Kibunango
Platinum Member
- Aug 29, 2006
- 8,420
- 2,271
Udokozi unaweza kuwepo sehemu yoyote, ila bongo wanaona udokozi ni halali kwao, mpaka kufikia hatua ya kuupa majina mazuri ili kuuharishisha!Mkuu mie nimeenda spain na italy na wanasafe ya kuweka vitu vya thamani na wanakuuliza hivyo hivyo kwamba if you have any jewellery please let us know we have a safe for our clients. Je nikuulize kule nako ni wezi? Nadhani suala la wadokozi ni la dunia nzima but kisiwe kigezo cha kuwanyima wazawa kazi ama sivyo haina maana basi ya kuitwa mzawa.
Kuna siku moja nilipata wageni kumi na moja, hawakupenda kukaa hoteli(kwa ajili ya usalama), hivyo waliniomba niwatafutie nyumba kubwa ambayo kwao. Nilipata nyumba ya ghorofa mbili katika eneo la Mji Mkongwe(ZNZ). Wageni wakaja na kuhifurahia nyumba hiyo. Asubuhi yake waligundua kuwa wameibiwa.
Ilikuwa ni kazi kweli kweli kwani wengine waliibiwa plastic zao za fedha na wengine hadi pasi za kusafiria. Huku na kule baada ya polisi waliweza kupata baadhi ya vitu na ni baada ya wageni hao kuondoka. Mbaya zaidi mchongo mzima ulifanywa na mwenye nyumba!