Serikalini ndiko unaweza kupata mshahara bila kufikiri sana

Mdanganywa

JF-Expert Member
Jun 15, 2009
620
342
Ninasoma gazeti la RAIA MWEMA la leo, uk. 09 kwenye RAI YA GENERALI ULIMWENGU nimekutana na sentensi anasema hivi"

"Mtu anayeshindwa kuhoji si mwandishi wa habari, anastahili aache kujiita hivyo na aende akatafute kazi katika idara ya serikali, kwani huko ndiko unaweza kupata mshahara bila kufikiri sana; Inakuja amri "fungia huyo", na hutaki kujua hasa ni kwa nini unafungia, unafungia tu, basi": {Generali Ulimwengu: RAIA MWEMA: June 21, 2017, pg. 09}.

Jadili
 
Kwenye nchi za kidkteta hutarajiwi kuhoji chochote zaidi ya kutii amri za 'Bwana Mkubwa'

Pia Jenerali angeongeza na ubunge wa CCM pia huihutaji kufikiri chochote zaidi ya kuitikia ndiyoooo kwenye hoja za chama chako

Kwani Kibajaji anaweza kufikiri nini?
 
Ni serikalini pekee muda wa kunywa chai ni masaa 3, lunch masaa 3 yanayobaki ni kupita makoridoni na kusoma magazeti!siku imeisha na bado raia ataambiwa aje kesho faili halionekani au niko bize:D:D:D:D:D:D:D:D:D
Mna raha sana mnaofanya Kazi huko serikalini ndio maana wengi wenu huwa mnaridhika na mishaara dhoofu sababu hamfanyi kazi
 
Kwenye nchi za kidkteta hutarajiwi kuhoji chochote zaidi ya kutii amri za 'Bwana Mkubwa'

Pia Jenerali angeongeza na ubunge wa CCM pia huihutaji kufikiri chochote zaidi ya kuitikia ndiyoooo kwenye hoja za chama chako

Kwani Kibajaji anaweza kufikiri nini?
Yes
 
aniombe radhi sn, niko serikalini na mshahara wangu naupata kwa kutumia nguvu ningi sn za kufikiri....kwani natakiwa kila mwezi nionyeshe nimefanya nini ktk kuongeza ufanisi,..la sivyo nitumbuliwe!

nataman ningekuwa mwandishi kwani kwangu naona kwa sasa ndio kz rahisi mno; ni kucheza na akili za mambumbumbu wa tz tu km wafanyavyo wasanii basi ambao kz yao ni kushangilia matukio ya kimbea tu...ulimwengu ana kazi rahisi kuliko mimi!!!
 
Ninasoma gazeti la RAIA MWEMA la leo, uk. 09 kwenye RAI YA GENERALI ULIMWENGU nimekutana na sentensi anasema hivi"

"Mtu anayeshindwa kuhoji si mwandishi wa habari, anastahili aache kujiita hivyo na aende akatafute kazi katika idara ya serikali, kwani huko ndiko unaweza kupata mshahara bila kufikiri sana; Inakuja amri "fungia huyo", na hutaki kujua hasa ni kwa nini unafungia, unafungia tu, basi": {Generali Ulimwengu: RAIA MWEMA: June 21, 2017, pg. 09}.

Jadili

Kwani wewe General Ulimwengu akisema kitu ndo basi?? Kwani vitu vyote vinavyofanywa na serikali havifai?? Mbona huyo Ulimwengu naye alikuwa serikalini na bado hata leo akipewa nafasi serikalini atashangilia kwa sana tu. Wakati mwingine tumieni akili zetu siyo kila kitu wanachosema hao wakina Ulimwengu mnafikiri ni sawa. Kwa taarifa yako watu wote wenye akili za kujitambua lazima wameajiriwa na serikali!! Unaweza ukamuona anafanyakazi private lakini mwajiriwa wa serikali. Wakati mwingine mjitambue!!
 
Kwani wewe General Ulimwengu akisema kitu ndo basi?? Kwani vitu vyote vinavyofanywa na serikali havifai?? Mbona huyo Ulimwengu naye alikuwa serikalini na bado hata leo akipewa nafasi serikalini atashangilia kwa sana tu. Wakati mwingine tumieni akili zetu siyo kila kitu wanachosema hao wakina Ulimwengu mnafikiri ni sawa. Kwa taarifa yako watu wote wenye akili za kujitambua lazima wameajiriwa na serikali!! Unaweza ukamuona anafanyakazi private lakini mwajiriwa wa serikali. Wakati mwingine mjitambue!!

Hoja za kizamani kwelikweli,

Unadhani hizi ni enzi za za kubabaisha watu kwa kuwatishia kwamba serikali fulani ina mkono mrefu hivyo jichunge unapoongea huko makazini.

Hao unaosema ni waserikali lakini wako private ndiyo wanapiga miayo kila leo, njaa tupu, uvivu tupu.

Sisi hatumuamini Ulimwengu. Ulimwengu ni msemaji wa tatizo lililopo. Jamaa mu wavivu hadi inaudhi.
 
Mfumo WA serikalini unaomsababishia Mtumishi WA umma aonekane hachapi kazi Mara nyingi husababishwa na Serikali yenyewe Kwani kutompatia mtumishi Huyo rasilimali zinazomwezesha kutimiza majukumu kwa wakati ipasavyo hakuwezi kumfanye Huyu mtumishi aonekane anafanya yake kwa ufasaha, tofauti na private Kwenye kila kitu, kuhusiana Na mtumishi kuwa mvivu huo Ni udhaifu wake binafsi
 
Hoja za kizamani kwelikweli,

Unadhani hizi ni enzi za za kubabaisha watu kwa kuwatishia kwamba serikali fulani ina mkono mrefu hivyo jichunge unapoongea huko makazini.

Hao unaosema ni waserikali lakini wako private ndiyo wanapiga miayo kila leo, njaa tupu, uvivu tupu.

Sisi hatumuamini Ulimwengu. Ulimwengu ni msemaji wa tatizo lililopo. Jamaa mu wavivu hadi inaudhi.
Nonsense comments. Huna chochote cha maana mbona ndio wanakuongoza mpaka sasa hivi?? Utabaki kulalama tu wakati uko chini yao. Acha kuwa mvivu wa kufikiri.
 
Nonsense comments. Huna chochote cha maana mbona ndio wanakuongoza mpaka sasa hivi?? Utabaki kulalama tu wakati uko chini yao. Acha kuwa mvivu wa kufikiri.

Walioko chini yao ni majambazi na mafisadi. mtu safi kama mimi hawajawahi kuniongoza na wala siwahitaji maana hawana watakachotaka kwangu au kupata kwangu. Hivyo ninajiongoza sijawahi kuongozwa. Labda wanakuongoza wewe.
 
Back
Top Bottom