Serikali yawatelekeza wanafunzi 29 Ukraine

Kumradhi wOrM: Nimekwambia unifikishie ujumbe huo lakini umeandika as if ni wewe unaandika. Ungeandika kwa niaba ya Invisibe. Hivyo nimeufuta.

Quarz,

Ujumbe huu nimeupeleka mbele ili ufanyiwe kazi. Kama kutakuwa na majibu nitayaweka hapa au nipe barua pepe ya mmoja wa wanafunzi hawa nimtumie majibu ya nitakachojibiwa.

Tatizo: Barua hii haina mikato, nukta wala funga semi. Baadhi ya sehemu zimeandikwa kama ni mawazo ya mtu mmoja hivyo umakini unahitajika zaidi.

Barua pepe yangu ni invisible-at-jamboforums-dot-com
 
jamani tuwapigie kelele jawa wanyonge ,lisipite hivi hivi ,haya ndio masuala ya kupigia kelele....au mnaonaje ,tuwashauri wafungue tawi la ccm,kiev ukraine...jamani bora upate tabu nyumbani kuna wajomba ...kuliko ukraine ambako hata day work hakuna
 
Kwanza ninawapa Pole sana waathirika hawa wa ucheweleweshwaji wa mikopo yao na mapungufu yake.Hali waliyonayo inanikumbusha zama hizo nikiwa Nchi JIRANI Na hapo Hali ilikuwa hivi hivi lakini cha kusikitisha karibu miongo miwili itimie tangu niwe katika dhahama kama lao, lakini kwa upande wa kiutendaji hakujabadilika kitu hasa katika swala la upelekwaji wa wanafunzi na utimizwaji wa mahitaji yao.
USHAURI:
Katika hao wanafunzi kumi na nne waunde mtandao wa kuwaunganisha wazazi au walezi wao waliopo nyumbani ili wajipange na walifuatilie swala kwa ukaribu zaidi kwa kutoa msukumo endelevu kwa wahusika ambao ni bodi ya mikopo na wizara ya elimu ya juu, sayansi na tekinolojia wa kulipatia ufumbuzi wa kudumu.Tukumbuke umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu na damu Nzito kuliko Maji.Na kila aliyeguswa na anauwezo wa kutoa msaada kwa njia yeyote kulipatia swala lao ufumbuzi wa kudumu basi ni vyema wakasaidia.
 
kama ccm wakikaa kimya wajamaa tufanye mpango wa kuwachangia hawa wabongo wasiadhirike huko ugenini wana JF...najua uwezo watu wanao maana hawa ccm noma sana...inatia uchungu bana...dah
 
kama ccm wakikaa kimya wajamaa tufanye mpango wa kuwachangia hawa wabongo wasiadhirike huko ugenini wana JF...najua uwezo watu wanao maana hawa ccm noma sana...inatia uchungu bana...dah

What a shame! Jamani wanabodi inabidi hii ishu ifikishwe kunakohusika kwani deadline 15 february ndo inafika.Kwa kweli hawa watu wanateseka na suala la kuwasaidia ni ishu ndani ya muda huu.Ila sasa Invisible alisema anawasiliana na wadau wa wizara sasa sijui wamemjibu vipi
 
Nadhani wanabodi mnakumbuka ile ishu ya vyuo expensive with low gredibility ili hali jamaa kama hawa wangeweza saidiwa kama kungekuwa na marshal plan
 
Jamani nani ana contacts za hawa vijana wetu huko...wasiliana nami

Juhudi za "Invisible"; "Mwanakijiji"; na wengineo katika mtandao huu zitakuwa mtihani mhimu sana wa chombo hiki (JF), katika kuamsha fikra za watu na watawala kuhusu jambo hili na mambo mengine mengi mhimu yanayoongelewa humu. Kwa kuanzia, itakuwa faraja sana kama tutaweza kufanikiwa kwa kuwawezesha hawa vijana kuendelea na shule bila ya matatizo haya yote!
Mimi ninapendekeza hivi: kwa wale wana-JF wenzetu waliopo pale nyumbani Dar; watafute njia ya haraka itakayoweza kuwafikishia taarifa kamilifu kabisa, wahusika wa moja kwa moja wa shauri hili. Ikiwezekana, vyombo vya habari vyote pia vipewe taarifa hii na wavitangaze haraka.

Bado ninayo imani kubwa kuwa serikali yetu hii inayo nia na ni ya kuwajali raia zake popote pale duniani walipo. Pengine hili tatizo linatokana tu na urasimu wa watu wachache wasiokuwa na msisimko na mtazamo mpya wa kuwaondolea matatizo wananchi.

Je, pengine kuna upande wa pili wa jambo hili ambao hatunao taarifa yake bado? Kama hivyo ndivyo, basi serikali inao wajibu wa kulielezea vizuri na kwa haraka kuliko kuwaacha hawa vijana wetu katika hali ngumu namna hii bila ya usuluhishi unaofaa.
Ninashangaa sana hizi balozi zetu za nje!!!!
 
Kumradhi wOrM: Nimekwambia unifikishie ujumbe huo lakini umeandika as if ni wewe unaandika. Ungeandika kwa niaba ya Invisibe. Hivyo nimeufuta.

Quarz,

Ujumbe huu nimeupeleka mbele ili ufanyiwe kazi. Kama kutakuwa na majibu nitayaweka hapa au nipe barua pepe ya mmoja wa wanafunzi hawa nimtumie majibu ya nitakachojibiwa.

Tatizo: Barua hii haina mikato, nukta wala funga semi. Baadhi ya sehemu zimeandikwa kama ni mawazo ya mtu mmoja hivyo umakini unahitajika zaidi.

Barua pepe yangu ni invisible-at-jamboforums-dot-com

"Invisible" Nadhani kuna upande wa pili wa shilingi hapa!
Huyu mwandishi angefanya jambo zuri sana kama angeshirikiana na wenzie walioorodheshwa kuandika hii taarifa kwa ufanisi kidogo. Haisaidii sana kuandika taarifa ndeeeefu, na kuwachosha wasomaji, hata wale ambao wangependa kutoa msaada katika utatuzi wa jambo husika!
These kids have to learn to present their arguments in a coherent manner. I know it will serve them well in their 'Medical and Pharmaceutical' fields for a start.
 
Hapo hata mimi sijaisoma hii barua yote nimesoma vipande pande tu..ila humu kuna waandishi wa habari wange copy wakatoa kwenye magazeti ya bongo nadhani hapo itakua fresh..maana hawa jamaa watakufa na baridi baridi inatakiwa kula saaana duh noma juu ya noma
 
Vyanzo vikuu vya malalamiko hayo;
1. Ufinyu wa kiwango cha mkopo unaotolewa na kutumwa katika thamani ya T.Shs mil. 3
2. Ucheleweshwaji na Utuumaji nusu nusu wa kiwango hicho kwa wakati muafaka ndani ya kipindi cha mwaka wa masomo kulingana na Sheria na taratibu za VYUO.

Ni aibu na fedheha kubwa ambazo serikali ya Tanzania inaendelea kujizolea huku UKRAINE siku hadi siku kupitia aina ya maisha yetu kama wanafunzi wanaosomeshwa na nchi yao,hali ya kukosa fedha za kujikimu ikiwa ni pamoja na chakula,mavazi ya hali hii ngumu ya baridi kali sana, baadhi yetu mavazi ya taaluma zetu na gharama zingine za kijamii ambazo zinapatikana vyuoni kama michezo,bima,usajili,utafiti wa kiafya,ulinzi,malazi ni vitu ambavyo vinapatikana nje ya ada zetu na ni miongoni mwa gharama za kufikirika zaidi kama vigezo vyetu vya kuomba mikopo yetu kuongezwa ukizingatia pia kwa ujumla gharama za maisha katika nchi hii ni kubwa, ucheleweshaji wa fedha zetu za ada iliyo NUSU NUSU kwetu zinatuzuia kuruhusiwa kuingia madarasani mara kwa mara wakati masomo yetu yanaendelea na mara kwa mara Ucheleweshwaji na Upungufu wa fedha za malazi (Accomodation) na usajili (Registration) kwa mihula ya masomo hutufanya tuishi kwa manyanyaso na woga mwingi zaidi ya swala msituni au panya aliyemuona paka! hali hii inatufanya tushindwekuwa na amani katika nafsi zetu.

Marekebisho katika suala zima la ugawaji mikopo ya nje ni suala la kufikirika kiundani zaidi na si suala la kisiasa kama ambavyo linachukulika, ni suala ambalo linahitaji uamuzi wa kitaaluma zaidi katika kuliamua kwa kuangalia tofauti ya mifumo ya maisha katika nchi za nje na ndani ya Tanzania, tunatumaini kama mliweza kufikiria uamuzi wa kuanzisha bodi ya mikopo na kututoa huko na kutuleta huku UKRAINE tunategemea pia suala kama hili mtakua mmelijadili kwa kina kabla ya kuamua kulitenda kwa kufuata taratibu ambazo mmeziweka wenyewe,kwa hiyo katika hali ya kawaida sana tunashindwa kuamini kama bado mnaendelea kutujadili na ili hali suala letu si la kuhitaji muda kama ambao mmeutumia kutufikiria wakati sisi tunaendelea kupata mateso makubwa na kusahau kama Serikali yetu mna jukumu la kutuhudumia na sisi tuna haki ya kuhudumiwa kama wanafunzi kulingana na sheria za kitaifa na kimataifa kwa kutuleta huku.

Pia tunapenda kufahamu kwa nini bodi ya mikopo inaendelea kufanya bajeti zake na kutuletea fedha zetu zikiwa kwenye thamani ya kiwango kidogo cha T.shillingi? na ili hali wanajua malipo yote huku tunafanya kwa kutumia dola ya Kimarekani na ndio ambayo inatumika hata katika matumizi mengine ya kawaida.
Hii inafanya hata mkopo wetu kubadilika badilika kama sio kushuka kiwango chake mara tu pesa yetu inaposhuka thamani yake ukiilinganisha na Dola ya kimarekani,utaona ni bora basi bajeti zetu zijadiliwe na kutumwa kwetu wakiiruhusu dola ya kimarekani itumike kama thamani ya kiwango cha pesa yetu katika mikopo yetu pia inakua sio jambo zuri sana kututumia pesa kidogo kidogo sana kiasi cha kutuacha muda mrefu katika hali ngumu kiasi ambacho hata zingine zinapokuja baadae sana zinatukuta katika madeni mengi na hivyo yote iliyokuja kuishia kulipa madeni na kubaki katika hali ngumu kama ya mwanzo hivyo kuendeleza maisha magumu tu.

Tuliomba mkopo wa dola za kimarekani 5000 kama kiwango cha chini kulingana na mahitaji ambayo tuliyaambatanisha katika fomu zetu za mikopo lakini bado wanatupa mikopo sawa ya shilingi za kitanzania milion 3 kiasi ambacho ukiibadilisha kwenda kwenye pesa ya kimarekani unapata dola chache mno! ,wanatupa mikopo bila kufanya utofauti wa mazingira ya maisha katika sehemu mbalimbali ambazo wanafunzi wake tunaishi.

Kwa huo mkopo ambao tunapewa wa shilingi za kitanzania milioni 3 ukweli ni kwamba hadi sasa kwa kiasi kilichobaki hata tukiamua tukilipe chote katika ADA ni kwamba bado hakitatosha bila sisi hapo kujikimu kwa suala lolote! sasa BODI wanapogawa mkopo kama huu kwetu bado ni tatizo na kunahitajika ufikiriwaji wa kina na wa haraka katika utatuzi wake,
BODI inahitaji kutufikiria upya na kwa haraka zaidi!

Kiasi hicho kidogo cha fedha mnachotuletea , na mnavyotuathiri sisi kisaikolojia kwa mateso tuyapatayo msitegemee kujenga chochote bali mtakua mnasaidia kubomoa mwanzo mzuri mliouanzisha mkiwa na nia na lengo zuri mawazoni mwenu….yaani kama ni mkulima ameamua kula mbegu zake zote mwenyewe… atapanda nini sasa? Sisi ni binadamu tutakapotumia muda mwingi kufikiria manyanyaso mnayotufanyia kwa njia moja au nyingine juu ya utoaji wenu wa fedha kwetu kama kiini cha matatizo yetu yote mnaweza kumkaribisha shetani katika mawazo yetu kwa kiasi kidogo cha fedha mnazotupa tena kwa kucheleweshwa; kwa kufikia hatua ya kuacha shule na kujiingiza katika maovu mengine huku tuliko kama njia ya kutafuta kuishi zaidi baada ya nyinyi kushindwa kutuhakikishia uhai wetu kama wanafunzi.

Hivyo katika kulifanikisha hili suala la marekebisho katika mikopo yetu ya walio nje ya Tanzania hasa sisi wa Ukraine ni la umuhimu mkubwa kwa sababu hakuna jinsi ya kutokuwepo hayo maongezo ya mikopo yetu ili tuendelee kusoma bila ya hivyo ni kwamba pesa hafifu mnyotupatia ya mkopo hata tukiamua tulale njaa sisi wenyewe hakiwezi kutosheleza kiasi cha ADA za vyuo ambazo zimebaki,
kwa hiyo mtagundua sasa si suala la kuendelea kujadiliwa zaidi bali ni suala la kuhitaji uamuzi wa haraka zaidi na busara ili kuhakikisha usalama wetu kitaaluma na kimaisha kulingana na mazingira tuliopo sisi wanafunzi wa kitanzania tunaotokea kwenye familia ambazo UMASKINI bado ni gumzo kubwa linalozisumbua!

Tunategemea mmetuleta huku mkiwa na lengo na nia nzuri ya kutafuta mabalozi wa kusaidia kulisukuma kwa haraka iwezekanavyo gurudumu zima la maendeleo ya nchi yetu kwa miaka ya usoni sasa ni lazima mtambue kuwa nyinyi ndio baba na mama zetu na familia zetu zipo nyuma yenu zikiendelea kuwashukuru kwa nafasi mlizotupa sisi kuja huku kujiendeleza kielimu kwa manufaa ya Tanzania nzima .hivyo tunaomba mtujali na kututhamini katika mawazo na hoja zetu za msingi tunazozitoa kwenu juu ya kiasi cha fedha mnachotupa sisi kama wanafunzi ambao tupo kwenye ngazi ya chuo kikuu hivyo ukomavu wa akili zetu katika kuhoji na kutoa mapendekezo ni mkubwa na kama wahusika tunaokutana na hali hiyo halisi hivyo hatutegemewi kupuuzwa zaidi ya hapo tutashindwa kujua zaidi kuwa mnatuweka kwenye kundi gani hasa la watu, au sisi ni wahuni? Na Si Wanafunzi? pengine kama ambavyo mnaweza kutufikiria hivyo kikawa kigezo cha kutufanyia manyanyaso haya yote katika suala la mikopo yetu mkidhani tunahitaji hizo fedha kwa starehe binafsi,

Ukweli ni kwamba, sisi ni watu wazima ambao sasa tunajukumu la kuandaa maisha yetu wenyewe hivyo vigezo mlivyovitumia kutuleta huku nafikiri vinaweza kututoa kutoka kwenye kundi kama hili la watu ( WAHUNI), tunaimani hata wazazi wetu wangeona aina ya maisha ambayo tunaishi huku wangelia sana na wangelijua hili mapema lingelitutokea wasingelituruhusu sisi kuja huku ili hali serikali inatufanya sisi kama watoto wa kambo.

Walimu wanakiri tunauwezo mzuri kitaaluma lakini upungufu wa ufanisi wetu unaenda ukipungua kwa sababu vichwa vyetu vinasongwa na mambo mengi vikiwemo NJAA! na mawazo juu ya hatma yetu huku ulaya.
Ikizingatiwa tunasoma kwa kirusi na ugumu wa masomo yetu unatupa wakati mgumu sana kwenda sambamba na wenzetu wa Kiukraine ila kadri muda unavyokwenda tunaendelea vizuri kitaaluma mpaka tunakuwa katika level moja,
ila tunajiuliza bado nani anahusika kutupa hali hii ngumu kifedha wakati ni suala ambalo linaweza likatatulika kwa wakati muafaka jibu linabaki palepale ni serikali ya Tanzania ambayo ndiyo iliyotuleta huku ikiitumia bodi yake ya mikopo.

Vilevile ni vigumu kwa sisi kutoamini ya kwamba hata Bodi inaweza kuonyesha ubaguzi wa aina fulani katika ugawaji wa mikopo! Ubaguzi ambao tunakutana nao huku kutoka kwa wazungu ambao si wastaarabu, ni ubaguzi ambao sasa Bodi inauonyesha waziwazi kwetu kwenye mtandao kwa kugawa viwango tofauti tofauti vya mikopo hasa kwa sisi wanafunzi wa vyuo vya Nje ili hali sisi wengine tunaendelea kunyanyasika na kufedheheka katika suala zima la kimaisha na kielimu.

Kama kuna juhudi zozote mmezifanya kama serikali kuhakikisha wengine waliopo nje wanapata mkopo sahihi kulingana na gharama za maisha ya sehemu husika basi tafadhali tunaomba fanyeni hivyo pia kwa wengine kama sisi ambao tunataabika huku ugenini!

Katika mazingira kama hayo ya wenzetu walio nchi nyingine wanaopata kiasi fulani cha fedha kikubwa kuliko chetu, ni kitu ambacho sisi binafsi kinatukatisha tamaa sana na pi kuona kuwa nyinyi mnaweza kuchangia kuharibu tamati ya malengo ambayo tumejiwekea baadae sisi na familia zetu kama pia si na watanzania ambao wako nyuma yetu wakitegemea siku moja tuje kuwa saidia katika nyanja mbalimbali za maendeleo.

Tunakutana na mambo mengi sana ambayo ni mazito kuliko uwezo wetu kuyatatua katika kila wakati mgumu wa kifedha ambao tunakutana nao,.mwanzo wa muhula huu wa mwaka wa masomo kwa mwaka 2006-2007 ambao ulianza tarehe 01/09/2006 tumekutana na mengi ambayo katika hali ya kawaida yametusononesha kwa kiasi kikubwa sana, tumeingia vyuoni mapema mwezi wa tisa baada ya kumaliza vizuri kozi zetu za lugha ya kirusi tayari kwa kuanza mwaka wa kwanza wa chuo, tukiwa na lengo na hamu kubwa ya kuanza kusoma huku mioyo yetu ikiwa na hamasa kubwa juu ya lengo lilotuleta huku Ukraine, na kama kitu muhimu sana katika maisha yetu huku nyuma kukiwa na serikali ya Tanzania na familia zetu ambazo wanahitaji msaada wetu mkubwa katika siku za baadae.

Lakini cha kushangaza baadhi yetu ( Hasa wa Chuo cha Medicine) walikaa zaidi ya wiki 3 bila kuingia madarasani huku wenzao wakiendelea na masomo!
Tumebaki katika hali ngumu sana kuielezea kifedha bila kujua hatma ya kuja kwa fedha zetu za ADA kutoka bodi ya mikopo, tunaishi maisha magum sana kiasi ambacho haielezeki! jinsi ambavyo tunasurubika. unaweza ukashindwa kuamini lakini ni hali ambayo haiwezi kuandikika ikafanana na uhalisia wa mateso ambayo tuliyapata kwa kipindi kile tulipowasili tu UKRAINE.

Serikali ndiyo inayojukumu na uwezo wa kushughulikia utatuzi wa usumbufu tunaoupata juu ya suala zima la malipo kwa Vyuo pia kwa kurejea fax ambazo tumezituma kwa bodi ya mikopo juu ya uongezaji wa mikopo yetu ni jambo la kupewa kipaumbele sana kwa sababu bado hatujui hasa inatumia vigezo gani kugawa mikopo tofauti tofauti kwa sisi wanafunzi wa kitanzania tunaosoma huku nje ya nchi kwa sababu ukweli ni kwamba hali na gharama za maisha huku tulipo ni kubwa sana na gharama nyingi tunazokutana nazo Vyuoni zipo nje ya ADA tunayolipa hivyo Tunaiomba chonde chonde! serikali yetu kama Chombo kilichotuleta huku kuhakikisha jitihada za makusudi zinafanyika kuhakikisha marekebisho ya haraka yanafanyika katika maongezo ya mikopoyetu kama kweli mnajali uwepo wetu huku tulipo.

Vyuo vyetu vinakosa imani na sisi kwa sababu mara kwa mara havipati taarifa sahihi kuhusiana na suala letu la malipo ya Ada pia inatupa wakati mgumu pia hata sisi wenyewe wanapotubana kwenye suala hili ambalo hata sisi liko nje ya uwezo wetu kama wanafunzi (tutokao katika familia duni za kimaskini) kuwahakikishia kiasi chao cha fedha wanazotudai kitakuja kwa wakati fulani muafaka.huwa mara kwa mara tunawasiliana na balozi wetu aliopo Urusi ( RUSSIA) mzee wetu Muheshimiwa balozi CHOKALA katika kila wakati mgumu kama huu wa kifedha ili aangalie ni jinsi gani ambavyo anaweza akawasiliana na Serikali ( Bodi) wakamuelewa ili sisi turuhusiwe kuingia madarasani mwetu lakini hata hivyo bado Suluhisho la kudumu halijapatikana hali ya kuwa tunakutana na suala lilelile la kusimamishwa shule kwa vipindi tofauti tofauti wakati VYUO wakizisubiri pesa zao ziwasili kwa muda muafaka kulingana na taratibu zao.

Mheshimiwa balozi mara kwa mara huandika fax kwa uongozi wa vyuo kuwataarifu hali halisi ya wanafunzi wao wanaosomeshwa na SERIKALI chini ya BODI ya mikopo na kwamba bodi haina experience ya muda mrefu ndio kwanza imeanzishwa hivyo kuwaomba wasiwe na wasi wasi juu ya suala letu la fedha hivyo waturuhusu tu tuweze kuingia madarasani.

Cha kusikitisha ni kwamba bado hali inazidi kuwa mbaya kutokana na ukosefu wa taarifa sahihi na za kuaminika kutoka BODI juu ya mfumo mzima wa malipo ya ADA zetu.

Siku ya tarehe12/01/2007 ambayo ilikua ni sikukuu ya MAPINDUZI huko Tanzania,ilikua ni siku mbaya sana kwa wanafunzi wenzetu wa Medicine baada ya chuo chao kuamua kuwasimamisha masomo kwa kipindi kingine na wengine kwenda kutolewa madarasani na kuwaambia kama suala lao la kifedha halitakuwa nasuluhisho la kudumu ni bora WAONDOKE wakatafute vyuo vingine huku wakiwapa muda wa siku chache kuhakikisha suala hilo limetatuliwa bila ya hivyo taratibu za kufukuzwa chuoni inabidi zianze kufuatwa kwa wao kusema wameshindwa kuwavumilia!!

Hili si jambo la busara hata kidogo ni kutaumiza tu sisi wanyonge ambao mazingira tuliopo ni magumu kifedha na hatuna wa kumtegemea isipokua serikali yetu ya Tanzania ambayo ndiyo iliyotuleta huku.

Mpaka sasa kwa mfano dhahiri ni kwamba; tayari wenzetu wa MEDICINE & PHARMACY wamefikia tamati ya maisha yao kielimu hapo chuoni kwao baada ya uongozi wa chuo kuamua kuwasimamisha tena masomo mwanzo huu wa muhula wa pili ambao umeanza tarehe 05/02/2007 wakiwapa muda wa mwisho wa kusubiri pesa zao za ADA kutoka bodi ya mikopo kwa siku 15 yani mpaka tarehe 15/02/2007!
Sasa jee waende wapi? Je serikali mko wapi? Mbona mnatutelekeza ugenini?
“NA SISI WENGINE TUPO KATIKA MKONDO HUO HUO WA KUFUKUZWA HIVI KARIBUNI!! Huku wengi wetu USAJILI (REGISTRATIONS) katika passports zetu zikiwa zimeshamalizika muda wake na hivyo kutupatia usumbufu na vyombo vya Usalama hasa POLISI ambao licha ya kutusumbua mitaani…pia hudiriki hata kutufuata mabwenini na kutukagua! SASA JAMANII AIBU GANI KWA TAIFAAA?!!”
Tunaomba msaada wenu muweze kutunusuru sisi huku kwa jitihada zozote ambazo kama serikali zitakua ndani ya uwezo wenu.

Hili sasa ni ombi kwa ngazi zote za serikali ya mheshimiwa raisi Jakaya M. Kikwete akishirikiana na mawaziri wa wizara mbalimbali,wabunge pamoja na mashirika yote yasiyo ya kiserikali, kwa sababu hizi aibu na fedheha tuzipatazo pia ni kwa Taifa zima!
Tunaomba suala hili lichukuliwe kiserikali zaidi baina ya nchi hizi mbili ili kutunusuru sisi wanafunzi wenu mliotuleta hapa kusoma

“Tafadhali Muheshimiwa Rais KIKWETE tunakuomba uingilie kati suala hili ili vijana wako tuondokane na zahma hii nzito na Kujenga Nguvu kazi ya Taifa Kwa ARI MPYA…. NGUVU MPYA….KASI MPYA!
Hasa ukirejea maneno yako ya busara uliyoyatoa katika mkutano mkubwa na WANAFUNZI wa Vyuo vya Elimu ya Juu uliofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar-es-salaam.”
UMOJA WA WANAFUNZI WA KITANZANIA WALIO KATIKA MATESO – UKRAINE.
 
Invisible,

tunaomba ujitahidi kwa kadri ya uwezo wako kuwasaidia hawa wa'funzi kwani si unaijua hii serikali yetu yaani mpaka ipigwe pressure ndio inazinduka katika usingizi mzito - Yaani hawa jamaa utadhani hawaijui hii hali inayowakuta wa'funzi ambao wanasoma njee? inasikitisha sana.. yaani nnasoma ile barua machozi yanataka kunitoka. Nawaombea Mungu awasaidie
 
JembaJemba,

Kifupi ni hivi:

Nilituma taarifa kwa vyombo vingi vya habari. Sina kumbukumbu ya vyombo vingapi vimeandika habari hii lakini hawa Habari Leo na Tanzania Daima wameandika nakiri. Aidha nawashukuru sana hawa kwa kuona uchungu dhidi ya vijana wetu wanaohangaika ughaibuni. Nahisi Mwananchi waliandika pia.

Tatizo:

Nilipiga simu RTD ambayo ni Radio ya Taifa kwa ujumla wake nikawa held hadi nikasinzia. Nikajaribu kutuma barua pepe lakini majibu niliyopata ni kama ifuatavyo:

Your message has encountered delivery problems:

Delivery failed User's mailbox quota exceeded or would be exceeded
 
Poleni sana wenzetu.
Hii system ya BODI YA MIKOPO NEEDS TO BE OVERHAULED.....Wana JF heads need to roll here.
Hii ni aibu kwa nchi wakati kiongozi wetu akiwa nje akitumia millions of shillings wengine huku wanalia njaa. Kwa kweli kama mwananchi ninayejua situation ya nje ya nchi I AM HURT!. Uzembe huu usivumiliwe it is the same case everywhere hata hapa nyumbani there not performing.With my IT ignorance this is a very simple task.Tunajua shule inafungwa na kufunguliwa lini sasa shida iko wapi?

Mbona hela za safari za WAKUBWA zipo , hazichelewi??? Zikihitajika zinapatikana tu wakati wowote?? TUKO SERIOUS KUILETA REAL MADRID KULIKO KULIPA ADA ZA SHULE????

Is time we set priorities as a nation. KASI MPYA IKO WAPI?

Mh Rais kama ni kweli unasoma humu, mimi kama raia wa Tanzania mwenye mapenzi mema na nchi hii NIKO VERY DISAPPOINTED. MH NINAITAFUTA NAMBA YAKO YA SIMU NA NIKIFANIKIWA KUIPATA I WILL SPEAK TO YOU PERSONALLY.
Mbona mambo hayaendi? What are we not doing right. Kitu simple kama kutuma hela? UKRAINE NI MBALI . HAYA NA HIZO ZA KUPELEKA CRBD??
I AM VERY DISAPPOINTED.
 
BBC wamefanya mahojiano na Balozi chokara kuhusu suala lao angalia dira ya dunia bbc leo..
 
Invisible,

thanx kwa moyo wako thabiti wa kuwasaidia ndugu zetu ambao matatizo yamewabana kwani hatujui kesho itakuwa kwa nani - Mungu atakulipa.

Tunaomba vile vile wale wote ambao wapo nyumbani na wana access na hawa jamaa wa mikopo basi watoe msaada wao, wenzetu wanaumia
 
Salam kwa Wanabodi wa JF.

Kuna maoni yametolewa kuhusu namna ya kusonga mbele kufikia utatuzi wa suala hili. Nami nachangia kama ifuatavyo:

Kwanza, waandishi wa habari walipaswa ku copy-and-paste taarifa ya awali toka kwa Quartz, ili waweze kuchapisha kwenye vyombo vyao. Never underestimate the power of the media. Hawakufanya hivyo, nitafanya mimi. Hili suala lazima litambuliwe na Watanzania wengi au wote ikiwezekana. Hawa ni ndugu zetu, hatuwezi kuwatelekeza.

Pili, limetolewa wazo la kuwachangia. Mimi nitajitahidi niongee na wadau fulani, tufanye hata fund-raiser moja tu, lakini ingekuwa muhimu tujue ni kiasi gani cha deni limebaki, ili angalau, kama inawezekana, tufanye fund-raiser ya kumaliza deni lote au kulipunguza, ndugu zetu hawa waweze kujikimu na kuendelea na masomo yao, kwani Serikali imewasahau. Huu ni uzembe uliokithiri. Aliyeboronga, mimi ningekuwa Rais, sio tu kwamba ningemfukuza kazi, ningemfunga jela pia. Ni criminal negligence!

Tatu, mwenye mawazo mengine achangie. Nawaombeni mnipe full amount ya deni pamoja na full names and addresses za ndugu zetu hawa.

Wasalaam,

MwanaHaki

Naomba kutoa hoja.
 
Hakuna mtu kuchangia wala nini, hiyo itakuwa njia rahisi ya kuidekeza serikali kuwajibika. Binafsi nasema kama tunataka kuchangia iwe under two conditions:

a. Serikali itamke hadharani kuwa imeshindwa kuwasomesha vijana hawa na kutimiza ahadi yake kwao.

b. Prof. Msolla ajiuzulu na kukubali kushindwa kuisimamia bodi ya mikopo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom