SFO: Fidia ya rada inawasubiri majaji

Msharika

JF-Expert Member
May 15, 2009
947
69





Na Mashaka Mgeta



23rd February 2010


email.png

B-pepe



printer.png

Chapa



comment_bubble.png

Maoni





headline_bullet.jpg
Ni ile Tanzania iliingizwa mjini
headline_bullet.jpg
Ununuzi wake ulikuwa bei mbaya
headline_bullet.jpg
Kesi inawasilishwa mahakamani



Chenge(4).jpg

Andrew Chenge



Taasisi ya Kuchunguza Makosa Makubwa ya jinai nchini Uingereza (SFO), imesema utaratibu wa kurejesha ‘vijisenti’ vya Tanzania vinavyotokana na kashfa ya rada, unategemea uamuzi wa Majaji nchini humo. Hayo yamo katika taarifa ya Ofisa Habari wa SFO, David Jones, aliyoituma kwa mwandishi wa habari wa gazeti hili kwa njia ya mtandao.
Jones alisema maelezo kuhusu shauri la SFO dhidi ya kampuni ya BAE System kuhusiana na mkataba uliofikiwa na Tanzania, bado hayajawasilishwa katika mahakama ya wazi jijini London.
Alisema baada ya kukamilisha uchunguzi wao, kitengo kinachohusika kitawasilisha shauri hilo mbele ya majaji ambao wataamua jinsi kiasi cha Paundi milioni 30 kitakavyolipwa na BAE System.
Jones alisema fedha hizo zinajumuisha malipo ya faini na fidia kwa Tanzania. Kwa mujibu wa Jones, shauri hilo litasikilizwa katika mahakama ya Southwark Crown iliyopo katikati ya Jiji la London.
“Tarehe ya kuanza kusikiliza shauri hili bado haijathibitishwa na mamlaka za huduma katika mahakama hiyo,” alisema.
Jones alisema hivi sasa SFO haiwezi kuzungumzia kwa kina masuala yaliyoulizwa na Nipashe na kwamba hata baada ya uamuzi kutolewa, watagusia maeneo yatakayoamuriwa na majaji.
“Ninaamini utaelewa muingiliano wa kisheria uliopo katika sakata hili,” alisema Jones katika taarifa hiyo.
Katika maswali yake Nipashe, pamoja na mambo mengine ilitaka kujua mamlaka ya kisheria ya SFO katika kudhibiti taasisi yoyote kwa kushindwa kuhifadhi kumbukumbu vizuri, kama ilivyodhihirika kwa BAE’s System.
BAE wamekubali kulipa fidia hiyo kama njia ya kufikisha hitimisho kesi ya rushwa iliyokuwa ikiwaandama, ikiangaliwa kama mbinu ya kukwepa kitiwa hatiani mbele ya safari kwa kesi kubwa ya rushwa ambayo ingekuwa na madhara makubwa zaidi kwake kibiashara duniani. Badala yake BAE waliafikiana na SFO kukiri kosa la uzembe wa kutokuweka kumbukumbu sahihi jinsi kamisheni ya ununuzi wa rada ya Tanzania ilivyogawanywa kwa madalali mbalimbali.
Pia Nipashe ilitaka kupata taarifa za viashiria vya rushwa katika hatua zote zilizofanikisha kusainiwa kwa mkataba na hatimaye ununuzi wa rada hiyo iliyoigharimu Tanzania Dola za Marekani milioni 60.
Kwa upande mwingine, Nipashe iliuliza kuhusu hatma ya uchunguzi wa akaunti ya aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, huko Jersey, Uingereza na jinsi inavyohusiana na kashfa ya rada.
HOJA YANGU: Watanzania PCCB wanasubiri Ushahidi gani zaidi?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom