Serikali yazuia huduma za Mabasi yasiyo na Mfumo wa Ufuatiliaji Gari (VTS)

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,370
8,107
Waziri Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhandisi Hamad Masauni ametoa agizo hilo baada ya kumalizika muda aliotoa kwa wamiliki wa Mabasi kufunga vifaa vya Mfumo wa Kufuatilia Gari (VTS) au GPS Tracker ili kudhibiti ajali.

Masauni amelitaka Jeshi la Polisi na Baraza la Taifa laUsalama Barabarani kuhakikisha wanayakamata mabasi yote yaliyokiuka utekelezaji wa agizo hilo.

Takwimu za ajali kutoka Jeshi la Polisi zinaonesha kati ya January hadi August 2022 watu 1,038 walifariki katika ajali 1,117 huku Magari ya Serikali yakiwa ni 11,5%.

=======================
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ameliagiza Jeshi la Polisi Nchini na Baraza la Taifa na Usalama barabarani kuhakikisha wanayakamata mabasi yote yasiyo na vizibiti mwendo

Masauni amesema hayo wakati akizindua baraza la Taifa la Usalama Barabarani makao makuu ya Nchi Dodoma ambapo, amesema miongoni mwa vyanzo vya ajali Nchini ni mwendo kasi unaosababishwa na madereva wazembe wasio fuata sheria za usalama barabarani kitendo kinachopelekea ajali nyingi hapa Nchini

Pia Maasauni ameliagiza Jeshi la Polisi kuanzia l24 October kukamata mabasi yote yasiyo na vizibiti mwendo ambapo amesema kuwa tayari alishatoa maelekezo hayo kuwa ifikapo September mwka huu mabasi yote yawe na vizibiti mwendo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jamanne Sagini ambaye Pia ni Mwenyekiti wa Balaza la Taifa la Usalama barabarani amesema baraza la Taifa la Usalama barabarani kwa kushirikiana na baraza la kazi litaendelea kutoa mafunzo ya Usalama barabarani kwa viongozi wa umma wakiwemo makatibu wakuu na wabunge ili kuwajengea uwezo wa kukemea matukio amabayo yanapelekea ajali kutokea.

Nae Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Atupele Mwakibete ambaye ni kaimu Mwenyekiti wa baraza hilo, amemshukuru Waziri Masauni kwa kumteua kuwa katika baraza hilo ambapo ameahidi kwakushirikiana na baraza na wadau wa Usalama barabarani na kutatua changamoto zilizopo

Aidha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza kamishina msaidizi mwandamizi wa Polisi SACP Wilbroad Mutafugwa amesema kuwa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani toka limeanzishwa kusimamia kamati za Mikoa na Wilaya umesaidia ikiwa ni pamoja na matumizi sahihi ya fedha zilizotokana na ada za ukaguzi wa magari mbalimbali.

MICHUZI BLOG
 
Nadhani vidhibiti mwendo vingewekwa kwenye magari ya Serikli na taasisi zake.

Maana kuna saa gari ya Serikali ina kupita kwenye maeneo hatarishi hadi una jiuliza huyu dereva kavuta bangi au kanywa ulanzi? Na matrafiki wana angalia tuu.

Ukiulizia taarifa za hivyo vifo alivyo toa waziri unaweza kukuta 30% ni magari ya serikali yame sababisha.
 
Hayo yote ya nini?

Sheria zisimamiwe ipasavyo.

Barabara zina alama za barabarani kudhibiti mwendo, kuonesha mwinuko, kona kali, mtelemko mkali.

Na sheria zingine ambazo zina muhusu mmiliki na dereva pamoja na abiria na watumiaji wengine wa barabara

Sheria zikisimamiwa tutakuwa tume fanikiwa... ila kama tutakuja kila siku kufunga speed limit ktk magari na kuweka matuta barabarani na vingine tutakavyo ona vina faa huku sheria zenyewe hatuzisimamii ipasavyo na kumuacha trafic ana kula rushwa, abiria ana shiriki ktk uvunjifu wa sheria na wana harakati hawa kemei jamii ila wao kazi yao ni kukemea serikali tu

Tuna kazi kufika safari tunayo elekea
 

Why Speed Governors?​

By the year 2020, road traffic injuries are expected to be in third place in reasons for hospitalised people.As per the National Crime Records Bureau Data (2015) 141,526 persons were killed and 477,731 injured in road traffic crashes in India in 2014. 27% of road deaths in India in 2013 was contributed by trucks, buses and other heavy vehicles. Speeding has been identified as one of the top three reasons for road crashes and deaths across the globe. This makes speed management a very important tool for improving road safety. Speed Governor is a device which can limit the vehicle speed to a preset limit, thus improving vehicle efficiency and road safety.
 
Huwa napata kigugumizi sana pale ninapoona watu wanaotakiwa kuwa na taarifa sahihi wanatoa taarifa butu .
Vts inayotumika kwa sasa sio kidhibiti mwendo, (speed governer) bali ni module ambayo hufanya speed ya chombo husika kuonekana na mamlaka , kiufupi vts ni gps tracker.
Sidhani kama waziri hana taarifa na hili ,speed govrner ilifeli kitambo sana tu
 
Rudisheni utaratibu wa Mabasi kutembea usiku kama zamani unatoka Mwanza saa 12 za jioni unaingia Dar saa 1 asubuhi mwendo mdogo mdogo.

Na yawe yenye viti vya kulaza.
 
Rudisheni utaratibu wa Mabasi kutembea usiku kama zamani unatoka Mwanza saa 12 za jioni unaingia Dar saa 1 asubuhi mwendo mdogo mdogo.

Na yawe yenye viti vya kulaza.
Mbona mabasi mengi tu yanasafiri usiku Tena kucha kabsa
mfano mabasi ya Mbeya to Mwanza via Dodoma
Unatoka Mbeya saa 12 asubuh unafika mwanza saa 12 asubuh siku nyingine
 
Mbona mabasi mengi tu yanasafiri usiku Tena kucha kabsa
mfano mabasi ya Mbeya to Mwanza via Dodoma
Unatoka Mbeya saa 12 asubuh unafika mwanza saa 12 asubuh siku nyingine
Yale ya kuondoka jioni na kufika asubuhi kama ilivyokuwa enzi za Mwinyi.
 
Nadhani vidhibiti mwendo binge wekwa kwenye magari ya serikli na taasisi zake.
Maana kuna saa gari ya serikali ina kupita kwenye maeneo hatarishi hadi una jiuliza huyu dereva kavuta bangi au kanywa ulanzi? Na matrafiki wana angalia tuu.
Ukiulizia taarifa za hivyo vifo alivyo toa waziri unaweza kukuta 30% ni magari ya serikali yame sababisha.
I second you on this one.
 
Huwa napata kigugumizi sana pale ninapoona watu wanaotakiwa kuwa na taarifa sahihi wanatoa taarifa butu .
Vts inayotumika kwa sasa sio kidhibiti mwendo, (speed governer) bali ni module ambayo hufanya speed ya chombo husika kuonekana na mamlaka , kiufupi vts ni gps tracker.
Sidhani kama waziri hana taarifa na hili ,speed govrner ilifeli kitambo sana tu
Vts inaondolewa wanakua wanatumia speed Governor tu
 
Waziri wangu speed sio tatizo, barabara zetu ndio tatizo kubwa,hazikujengwa kwa kufuata vipimo vya barabara kuu, kile kipande cha kutoka ubungo hadi mbezi (T1),zile corners, miinuko na miteremko ya barabara ile ni hazard tupu, uendeshaji pale wa gari ni mgumu mno kutokana na muundo wa barabara, pls waziri wangu mchukue na waziri mwenzako wa ujenzi, msafiri kwenda Zambia na uangalie ile barabara inayojengwa(Chinese company)kutoka Isoka hadi chinsali, then ile ya kutoka Kafue hadi kazungula border post, then urudi hapa nyumbani ulinganishe na ya kwetu, tunafeli hapa big time na volume ya magari route ya lusaka to kazungula ni kubwa mara 4 kulinganisha na hii T1 yetu, ajali ni za nadra sana kwa wenzetu, livingstone to lusaka ni kama 450km, bus pale inachukua 5 to 6 hrs, hiyo ni almost distance ya Dar to Moshi
 
Hayo yote ya nini?

Sheria zisimamiwe ipasavyo...

Barabara zina alama za barabarani kudhibiti mwendo, kuonesha mwinuko, kona kali, mtelemko mkali...

Na sheria zingine ambazo zina muhusu mmiliki na dereva pamoja na abiria na watumiaji wengine wa barabara

Sheria zikisimamiwa tutakuwa tume fanikiwa... ila kama tutakuja kila siku kufunga speed limit ktk magari na kuweka matuta barabarani na vingine tutakavyo ona vina faa huku sheria zenyewe hatuzisimamii ipasavyo na kumuacha trafic ana kula rushwa, abiria ana shiriki ktk uvunjifu wa sheria na wana harakati hawa kemei jamii ila wao kazi yao ni kukemea serikali tu...

Tuna kazi kufika safari tunayo elekea
Wewe ni mwana chama chakavu unayo nafasi ya kuwashauli wajinga wenzako Ili kuyafanya hayo
 
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jamanne Sagini ambaye Pia ni Mwenyekiti wa Balaza la Taifa la Usalama barabarani amesema baraza la Taifa la Usalama barabarani kwa kushirikiana na baraza la kazi litaendelea kutoa mafunzo ya Usalama barabarani kwa viongozi wa umma wakiwemo makatibu wakuu na wabunge ili kuwajengea uwezo wa kukemea matukio amabayo yanapelekea ajali kutokea.
Niacheni nicheke mie 🤣 nchi yangu Tanzania
 
ambapo amesema kuwa tayari alishatoa maelekezo hayo kuwa ifikapo September mwka huu mabasi yote yawe na vizibiti mwendo.

Ina maana walimdharau au
Masauni amesema hayo wakati akizindua baraza la Taifa la Usalama Barabarani makao makuu ya Nchi Dodoma ambapo, amesema miongoni mwa vyanzo vya ajali Nchini ni mwendo kasi unaosababishwa na madereva wazembe wasio fuata sheria za usalama barabarani kitendo kinachopelekea ajali nyingi hapa Nchini
Hii inasubiri ceremonial events ili itangazwe
 
Back
Top Bottom