Serikali yazuia wanachama wa NHIF kwenda kuchukua dawa maduka ya nje kwa kufuta matumizi ya form 2c

tutafikatu

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
3,232
4,448
Kuna waraka umetolewa na Wizara ya Afya, ukitoa taarifa kwamba kuanzia tarehe 01 Juni 2022 hatua kwa hatua kutasitishwa matumizi ya form 2c. Form 2c ni fomu inayotumika na hospitali zinazohudumia wagonjwa wa NHIF kujaza dawa zisizokuwepo hospitali, ili mgonjwa au ndugu wa mgonjwa akachukue dawa husika kwenye maduka binafsi (mengine yako nje ya hospitali ila yanamilikiwa na hospitali husika au serikali) nje ya hospitali.

Maduka haya ya dawa, huingia mikataba ya kisheria na NHIF ya kutoa huduma kwa wateja wao. Ingawa waraka huu unasitisha utoaji wa form 2c kwa vituo vyote vya afya hata binafsi, ukweli malengo makuu ni hospitali za Serikali, lakini kwa sababu form 2c zinatumika na hospitali zote zilizoingia makubaliano na NHIF kutoa huduma kwa wanachama wake, hivyo imebidi tu nazo wazihusishe.

Huu ni uamuzi wenye faida na hasara. Binafsi kama mfamasia naamini kuna hasara zaidi. Ukisoma waraka huu unaweza gundua mambo kadhaa hasi toka Serikali kwa watumishi wake wa afya na maduka ya dawa.

Mtazamo wa Serikali
  1. Kwamba watumishi wa hospitali wanafanya makusudi kuhakikisha hospitali zao zinakosa dawa zote ili kutoa mwanya kwa maduka ya dawa yaliyopo nje ya hospitali kufanya biashara
  2. Kwamba maduka ya dawa binafsi ni chanzo cha dawa kukosekana ndani ya hospitali.
  3. Kwamba maduka ya dawa yanapata faida kubwa ambayo ilipaswa iingie ndani ya mifuko ya hospitali na kuzisaidia hospitali kujiendesha.
  4. Kwamba kukosekana kwa dawa kunasababisha usumbufu mkubwa kwa wagonjwa
  5. Kwamba tatizo la kukosekana kwa dawa linaweza tatuliwa mara moja kwa kutoa mikopo kwa vituo hivi vya afya ili viweze nunua dawa za kutosha kuwafanya wateja wao wasiende kuchukua dawa nje ya hospitali.
  6. Kwamba hospitali inaweza kuwa na dawa zote zilizopo kwenye soko, bila kujali sababu zinazochangia manunuzi kama uhitaji wa mara kwa mara n.k.
  7. Kwamba ubora wa dawa unafanana, hakuna nia ya kuwa na alternative brand
  8. Kwamba serikali yenyewe ipo juu ya mikono ya sheria na inaweza vunja mikataba waliyoingia NHIF na maduka ya madawa bila kuwa na madhara yoyote.
Serikali inasahau
  1. Kuwa imekuwa ikitoa bajeti hewa za dawa.
  2. Kwamba asilimia 99 ya matatizo ya ukosefu wa dawa inayasabisha yenyewe na sheria zake za manunuzi
  3. Kwamba serikali huwa haikiri mapungufu yake katika kuchangia upatikanaji wa dawa endelevu ndani ya vituo
  4. Imewaambia MSD kama hospitali zake zimeenda kununua dawa na dawa huziko hazipo, basi itabidi wajieleze kwa nini dawa husika hazipo, na hii kuifanya MSD kutotoa vibali vya out of stock ili kuruhusu hizi hospitali za Serikali kwenda kununua dawa kwa washitiri na kuendelea kutoa huduma.
  5. Inasingizia sana upotevu wa dawa kama ni chanzo kikubwa cha dawa kutokuwapo hospitalini.
  6. Kwamba Serikali malengo yake makuu ni kusimamia utoaji huduma bora za afya na si kutengeneza ushindani na maduka ya dawa.
  7. Kwamba Serikali yenyewe haifanyi biashara kwenye afya, ndio maana, mishahara ya watumishi wa afya inatoka kwenye kapu kuu, ila hawa wenye maduka mishahara yao inatoka kwenye mauzo hayo hayo yatokayo kwenye maduka
  8. Haya maduka ya dawa yaliingia mikataba ya kisheria na NHIF kutoa dawa
  9. Kwamba watapoteza ajira katika sekta binafsi.

Nini kitatokea
  1. Hakuna hospitali itaweza kuwa na dawa zote, hakuna. Kama itaweza basi kuna dawa nyingi zita expire, kwa sababu ama zina shelf life fupi au zina matumizi madogo.
  2. Wagonjwa wengi wataanza malalamiko pale watakapokuwa wanasubirishwa kupata dawa wanayotaka wao ambayo haipo hospitali (maana hospitali itabidi ikanunue dawa haraka ili kumpa mgonjwa husika.
  3. Wizara itashindwa vibaya na kurejesha utaratibu wa nyuma

Maoni
  1. Serikali isiwaonee donge wenye maduka ya dawa, kama inaona wanapata faida kubwa isimamie na kurekebisha sheria zake za manunuzi, na kuondoa vyanzo vya ukosefu wa dawa katika vituo vyake. Hii tu itaondoa maduka ya dawa.
  2. Serikali iondoe imani ya kuwa sekta binafsi ni mshindani, wakati huohuo inataka mamilioni ya Watanzania wajiajiri wenyewe.
  3. Watumishi waliopo wizarani wawe na historia ya kufanya kazi vituo vya afya, kuna watu toka waanze kazi wapo kwenye uongozi, hawajui jinsi vitu viendeshwavyo mahospitalini na bado wanapewa nafasi za kufanya maamuzi magumu kuhusu hospitali.
  4. Serikali ifanye maamuzi kwa kuonesha inaheshimu sheria kwa kupitia mikataba iliyopo kabla ya kufanya maamuzi makubwa. Kutojali huku kumefanya tuwe wahanga hasa kwenye mikataba ya kimataifa
Screenshot_20220528-104958_Google PDF Viewer.png

Screenshot_20220528-105007_Google PDF Viewer.png

Screenshot_20220528-105012_Google PDF Viewer.png

Pia soma > Serikali yasitisha matumizi ya Fomu ya 2C inayotumika kuchukua dawa maduka ya nje
 
Asante sana. Umeelezea kitaalam sana na nadhani serikali inatakiwa isikilize wadau muhimu kama ninyi kabla ya kukurupuka. Mengi iliyosema ni kweli. Hakuna duka lenye uwezo wa kuwa na kila aina ya dawa na wakifanya hivi kwa eg sehemu za hospital ni hasara kuliko faida.
 
Kuna waraka umetolewa na Wizara ya Afya, ukitoa taarifa kwamba kuanzia tarehe 01 Juni 2022 hatua kwa hatua kutasitishwa matumizi ya form 2c. Form 2c ni fomu inayotumika na hospitali zinazohudumia wagonjwa wa NHIF kujaza dawa zisizokuwepo hospitali, ili mgonjwa au ndugu wa mgonjwa akachukue dawa husika kwenye maduka binafsi (mengine yako nje ya hospitali ila yanamilikiwa na hospitali husika au serikali) nje ya hospitali. Maduka haya ya dawa, huingia mikataba ya kisheria na NHIF ya kutoa huduma kwa wateja wao. Ingawa waraka huu unasitisha utoaji wa form 2c kwa vituo vyote vya afya hata binafsi, ukweli malengo makuu ni hospitali za serikali, lakini kwa sababu form 2c zinatumika na hospitali zote zilizoingia makubaliano na NHIF kutoa huduma kwa wanachama wake, hivyo imebidi tu nazo wazihusishe.

Huu ni uamuzi wenye faida na hasara. Binafsi kama mfamasia naamini kuna hasara zaidi. Ukisoma waraka huu unaweza gundua mambo kadhaa hasi toka serikali kwa watumishi wake wa afya na maduka ya dawa.

Mtazamo wa serikali

  1. Kwamba watumishi wa hospitali wanafanya makusudi kuhakikisha hospitali zao zinakosa dawa zote ili kutoa mwanya kwa maduka ya dawa yaliyopo nje ya hospitali kufanya biashara
  2. Kwamba maduka ya dawa binafsi ni chanzo cha dawa kukosekana ndani ya hospitali.
  3. Kwamba maduka ya dawa yanapata faida kubwa ambayo ilipaswa iingie ndani ya mifuko ya hospitali na kuzisaidia hospitali kujiendesha.
  4. Kwamba kukosekana kwa dawa kunasababisha usumbufu mkubwa kwa wagonjwa
  5. Kwamba tatizo la kukosekana kwa dawa linaweza tatuliwa mara moja kwa kutoa mikopo kwa vituo hivi vya afya ili viweze nunua dawa za kutosha kuwafanya wateja wao wasiende kuchukua dawa nje ya hospitali.
  6. Kwamba hospitali inaweza kuwa na dawa zoote zilizopo kwenye soko, bila kujali sababu zinazochangia manunuzi kama uhitaji wa mara kwa mara n.k.
  7. Kwamba ubora wa dawa unafanana, hakuna nia ya kuwa na alternative brand
  8. Kwamba serikali yenyewe ipo juu ya mikono ya sheria na inaweza vunja mikataba waliyoingia NHIF na maduka ya madawa bila kuwa na madhara yoyote.
Serikali inasahau
  1. Kuwa imekuwa ikitoa bajeti hewa za dawa.
  2. Kwamba asilimia 99 ya matatizo ya ukosefu wa dawa inayasabisha yenyewe na sheria zake za manunuzi
  3. Kwamba serikali huwa haikiri mapungufu yake katika kuchangia upatikanaji wa dawa endelevu ndani ya vituo
  4. Imewaambia MSD kama hospitali zake zimeenda kununua dawa na dawa huziko hazipo, basi itabidi wajieleze kwanini dawa husika hazipo, na hii kuifanya MSD kutotoa vibali vya out of stock ili kuruhusu hizi hospitali za serikali kwenda kununua dawa kwa washitiri na kuendelea kutoa huduma
  5. Inasingizia sana upotevu wa dawa kama ni chanzo kikubwa cha dawa kutokuwapo hospitalini.
  6. Kwamba serikali malengo yake makuu ni kusimamia utoaji huduma bora za afya na si kutengeneza ushindani na maduka ya dawa.
  7. Kwamba serikali yenyewe haifanyi biashara kwenye afya, ndio maana, mishahara ya watumishi wa afya inatoka kwenye kapu kuu, ila hawa wenye maduka mishahara yao inatoka kwenye mauzo hayo hayo yatokayo kwenye maduka
  8. Haya maduka ya dawa yaliingia mikataba ya kisheria na NHIF kutoa dawa
  9. Kwamba watapoteza ajira katika sekta binafsi.

Nini kitatokea
  1. Hakuna hospitali itaweza kuwa na dawa zote, hakuna. Kama itaweza basi kuna dawa nyingi zita expire, kwa sababu ama zina shelf life fupi au zina matumizi madogo.
  2. Wagonjwa wengi wataanza malalamiko pale watakapokuwa wanasubirishwa kupata dawa wanayotaka wao ambayo haipo hospitali (maana hospitali itabidi ikanunue dawa haraka ili kumpa mgonjwa husika.
  3. Wizara itashindwa vibaya na kurejesha utaratibu wa nyuma

Maoni
  1. Serikali isiwaonee donge wenye maduka ya dawa, kama inaona wanapata faida kubwa isimamie na kurekebisha sheria zake za manunuzi, na kuondoa vyanzo vya ukosefu wa dawa katika vituo vyake. Hii tu itaondoa maduka ya dawa.
  2. Serikali iondoe imani ya kuwa sekta binafsi ni mshindani, wakati huo huo inataka mamilioni ya watanzania wajiajiri wenyewe.
  3. Watumishi waliopo wizarani wawe na historia ya kufanya kazi vituo vya afya, kuna watu toka waanze kazi wapo kwenye uongozi, hawajui jinsi vitu viendeshwavyo mahospitalini na bado wanapewa nafasi za kufanya maamuzi magumu kuhusu hospitali
  4. Serikali ifanye maamuzi kwa kuonesha inaheshimu sheria kwa kupitia mikataba iliyopo kabla ya kufanya maamuzi makubwa. Kutojali huku kumefanya tuwe wahanga hasa kwenye mikataba ya kimataifa
View attachment 2241985
View attachment 2241986
View attachment 2241987
Hii nchi ni ya ajabu sana. Matatizo yao ya utawala wana yarudisha kwa wananchi kuwapa shida.
Kwa mfano tatizo la mafuta ya kula ni ujinga na uzembe wa vyombo vya serikali kushindwa kuzuia waingizaji wa mafuta ghafi eitha kwa kutokuweza kugundua au kupitisha kwa ajili ya hongo. Serikali ikaona dawa ni kuongeza kodi mafuta ghafi na wabunge wetu vipofu wakapitisha kuwa sheria. Huu ni upuuzi wa hali ya kiwango cha lami.
Mwisho wa siku wananchi tunauziwa nafuta ya kupikia tshs 9000/ kwa lita. Mawazo mgando.
Sasa wanakuja na sheria za kuzuia kununua dawa kwa NHIF maduka ya nje. Je? Kama maduka ya serikali hiyo dawa haipo tufe????
Huu ni upuuzi mwingine wa mawazo mgando. Serikali iwajibike kwa wananchi wake. Kama kuna watumishi wasio waadilifu hao ndio wa kuondoa na sio kututesa.
 
Kuna waraka umetolewa na Wizara ya Afya, ukitoa taarifa kwamba kuanzia tarehe 01 Juni 2022 hatua kwa hatua kutasitishwa matumizi ya form 2c. Form 2c ni fomu inayotumika na hospitali zinazohudumia wagonjwa wa NHIF kujaza dawa zisizokuwepo hospitali, ili mgonjwa au ndugu wa mgonjwa akachukue dawa husika kwenye maduka binafsi (mengine yako nje ya hospitali ila yanamilikiwa na hospitali husika au serikali) nje ya hospitali.

Maduka haya ya dawa, huingia mikataba ya kisheria na NHIF ya kutoa huduma kwa wateja wao. Ingawa waraka huu unasitisha utoaji wa form 2c kwa vituo vyote vya afya hata binafsi, ukweli malengo makuu ni hospitali za Serikali, lakini kwa sababu form 2c zinatumika na hospitali zote zilizoingia makubaliano na NHIF kutoa huduma kwa wanachama wake, hivyo imebidi tu nazo wazihusishe.

Huu ni uamuzi wenye faida na hasara. Binafsi kama mfamasia naamini kuna hasara zaidi. Ukisoma waraka huu unaweza gundua mambo kadhaa hasi toka Serikali kwa watumishi wake wa afya na maduka ya dawa.

Mtazamo wa Serikali
  1. Kwamba watumishi wa hospitali wanafanya makusudi kuhakikisha hospitali zao zinakosa dawa zote ili kutoa mwanya kwa maduka ya dawa yaliyopo nje ya hospitali kufanya biashara
  2. Kwamba maduka ya dawa binafsi ni chanzo cha dawa kukosekana ndani ya hospitali.
  3. Kwamba maduka ya dawa yanapata faida kubwa ambayo ilipaswa iingie ndani ya mifuko ya hospitali na kuzisaidia hospitali kujiendesha.
  4. Kwamba kukosekana kwa dawa kunasababisha usumbufu mkubwa kwa wagonjwa
  5. Kwamba tatizo la kukosekana kwa dawa linaweza tatuliwa mara moja kwa kutoa mikopo kwa vituo hivi vya afya ili viweze nunua dawa za kutosha kuwafanya wateja wao wasiende kuchukua dawa nje ya hospitali.
  6. Kwamba hospitali inaweza kuwa na dawa zote zilizopo kwenye soko, bila kujali sababu zinazochangia manunuzi kama uhitaji wa mara kwa mara n.k.
  7. Kwamba ubora wa dawa unafanana, hakuna nia ya kuwa na alternative brand
  8. Kwamba serikali yenyewe ipo juu ya mikono ya sheria na inaweza vunja mikataba waliyoingia NHIF na maduka ya madawa bila kuwa na madhara yoyote.
Serikali inasahau
  1. Kuwa imekuwa ikitoa bajeti hewa za dawa.
  2. Kwamba asilimia 99 ya matatizo ya ukosefu wa dawa inayasabisha yenyewe na sheria zake za manunuzi
  3. Kwamba serikali huwa haikiri mapungufu yake katika kuchangia upatikanaji wa dawa endelevu ndani ya vituo
  4. Imewaambia MSD kama hospitali zake zimeenda kununua dawa na dawa huziko hazipo, basi itabidi wajieleze kwa nini dawa husika hazipo, na hii kuifanya MSD kutotoa vibali vya out of stock ili kuruhusu hizi hospitali za Serikali kwenda kununua dawa kwa washitiri na kuendelea kutoa huduma.
  5. Inasingizia sana upotevu wa dawa kama ni chanzo kikubwa cha dawa kutokuwapo hospitalini.
  6. Kwamba Serikali malengo yake makuu ni kusimamia utoaji huduma bora za afya na si kutengeneza ushindani na maduka ya dawa.
  7. Kwamba Serikali yenyewe haifanyi biashara kwenye afya, ndio maana, mishahara ya watumishi wa afya inatoka kwenye kapu kuu, ila hawa wenye maduka mishahara yao inatoka kwenye mauzo hayo hayo yatokayo kwenye maduka
  8. Haya maduka ya dawa yaliingia mikataba ya kisheria na NHIF kutoa dawa
  9. Kwamba watapoteza ajira katika sekta binafsi.

Nini kitatokea
  1. Hakuna hospitali itaweza kuwa na dawa zote, hakuna. Kama itaweza basi kuna dawa nyingi zita expire, kwa sababu ama zina shelf life fupi au zina matumizi madogo.
  2. Wagonjwa wengi wataanza malalamiko pale watakapokuwa wanasubirishwa kupata dawa wanayotaka wao ambayo haipo hospitali (maana hospitali itabidi ikanunue dawa haraka ili kumpa mgonjwa husika.
  3. Wizara itashindwa vibaya na kurejesha utaratibu wa nyuma

Maoni
  1. Serikali isiwaonee donge wenye maduka ya dawa, kama inaona wanapata faida kubwa isimamie na kurekebisha sheria zake za manunuzi, na kuondoa vyanzo vya ukosefu wa dawa katika vituo vyake. Hii tu itaondoa maduka ya dawa.
  2. Serikali iondoe imani ya kuwa sekta binafsi ni mshindani, wakati huohuo inataka mamilioni ya Watanzania wajiajiri wenyewe.
  3. Watumishi waliopo wizarani wawe na historia ya kufanya kazi vituo vya afya, kuna watu toka waanze kazi wapo kwenye uongozi, hawajui jinsi vitu viendeshwavyo mahospitalini na bado wanapewa nafasi za kufanya maamuzi magumu kuhusu hospitali.
  4. Serikali ifanye maamuzi kwa kuonesha inaheshimu sheria kwa kupitia mikataba iliyopo kabla ya kufanya maamuzi makubwa. Kutojali huku kumefanya tuwe wahanga hasa kwenye mikataba ya kimataifa
View attachment 2241985
View attachment 2241986
View attachment 2241987
Kwanza bei ya dawa kwa hospital za serikali ni mara mbili ya hospital binafsi.
 
Kuna waraka umetolewa na Wizara ya Afya, ukitoa taarifa kwamba kuanzia tarehe 01 Juni 2022 hatua kwa hatua kutasitishwa matumizi ya form 2c. Form 2c ni fomu inayotumika na hospitali zinazohudumia wagonjwa wa NHIF kujaza dawa zisizokuwepo hospitali, ili mgonjwa au ndugu wa mgonjwa akachukue dawa husika kwenye maduka binafsi (mengine yako nje ya hospitali ila yanamilikiwa na hospitali husika au serikali) nje ya hospitali.

Maduka haya ya dawa, huingia mikataba ya kisheria na NHIF ya kutoa huduma kwa wateja wao. Ingawa waraka huu unasitisha utoaji wa form 2c kwa vituo vyote vya afya hata binafsi, ukweli malengo makuu ni hospitali za Serikali, lakini kwa sababu form 2c zinatumika na hospitali zote zilizoingia makubaliano na NHIF kutoa huduma kwa wanachama wake, hivyo imebidi tu nazo wazihusishe.

Huu ni uamuzi wenye faida na hasara. Binafsi kama mfamasia naamini kuna hasara zaidi. Ukisoma waraka huu unaweza gundua mambo kadhaa hasi toka Serikali kwa watumishi wake wa afya na maduka ya dawa.

Mtazamo wa Serikali
  1. Kwamba watumishi wa hospitali wanafanya makusudi kuhakikisha hospitali zao zinakosa dawa zote ili kutoa mwanya kwa maduka ya dawa yaliyopo nje ya hospitali kufanya biashara
  2. Kwamba maduka ya dawa binafsi ni chanzo cha dawa kukosekana ndani ya hospitali.
  3. Kwamba maduka ya dawa yanapata faida kubwa ambayo ilipaswa iingie ndani ya mifuko ya hospitali na kuzisaidia hospitali kujiendesha.
  4. Kwamba kukosekana kwa dawa kunasababisha usumbufu mkubwa kwa wagonjwa
  5. Kwamba tatizo la kukosekana kwa dawa linaweza tatuliwa mara moja kwa kutoa mikopo kwa vituo hivi vya afya ili viweze nunua dawa za kutosha kuwafanya wateja wao wasiende kuchukua dawa nje ya hospitali.
  6. Kwamba hospitali inaweza kuwa na dawa zote zilizopo kwenye soko, bila kujali sababu zinazochangia manunuzi kama uhitaji wa mara kwa mara n.k.
  7. Kwamba ubora wa dawa unafanana, hakuna nia ya kuwa na alternative brand
  8. Kwamba serikali yenyewe ipo juu ya mikono ya sheria na inaweza vunja mikataba waliyoingia NHIF na maduka ya madawa bila kuwa na madhara yoyote.
Serikali inasahau
  1. Kuwa imekuwa ikitoa bajeti hewa za dawa.
  2. Kwamba asilimia 99 ya matatizo ya ukosefu wa dawa inayasabisha yenyewe na sheria zake za manunuzi
  3. Kwamba serikali huwa haikiri mapungufu yake katika kuchangia upatikanaji wa dawa endelevu ndani ya vituo
  4. Imewaambia MSD kama hospitali zake zimeenda kununua dawa na dawa huziko hazipo, basi itabidi wajieleze kwa nini dawa husika hazipo, na hii kuifanya MSD kutotoa vibali vya out of stock ili kuruhusu hizi hospitali za Serikali kwenda kununua dawa kwa washitiri na kuendelea kutoa huduma.
  5. Inasingizia sana upotevu wa dawa kama ni chanzo kikubwa cha dawa kutokuwapo hospitalini.
  6. Kwamba Serikali malengo yake makuu ni kusimamia utoaji huduma bora za afya na si kutengeneza ushindani na maduka ya dawa.
  7. Kwamba Serikali yenyewe haifanyi biashara kwenye afya, ndio maana, mishahara ya watumishi wa afya inatoka kwenye kapu kuu, ila hawa wenye maduka mishahara yao inatoka kwenye mauzo hayo hayo yatokayo kwenye maduka
  8. Haya maduka ya dawa yaliingia mikataba ya kisheria na NHIF kutoa dawa
  9. Kwamba watapoteza ajira katika sekta binafsi.

Nini kitatokea
  1. Hakuna hospitali itaweza kuwa na dawa zote, hakuna. Kama itaweza basi kuna dawa nyingi zita expire, kwa sababu ama zina shelf life fupi au zina matumizi madogo.
  2. Wagonjwa wengi wataanza malalamiko pale watakapokuwa wanasubirishwa kupata dawa wanayotaka wao ambayo haipo hospitali (maana hospitali itabidi ikanunue dawa haraka ili kumpa mgonjwa husika.
  3. Wizara itashindwa vibaya na kurejesha utaratibu wa nyuma

Maoni
  1. Serikali isiwaonee donge wenye maduka ya dawa, kama inaona wanapata faida kubwa isimamie na kurekebisha sheria zake za manunuzi, na kuondoa vyanzo vya ukosefu wa dawa katika vituo vyake. Hii tu itaondoa maduka ya dawa.
  2. Serikali iondoe imani ya kuwa sekta binafsi ni mshindani, wakati huohuo inataka mamilioni ya Watanzania wajiajiri wenyewe.
  3. Watumishi waliopo wizarani wawe na historia ya kufanya kazi vituo vya afya, kuna watu toka waanze kazi wapo kwenye uongozi, hawajui jinsi vitu viendeshwavyo mahospitalini na bado wanapewa nafasi za kufanya maamuzi magumu kuhusu hospitali.
  4. Serikali ifanye maamuzi kwa kuonesha inaheshimu sheria kwa kupitia mikataba iliyopo kabla ya kufanya maamuzi makubwa. Kutojali huku kumefanya tuwe wahanga hasa kwenye mikataba ya kimataifa
Pia soma > Serikali yasitisha matumizi ya Fomu ya 2C inayotumika kuchukua dawa maduka ya nje
Nimepitia point kwa point maelezo yako nimeona umeongea Mambo ya msingi sana yanayo gusa maisha yetu. Lakini akina Paschal Malaya wanaacha kuongelea mambo haya kutwa kuwapigania malaya wenzie wa Covid19 wanao tafuna fedha za walipa kodi ktk Bunge la mazuzu.
 
Nimepitia point kwa point maelezo yako nimeona umeongea Mambo ya msingi sana yanayo gusa maisha yetu. Lakini akina Paschal Malaya wanaacha kuongelea mambo haya kutwa kuwapigania malaya wenzie wa Covid19 wanao tafuna fedha za walipa kodi ktk Bunge la mazuzu.
Hawezi zungumzia mambo kama haya anajua hakuna bahasha huku
Kila siku wabunge 19 wabunge 19

Ova
 
Kuna waraka umetolewa na Wizara ya Afya, ukitoa taarifa kwamba kuanzia tarehe 01 Juni 2022 hatua kwa hatua kutasitishwa matumizi ya form 2c. Form 2c ni fomu inayotumika na hospitali zinazohudumia wagonjwa wa NHIF kujaza dawa zisizokuwepo hospitali, ili mgonjwa au ndugu wa mgonjwa akachukue dawa husika kwenye maduka binafsi (mengine yako nje ya hospitali ila yanamilikiwa na hospitali husika au serikali) nje ya hospitali.

Maduka haya ya dawa, huingia mikataba ya kisheria na NHIF ya kutoa huduma kwa wateja wao. Ingawa waraka huu unasitisha utoaji wa form 2c kwa vituo vyote vya afya hata binafsi, ukweli malengo makuu ni hospitali za Serikali, lakini kwa sababu form 2c zinatumika na hospitali zote zilizoingia makubaliano na NHIF kutoa huduma kwa wanachama wake, hivyo imebidi tu nazo wazihusishe.

Huu ni uamuzi wenye faida na hasara. Binafsi kama mfamasia naamini kuna hasara zaidi. Ukisoma waraka huu unaweza gundua mambo kadhaa hasi toka Serikali kwa watumishi wake wa afya na maduka ya dawa.

Mtazamo wa Serikali
  1. Kwamba watumishi wa hospitali wanafanya makusudi kuhakikisha hospitali zao zinakosa dawa zote ili kutoa mwanya kwa maduka ya dawa yaliyopo nje ya hospitali kufanya biashara
  2. Kwamba maduka ya dawa binafsi ni chanzo cha dawa kukosekana ndani ya hospitali.
  3. Kwamba maduka ya dawa yanapata faida kubwa ambayo ilipaswa iingie ndani ya mifuko ya hospitali na kuzisaidia hospitali kujiendesha.
  4. Kwamba kukosekana kwa dawa kunasababisha usumbufu mkubwa kwa wagonjwa
  5. Kwamba tatizo la kukosekana kwa dawa linaweza tatuliwa mara moja kwa kutoa mikopo kwa vituo hivi vya afya ili viweze nunua dawa za kutosha kuwafanya wateja wao wasiende kuchukua dawa nje ya hospitali.
  6. Kwamba hospitali inaweza kuwa na dawa zote zilizopo kwenye soko, bila kujali sababu zinazochangia manunuzi kama uhitaji wa mara kwa mara n.k.
  7. Kwamba ubora wa dawa unafanana, hakuna nia ya kuwa na alternative brand
  8. Kwamba serikali yenyewe ipo juu ya mikono ya sheria na inaweza vunja mikataba waliyoingia NHIF na maduka ya madawa bila kuwa na madhara yoyote.
Serikali inasahau
  1. Kuwa imekuwa ikitoa bajeti hewa za dawa.
  2. Kwamba asilimia 99 ya matatizo ya ukosefu wa dawa inayasabisha yenyewe na sheria zake za manunuzi
  3. Kwamba serikali huwa haikiri mapungufu yake katika kuchangia upatikanaji wa dawa endelevu ndani ya vituo
  4. Imewaambia MSD kama hospitali zake zimeenda kununua dawa na dawa huziko hazipo, basi itabidi wajieleze kwa nini dawa husika hazipo, na hii kuifanya MSD kutotoa vibali vya out of stock ili kuruhusu hizi hospitali za Serikali kwenda kununua dawa kwa washitiri na kuendelea kutoa huduma.
  5. Inasingizia sana upotevu wa dawa kama ni chanzo kikubwa cha dawa kutokuwapo hospitalini.
  6. Kwamba Serikali malengo yake makuu ni kusimamia utoaji huduma bora za afya na si kutengeneza ushindani na maduka ya dawa.
  7. Kwamba Serikali yenyewe haifanyi biashara kwenye afya, ndio maana, mishahara ya watumishi wa afya inatoka kwenye kapu kuu, ila hawa wenye maduka mishahara yao inatoka kwenye mauzo hayo hayo yatokayo kwenye maduka
  8. Haya maduka ya dawa yaliingia mikataba ya kisheria na NHIF kutoa dawa
  9. Kwamba watapoteza ajira katika sekta binafsi.

Nini kitatokea
  1. Hakuna hospitali itaweza kuwa na dawa zote, hakuna. Kama itaweza basi kuna dawa nyingi zita expire, kwa sababu ama zina shelf life fupi au zina matumizi madogo.
  2. Wagonjwa wengi wataanza malalamiko pale watakapokuwa wanasubirishwa kupata dawa wanayotaka wao ambayo haipo hospitali (maana hospitali itabidi ikanunue dawa haraka ili kumpa mgonjwa husika.
  3. Wizara itashindwa vibaya na kurejesha utaratibu wa nyuma

Maoni
  1. Serikali isiwaonee donge wenye maduka ya dawa, kama inaona wanapata faida kubwa isimamie na kurekebisha sheria zake za manunuzi, na kuondoa vyanzo vya ukosefu wa dawa katika vituo vyake. Hii tu itaondoa maduka ya dawa.
  2. Serikali iondoe imani ya kuwa sekta binafsi ni mshindani, wakati huohuo inataka mamilioni ya Watanzania wajiajiri wenyewe.
  3. Watumishi waliopo wizarani wawe na historia ya kufanya kazi vituo vya afya, kuna watu toka waanze kazi wapo kwenye uongozi, hawajui jinsi vitu viendeshwavyo mahospitalini na bado wanapewa nafasi za kufanya maamuzi magumu kuhusu hospitali.
  4. Serikali ifanye maamuzi kwa kuonesha inaheshimu sheria kwa kupitia mikataba iliyopo kabla ya kufanya maamuzi makubwa. Kutojali huku kumefanya tuwe wahanga hasa kwenye mikataba ya kimataifa
Pia soma > Serikali yasitisha matumizi ya Fomu ya 2C inayotumika kuchukua dawa maduka ya nje
Mkuu umeandika kitaalam sana na nimekuelewa...
Kongole nyingi kwako

Ova
 
Nilimpeleka mgonjwa wangu hospital moja ya rufaa mkoa fulani, Daktari aliandika dawa nikanunua kwenye duka la hospitali husika isipokuwa dawa moja hawakuwa nayo. Hivyo nikaenda kununua duka la nje, nilipofika nilimuomba muhudumu anipigie hesabu zile dawa nilizonunua hospitali, nilishangazwa aliponipa bei yao kuwa ni Tsh. 39,500/= wakati hospitali nilinunua Tsh. 54,000/= . Nikasema sitonunua tena dawa kwenye maduka ya hospitali/serikali.

Sent from my TECNO KD7 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu umeandika kitaalam sana na nimekuelewa...
Kongole nyingi kwako

Ova
Leo nimekuwa mhanga wa katazo hili nilikuwa na mgonjwa kavunjika mguu so tukapata huduma ya pop(mhogo) then wakat nataka nipatiwe magongo hospital hawana kwa kwel roho imeniuma imenitoka 68'000 cash ninunue wakat nina bima Serikali iangalie jambo hili tutakufa wengi wakat una bima yako na tulikuwa
Referral hospital
 
Hii nchi kuna watu wanafanya maamuzi kama vile tumejitosheleza kwa kila kitu.

Eti kama hospitali haina dawa, wakuambie siku ya kuja kuchukua watakapo kuwa wameileta.

Unashindwa kuelewa hao waliokaa ni watanzania kweli?

Hata kama kuna uhuni kwenye utoaji wa hizo fomu nadhani kuna namna za kudhibiti na sio kuzuia upatikanaji wa huduma.

Leo tunazungumza huduma ya afya kwa wote, sasa itafanikiwaje.

Ni wakati sasa zile kampuni binafsi za bima zirudi hawa NHIF wapambane kupata wateja.

Naona wameelemewa na haya makampuni makubwa. Wataanza kukataliwa na wafanyakazi.

Binafsi bado naamini kabisa NHIF ni moja ya taasisi nzuri katika kutoa huduma za afya, ila inahitaji watu wasiokuwa na uswahili kwa kufanya kazi. Waachane na tabia za kimazoe, muda wote wawe kiushindani.

Wasingatie sera bora za huduma kwa wateja wao, maana ya wagonjwa na wale wanaotoa hizo huduma ( hospitali, maabara, maduka ya dawa) ikiwa ni pamoja na kuwalipa kwa wakati.

Serikali pia iachane na kuingilia mambo ya fedha, zaidi ihakikishe sera za afya zinafanikishwa ipasavyo.
 
Leo nimekuwa mhanga wa katazo hili nilikuwa na mgonjwa kavunjika mguu so tukapata huduma ya pop(mhogo) then wakat nataka nipatiwe magongo hospital hawana kwa kwel roho imeniuma imenitoka 68'000 cash ninunue wakat nina bima Serikali iangalie jambo hili tutakufa wengi wakat una bima yako na tulikuwa
Referral hospital
Pole sana mkuu

Inaumiza sana hali hii

Na hatuwasiki wanasiasa sijui viongozi wakizungumzia mambo haya
Hali ni mbaya sana

Ova
 
Hii nchi kuna watu wanafanya maamuzi kama vile tumejitosheleza kwa kila kitu.

Eti kama hospitali haina dawa, wakuambie siku ya kuja kuchukua watakapo kuwa wameileta.

Unashindwa kuelewa hao waliokaa ni watanzania kweli?

Hata kama kuna uhuni kwenye utoaji wa hizo fomu nadhani kuna namna za kudhibiti na sio kuzuia upatikanaji wa huduma.

Leo tunazungumza huduma ya afya kwa wote, sasa itafanikiwaje.

Ni wakati sasa zile kampuni binafsi za bima zirudi hawa NHIF wapambane kupata wateja.

Naona wameelemewa na haya makampuni makubwa. Wataanza kukataliwa na wafanyakazi.

Binafsi bado naamini kabisa NHIF ni moja ya taasisi nzuri katika kutoa huduma za afya, ila inahitaji watu wasiokuwa na uswahili kwa kufanya kazi. Waachane na tabia za kimazoe, muda wote wawe kiushindani.

Wasingatie sera bora za huduma kwa wateja wao, maana ya wagonjwa na wale wanaotoa hizo huduma ( hospitali, maabara, maduka ya dawa) ikiwa ni pamoja na kuwalipa kwa wakati.

Serikali pia iachane na kuingilia mambo ya fedha, zaidi ihakikishe sera za afya zinafanikishwa ipasavyo.
Kwa hiyo kama hawana madawa fulani,mgonjwa asubirie mpaka madawa wayalete ndiyo wampatie
Hii haijakaa vizuri

Ova
 
Leo nimekuwa mhanga wa katazo hili nilikuwa na mgonjwa kavunjika mguu so tukapata huduma ya pop(mhogo) then wakat nataka nipatiwe magongo hospital hawana kwa kwel roho imeniuma imenitoka 68'000 cash ninunue wakat nina bima Serikali iangalie jambo hili tutakufa wengi wakat una bima yako na tulikuwa
Referral hospital
Pole sana mkuu, hii ndio nchi yetu.

Upole wetu wenye nchi ndio unatufikisha huku
 
Watumishi waliopo wizarani wawe na historia ya kufanya kazi vituo vya afya, kuna watu toka waanze kazi wapo kwenye uongozi, hawajui jinsi vitu viendeshwavyo mahospitalini na bado wanapewa nafasi za kufanya maamuzi magumu kuhusu hospitali.
Hili suala linalitafuna sekta nyingi sana sio afya tu! Mtu anaajiriwa moja kwa moja makao makuu hajui ngazi za chini uhalisia upoje the unakuta ndio mtoa maamuzi
 
Back
Top Bottom