Serikalini Wamekosekana Watu Wanaojua Crisis Management

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,489
40,999
Kwa mafunzo niliyoyapata toka kwa wakufunzi wa NATO, kuna vitu vya kuzingatia mara kunapokuwa na Crisis.

1) Automatically the most Senior Officer becomes the Crisis Management Manager. Maana yake, yule mwenye cheo kikubwa kuliko wote, moja kwa moja anakuwa Meneja wa Menejimenti ya Janga

2) Formation of Crisis Management Teams. Huwezi kuwa na timu moja kwenye Menejimenti ya Janga. Timu zinaweza kutofautiana kufuatana na aina ya janga, lakini msingi wake huwa haubadiliki:
a) Kamati ya Upashaji habari. Kukiwa na janga ni lazima kuwe na constant communication, kati ya kamati, kamati na idara za uokozi, kati ya kamati na jamii. Inategemea aina ya janga. Lakini mara nyingi inashauriwa, utoaji wa taarifa uwe kila baada ya nusu saa mpaka masaa 2. Usipofanya hivyo, unajenga mazingira ya watu kuzigeuza hisia kuwa habari kamili. Unataka kuliziba hilo pengo kwa utoaji wa habari za mara kwa mara. Ndiyo maana wenzetu wanakuwa na live updates.

b) Kamati ya uokozi. Kamati hii, umahiri wake upo katika kuwaokoa watu wengi kadiri inavyowezekana. Ufanisi wa kamati hii hutegemea nyenzo walizo nazo, taarifa wanazozipata toka idara za uchunguzi na intelijensia, ushirikiano wa haraka wanaoupata toka mamlaka za uamuzi. Lakini kwa vile yule mkubwa kabisa ndiye Meneji wa Menejimenti Timu, maamuzi hufanyika mara moja na kwa haraka.

b) Kamati ya uchunguzi na intelijensia. Kamati hii ndiyo yenye jukumu muhimu sana la kuzifanya kamati zote zitende kwa ufanisi. Wao hutoa taarifa sahihi za ukubwa wa janga, mwelekeo wa janga, uwezo wa kulikabili janga, uwezo uliopo wa kulishinda janga, mapungufu ya uwezo na mapendekezo ya njia za haraka za kulishinda janga. Kwa janga lililopo, kamati hii ndiyo ingekuwa pia na uwezo wa kutafuta taarifa za uwezekano wa wagonjwa ambao ama kwa kutojua au kwa makusudi wanaamua kutokwenda kuzitafuta huduma za afya kwa hofu ya kwenda kufungiwa bila kupewa huduma za kuwasaidia.

c) Kamati ya Rasilimali. Kamati hii kazi yake kubwa ni kutafuta rasilimali zinazohitajika. Wanapokea zaidi taarifa toka kwenye kamati ya uokozi na ya intelijensia. Kamati hii moja kwa moha inasimamiwa na Meneja.

d) Kamati ya Elimu na Uinuaji wa Morali. Hii kamati kazi yake ni kuwaeleimisha watu, kuwahamasisha na kujenga morali ya mapambano.

Kwetu hapa, kuhusiana na tatizo hili la Corona, inaonekana kuna tatizo kubwa katika menejimenti. Yawezekana hatuna wataalam wanaofahamu mbinu za kukabiliana na majanga, au wamepuuzwa.

Ni jambo la ajabu mno, kuona inapita hata siku nzima au 2 au hata 3, Waziri wa afya, ambaye nadhani ndiye kiongozi wa kamati ya Upashaji habari, hajasema lolote.

Kwa mtu anayejua wajibu wake, hawezi kufanya kosa kama hilo ambalo ni la wazi mno. Hata kuwaambia wananchi kuwa, leo hatuna maambukizi wala kifo, ni habari. Unakuwa umezuia ombwe ambalo watu watajaza habari zao.

Kwa nini tunashindwa hata kwenye basics tu. Ukiangalia TBC ni upuuzi mtupu. Ukiangalia TV stations za nchi nyingine, vipindi vingine vinaendelea, lakini chini au pembeni, unaona updates. Na ni nadra sana ikapita hata saa moja bila ya kusikia ujumbe unaohusiana na tatizo la Corona. TBC wanaona kuonesha taarabu au miziki ni muhimu zaidi kuliko kutoa elimu kwa watu, elimu ambayo ingeweza kusikia watu kuchukua tahadhari zaidi.

Labda tuseme kuwa sisi Tanzania hatupo kwenye mapambano dhidi ya Coronavirus. Huwezi kusema upo kwenye mapambano, halafu habari za hayo mapambano unaziweka kwenye mafaili.

Serikali yetu inaonekana kushindwa kumeneji mapambano haya au kwa makusudi, au kwa kutokujua au kwa ukaidi. Vyovyote iwavyo, kuna nafasi ya kujirekebisha.

Kwenye mapambano kama haya, Rais ndiye Meneja wa Menejimenti ya Crisis. Meneja wa Crisis anakaa hata wiki bila ya kuzungumza na watu wake ambao wanahitaji kusikia mipango, mbinu, mwelekeo na mwanga uliopo kuelekea ushindi. Hii inafikirisha, inaleta wasiwasi na kukatisha tamaa.
 
To be honest! Toka nisome ule waraka wa Baba Askofu Niyemugizi, nimekaa nikafikiria sana.

This is a defining moment, not only for our beloved country, but the whole world!

Kwa uhakika kabisa, viongozi walioenda kwenye kikombe cha babu, wasingeweza kukabiliana na janga ama acrisis kama hii!

Ni kweli kabisa kuwa watawala wetu wanatu reflect sisi wananchi wenyewe na kuna mtu huwa alikuwa anasema tusijilaumu na kutaka tupate viongozi walio tofauti na sisi.

Sasa dini na imani ndivyo vimeachwa vilivushe Taifa ambalo kwa kiasi kikubwa liko nyuma kwasababu ya mambo kama hayo! I am sad beyond words to explain!

Kwa kumalizia, niseme tu huko mbeleni, tutatambuwa tabia halisi za wanadamu nyakati za dhiki. Huwa wanasema ukweli wa mtu alivyo, huwa unaonekana wakati wa shida! Na pia ni nasema kuwa viongozi wa ukweli, watajulikana kipindi hiki cha mahangaiko na shida na taabu za wananchi!

Uzuri ama ubaya wa mtu, hufahamika wakati wa dhiki.

Ni wakati wa kufahamu huo ukweli, maana kuongoza siyo kukusanya kodi zetu pekee na kuzitumia unavyotaka!

Kuna mambo mengi tu ambayo Mungu atakuwa ameyaingilia kwa niaba ya watu walio wake.

Kama kuna wanaomuhubiri Mungu anayependa uonevu na ukatili, wajiandae. Hii ni kazi ya Mungu mwenyewe. Maana wenye macho hawakuona na wala wenye masikio hawakusikia!
 
Sina nia la kulaumu bali kushauri ili penye udhaifu pasahihishwe.

Nchi yetu na Afrika nzima huwezi kulinganisha na hayo mataifa uliyoyataja:

1) Mataifa hayo, kutokana na uwezo wa kiuchumi wa mtu mmoja mmoja, mwingiliano na mataifa mengine ni mkubwa maradufu ya Tanzania. Watu wetu hawasafiri kama watu wa mataifa hayo, kwa hiyo tulikuwa na nafasi ya kudhibiti maambukizi kabla ya kuingia au kabla ya kuingia.

2) Ugonjwa umeingia kwetu wakati tayari tunajua mengi kuhusiana na huu ugonjwa. Laiti sisi ndiyo tungekuwa stop ya pili baada ya China, na hayo mataifa yangekuwa stop ya tatu kama tulivyo sisi, hayo mataifa wasingeathirika kama tulivyoathirika sisi. Hakuna ugonjwa ulioanzia Afrika ambao uliwahi kuwa janga kwa Ulaya au America.

3) Sisi tumeshindwa kutumia nafasi ya ugonjwa kutoanzia kwenye bara letu la Afrika.
NATO(USA, Britain, Canada...) hizo nchi zenyewe zimeshindwa kudhibiti hilo janga.

Tuache kulaumiana mkuu...tufuate maelekezo ya madactari bhasi.

Hii kitu ni kama muziki mkuu lazima tuicheze...
 
Tufuate wataalamu wanachosema...tusiilaumu sana serikali...
Wataalam yawezekana wakatoa elimu nzuri lakini ili elimu hiyo iweze kuwafikia watu wote wenye uelewa wa aina mbalimbali, inahitaji sana nguvu ya serikali.

Serikali ndiyo inaweza kutoa msukumo mkubwa kwa yale wanayoyasema wataalam kuwafikia wananchi wote.

Serikali ndiyo inayoweza kuhakikisha kila taasisi, binafsi na za umma, zinatoa msukumo wa pekee kupambana na Corona. Serikali ikipuuza tatizo au ikataka kuendesha mapambano kwa usiri usiri, wote huko chini, ndivyo watakavyofanya.
 
To be honest! Toka nisome ule waraka wa Baba Askofu Niyemugizi, nimekaa nikafikiria sana.

This is a defining moment, not only for our beloved country, but the whole world!

Kwa uhakika kabisa, viongozi walioenda kwenye kikombe cha babu, wasingeweza kukabiliana na crisis Kama hii!

Ni kweli kabisa kuwa watawala wetu wanaya reflect sisi wananchi wenyewe na kuna mtu huwa alikuwa anasema tusijilaumu na kutaka tupate viongozi walio tofauti na sisi.

Sasa dini na imani ndivyo vimeachwa vilivushe Taifa ambalo kwa kiasi kikubwa liko nyuma kwasababu ya mambo kama hayo! I am sad beyond words to explain!
Mkuu watanzania wenye uwezo zaidi ya magu mbona tupo wengi tu, sema mfumo wetu wa kupata viongozi na siasa chafu zinazofanywa na CCM ndo zinatupatia hawa incompetent individuals
 
Bams, mimi nimefundishwa Crisis Management kwenye mafunzo yaliyotolewa na WARSAW PACT. Hayo yote uliyoyasema yapo Tanzania. Tatizo ni kule kukariri.
 
Bams, mimi nimefundishwa Crisis Management kwenye mafunzo yaliyotolewa na WARSAW PACT. Hayo yote uliyoyasema yapo Tanzania. Tatizo ni kule kukariri.
Unamaanisha watu wanakariri lakini hawaelewi ni wakati gani na kwa namna gani watumie mafunzo wanayopewa?
 
Unamaanisha watu wanakariri lakini hawaelewi ni wakati gani na kwa namna gani watumie mafunzo wanayopewa?
Hapana. Wewe ndio unafikiri kile ulichofundishwa ndio kifanyike vilevile kama copy and paste. Lakini kumbe inawezekana kufanyanyika tofauti tofauti kutokana na utofauti wa contexts.
 
Mkuu kuhusu kutoa taarifa ,usimlaumu Waziri wa Afya,Mbona MAKONDA yeye ndie msemaji wa Corona.
 
Hapana. Wewe ndio unafikiri kile ulichofundishwa ndio kifanyike vilevile kama copy and paste. Lakini kumbe inawezekana kufanyanyika tofauti tofauti kutokana na utofauti wa contexts.
Wewe ndiyo unapotosha; kwa maana hiyo unataka kusema Tanzania ndiyo inatumia best way kuliko nchi zote duniani? wewe umeona wapi nchi inapambana na ugonjwa wa mlipuko kama Corona inapita zaidi ya siku mbili bila taarifa kutoka kwa serikali?

Ummy Mwalimu waziri na Mama Samia Suluhu makamu wa rais wamehudumu kwenye ofisi ya mazingira kwa muda mrefu unadhani hawajui umuhimu wa kutoa taarifa kwa haraka na kwa wakati nyakati kama hizi?
Tatizo ni Mh Rais ambae anataka kila kitu mpaka aseme yes au no utafikiri anaongoza nchi kwa kufuata nyota na mashetani flani kama yule Roy Domnics aliyewahi kua kocha wa timu ya Ufaransa.
 
Hapana. Wewe ndio unafikiri kile ulichofundishwa ndio kifanyike vilevile kama copy and paste. Lakini kumbe inawezekana kufanyanyika tofauti tofauti kutokana na utofauti wa contexts.
Wewe ndiyo unapotosha; kwa maana hiyo unataka kusema Tanzania ndiyo inatumia best way kuliko nchi zote duniani? wewe umeona wapi nchi inapambana na ugonjwa wa mlipuko kama Corona inapita zaidi ya siku mbili bila taarifa kutoka kwa serikali?

Ummy Mwalimu waziri na Mama Samia Suluhu makamu wa rais wamehudumu kwenye ofisi ya mazingira kwa muda mrefu unadhani hawajui umuhimu wa kutoa taarifa kwa haraka na kwa wakati nyakati kama hizi?

Tatizo ni Mh Rais ambae anataka kila kitu mpaka aseme yes au no utafikiri anaongoza nchi kwa kufuata nyota na mashetani flani kama yule Roy Domnics aliyewahi kua kocha wa timu ya Ufaransa.
 
Back
Top Bottom