Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,500
- 9,279
SERIKALI imezindua mpango wa jamii shirikishi na harakishi wa chanjo dhidi ya UVIKO-19 wenye mambo 10 ikiwamo kuwapo kwa chanjo tembezi (mobile vaccination site) na kuwafuata wananchi walio tayari kuchanjwa kwa hiari.
Mpango huo ulizinduliwa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, Dk. Dorothy Gwajima, kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa waganga wakuu wa mikoa na halmashauri uliofanyika jijini hapa.
Akitoa maelezo ya mpango huo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi, alisema mpango huo unalenga kuongeza vituo vya kuchanja kutoka 550 hadi 6,784, kuharakisha wananchi kuchanjwa mapema.
“Kwenye chanjo tembezi magari tumeshaagiza na nimeagiza tangu juzi, taasisi zetu na halmashauri zitoe magari kwa ajili ya kutekeleza huu mpango, nimesikia baadhi ya wakurugenzi wanasuasua kutoa magari, MSD na Mpango wa chanjo wametoa, TB bado hawajatoa, huu ni mpango wa kitaifa, nataka yatoke ndani ya saa 24 zijazo kwa taasisi zote ambazo bado,” alisema.
Alisema utasimamiwa na wakuu wa mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa na Waganga Wakuu wa Mikoa.
“Ni mwezi sasa tangu Rais Samia Suluhu Hassan azindue utoaji chanjo ambapo watu zaidi ya 350,000 hadi sasa wamechanja, bado tunahitaji wananchi wachanje mapema iwezekanavyo kutokana na asili ya ugonjwa wenyewe,” alisema.
Alisema ugonjwa huo ni wa mlipuko na unasambaa haraka na uchanjaji ni njia pekee ya kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo.
Alibainisha kuwa vikundi, viongozi wa kijamii na serikali za mitaa ndiyo muhimili wa kuhamasisha chanjo mijini na vijijini.
“Mpango huo pia unalenga elimu itatolewa kupitia njia za asili za ngoma, kwaya, muziki, maigizo, semina, mikutano na pia TV na redio jamii, kutumia pia viongozo wa serikali, kijamii, kidini, wabunge, wasanii, watu maarufu, wataalamu, wawakilishi wa vikundi vya kijamii kama vile Vicoba,” alisema.
Alisema kila halmashauri itakuwa na lengo la kufikia kwa muda maalum utakaopangwa na kuwafuata wananchi walio tayari kuchanjwa bila wao kulazimika kwenda vituoni.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, alisema lengo la mpango huo ni kuharakisha utoaji chanjo kwa kuwa hadi sasa haujafikia nusu ya chanjo zilizoletwa zaidi ya milioni moja.
“Tutakutana na wakuu wa mikoa na timu mbalimbali kama sehemu ya uraghabishi na kupata nafasi ya kutoa ufafanuzi wa hoja mbalimbali, RMO utahitajika kufanya hili, tutatumia redio za kijamii,” alisema.
Aliwataka waganga hao kufuatilia matumizi ya fedha za mpango huo na kutoa taarifa ya matumizi yake kwake na fedha zitapelekwa wiki ijayo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kwa ajili ya kazi hiyo.
Ippmedia
Mpango huo ulizinduliwa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, Dk. Dorothy Gwajima, kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa waganga wakuu wa mikoa na halmashauri uliofanyika jijini hapa.
Akitoa maelezo ya mpango huo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi, alisema mpango huo unalenga kuongeza vituo vya kuchanja kutoka 550 hadi 6,784, kuharakisha wananchi kuchanjwa mapema.
“Kwenye chanjo tembezi magari tumeshaagiza na nimeagiza tangu juzi, taasisi zetu na halmashauri zitoe magari kwa ajili ya kutekeleza huu mpango, nimesikia baadhi ya wakurugenzi wanasuasua kutoa magari, MSD na Mpango wa chanjo wametoa, TB bado hawajatoa, huu ni mpango wa kitaifa, nataka yatoke ndani ya saa 24 zijazo kwa taasisi zote ambazo bado,” alisema.
Alisema utasimamiwa na wakuu wa mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa na Waganga Wakuu wa Mikoa.
“Ni mwezi sasa tangu Rais Samia Suluhu Hassan azindue utoaji chanjo ambapo watu zaidi ya 350,000 hadi sasa wamechanja, bado tunahitaji wananchi wachanje mapema iwezekanavyo kutokana na asili ya ugonjwa wenyewe,” alisema.
Alisema ugonjwa huo ni wa mlipuko na unasambaa haraka na uchanjaji ni njia pekee ya kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo.
Alibainisha kuwa vikundi, viongozi wa kijamii na serikali za mitaa ndiyo muhimili wa kuhamasisha chanjo mijini na vijijini.
“Mpango huo pia unalenga elimu itatolewa kupitia njia za asili za ngoma, kwaya, muziki, maigizo, semina, mikutano na pia TV na redio jamii, kutumia pia viongozo wa serikali, kijamii, kidini, wabunge, wasanii, watu maarufu, wataalamu, wawakilishi wa vikundi vya kijamii kama vile Vicoba,” alisema.
Alisema kila halmashauri itakuwa na lengo la kufikia kwa muda maalum utakaopangwa na kuwafuata wananchi walio tayari kuchanjwa bila wao kulazimika kwenda vituoni.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, alisema lengo la mpango huo ni kuharakisha utoaji chanjo kwa kuwa hadi sasa haujafikia nusu ya chanjo zilizoletwa zaidi ya milioni moja.
“Tutakutana na wakuu wa mikoa na timu mbalimbali kama sehemu ya uraghabishi na kupata nafasi ya kutoa ufafanuzi wa hoja mbalimbali, RMO utahitajika kufanya hili, tutatumia redio za kijamii,” alisema.
Aliwataka waganga hao kufuatilia matumizi ya fedha za mpango huo na kutoa taarifa ya matumizi yake kwake na fedha zitapelekwa wiki ijayo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kwa ajili ya kazi hiyo.
Ippmedia