Sexually transmitted demons/maambukizi ya mashetani kwa njia ya ngono. Nini uhalisia wa janga hili?

Ni kweli sina dini ila nina Mungu

Msingi wa dini ni ibada za wafu

dini ni tegemeo la watu wapumbavu na wajinga,

Mungu ni tegemeo la watu wenye busara, hekima na maarifa
Huyo Mungu unayemtegemea ni wa aina gani?
 
Imani hufunzwa inategemea aliekufunza alitaka uelekee mlengo gani!, majini mapepo, mizimu nk vyote ni nadharia unaweza kuvigeuza upendavyo kiimani. Binafsi siamini katika hivyo kwa hiyo haviniathiri kifikira.
 
Msingi wa dini yeyote ile ni ibada za wafu,

hivi ulishawahi kumwona shetani? km bado unapata wapi ujasiri wa kumzungumzia hapa ili hali hujawahi kukutana nae?

kwanini hamtaki kukubali ukweli kuwa kuna baadhi ya mambo yaliyo nje ya uwezo wenu, mwatakiwa muyaache km yalivyo kuliko kupotosha watu na kuwatia hofu

ukweli kuwa Shetani/Majini wapo imebaki kuwa ni SIRI YA MUNGU hakuna ajuaye

km kuna maisha baada ya kifo nayo Imebaki kuwa ni SIRI YA MUNGU hakuna ajuaye

hizi imani za kijinga kutaka kuaminishana kakakuona ni chura na chura ni kakakuona tunataka zikome, muda wake umekwisha

hakuna mtu mwenye chuki wala hasira hapa,
Ha ha ha ha unasema huamini majini na shetani sababu hujawahi kumuona na bado unasema haya mambo ni siri ya Mungu, ushawahi kumuona huyo Mungu!?
 
Sio mizimu tu hata miungu ya ukoo fulani unaweza kuibeba ndani yako. Na magonjwa yao pia . utakuta hata hukuwa na hayo magonjwa lakin unajikuta unayo ( na ww unakuwa wa1 kuwa nayo ktk ukoo wenu)

Yeye aziniye na kahaba amekuwa mwil mmoja naye

## kama ni mwil mmoja vyote alivyo kuwa navyo mwenza waka na ww unapata( mwil mmoja)
 
Haswa ndo maana sie waislam kuna dua unaomba kabla ya kuingiliana wana ndoa na kuna taaratibu nyingi kwenye kujamiana, maana yake mnaji kinga na shetani.
In the Name of Allah. O Allah, keep the shaytaan away from us and keep the shaytaan away from what You have blessed us with.

Note: *Mtume wa Mwenyezi Mungu amani iwe ju yake amesema haya. yoyote atakae sema hio dua na kama mke waake usiku huo ndo anakua mja mzito basi sheytani atoweza kumdhuru mtoto. ina maana hi kitu ulio leta hapa ina ukweli.
 
Kun kaukweli kidogi kwani kwa mujibu wa Mtume Muhammad,anasema zinaa inarithisha ufukara,zinaa inafupisha umri wa mtu wa kuishi,zinaa inarithiwa kizazi hadi kizazi inatabia ya kujirudia na urithi ktk familia mfano km baba au mama utazini basi lazima mwanao nayeye atakuja kuziniwa au kizini sana ,
 
Haswa ndo maana sie waislam kuna dua unaomba kabla ya kuingiliana wana ndoa na kuna taaratibu nyingi kwenye kujamiana, maana yake mnaji kinga na shetani.
In the Name of Allah. O Allah, keep the shaytaan away from us and keep the shaytaan away from what You have blessed us with.

Note: *Mtume wa Mwenyezi Mungu amani iwe ju yake amesema haya. yoyote atakae sema hio dua na kama mke waake usiku huo ndo anakua mja mzito basi sheytani atoweza kumdhuru mtoto. ina maana hi kitu ulio leta hapa ina ukweli.
Sasa inakuwaje waumini wengi wa uislamu ndio wenye kuvisha watoto hirizi mikononi na viunoni kama walishafanyiwa dua kabla ya mimba haijatungwa?
 
kaka niku famishe kitu kwa faida yako na wengine pia,kuna uislam kama uislam dini, na kuna mtu kama mtu natabia zake na imani yake, uislam umekataza mambo hayo.hupaswi kujikinga kwa hirizi wala chale kama wafanyavyo/wafanyiwavyo wengi miongoni mwa jamii ya wanaadamu na la kusikitisha zaidi katika kundi la wanaoamini na kufanya ushirikina huu ni waislam kwa sababu wengi wetu hawa somi dini kiundani zaidi. ndo maana mwanzo nikasema kuna dini na mtu kama mtu.
Ndugu yangu shirki ni jambo baya sana na ni miongoni mwa dhambi kubwa ambayo Mwenyezi Mungu amemuambia Mtume wake kuwa:
Na kwa yakini yamefunuliwa kwako na kwa walio kuwa kabla yako: Bila ya shaka ukimshirikisha Mwenyezi Mungu a'mali zako zitaanguka, na lazima utakuwa miongoni mwa wenye kukhasiri

Huyo ni mtume wa Mwenyezi Mungu vipi mimi na wewe watu wakawaida? so kabla ya Mtume kuwa walifunuliwa wazi kua hayo mambo sio. ni hayo tuh ndugu yangu.

SO watu wanafanya mambo ya hirizi, mara mvuje wana amini itawalinda hizo ni imani potofu pengine wana rithi kwa babu zao au baba zao kua inalinda ila katika uislam hakuna
 
Kuna mtu anakupa chupa ya maji kilimanjaro imewekwa dawa ukinywa tu ina flash uchafu wote dawa hiyo ni sh 142,000. Namba ya sms yake ni 0766112752 ila kwa masharti ya kwamba usirudie tena kufanya uzinzi, lazima utafute pa kutulia ni vema utakaye tulia naye akanywa hayo maji. Ukinywa utaaikia mabadiliko makubwa sana ikiwa na tumboni kusikia kama kuna mgogoro unaoendelea. Chanzo cha wengi kujikuta wana matatizo mengi ni pamoja na kuwa walifanya mapenzi na watu wenye majini.
mwizi huyo
 
damu inahusikaje pale mkuu,
Ni kweli mashetani yanacontrol mfumo wa fahamu ndio maana yanaweza kumzima mtu macho akawa kipofu akiombewa yakafukuzwa anaona.
Naomba uyaweke hayo Mengi.
Maana lengo hapa ni kupata hitimisho la uhalali au uhalamu wa fundisho hili kwa ushahidi sio ushuhuda
Swali jingine je kwa wale wanaongezewa damu hospitalini inakuwaje ikiwa kawekewa damu ya mtu aliyekua na pepo wachafu?
 
nilikuuliza, narudia tena

Ulimwengu wa roho ni upi?

na

Ulimwengu wa Mwili ni upi? nijibu halafu tusonge mbele
Ndugu umesema vyema kwenye post ya nyuma unaamini uwepo wa MUNGU ila maswali yako yanatia mashaka huamini ulimwengu wa Roho.
Hapa nashindwa kukuelewa huyo MUNGU wako unamuabudu vipi ikiwa mambo ya kiroho hukubaliani nayo.
 
Lakini nafikili pia,upatapo mpenzi huko mlikokutana kuna nyakati nguvu za asili hukushuhudia juu ya uliempata,unaweza ona tu mapema kua hapa nilipoingia siyo pangu,sasa inahitaji roho ngumu kupanasuka,maana unakua unavutwa.tatizo ni ile hali ya kushindwa kuuhimili udhaifu unaendelea na mahusiano kwa kutumia akili na mwili,lakini nguvu ya asili,roho,inakwambia hapo ulipo kimbia
 
Mkuu hapa physics wala biology haihusiki kabisa.
Mkuu naomba kuongezea swali la uhafamu hapa kidogo, ni energy zipi hizo kama sio hzi za physics, chemistry au bios?, na chanzo chake ni nini na unawezaje kutambua na zinamsaada gani binadamu ilhali kuzitambua sio kazi rahisi au kwanini zinakua na usiri ndani yake m
 
Mseza Mkulu,

Hii ngumu kumeza, lakini vumilia tu, ili shetani atutandike inabidi atangaze kuwa hayupo kwa sababu haonekani kwa macho.
Nikirejea kwenye mada yako, nikurudishe nyuma kwenye kitabu cha Hesabu sura ya 22 mpaka 25, nitaeleza kwa kifupi ukipata muda kasome.
Ili ibada ya sanamu(au miungu mingine) itimie mambo manne lazima yatimie
1. Lazima uvutiwe na uzuri wa ile sanamu
2. Lazima ushiriki chakula kilichotolewa kwa hiyo miungu
3. Lazima usujudu kuabudu hiyo miungu
4. Lazima utoe sadaka ya damu kwa hiyo miungu (hapa ni damu za watu, direct or indirect)
Nisikuamishe vumilia, hapo penye kitabu cha hesabu Balaam amepewa dili la kuwalaani wana wa Israel, anapanga madhabahu yake saba ya uchawi inashindikana kuwalaani, maana pale ilikuwa mapambano kati ya madhabahu, madhabahu ya kishetani na madhabahu ya Mungu.
Part 2 jinsi gani sasa ya kupitisha ile laana ambayo imeshindikana kuipitisha kwa njia ya madhabahu, njia ya werevu wa siri pale ikawa ni ngono, anatumwa motto wa kwanza wa kike wa kuhani wa baali na timu yake kwa ajili ya kufanikisha hilo.
Cha kwanza wanaume wanavutiwa na uzuri wa mabinti hawa( hatua ya kwanza ya uabudu sanamu). Wanawavuta kwenye ngono wanaingia laini, wanakaribishwa kwenye sherehe iliyoandaliwa kwa miungu yao tena wanaambiwa kabisa nyinyi kwenye shughuli ya kuabudu hamtakuwepo ila mtashiriki chakula tu (wanaingia laaini, hatua ya pili inakamilika)
Wanazaa watoto nao, wanawaambia inabidi kutoa sadaka ya kuteketeza ya watoto ambayo inahitaji motto mmoja tu wako wanaingia laini( hatua ya tatu na ya nne inatimia) laana iliyoshindikana kupelekwa kwa njia ya madhabahu inakamilishwa na ngono. Ngono ndio njia rahisi ya kukuunganisha na madhabahu zote za kuabudu sanamu.
Ukisoma pale mbele unaona Mungu alivyojawa hasira na mtego huo uliofanikiwa, mpaka kulinganisha hasira yake na alitokuwa nayo Finehasi na kummpa agano la ukuhani wa milele.
Njia rahisi ya kuua imani ya Mungu wa kweli ni ngono tu, maana hapo panakamilishwa uabudu sanamu kwa haraka, kama uamini angalia hatua za Daudi kwa mke wa Uria, zilikamilishwa kama nilivyoainisha hapo juu.

Na kwa wakatoliki wasome kitabu cha Yoshua bin Sira anaeleza wazi kuwa ngono ni kama moto ulivyo kwenye kuni kavu ukishaingia hautazimika mpaka kuni zimeisha, ndivyo ngono ifanyavyo kazi kwenye mwili wako ukiindekeza haitoki mpaka imekuteketeza.

Ngono nje ya ndoa mwisho wake mauaji, kafumaniwa, kajinyonga, katoa mimba, kamtangaza vibaya mbele za watu(katuma picha za uchi wa mwezie), kafilisika, kamnyangánya kigari alichomuhonga, kafukuzwa kazi na moto wake unaanza taratibu ninastress,
Shetani haji bali kuiba, kuvunja, kuharibu na mwisho nikuua, shetani hajawahi kuwa rafiki wa binadamu hata siku moja. Unakumbuka Ayubu mara ya kwanza anamwambia Mungu gusa mali zake atakukufuru, aliposhindwa anasemaje?
Wewe Mungu mali si kitu mambo ni mfupa kwa mfupa, ngozi kwa ngozi hapo lazima akukufuru kwa hiyo anahamia kwenye kumtandika kwa magonjwa.

Kwa wale ambao mnasubiri kuona vitu vya rohoni kwa macho endelea kukusanya laana za kutoka kila upande za kifipa twende, wa wajaluo chukua, za wanyasa beba, za wadigo twende kazi, za kichina kama kawaida, za kimangáti we beba, za kizaramo mia tano mia tano
Daah, sasa tutakuwa wageni wa nani? maana naona kila kona iko tight! kazi ipo...
 
4688558_images_jpeg68d5535b971d558f594f10a5affd0a71

4689005_demon_jpegfc6309e2ec7b9161ad09d5369d041206


Dunia haijawahi kuchoka kupokea elimu mpya kutoka katika hazina ya Fikra za wakazi wake. Yawezekana Ikawa kweli au mbinu za werevu wachache kutia hofu wakazi wa dunia lakini Gonjwa hili linasadikiwa kukua kwa kazi ya ajabu kwa mujibu ya watu waliozama katika mlengo huo wa maarifa.

SEXUALLY TRANSMITTED DEMONS NI NINI?
Kwa uhalisia Tendo la ndoa lilihifadhiwa kwa ajili ya Mtu mme na mke. Nje ya hapo utakutana na Uzinifu,Uasherati,Usagaji,Ushoga na kila uchafu kwa wa kingono kwa aina zake. Hapa inaelezwa kwamba Mtu mwenye majini (Kwa waislamu MAJINI WACHAFU) au Mashetani/Mapepo akifanya tendo la ndoa na mtu asiyenayo, Ule muunganiko Unatoa fursa ya kushea Majini hayo kati ya pande mbili.

Maelezo yanaenda mbali zaidi kwamba Sio majini tu ya kawaida haya bali hadi mizimu ya mmoja wa washiriki inafunguliwa milango inaingia kwa upande wa pili. Ukifikiri sana uhalisia wa Elimu hii basi unamfikiria mtu ambaye ameshafanya ngono na watu zaidi ya 500 atakuwa amejizolea Mashetani kiasi gani kama wapenzi walikuwa wabebaji wa Mashetani.

ELIMU HII
Imetapakaa katika imani ka kiprotestanti, na baadhi ya mielekeo michache ya kiimani na changamoto ni uhalisia wa haya mambo maana yako katika Frequency/Mawimbi yaliyo nje ya uwezo wa Macho na Darubini.

MASWALI YANAOYOBAKI KWETU
1:Je Majini/Mapepo/Maraika wachafu na Mashetani wanawezaje kuhama kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine Kupitia ngono.

2:Je Ni nini Dalili ya mtu anayesumbuliwa na SSexually Transmitted Demons?

3:Tiba yake ni nini?
4:Je watu wote wasio wasiamini katika uwepo wa Mungu,Mapepo na dhana ya Dhambi ni wahanga wa hii janga au wao wanakaa kwenye kundi lipi?

5:Je kunauwezekano wa kukwaa janga hili kwa njia ya Masturbation?

6:Je hizi ni story za kutisha waumini ili waachane na ngono nje na kabla ya ndoa na ni njia ya wajanja wachache kupiga pesa kwa kuwatibu kiimani wahanga huku sadaka zikitiririka kwa pembeni?

7:Watafiti wa Jambo hili wanasema karibu 70% wa watu wanaoshiriki tendo la ndoa nje ya ndoa wanamashetani, Je huu ni Ushahidi wa kutosha kuamini uwepo wa janga hili?



karibu useme chochote katika upande huu wa fikra, Dunia ina mambo.

Note:Mada hii haina uhusiano na mwanadamu kufanya mapenzi na Mashetani.
LENGO: Lengo kuu la bandiko hili sio kutisha watu kama ilivyoibuka kwenye maelezo bali ni kujua UHALALI AU UBATILI WA IMANI hii Kwa USHAHIDI WA VYANZO VYA BIBILIA/QURAN AU CHOCHOTE KATIKA IMANI ZA KIAFRIKA
Duh hii kuna watu nahis wana matatizo hayo maana unakuta mtu ni mpenda ngono hatar huenda kuna ukwel
 
Back
Top Bottom