaweza pia akaachana nayo vile vile kama ataona hayana maana Kwake.
Kabisa kabisa hana haja ya kupuuza labda kama hataki mafanikio zaidi na zaidi basi apuuzie tu ushauri wako
 
kwa nini mbona nimeuliza swali lenye mantiki au tatizo nini hapo mbn sijaona tatizo,kuna muswada niliona wakupandisha bei ya kurenew leseni natka kufahamu utaratibu sasa upoje kama ni gharama gani inatumika
Mkuu tatizo bila shaka ni context ya swali lako. Ungeuliza hili swali kwenye mazingira sahihi isingeleta shida sana
 
Swali la nyongeza hivi eangle yule ndege tai anataga au anazaa? Na je akiumwa anaweza kupewa dawa aina ya gentamycin
 
oooh
Mkuu tatizo bila shaka ni context ya swali lako. Ungeuliza hili swali kwenye mazingira sahihi isingeleta shida sana
ok,mimi nimeona madharani watu tupo na mimi na swali naloitaji jibu nikaona haitakua na shida maana ni inshu ambyo nilitaka ifahamu,ila kwa sababu nimuuliza kitu ambacho sio kibaya nadhani nikipata jibu kwa anaefahamu itanifahaa zaidi.hata kama ww unafahamu basi naomb unifahamishe
 
Cool down mzaz ngj watakuja kukusaidia wajuzi wa hiyo kitu
oooh

ok,mimi nimeona madharani watu tupo na mimi na swali naloitaji jibu nikaona haitakua na shida maana ni inshu ambyo nilitaka ifahamu,ila kwa sababu nimuuliza kitu ambacho sio kibaya nadhani nikipata jibu kwa anaefahamu itanifahaa zaidi.hata kama ww unafahamu basi naomb unifahamishe
 
Kocha wazamani Wa England alikuwa Mtaliano alikuwa ajui English FA wakatangaza wanaitaji mwl atakaye mfundisha kocha wa kuongea kiingereza kwa Wiki moja, na kweli Mwl alipatikana na kocha akafundishwa lugha wiki moja akajua kuongea kingereza.
 
Yaaani shafii Dauda huyu ninaemfahamu hajui Kiiingereza au shafii mwingine? Mbona mi nmemfuatilia interviews zake yupo vzr ? Labda km unataka aongee haraka haraka kitu ambacho naona hawezi kwani hata kiswahili hawezi kuongea haraka. Yupo vzr bana!
 
Wewe Mleta hii thread rudia kuandika uliyoandika kwa Kiingereza tujue kweli unamkosoa Shafii kwa haki sio kuwa unamuonea Wivu
 
Basi nmegundua wewe hujui kiingereza. Wanaojua watakwambia jamaa lugha inampiga chenga.

Yaaani shafii Dauda huyu ninaemfahamu hajui Kiiingereza au shafii mwingine? Mbona mi nmemfuatilia interviews zake yupo vzr ? Labda km unataka aongee haraka haraka kitu ambacho naona hawezi kwani hata kiswahili hawezi kuongea haraka. Yupo vzr bana!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom