Serikali yavunja rekodi ya ukusanyaji mapato na akiba ya dola!

Wana JF kuna habari katika gazeti la habari leo linalosema kuwa serikali ya JK imevunja rekodi ya ukusanyaji wa mapato mwezi Dec, 2010 kwa kukusanya 587bill kati ya malengo ya 570bill na huku ikionyesha kuwa saizi serikali ina akiba ya dola 3.8bill, kiwango hiki ni kikubwa kuliko nchi zote za Afrika Mashariki kwa sasa.
Hoja yangu iko hapa, kama ni kweli basi serikali ya JK inahitaji pongezi kwa kazi nzuri iliyofanya lakini inahitaji kuthamini hasa mfumuko wa bei ambao kwa kiasi kikubwa umesababishwa na kushuka kwa thamani ya Tshs ambayo imesababisha uagizaji wa bidhaa kutoka nje kuwa ghali zaidi hususani mafuta ambayo yanamekuwa yakipanda kila kukicha.
Athari ya kupanda kwa mafuta kutokana na kushuka kwa Tshs kuna dirct impact kwenye ongezeko la bei ambalo ndilo kilio cha wananchi wengi kwa sasa.
Hakuna haja ya kujisifu kwenye makaratasi wakati hali halisi ni mbaya.
Source: HabariLeo | BoT yavunja rekodi akiba ya dola na HabariLeo | TRA yavunja rekodi,yakusanya bil. 580/-.
Nawakilisha kwa mjadala zaidi.

Gazeti la habari leo! Mhhhhh siamini
 
Ukitaka ukosoaji wako uskilizwe, basi kubali mema yakifanyika sio unasema mabaya tuu. JF is too subjective (CHADEMA) and only an objective outlook can lead to the development of Tanzanian society. Bahati mbaya sana quality ya hii forum imekuwa takataka, bora ata ingekuwa kinyesii ni mbolea.. I blame Moderators.... hawana policy objectives... I also blame watu wanaotumia jazba badala ya uchambuzi wa kina na wa haki wa mwenendo wa mambo Tanzania. Mtaishia kuwa wapigakelele tuu. PLZ BLV
 
Rula its Possible labda kwa hii mbinu ya kuunda noti mpya, lakini ki-uchumi ni ndoto kutoka wapi wewe unaishi wapi Rula maana kila kitu kipo wazi na kinaonekana huwezi kuongeza mapata bila kuongezeka kwa "Economic activities" kama "Business Activities" na Investments hasa kwenye land wewe umeona wapi ongezeko la Investments na activities au upo vitani Afganstan???!!!
Mkuu umenifurahisha kutokana na argument yako, nipo Tz mkuu.
 
Mbopo, nimetamani sana kukutukana lakini kwa ethics, believe yangu na kuthamini mawazo ya mtu, nalazimika kuwa kimya, ila kusikitika kwa mtazamo wako huo. Jamani hii ina hitaji degree ngapi mtu kuweza kuona mapungufu mengi ya serikali hii compare kwa hayo unayodhani wameweza kufanya, if u weigh out equal to zero. Hebu point put at least 5 good things ambazo mwananchi wa kawaida anaweza simama , akajisifu na kusema serikali yangu hapa imefanya kitu. Give us example come on. JAMANI TUBADIRIKE, KAMA KIZAZI HIKI TUNAWEZA PINGANA KWA MAMBO YALIYOWAZI INAKUWAJE KWA KIZAZI CHA NYERERE WAZEE WETU HUKO VIJIJINI? This is absolutely very low to urge.
 
..wameongeza bidii ya kukusanya mapato ili wawalipe DOWANS.

..kabla ya kupongeza inabidi ujiulize sababu zilizopelekea ongezeko la ukusanyaji mapato.

..je, huko nyuma kulikuwa na mianya ya kukwepa kodi?

..je, idadi ya walipa kodi imeongezeka?

..je tumewakamua zaidi walipa kodi waaminifu?
 
Sidhani kama kuna ukweli katika hili kwani pia kuna tetesi kuwa mwezi november serikali ilikopa pesa kwa ajili ya mishahara ya watumishi wake Stanbinc Bank...kwani ilikuwa imeisha exhaust source zake zote za pesa,,,yakiwemo mashirika ya umma kama NSSF,NHIF, na mengineyo ambayo huwa inatabia ya kuchota pesa wawapo i deep shit***
Na ukweli kwa wale ambao wanafanya kazi serikalini kuanzia julai 2010 serikali ilianza kubana sana matumizi kwani pesa zilizokuwa zikitumwa katika taasisi zake zilikuwa zimepungua kwa kiasi kikubwa sehemu zingine kwa zaidi ya asilimia 400% hali amabayo imejeopardize shughuli nyingi muhimu na hadi sasa hali ni bado tete na hakieleweki...
WANAJARIBU KURUDISHA IMANI WA WATU WAKE...
 
Mie huwa nasema watu humu JF sio great thinkers at all, ni Great Tanker. Kwa mujibu wa Takwimu za TRA mapato mengi hukusanywa mwezi March, June, Sept. na Dec. Hili linatokana na makampuni mengi kulipa zile ‘ Quarterly Provisional Tax’ kutokana na sheria ya kodi Income Tax Act No. 11 ya 2004. Kwa hiyo ni kweli kabisa hizo pesa zimekusanywa na mfanye tafiti sio kujibu humu kibubusa tu


Me nazan we ndo great tanker mana ungekua great thinker ungejua sbb hawana iyo info uliyonayo wewe ndo mana wamefikilia ivyo
 
BOT na TRA Watanzania tunataka details please. Nimesoma kuna wanachama wa CCM wanataka tuwapige kiss mashavuni TRA na BOT kwa kazi zao, this is not going to happen any time soon...What Tanzanians are asking is this.
1. Huu ukosanyaji kodi umetoka wapi? Wananchi, wafanya biashara, viwanda, mafisadi?
2. BOT, maana ya mapato ni nini? tupe details interest za mikopo kwa mabanki, viwanda, CCM, NEC, JK, au mafisadi? Watanzania tunataka kujua so next time if the amount ikiwa low or higher we should know where are shortcomings...
3. Mikakati gani mnapanga BOT na TRA kuimprove revenues na walipa kodi na systems lini zitakuwa openly to Tanzanians kujua kinachoendelea BOT na TRA? Sijui kama mnajua siku zinakuja hamtakwepa haya? Mnachoficha ni nini?
- Taratibu za ulipaji kodi na mikopo, financial policies za nchi BOT lazima ziwe wazi ili kila Mtanzania aweze kucontribute sio Ofisi ya JK na Waziri wa fedha...elimu zenu zinaonekana ni kutoka chini ya mipapai hata kama mlikuwa na GPA 4.0 college.

"BOT na TRA sio matawi ya CCM kama UVCCM, hivi ni vyombo vya Taifa na utumishi wenu ni hasara kubwa kwa Taifa...kuna ulazima muangalie utandaji wenu ili kuikomboa Tanzania mijini na vijijini - where is Uzalendo wenu?"
 
Sidhani kama kuna ukweli katika hili kwani pia kuna tetesi kuwa mwezi november serikali ilikopa pesa kwa ajili ya mishahara ya watumishi wake Stanbinc Bank...kwani ilikuwa imeisha exhaust source zake zote za pesa,,,yakiwemo mashirika ya umma kama NSSF,NHIF, na mengineyo ambayo huwa inatabia ya kuchota pesa wawapo i deep shit***
Na ukweli kwa wale ambao wanafanya kazi serikalini kuanzia julai 2010 serikali ilianza kubana sana matumizi kwani pesa zilizokuwa zikitumwa katika taasisi zake zilikuwa zimepungua kwa kiasi kikubwa sehemu zingine kwa zaidi ya asilimia 400% hali amabayo imejeopardize shughuli nyingi muhimu na hadi sasa hali ni bado tete na hakieleweki...
WANAJARIBU KURUDISHA IMANI WA WATU WAKE...
Hapo mimi ndipo ninaposhangaa, kuna ukweli kuwa matumizi ya serikali yamepunguzwa sana halafu tena unatuambia serikali imevunja rekodi katika ukusanyaji kisha Benno anakazia kuwa akiba ta dola ni kubwa kuweza kutufikisha import kwa miezi sita!
Hapa ni lazima kutakuwa na propaganda tu. Ndiyo maana nikaamua kushare issue hii na wana JF ambao kwangu mimi ni greater thinkers.
 
....Mtu anayesema kwa sasa kuwa mapato ya serikali yako sawa ..tutamuomba alete bank statement ya akaunti yetu ya nje....kiashirio cha mapato ya nchi kuwa sawa na economic activities.....viwanda vingi vimesimamisha uzalishaji....,hakuna umeme...! matumizi ya makampuni yanaongezeka kwa ajili ya kununua mafuta ya generators
Serikali inashindwa kulipia huduma za wazabuni kwa wakati...ie kuna miradi ya barabara imesimama ..inayoendelea ni ya makampuni makubwa yenye mitaji....

Matukio ya baadhi ya watumishi wa umma kukatwa mshahara sio bahati mbaya bali ni delaying tactics ....ndio maana wanasema watawalipa kwenye mwezi ujao...does it get to your head unakata watu 30,000 na zaidi mshahara ...unasema ni bahati mbaya??

Internal borrowing ya serikali imepunguza kwa kiasi kikubwa kasi waliokuwa nayo mabenki kujitangaza na kupeleka mikopo kwa watu wa chini.....kwani sasa mabenk na taasisi za pesa wanaikopesha serikali..risk free lending...kiuchumi ukitaka taasisi za fedha zipeleke huduma kwa watu....gorvernment need starve them..ikiacha kukopa ..na mabenki biashara yao ni kukopesha pesa ni lazima utayaona mabenki yanahangaika mitaani kuwadikia wananchi wa kawaida....

Katika hali tuliyonayo siamini kama serikali yetu inazopesa...tena kusema tuna reserve kubwa kuliko kenya ..du ..sielewi!
 
..Hata hizi kelele kwa bodi ya mikopo ni wanatolewa kafara tu...ni wazi kama wangekuwa wamepewa pesa ya kutosha na wakazembea ..sasa hivi viongozi wa bodi wangekuwa kizuizini mafia....ni siasa tu lakini serikali hii siri wanaijuwa kuwa pesa wanapeleka bodi kwa mafungu sana kiasi inawawia bodi ugumu kiasi cha kulazimu kuitumia pesa kidogo waliyonayo kama maji ya zimamoto......yaani wakisikia mgomo ndio wanapeleka pesa ...hii nimbaya kwasaababu italeta migomo nchi nzima na mwisho watashindwa kuwalipa wote..na itasababisha vuruugu kubwa saana nchini!!
 
Sikujua kwamba hajaweza kuongeza hata peny ya dola toka aondoke Mkapa akiondoka ndio pesa alizosema ametuachia hata KIkwete mwenyewe alivyofungua Bunge 2005 alisema sasa swali huyu chaliiiii mkwere tumuulize kwa nini hajaongeza kuweka akiba jamani kweli huyu ovyo aondoke
 
Sikujua kwamba hajaweza kuongeza hata peny ya dola toka aondoke Mkapa akiondoka ndio pesa alizosema ametuachia hata KIkwete mwenyewe alivyofungua Bunge 2005 alisema sasa swali huyu chaliiiii mkwere tumuulize kwa nini hajaongeza kuweka akiba jamani kweli huyu ovyo aondoke
Kweli mzee wetu tutamkumbuka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom