Serikalini; Utaratibu wa Ujenzi kwa Kutumia Force Account hauna Ufanisi ,turudi kutumia Wakandarasi

Opportunity Cost

JF-Expert Member
Dec 10, 2020
9,035
6,907
Habari zenu wanajamvi.

Serikali ya awamu ya Tano ilileta na Kuanzisha utaratibu wa ujenzi wa miradi mbalimbali kwa kutumia Force Account badala ya Wakandarasi kwa madai kwamba Force Account inapunguza gharama za ujenzi.

Lakini kwa hali ya kawaida wanaofanya makisio ya gharama za ujenzi yaani maximum ceiling price za miradi ni staff wa serikali sasa hiyo gharama kubwa ambayo inasemekana kuletwa na wakandarasi ni ipi?

Force Account ina hasara nyingi kuliko faida ambayo ni ya kusadikika,

1.Miradi kujengwa Chini ya kiwango.

Miradi mingi ya Force Account kama majengo,miradi ya maji nk imejengwa chini ya Kiwango bila kufuata viwango vya kihandisi.

Hapo awali miradi ya ujenzi ya serikali ilikuwa inajengwa kwa kufuata kanuni za kihandisi hivyo kuwa na ubora unostahili kiasi kwamba hata majanga yakitokea kama upepo,mafuriko na matetemeko inaweza kuhimili na kuwa kimbilio kwa wananchi.Lakini kwa sasa miradi mingi iko chini ya Kiwango na ujenzi wake umefanywa kienyeji kwa vile wanatumia local fundi na mtu yeyote ambae,yaani kila layman ni mtaalamu kwa sasa.

Kwa kutumia Force Account huwezi kuta quality control inafanyika kwa kutumia tests mbalimbali za kudhibiti ubora,wakati ukitumia wakandarasi udhibiti wa ubora unafanyika.

Yaani unavyojenga jengo lako huko mtaani ndivyo inafanyika.eg Hostel za Magufuli na expansion joint na Uhuru Hospital na ishu ya Lift.

2.Kukosesha serikali kodi na mapato.

Miradi karibu yote ya Force Account hailipiwi VAT na tozo nyingine kama tozo za Madini Ujenzi kwa sababu inafanywa na Serikali.

Kama miradi hii ingefanywa na wakandarasi, serikali ingepata VAT na kukusanya kodi mbalimbali na regulation na udhibiti mwingine ungefanyika vizuri.

3.Kupungua kwa ajira hasa za Wataalamu.

Ujenzi wa force Account umepunguza na kupoteza fursa za ajira hasa za Wataalamu kama wahandisi,technicians nk.Kwa sasa wanatumia wahandisi au layman wa taasisi husika kwa kushirikiana na mafundi mchungo.Kama Wakandarasi wangetymika inamaana ni takwa la kimkataba kutumia wataalamu wa fani husika kwenye ujenzi na hivyo ingepanua wigo kwa wasio na ajira mtaani kupata fursa.

4.Kuongezeka kwa wizi wa fedha za umma na urasimu wa kufanya maamuzi.

Kwa sasa watu wanaoitwa local fundi hawezi pata Kazi hadi awe amewekwa na wenye mradi,matokeo yake Ili fundi upate Kazi lazima uhonge au ukubali kutumika kama kipitisha fedha za wenye mradi.

Wanaojiita wahandisi huwa wanasubiri fundi akosee afu wamwambie afumue nae anajiongeza kwa kumpa mgao ilimradi kila mtu anakula kwa nafasi yake.

Yote haya yanawezekana kwa sababu kuna lundo la wasimamizi mara kamati,DED,DC,Afisa ugavi,Injinia,Wakuu wa Idara,Watendaji wa Kata na Vijiji na swkretariat hapo bado Diwani na watu wa Chama sasa matokeo yake miradi mingi iko chini ya Kiwango na kinachofanyika ni kufunika kombe mwanaharamu apite.

Afadhari kutumia Wakandarasi maana kama ni rushwa ni wakati wa kutafuta Kazi baada ya hapo kila mtu afe na mzigo wake kwa hiyo liability inabebwa na contractor ni rahisi kumbana but huko kwenye Force Account pesa ikitumika vibaya na ujenzi chini ya Kiwango inakuwa imetoka hiyo kinachobaki ni danadana.

5.Ujenzi kutokamilika kwa wakati.

Force Account inategemea uwepo wa pesa bila pesa kila kitu kinasimama na hivyo ujenzi huwa haukamiliki kwa wakati matokeo yake kuchelewa kwa huduma.

Ukitumia wakandarasi mara nyingi kama wamechaguliwa vizuri wanaweza kutumia mtaji wao wakabaki wanaidai serikali hivyo kuwahi kukamilika kwa miradi na huduma.Miradi inayochelewa ni ile mikubwa ya mabilioni ambayo mkandarasi anaanza kwa mtaji wake afu ndio serikali inatakiwa kitimiza wajibu wake.

Lakini vimiradi vya chini ya milioni 500 wakandarasi wanafanya vizuri kabisa na wanakuwa wameikopesha serikali.Walio vizuri zaidi wanaweza hata kukamilisha miradi ya mabilioni pia.

6.Risks na Liabilities kubebwa na Umma.

Ukitumia Force Account ni kwamba miradi ikiwa mibovu au kutokamilika kwa wakati mzigo wote unaangalia kwa umma,hakuna wa kumuwajibisha na ku claim.

Ukitumia mkandarasi mradi ukiwa chini ya Kiwango anarudia kwa gharama zake na pia uangalizi kwa mda fulani unakuwa juu yake.Akichelewesha mradi anakatwa pesa na kupokwa mradi kwa hiyo hasara kwa serikali inapungua kuliko kutumia Force Account.

Juu ya hilo usimamizi ni juu ya mkandarasi wataalamu wa serikali ni kuhakikisha quality control ambayo haifanywi ukitumia Force Account

WITO NA USHAURI.

Serikali irudishe utaratibu wa kutumia Wakandarasi ila tuu iimarishe sheria za manunuzi Ili mkandarasi mwenye uwezo na mtaji ndio afanye Kazi na wale wengine wanaweza kuungana .

Ishu ya gharama kubwa ni propaganda za wapigaji kwa mfano kwa sasa kujenga chumba 1 cha darasa kilichokamilika kwa force Account ni Tsh.25 m,,sasa ukiwa na package ya vyumba 4 ni mil.100,sasa mkandarasi gani atashindwa kuchukua tender hii?

Kama kuna ulazima wa kutumia Force Account basi watumie kwenye miradi ya ujenzi ambayo haizidi 50 mil.maana faida za kutumia mkandarasi ni kubwa kuliko Force Account.

Mwisho Ingefaa serikali ipeleke Tarura wizara ya ujenzi kama ilivyo Tanesco na REA.Juu ya hilo TBA wawepo kwenye kila Halmashauri badala ya ile idara ya Ujenzi Ili wasimamie ujenzi wote unaofanyika kwa ngazi hiyo.
 
Acha wivu wewe umetumwa na wakandarasi wenye makampuni wanaokosa kazi baada ya force account kuja. Mi ninesoma maelezo yako yote na yote siyo ya kweli. Mfano;

Umesema miradi kuwa chini ya kiwango, kwenye force account fundi anaetekeleza mradi lazima awe amepita veta na anasimamiwa na ma engineer wawili, muhandisi wa mradi na engineer wa wa taasisi kama vile engineer wa halimashauri ambae ni mkuu wa idara. Engineer wa mradi, anakaa badala ya engineer wa kampuni kwenye ukandarasi, tofauti huyu anakuwa mtumishi wa serikali. Sasa nikuulize yupi stasimamia ubora ni huyo unaemlipa kampuni au mwajiliwa wa serikali?
Fundi anaejenga ndiye yuleyule uliyekuwa unajenga kwenye makampuni tofauti hapa ni kwamba bosi ni yeye humtumi Tena kama zamani. Eti miradi inakuwa chini ya kiwango hayo magorofa yaliyokuwa yanaanguka kabla hata hayajakaa watu hayakujengwa na wakandarasi? Hizo barabara mbovu zinazokataliwa na serikali Kila siku zinajengwa na force account?

Eti force account hatulipi Kodi nani kakwambia? Tunalipa withholding tax 5% na tunakadiriwa Tena tunalipa Kodi ya mapato.tunalipa levi ya halimashauri nk.

Force akaunti imeongeza ajira kubwa mno na imepunguza unyonyaji wa wakandarasi Kwa mafundi. Sio kwelii kwamba imepunguza ajira, mfano Bado miradi mikubwa inafanywa na makampuni, barabara hazijengwi na force akount, Wala miradi mikubwa ya maji. Kwenye Hilo darasa Moja ambalo inaletwa mil 25 sisi tunajenga Kwa labour chaji ya mil 2, wakandarasi hawawezi kukubali, na wakikubali lazima wataichakachua cement na vifaa vingine ili wapate faida, tunajua mlivyokuwa mnachakachua cement, nondo nk, si sisi tulikuwa tunawajengea?

Ni mkandarasi gani alikuwa hahongi? Mnahonga kupata kazi, mnahonga eng mkaguzi, mnahonga kupitisha malipo nk.
Hivi kweli, local fundi awe ghali kuliko kampuni? Kampuni ikiomba kazi, inatakiwa kulipa wabia, ilipe enginia wa kampuni ilipe site for men, hawa wote hawashiki mwiko Wala nyundo ni mabwana wakubwa, sasa ikishalipa hao wakubwa Tena wanakula pakubwa ndiyo Kwa shida alipwe fundi, halafu na magharama yote hayo Bado eti m bid kuliko local fundi? Na Kwa taarifs yenu sasa hivi tumeshaunda chama Cha mafundi nchi nzima mkiua force account na sisi hatutawajengea mtapambana na Hali zenu.mtashika wenyewe Miko na makoleo wanyonyaji wakubwa nyie, mlikuwa mnalipwa mahela makubwa huku mna tulipa 10000, na msaidizi 5000 hivi mnaweza kuishi Kwa vihela hivyo? Sasa hivi tunajenga, bia tunakunywa wote na magari tunagombea parking. Magufuli mungu amlaze mahali pema peponi.

Kuhusu kumaliza mitlradinkwa wakati, force account inamaliza miradi kuliko wakandarasi angalieni hospitali za wilaya, vituo vya afya shule mpya, nyumba za waalimu,madarasa ya kovid nk vyote vimeisha Kwa wakati.

Ukweli ni kwamba force account ni nafuu kuliko kutumia mkandarasi, pia inaajili watu wengi zaidi, kikubwa zaidi inainua mafundi wa chini kimaisha na kupunguza umasikini Kwa wananchi.

Pamoja na mazuri yake zipo changamoto za kufanyia kazi na sio kuifuta. Baadhi ya changamoto ni :
(1) kupunguza ubora wa miradi Kwa sababu ya kukimbizana na muda uliowekwa. Mfano madarasa ya kovid yalitakiwa kujengwa ndani ya mwezi Moja kituambacho kitaalamu sio sawa, Kuna meneo kama zege yanahitaji muda wa kukomaa kabla ya kupandisha mzigo wa ukuta, sio chini ya siku 14, badala ya leo unsmwaga jamvi kesho unasnza ukuta. Lipu pia inahitaji siku za kukomaa kabla ya kusikimu, hata skimming I shitsji muda wa kukomaa kabla ya rangi na hasa wakati huu ambao tunatumia rangi za silk ambazo ni kama sticker hazipitishi hewa.

Ma engineer wafanye site supervision badala ya site visiting, engineer au technician awepo site muda wote ili kudhibiti ubora.

Mafundi walipwe mapema Kwa sababu hawana mitaji na mikataba Yao ni vigumu kupata mikopo bank.
 
Habari zenu wanajamvi.

Serikali ya awamu ya Tano ilileta na Kuanzisha utaratibu wa ujenzi wa miradi mbalimbali kwa kutumia Force Account badala ya Wakandarasi kwa madai kwamba Force Account inapunguza gharama za ujenzi.

Lakini kwa hali ya kawaida wanaofanya makisio ya gharama za ujenzi yaani maximum ceiling price za miradi ni staff wa serikali sasa hiyo gharama kubwa ambayo inasemekana kuletwa na wakandarasi ni ipi?

Force Account ina hasara nyingi kuliko faida ambayo ni ya kusadikika,

1.Miradi kujengwa Chini ya kiwango.

Miradi mingi ya Force Account kama majengo,miradi ya maji nk imejengwa chini ya Kiwango bila kufuata viwango vya kihandisi.

Hapo awali miradi ya ujenzi ya serikali ilikuwa inajengwa kwa kufuata kanuni za kihandisi hivyo kuwa na ubora unostahili kiasi kwamba hata majanga yakitokea kama upepo,mafuriko na matetemeko inaweza kuhimili na kuwa kimbilio kwa wananchi.Lakini kwa sasa miradi mingi iko chini ya Kiwango na ujenzi wake umefanywa kienyeji kwa vile wanatumia local fundi na mtu yeyote ambae,yaani kila layman ni mtaalamu kwa sasa.

Kwa kutumia Force Account huwezi kuta quality control inafanyika kwa kutumia tests mbalimbali za kudhibiti ubora,wakati ukitumia wakandarasi udhibiti wa ubora unafanyika.

Yaani unavyojenga jengo lako huko mtaani ndivyo inafanyika.eg Hostel za Magufuli na expansion joint na Uhuru Hospital na ishu ya Lift.

2.Kukosesha serikali kodi na mapato.

Miradi karibu yote ya Force Account hailipiwi VAT na tozo nyingine kama tozo za Madini Ujenzi kwa sababu inafanywa na Serikali.

Kama miradi hii ingefanywa na wakandarasi, serikali ingepata VAT na kukusanya kodi mbalimbali na regulation na udhibiti mwingine ungefanyika vizuri.

3.Kupungua kwa ajira hasa za Wataalamu.

Ujenzi wa force Account umepunguza na kupoteza fursa za ajira hasa za Wataalamu kama wahandisi,technicians nk.Kwa sasa wanatumia wahandisi au layman wa taasisi husika kwa kushirikiana na mafundi mchungo.Kama Wakandarasi wangetymika inamaana ni takwa la kimkataba kutumia wataalamu wa fani husika kwenye ujenzi na hivyo ingepanua wigo kwa wasio na ajira mtaani kupata fursa.

4.Kuongezeka kwa wizi wa fedha za umma na urasimu wa kufanya maamuzi.

Kwa sasa watu wanaoitwa local fundi hawezi pata Kazi hadi awe amewekwa na wenye mradi,matokeo yake Ili fundi upate Kazi lazima uhonge au ukubali kutumika kama kipitisha fedha za wenye mradi.

Wanaojiita wahandisi huwa wanasubiri fundi akosee afu wamwambie afumue nae anajiongeza kwa kumpa mgao ilimradi kila mtu anakula kwa nafasi yake.

Yote haya yanawezekana kwa sababu kuna lundo la wasimamizi mara kamati,DED,DC,Afisa ugavi,Injinia,Wakuu wa Idara,Watendaji wa Kata na Vijiji na swkretariat hapo bado Diwani na watu wa Chama sasa matokeo yake miradi mingi iko chini ya Kiwango na kinachofanyika ni kufunika kombe mwanaharamu apite.

Afadhari kutumia Wakandarasi maana kama ni rushwa ni wakati wa kutafuta Kazi baada ya hapo kila mtu afe na mzigo wake kwa hiyo liability inabebwa na contractor ni rahisi kumbana but huko kwenye Force Account pesa ikitumika vibaya na ujenzi chini ya Kiwango inakuwa imetoka hiyo kinachobaki ni danadana.

5.Ujenzi kutokamilika kwa wakati.

Force Account inategemea uwepo wa pesa bila pesa kila kitu kinasimama na hivyo ujenzi huwa haukamiliki kwa wakati matokeo yake kuchelewa kwa huduma.

Ukitumia wakandarasi mara nyingi kama wamechaguliwa vizuri wanaweza kutumia mtaji wao wakabaki wanaidai serikali hivyo kuwahi kukamilika kwa miradi na huduma.Miradi inayochelewa ni ile mikubwa ya mabilioni ambayo mkandarasi anaanza kwa mtaji wake afu ndio serikali inatakiwa kitimiza wajibu wake.

Lakini vimiradi vya chini ya milioni 500 wakandarasi wanafanya vizuri kabisa na wanakuwa wameikopesha serikali.Walio vizuri zaidi wanaweza hata kukamilisha miradi ya mabilioni pia.

6.Risks na Liabilities kubebwa na Umma.

Ukitumia Force Account ni kwamba miradi ikiwa mibovu au kutokamilika kwa wakati mzigo wote unaangalia kwa umma,hakuna wa kumuwajibisha na ku claim.

Ukitumia mkandarasi mradi ukiwa chini ya Kiwango anarudia kwa gharama zake na pia uangalizi kwa mda fulani unakuwa juu yake.Akichelewesha mradi anakatwa pesa na kupokwa mradi kwa hiyo hasara kwa serikali inapungua kuliko kutumia Force Account.

Juu ya hilo usimamizi ni juu ya mkandarasi wataalamu wa serikali ni kuhakikisha quality control ambayo haifanywi ukitumia Force Account

WITO NA USHAURI.

Serikali irudishe utaratibu wa kutumia Wakandarasi ila tuu iimarishe sheria za manunuzi Ili mkandarasi mwenye uwezo na mtaji ndio afanye Kazi na wale wengine wanaweza kuungana .

Ishu ya gharama kubwa ni propaganda za wapigaji kwa mfano kwa sasa kujenga chumba 1 cha darasa kilichokamilika kwa force Account ni Tsh.25 m,,sasa ukiwa na package ya vyumba 4 ni mil.100,sasa mkandarasi gani atashindwa kuchukua tender hii?

Kama kuna ulazima wa kutumia Force Account basi watumie kwenye miradi ya ujenzi ambayo haizidi 50 mil.maana faida za kutumia mkandarasi ni kubwa kuliko Force Account.

Mwisho Ingefaa serikali ipeleke Tarura wizara ya ujenzi kama ilivyo Tanesco na REA.Juu ya hilo TBA wawepo kwenye kila Halmashauri bdala ya ile idara ya Ujenzi Ili wasimamie ujenzi wote unaofanyika kwa ngazi hiyo.
Force account ililetwa na raisi JUHA a
 
Miradi ya kujengwa na wakandarasi ambayo itakuwa na ubora ni ile ya makampuni ya kimataifa tu basi.Lakini eti sijui wakandarasi wa ndani,hao ni wababaishaji hakuna mfano.Kazi zinafanyika kwa kusua sua sana,ubora mpaka unajiuliza hivi hapa kuna mhandisi au kilaza mmoja hivi.Alafu mara nyingi,wanatoa sana rushwa hivyo ubora wa mradi unashuka mno.
 
Majengo mengi ya umma yaliyojengwa karibuni yanavuja balaa. Niliingia jengo moja la hospital ile gypsum imeloa hadi inashangaza juu ya utashi wa mafundi waliotumika kujenga majengo muhimu kama yale.
 
Watu wanapotekeleza mradinkwa kutumia force account.Hawajenhi tu kama wanavyoyaka,wanatumia specifications zilizotolewa na wahandisi.Shida wahandisi wetu,wamekariri.Lazima ukuta uskim na white cement,lazima uweke gypsum,lazima uweke tiles.Ila hawatoi indepth echnicalities za kufanya hayo.
Alafu wamekariri tu,wanavyofanya mtaano wao wanahamisha hivyo hivyo.
Wao wamejikita sana kwenye manondo na simenti yawe mengi basi.
 
Back
Top Bottom