Serikali yautetea Muswada wa sheria ya Umeme

August

JF-Expert Member
Jun 18, 2007
8,378
4,033
huu ni ujumbe au mchango wangu kwa Sirikali
Naomba waziri na Serekali ya Tanzania waelewe , sio kwamba watu wanapinga huo mswada, bali timining yake ndio mbaya, kwa sababu wameua shirika la TANESCO kwa maksudi nna baadhi ya watu kujipatia mitaji/mtaji wa kuwekezea kwenye umeme nk halafu watu hao hao wanakuja na mswada wa umeme.Kwa maana nyingine mswada huu unakuwa kama si endelevu , au competitive , kwa sababu mwekezaji moja kashikiliwa chini, i.e kafilisiwa na wakati mwekezaji mwingine anawezeshwa anafungliwa njia. Na anaye fanya hivyo ni mtu huyo huyo, i.e aliye mnyonga mwingine ndio anapata nafasi ya kuwekeza iwe directly or indirectly.
hivyo ni vizuri tuka shughulikia matatizo ya huyu ndugu yetu TANESCO na sababu zilizo mfikisha hapo kabla ya kwenda hatua nyingine.
Hivyo ni juu ya serekali kuharakisha mapitio ya mikataba mibovu iwe ya Tanesco au ya madini kabla hatujapelekana Mbele, kama wanaona kuna umuhimu wa kupitisha huu mswada huu wa Sasa.

Ya Chni ni maelezo ya Sirikali
Serikali yautetea Muswada wa sheria ya Umeme
*Yadai hauna harufu ya rushwa

Na Kizitto Noya


WIZARA ya Nishati na Madini imemsafisha aliyekuwa waziri wake Nazir Karamagi na kusema, hakuna msukumo wowote wa kifisadi katika kutengeneza muswada wa Sheria Mpya ya Umeme na Mafuta ya Petroli unaotarajiwa kuwasilishwa Bungeni mwezi ujao.


Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa fikra zilizojengeka kwamba kuna ujanja katika kutengeneza muswada huo hazina mantiki wala ukweli wowote.


"Wazo kwamba kuna kitu 'nyuma ya pazia' katika kutengeneza muswada huo ni potofu. Napenda kuueleza umma na ndugu zangu (waandishi) mnisaidie kwamba sio kweli, wizara inafanya hivyo kwa maslahi ya Taifa, kusiwe na wazo kwamba msukumo huo wa muswada wa Sheria mpya ya Umeme una maslahi kwa mtu," alisema Ngeleja.


Kauli ya Ngeleja imekuja juma moja tangu wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waukatae tena muswada huo wenye lengo la kufungua milango kwa wawekezaji wa nje kuwekeza katika sekta ya umeme wakidai kuwa bado una harufu ya aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi.


Ngeleja aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa kukataliwa kwa muswada huo kwa sababu yoyote ile, hakutaondoa umuhimu wa kuifanyia marekebisho sheria ya umeme ya mwaka 1931 ambayo kulingana na mabadiliko ya kijamii, imepitwa na wakati.


"Sheria hii ya Umeme ilitungwa mwaka 1931 na ina upungufu mwingi, ni lazima ifanyiwe marekebisho ili iende na wakati,"alisisitiza Ngeleja na kuendelea:


"Hoja kwamba sekta binafsi kwenye umeme itakwamisha mpango wa serikali kupeleka nishati hiyo vijijini siyo kweli kwani hata Tanesco haiwajibiki kupeleka umeme vijijini,"


Alisema hoja hiyo imepitwa na wakati kwani hata Tanesco haiwajibiki kupeleka umeme vijijini bali Serikali kupitia Wakala wa Umeme vijijini (REA) katika mkataba ulioingiwa mwaka 2005.


"Tutunge sheria hii au tusitunge, Tanesco siyo suluhu la tatizo la umeme vijijini, kazi hiyo ni ya serikali kupitia Wakala wa Kusambaza Umeme (REA) tangu mwaka 2005," alisema.


Alisema katika muswada huo wa sheria hiyo mpya, serikali imejitahidi kukwepa kubinafsisha huduma ya umeme kwenye maeneo yanayoweza kuliathiri taifa kama ubinafsishaji wa miundombinu yake.


Alieleza kuwa katika sheria hiyo mpya serikali iliruhusu uwekezaji katika uzalishaji na usambazaji wa umeme maeneo ambayo tayari yamekuwa yakiendeshwa na kampuni za nje.


"Sisi tunaruhusu soko huria katika uzalishaji na usambazaji na siyo usafirishaji na hili sio jambo geni kwani hata sasa maeneo haya tayari yako huru kwa wawekezaji,"alisema.


Hata hivyo alibainisha kuwa kauli za wabunge hao kuhusu muswada huo hazikutolewa ili kuukubali wala kuukwamisha bali ni mapendekezo yatakayotumika kuuboresha zaidi kabla haujaingia bungeni.


"Kukataliwa kwa Muswada huo ni changamoto kwa serikali katika kuuboresha zaidi kwani hayo ni mapendekezo tu na sio msimamo wa mwisho wa wabunge," alisema.


Wabunge hao walionyesha kukerwa na muswada huo katika mjadala uliofanyika Machi 18 mwaka huu jijini Dar es Salaam kuhusiana na mapendekezo ya serikali kutunga sheria mpya ya umeme itakayoruhusu uwekezaji katika sekta hiyo.


Wabunge hao walisema hawajaona tofauti yoyote katika muswada huo na uliowasilishwa mara ya kwanza ambao ulipitiwa na kutolewa mapendekezo ya mabadiliko katika baadhi ya vipengele. chini ya aliyekuwa na waziri wa wizara hiyo, Nazir Karamagi


Walisema muswada huo pia hauonyeshi mpango wowote wa kuweka umeme maeneo ya vijijini ambako ndio kuna wananchi wengi.


Mbunge wa Karatu Dk Willibrod Slaa alitoa angalizo kuwa kwa sasa hakuna kampuni yoyote ya uwekezaji inayoweza kupeleka umeme vijijini na kuitaka serikali kuhakikisha inatekeleza jukumu hilo yenyewe na kuongeza kuwa kuukubali mswada huo ni sawa na kuiweka nchi mikononi mwa wawekezaji.
 
Ngeleja Bwana

tatizo siyo kukataa mswaada tatizo ni watu kutoamini serikali na mipango yake basi tu. Hakikisha wote waliofikisha Tanesco ilipo wanachukuliwa hatua kwanza na hakikisha mnarudisha tanesco katika hali nzuri ya kibiashara kwa kuondoa Mirija yote. Baada ya hapo leteni Mswaada uone kama hautapita.

Unaacha gari la mwenzako umelitoa tairi, huku unatoa competitive tenda ya kutoa usafiri? Unafikiri mwenzako atakubali? Hapa lazima kieleweke, waliofikisha Tanesco ilipo washughulikiwe kwanza vinginevyo watanzania wamehamua kukaa gizani.

Mpaka serikali ifanye kazi yake. Hivi Ngereja hajui waliofikisha tanesco ilipo? Vunja mkataba wa Richmond, na mingineyo au Serikali iingie makubaliano nao ya kuwalipa gharama zao basi.
 
"Hoja kwamba sekta binafsi kwenye umeme itakwamisha mpango wa serikali kupeleka nishati hiyo vijijini siyo kweli kwani hata Tanesco haiwajibiki kupeleka umeme vijijini," Alisema hoja hiyo imepitwa na wakati kwani hata Tanesco haiwajibiki kupeleka umeme vijijini bali Serikali kupitia Wakala wa Umeme vijijini (REA) katika mkataba ulioingiwa mwaka 2005. "Tutunge sheria hii au tusitunge, Tanesco siyo suluhu la tatizo la umeme vijijini, kazi hiyo ni ya serikali kupitia Wakala wa Kusambaza Umeme (REA) tangu mwaka 2005," alisema.

I mean very arrogant, kwanza sisi wananchi we do not need this nonesense and empty debate, hiii awapelekee wabunge tuliowachagua waliomkatalia in the first place, sasa kwa nini anakimbilia kwenye media, badala ya kusubiri bunge? Kama kweli ana uhakika kuwa itapita bungeni then why anaweka mkwara?

Hivi wananchi tunakuwa wajinga kiasi gani, kwamba tumeona NET GROUP ya Mkapa, na yote waliyotufanyia, sasa huyu waziri hana hata aibu kusema kuwa kusambazwa kwa umeme vijijini ni kazi ya independent contractor? Kwani hao wabunge walimkatalia hawayajui hayo anayoyasema? Hiyo sheria ya mawakala kwani ilipitishwa na nani si wabunge, sasa kama wameamua kuwa haifai si moja ya kazi yao kwenye kikako kijacho itakuwa ni kuibadili tu kwa kura 2/3 za wabunge wote, kwa sababu kitendo cha wabunge kumkatalia maana yake ni kwamba hata sheria hii hawakubaliani nayo, ambayo ililetwa bungeni na 'mjanja" Karamagi/Msabaha, na wabunge wakalazimishwa kuipitisha na Lowassa,

Sasa kwa nini huyu waziri anashindwa kusoma alama za nyakati kuhusu wanachokikataa wabunge ni pamoja na mswaada mzima wa 2005 na hiyo REA? ndio maana ninasema kuwa the man ana sounds to be an-arrogant leader kama he is one!
 
Cha ajabu wanaopinga huo muswada hawana sababu zaidi ya majungu yanayomzunguka Karamagi na Tanesco,na cha ajabu hata DK Slaa hajui kuwa kazi ya kupeleka umeme vijijini si kazi ya Tanesco maana ndio utetezi wake wa kuikataa hii bill,na sijui kwanini hapa TANESCO ni issue,kumbukeni Tanesco is not the law ni kampuni tuu tena maskini na iliyoshindwa kazi na wengine wana demand Tanesco iwezeshwe ndio bill ipite,sijui kuna faida gani hapo kwa nchi au katika swala zima la kuleta umeme kwa wananchi? Tanesco ni kampuni kama kampuni nyingine na imeshindwa kazi under monopoly na ni hasara tuu kwa taifa na hakuna chochote tunachopata zaidi ya ukosefu wa umeme,umaskini na bei mbaya ya umeme,tukiendelea kuunda bill kwa kutumia majungu hatutafika popote maana kinachoendelea sasa na hao wabunge ni majungu tuu na wala hakuna fact yeyote ya ku support tuhuma zao,kama kuna watu wamehujumu Tanesco na wanawajua wapeleke kesi ila sio kukataa,statistics zinasikitisha sana kuhusu swala la umeme na hakuna mchawi mwingine zaidi ya sheria zilizopo ambazo zinaipa monopoly Tanesco na mafisadi wenzake ambao wameshirikiana kutuingiza kwenye mikataba ya mabilioni huku hakuna umeme na uliopo ni bei mbaya sana kwa mwananchi wa kawaida,haiingii akilini kutetea Tanesco wakati wanaopata umeme kutoka hiyo kampuni ni less than 10% na ni hasara kila siku na kashfa kibao miaka kibao,wabunge acheni makampuni yafanye kazi hakikisheni tuu mnakusanya kodi zenu na kusimamia fair play kwenye hiyo sector....sijui kama mnajua kuna kampuni kule Mtwara ina uwezo wa kuzalisha zaidi ya 500MW lakini hawawezi kuanza kazi kwa sababu ya sheria zilizopo zinazoipa Tanesco monopoly,its time kuacha majungu kwenye vitu vinavyohusu maisha na maendeleo ya watu.
 
I mean very arrogant, kwanza sisi wananchi we do not need this nonesense and empty debate, hiii awapelekee wabunge tuliowachagua waliomkatalia in the first place, sasa kwa nini anakimbilia kwenye media, badala ya kusubiri bunge? Kama kweli ana uhakika kuwa itapita bungeni then why anaweka mkwara?

Hivi wananchi tunakuwa wajinga kiasi gani, kwamba tumeona NET GROUP ya Mkapa, na yote waliyotufanyia, sasa huyu waziri hana hata aibu kusema kuwa kusambazwa kwa umeme vijijini ni kazi ya independent contractor? Kwani hao wabunge walimkatalia hawayajui hayo anayoyasema? Hiyo sheria ya mawakala kwani ilipitishwa na nani si wabunge, sasa kama wameamua kuwa haifai si moja ya kazi yao kwenye kikako kijacho itakuwa ni kuibadili tu kwa kura 2/3 za wabunge wote, kwa sababu kitendo cha wabunge kumkatalia maana yake ni kwamba hata sheria hii hawakubaliani nayo, ambayo ililetwa bungeni na 'mjanja" Karamagi/Msabaha, na wabunge wakalazimishwa kuipitisha na Lowassa,

Sasa kwa nini huyu waziri anashindwa kusoma alama za nyakati kuhusu wanachokikataa wabunge ni pamoja na mswaada mzima wa 2005 na hiyo REA? ndio maana ninasema kuwa the man ana sounds to be an-arrogant leader kama he is one!

..Field Marshall M net sio kampuni ya umeme is just management consultant firm na hawakuja na mtaji wowote kuongeza chochote katika usambazaji au uzalishaji wa umeme,basically walikuja kusaidia kukusanya madeni ya Tanesco na kujaribu kubadili muundo wa kiutawala ndani ya Tanesco..just BS za Mkapa,mtake msitake sheria zilizopo sasa hivi za umeme(monopoly) hazisaidii kitu na zinaturudisha nyuma sector zote za maendeleo, ndio maana only 10% ya nchi ndio ina umeme na ni very expensive,na lazima mkubali Tanesco haina uwezo wa kuzalisha na kusambaza umeme 100% kwa nchi nzima kwa hiyo makampuni mengine lazima yaruhusiwe kufanya kazi la sivyo tutaenda miaka mingine 50 with the same problem,kuna tatizo gani watu wakaja na mitaji yao wakapewa uwezo wa kuzalisha na kuuza,haya sio madini jamani mana hawachukui kitu kutoka kwetu ni wanatuuzia tuu umeme.
 
basically walikuja kusaidia kukusanya madeni ya Tanesco na kujaribu kubadili muundo wa kiutawala ndani ya Tanesco..

Mkuu wangu Koba,

Hivi unajua kuwa hawa NET ndio waliotumalizia maji yetu kule Mtera, kwa kumtumia mtoto wa Mkapa, Peter kuwalazimisha wataalamu kutoa umeme tu huku wakijua kuwa maji hayatoshi na yanahitaji kuachwa kabisa? je hiyo ilikuwa part ya mkataba wao kuingilia mabwawa?

Halafu walichobadili kwenye muundo na utawala wa Tanesco, so far ni kipi, maan wangefanya kazi nzuri, basi tusingekuwa na huu mjadala kabisaaa na hata waziri asingesumbuana na wabunge? au?
 
Cha ajabu wanaopinga huo muswada hawana sababu zaidi ya majungu yanayomzunguka Karamagi na Tanesco,na cha ajabu hata DK Slaa hajui kuwa kazi ya kupeleka umeme vijijini si kazi ya Tanesco maana ndio utetezi wake wa kuikataa hii bill,na sijui kwanini hapa TANESCO ni issue,kumbukeni Tanesco is not the law ni kampuni tuu tena maskini na iliyoshindwa kazi na wengine wana demand Tanesco iwezeshwe ndio bill ipite,sijui kuna faida gani hapo kwa nchi au katika swala zima la kuleta umeme kwa wananchi? Tanesco ni kampuni kama kampuni nyingine na imeshindwa kazi under monopoly na ni hasara tuu kwa taifa na hakuna chochote tunachopata zaidi ya ukosefu wa umeme,umaskini na bei mbaya ya umeme,tukiendelea kuunda bill kwa kutumia majungu hatutafika popote maana kinachoendelea sasa na hao wabunge ni majungu tuu na wala hakuna fact yeyote ya ku support tuhuma zao,kama kuna watu wamehujumu Tanesco na wanawajua wapeleke kesi ila sio kukataa,statistics zinasikitisha sana kuhusu swala la umeme na hakuna mchawi mwingine zaidi ya sheria zilizopo ambazo zinaipa monopoly Tanesco na mafisadi wenzake ambao wameshirikiana kutuingiza kwenye mikataba ya mabilioni huku hakuna umeme na uliopo ni bei mbaya sana kwa mwananchi wa kawaida,haiingii akilini kutetea Tanesco wakati wanaopata umeme kutoka hiyo kampuni ni less than 10% na ni hasara kila siku na kashfa kibao miaka kibao,wabunge acheni makampuni yafanye kazi hakikisheni tuu mnakusanya kodi zenu na kusimamia fair play kwenye hiyo sector....sijui kama mnajua kuna kampuni kule Mtwara ina uwezo wa kuzalisha zaidi ya 500MW lakini hawawezi kuanza kazi kwa sababu ya sheria zilizopo zinazoipa Tanesco monopoly,its time kuacha majungu kwenye vitu vinavyohusu maisha na maendeleo ya watu.

Ndugu yangu naona umekurupuka tu na kuanza kutoa shutuma. wabunge siku hizi ndugu yangu wanapata misaada kutoka kwa wataalam mbalimbali wanaopenda nchi yao na vijana wanaosoma hiyo miswada na kucompare nchi nyingine duniani. Usione wabunge ni wajinga.

Kwani muswada unataka nini hasa kwenye hili?? Umeusoma ukaelewa??

Ngoja nikupe picha tu, walichokuwa wanataka kina Lowassa, Rostam/Karamagi ni kuwa na permanent Richmond na sio small tender ya miaka miwili tu. Muswada unazungumzia zaidi uzalishaji wa umeme na sio miundombinu iwe privatized. Hiyo mwanangu ni code name ya kuwa na lucrative power generation contract which will be force fed by long term contract to Tanesco since the law stipulates only Tanesco can own the transportation system.

Kinachotakiwa kufanywa ni very simple:::

1. Serikali kuondoa mikataba yote ya IPTL, SONGAS, KIWIRA, ALSTOM, DOWANS kwenye responsibility ya Tanesco na kuwapa hao wawekezaji wanaopigiwa kelele.

Tanesco will then be in a level playing field, then we can start market forces talk.

Bila hilo ni mchezo wa kuigiza tu na itakuwa vigumu sana na hii new internet age kwa serikali kuget away na hivi videal mshenzi bila wananchi kuambiwa ukweli.
 
Kinachotakiwa kufanywa ni very simple:::

1. Serikali kuondoa mikataba yote ya IPTL, SONGAS, KIWIRA, ALSTOM, DOWANS kwenye responsibility ya Tanesco na kuwapa hao wawekezaji wanaopigiwa kelele.

Tanesco will then be in a level playing field, then we can start market forces talk.

moelex23 I support you 100%. Kuna ugumu gani kufuta hiyo mikataba ya makampuni yaliyotajwa hapo juu?? Mawazo yangu, mikataba hiyo ifutwe tanesco ibakie kama yenyewe, then hao wengine kama wanataka wazalishe umeme wao na kuusambaza na kuuza kwa wanachi. Kwa sasa hapo Tanesco walipo hawawezi kushindana na wakina IPTL, Richmond wakati huo huo waendelee kuwalipa Mabilioni ya shilingi kwa mwezi.

Ngeleja nadhani ana uwezo mkubwa sana ila sasa anapata mashinikizo ya kisiasa zaidi. Siamini kuwa Ngeleja ninayemfahamu mimi haelewi kuwa kuna mapungufu Tanesco pia kuna Mapungufu kwenye hiyo mikataba, na pia akiruhusu makampuni mengine kutoka nje kuja kushindana na Tanesco ambayo ni marehemu ndio kuizika kabisa.

Cha maana naona waiweke kwanza sawa hiyo mikataba ya hayo makampuni yanayoinyonya Tanesco ndio wafikie huko kwenye kuruhusu makampuni mengine ya nje.
 
Serekali inacho taka ni sawa na kuweka carpet mpya ndani ya nyumba bila kutoa vumbi.
Sasa ili tusi fukie au kuficha vumbi chini ya carpet, kwanza tujiulize tumetoka wapi na tunakwenda wapi, na wapi tulipopotea.
Na kuhusu suala la umeme vijiji lilikuwepo kabla ya hiyo sheria ya kitaperi 2005. Je nini ilikuwa sababu ya hiyo act 2005? Maana najua na kukumbuka kuwepo kwa mradi wa Umeme vijijini toka enzi za Mwalimu.
Pili nini ulikuwa mpango wa muda mrefu wa uzalishaji umeme bongo pale wizarani na TANESCO, maana wote hao walikuwa na mipango ya muda mrefu.Na vyanzo vyake vilikuwa vipi? ( Master Plan ya Uzalishaji na Usambazaji Umeme Bongo iwe mjini au vijijini.) Ndio ijadiliwe kwanza tukijiridhisha na uzuri wake au ubaya wake ndipo tuweke hii nyongeza ya the pproposed energy bill.
 
..Field Marshall M net sio kampuni ya umeme is just management consultant firm na hawakuja na mtaji wowote kuongeza chochote katika usambazaji au uzalishaji wa umeme,basically walikuja kusaidia kukusanya madeni ya Tanesco na kujaribu kubadili muundo wa kiutawala ndani ya Tanesco..just BS za Mkapa,mtake msitake sheria zilizopo sasa hivi za umeme(monopoly) hazisaidii kitu na zinaturudisha nyuma sector zote za maendeleo, ndio maana only 10% ya nchi ndio ina umeme na ni very expensive,na lazima mkubali Tanesco haina uwezo wa kuzalisha na kusambaza umeme 100% kwa nchi nzima kwa hiyo makampuni mengine lazima yaruhusiwe kufanya kazi la sivyo tutaenda miaka mingine 50 with the same problem,kuna tatizo gani watu wakaja na mitaji yao wakapewa uwezo wa kuzalisha na kuuza,haya sio madini jamani mana hawachukui kitu kutoka kwetu ni wanatuuzia tuu umeme.

Probably na wewe unataka ujipatie ka mkataba kauzalishaji na usambazaji umeme! Sio vibaya ila where fact are discussed it better to stick to them! Hivi wewe umeusoma ule mswada lakini?

Usitumie statistics mbovu kama hizi eti 10% ndio ina umeme ivi 10% ya Tz si ni mikoa 2.7! Una uhakika na hizi takwimu? na je hao unaowashabikia waje kufanya uzalishaji na usambazaji kwa 90% ya Tz iliyobaki kwa rekodi zako una uhakika na uwezo wao? na je ni kitu gani kinaifanya Tanesco isiweze???
Suala la muhimu ni kuipunguzia Tanesco mizigo mizito iliyojitwika ili waweze kukamilisha miradi yao!!
 
Ndugu yangu naona umekurupuka tu na kuanza kutoa shutuma. wabunge siku hizi ndugu yangu wanapata misaada kutoka kwa wataalam mbalimbali wanaopenda nchi yao na vijana wanaosoma hiyo miswada na kucompare nchi nyingine duniani. Usione wabunge ni wajinga.

Kwani muswada unataka nini hasa kwenye hili?? Umeusoma ukaelewa??

Ngoja nikupe picha tu, walichokuwa wanataka kina Lowassa, Rostam/Karamagi ni kuwa na permanent Richmond na sio small tender ya miaka miwili tu. Muswada unazungumzia zaidi uzalishaji wa umeme na sio miundombinu iwe privatized. Hiyo mwanangu ni code name ya kuwa na lucrative power generation contract which will be force fed by long term contract to Tanesco since the law stipulates only Tanesco can own the transportation system.

Kinachotakiwa kufanywa ni very simple:::

1. Serikali kuondoa mikataba yote ya IPTL, SONGAS, KIWIRA, ALSTOM, DOWANS kwenye responsibility ya Tanesco na kuwapa hao wawekezaji wanaopigiwa kelele.

Tanesco will then be in a level playing field, then we can start market forces talk.

Bila hilo ni mchezo wa kuigiza tu na itakuwa vigumu sana na hii new internet age kwa serikali kuget away na hivi videal mshenzi bila wananchi kuambiwa ukweli.

...mimi sitakuita umekurupuka lakini naona hujaelewa nini kinachokusudiwa kwenye hiyo bill na ninakushauri kasome uelewe kwanza kabla ya kuleta any debate,bill inachotaka kufanya ni very simple KUONDOA SHERIA YA 1931 INAYOIPA TANESCO MONOPOLY,sasa sijui mambo ya mikataba ya mafisadi wa IPTL,Richmond etc imeingia vipi hapo? hatuongelei kampuni hapa(Tanesco),tunaongea sheria ambazo zita guide sector ya umeme Tanzania,hayo mambo ya inefficient ya Tanesco na hizo kampuni za kifisadi zilizoingia mkataba nayo ni issue nyingine kabisa na kukataa au kukubali hii bill wala haitasaidia kubadilisha hiyo mikataba kabisa,educate yourself!
 
umProbably na wewe unataka ujipatie ka mkataba kauzalishaji na usambazaji eme! Sio vibaya ila where fact are discussed it better to stick to them! Hivi wewe umeusoma ule mswada lakini?

Usitumie statistics mbovu kama hizi eti 10% ndio ina umeme ivi 10% ya Tz si ni mikoa 2.7! Una uhakika na hizi takwimu? na je hao unaowashabikia waje kufanya uzalishaji na usambazaji kwa 90% ya Tz iliyobaki kwa rekodi zako una uhakika na uwezo wao? na je ni kitu gani kinaifanya Tanesco isiweze???
Suala la muhimu ni kuipunguzia Tanesco mizigo mizito iliyojitwika ili waweze kukamilisha miradi yao!!

...thats a cheap shot hapo,hiyo 10% is a factual,seems unaoperate through majungu na sio statistics,anyway hakuna sababu ya kuendelea kubishana ila to me sioni sababu ya kuendelea kuipa Tanesco monopoly na kupump more money wakati sector inaendelea kurudi nyuma
 
Huo mswada tutaupataje ili tuweze kuuona???

About the electricity distribution in TZ, check this out from Tanesco website http://www.tanesco.com/ under >> National Grid >> Transmission

The Distribution System Network Supply Voltage are 33 kV and 11 kV which serve as the back bone stepped down by distribution transformers to 400/230 volts for residential, light commercial and light industrial supply. There are big commercial and heavy industries supplied directly at 33 kV and 11 kV. By the end of year 2006, there were estimated 9,796 km of 33 kV lines; 4,439 km of 11 kV lines, 21,225 km of LV lines and 7,203 distribution transformers, connecting 602,500 customers in Tanzania Mainland.



The major challenges facing the transmission and distribution systems are:



(i) In order to enhance power supply and meet future demand, it is proposed to look for capital for strengthening the high voltage power lines and embark on urgent maintenance, upgrading and expansion of the current transmission and distribution systems. This would reduce the frequency of power interruptions and improve voltage conditions at consumer’s premises.



(ii) Vandalism of tower members has also been an acute problem associated with the transmission lines while in the distribution side there are problems of theft of transformer oil, stealing conductors, and outright theft of electricity through illegal service lines and meter tampering. This is despite efforts to make villages to participate more in the security of the lines by engaging in village contracts; starting a Hotline Centre in Dar es Salaam where confidential tip-offs of suspects are handsomely rewarded; and intensified public education using the mass media and outdoor advertisements.
 
#^$^$&$&*((+()&(^*$$^&..........Damn Ngeleja ............wanao-support muswada y'all don't know what is behind.

Huu muswada ni wa kuwafunika na kuwanufaisha MAFISADI wa IPTL, SONGAS, RICHMOND, KIWIRA and more to come
 
...thats a cheap shot hapo,hiyo 10% is a factual,seems unaoperate through majungu na sio statistics,anyway hakuna sababu ya kuendelea kubishana ila to me sioni sababu ya kuendelea kuipa Tanesco monopoly na kupump more money wakati sector inaendelea kurudi nyuma

Ndugu yangu Koba TANESCO ni ya waTZ wabunge wanahaki kuipatia kinga zote kwani hapo ilipo wanajua ni mafisadi pekee wameweza kuprogram na kufanikiwa kuilaza ICU,Sasa kiulaini kabisa hao wahusika mafisadi ndio haohao tayari wamejiandaa kuitibu TANESCO kwa kuja na sheria ambayo wabunge na wanainchi kwa ujumla wameishutukia na kusema bado kuna harufu ya Kikaramangi ndani ya pazia na ni wazi kuwa Wazee nao na kampuni zao wanatia mkazo sheria ipite ama sivyo watakula hasara, ila kwa kifupi ni kwamba katika ngoma hii Serikali imeng'ang'ania Ugali na wabunge wana mboga mkononi halafu ukisema suu namwaaga na tukose wote
 
...mimi sitakuita umekurupuka lakini naona hujaelewa nini kinachokusudiwa kwenye hiyo bill na ninakushauri kasome uelewe kwanza kabla ya kuleta any debate,bill inachotaka kufanya ni very simple KUONDOA SHERIA YA 1931 INAYOIPA TANESCO MONOPOLY,sasa sijui mambo ya mikataba ya mafisadi wa IPTL,Richmond etc imeingia vipi hapo? hatuongelei kampuni hapa(Tanesco),tunaongea sheria ambazo zita guide sector ya umeme Tanzania,hayo mambo ya inefficient ya Tanesco na hizo kampuni za kifisadi zilizoingia mkataba nayo ni issue nyingine kabisa na kukataa au kukubali hii bill wala haitasaidia kubadilisha hiyo mikataba kabisa,educate yourself!

Koba unaweza kushinda katika mambo mengine hila kwa hili labda kama sisi ni wageni katika tanzania utashinda. Lakini tanzania tunayoijua You cant convice us!
 
Hivi watu mnafikiri Mkapa na Yona kuwahi na kuihodhi Kiwira walikuwa wajinga eeehhh
 
....endeleeni kutetea monopoly & give more money to Tanesco,lakini at the end of the day this is what you get,na msitegemee chochote kama fundamental changes katika sheria zetu za umeme hazitabadilika.




wafanyakazi kuandamana kupinga bei ya umeme

2008-03-27 08:36:55
Na Thobias Mwanakatwe, PST Mbeya


Zaidi ya wafanyakazi 10,000 wa mkoani Mbeya, wamepanga kuandamana Jumamosi hii kwa kuvishirikisha vyama vyote vya wafanyakazi nchini kupinga pendekezo la Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) la kuongeza bei ya umeme.

Tamko la kufanyika kwa maandamano hayo, lilitolewa jana kwenye Mkutano Mkuu wa viongozi wote wa matawi kutoka vyama shiriki vya Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi (TUCTA) uliofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Wafanyakazi jijini Mbeya.

Mkutano huo uliowajumuisha wajumbe kutoka wilaya zote za mkoa huo ambao kwa kauli moja walikubaliana kuandamana ili kupinga nia ya Tanesco kuongeza tena bei ya umeme na kuwaongezea wananchi ukali wa maisha.

Wajumbe wa mkutano huo walisema katika maandamano hayo watashinikiza pia wale wote waliohusika kwenye kashfa ya mikataba mibovu ya umeme kushughulikiwa haraka badala ya siasa za vyama kuingizwa kwenye masuala mazito ya kitaifa na kuwaacha wananchi wakiendelea kuumia.

Mratibu wa mkoa wa TUCTA, Bw. Thomas Kasombwe, alisema kuwa uamuzi huo wa kuandamana kwa amani wameona kuwa ndiyo njia pekee itakayoweza kuifikishia ujumbe serikali kuwa wakati wa mafisadi kuendelea kuitafuna nchi unaelekea kikomo.

Alisema mbali ya kuitaka serikali isitishe mara moja ulipaji wa fedha hizo kwenye kampuni hewa ya Richmond kwa upande mwingine waliipongeza serikali kwa hatua iliyochukua ya kuanza kushughulikia suala la kampuni hiyo na kutaka wote waliohusika kuchukuliwa hatua kali.

Kasombwe alisema kuwa maandamano hayo makubwa na ya aina yake yatahudhuriwa na wananchi wa kawaida ambao kwa kiasi kikubwa ndio waathirika wa kwanza hasa ikilinganishwa kuwa vipato vyao ni vya chini na hawawezi kumudu kabisa kuendelea kulipia gharama kubwa za umeme.

Mgeni rasmi katika maandamano hayo atakuwa Naibu Katibu Mkuu wa TUCTA, Taifa Bw. Nicolaus Mgaya, atakayepokea maandamano yao katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine pia yataongozwa na vikundi kadhaa vya burudani.

SOURCE: Nipashe
 
....endeleeni kutetea monopoly & give more money to Tanesco,lakini at the end of the day this is what you get,na msitegemee chochote kama fundamental changes katika sheria zetu za umeme hazitabadilika.




wafanyakazi kuandamana kupinga bei ya umeme

2008-03-27 08:36:55
Na Thobias Mwanakatwe, PST Mbeya


Zaidi ya wafanyakazi 10,000 wa mkoani Mbeya, wamepanga kuandamana Jumamosi hii kwa kuvishirikisha vyama vyote vya wafanyakazi nchini kupinga pendekezo la Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) la kuongeza bei ya umeme.

Tamko la kufanyika kwa maandamano hayo, lilitolewa jana kwenye Mkutano Mkuu wa viongozi wote wa matawi kutoka vyama shiriki vya Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi (TUCTA) uliofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Wafanyakazi jijini Mbeya.

Mkutano huo uliowajumuisha wajumbe kutoka wilaya zote za mkoa huo ambao kwa kauli moja walikubaliana kuandamana ili kupinga nia ya Tanesco kuongeza tena bei ya umeme na kuwaongezea wananchi ukali wa maisha.

Wajumbe wa mkutano huo walisema katika maandamano hayo watashinikiza pia wale wote waliohusika kwenye kashfa ya mikataba mibovu ya umeme kushughulikiwa haraka badala ya siasa za vyama kuingizwa kwenye masuala mazito ya kitaifa na kuwaacha wananchi wakiendelea kuumia.

Mratibu wa mkoa wa TUCTA, Bw. Thomas Kasombwe, alisema kuwa uamuzi huo wa kuandamana kwa amani wameona kuwa ndiyo njia pekee itakayoweza kuifikishia ujumbe serikali kuwa wakati wa mafisadi kuendelea kuitafuna nchi unaelekea kikomo.

Alisema mbali ya kuitaka serikali isitishe mara moja ulipaji wa fedha hizo kwenye kampuni hewa ya Richmond kwa upande mwingine waliipongeza serikali kwa hatua iliyochukua ya kuanza kushughulikia suala la kampuni hiyo na kutaka wote waliohusika kuchukuliwa hatua kali.

Kasombwe alisema kuwa maandamano hayo makubwa na ya aina yake yatahudhuriwa na wananchi wa kawaida ambao kwa kiasi kikubwa ndio waathirika wa kwanza hasa ikilinganishwa kuwa vipato vyao ni vya chini na hawawezi kumudu kabisa kuendelea kulipia gharama kubwa za umeme.

Mgeni rasmi katika maandamano hayo atakuwa Naibu Katibu Mkuu wa TUCTA, Taifa Bw. Nicolaus Mgaya, atakayepokea maandamano yao katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine pia yataongozwa na vikundi kadhaa vya burudani.

SOURCE: Nipashe


na Irene Mark

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja, amesema hakutakuwa na mgawo wa umeme mwaka huu.
Alitoa kauli hiyo alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana alipokuwa akizungumzia ugunduzi wa gesi asilia katika eneo la Uyuni, Mashariki mwa Kisiwa cha Songosongo wilayani Kilwa.

Alisema ipo mikakati ya makusudi ya kuzuia kuwapo kwa hali hiyo nchini licha ya maji yaliyopo kwenye vyanzo mbalimbali vya nishati hiyo muhimu kutosha kwa kipindi hiki.

“Hakuna mgawo wa umeme, kwa sasa maji yapo ya kutosha katika mabwawa yetu…kwa hali hii hatuutarajii mgawo kwa mwaka huu kabisa lakini pia tuombe Mungu hali isibadilike.

“Hali ya maji, mipango na mikakati yetu ipo vizuri, napenda kuwahakikishia kuwa hakuna mgawo mwaka huu,” alisisitiza Ngeleja na kuongeza kwamba, serikali inajitahidi kuzuia hali hiyo kama ilivyotokea mwaka 2006.
Siku saba zilizopita, Mkurugenzi wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO), Idris Rashid, alikaririwa akitahadharisha kuwapo kwa mgawo wa umeme nchini.

Alisema kutokuwapo kwa mvua za kutosha ni moja ya sababu zitakazoleta mgawo wa umeme mwakani, licha ya shirika hilo kuhitaji sh trilioni 1.6 kwa ajili ya kujiimarisha kiuchumi.

Kuhusu gesi hiyo, alisema kampuni iliyoigundua ni Ndovu Resources Ltd kutoka Australia, yenye mkataba wa kutafuta mafuta ya petroli na gesi tangu Mei 19, mwaka 1999.

Alisema licha ya kugundua uwepo wa gesi hiyo, Kampuni ya Ndovu pia imechimba visima vitatu katika maeneo ya Uyuni, Kiliwani na Kiliwani North.

Alisema gesi hiyo iligundulika Machi 13 mwaka huu, kufanya visima vinavyotoa gesi nchini kufikia vinne katika maeneo mbalimbali nchini, yakiwamo yanayopakana na Bahari ya Hindi. Pamoja na Uyuni, maeneo mengine yaliyogunduliwa gesi ni Songosongo, Mnazi Bay na Mkuranga.

Katika hilo, alibainisha kwamba kutokana na ugunduzi wa visima hivyo vya gesi, serikali inaokoa kiasi kikubwa cha fedha zilizotakiwa kutumika kwa kuagiza mafuta ya dizeli nje ya nchi kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli mbalimbali.

“Mfano katika mradi wa Songosongo kuanzia Juni 2004, gesi inayozalishwa inasaidia kutengeneza umeme kama nishati ya viwandani. Kiasi cha gesi kilichothibitishwa ni takriban futi za ujazo 540 bilioni.

Katika kipindi hiki taifa limeokoa dola za Marekani 992 milioni na vivyo hivyo katika mradi wa Mnazi Bay, ulioanza kuzalisha gesi ya ujazo wa futi 400 bilioni tangu Desemba mwaka 2006, umeokoa dola za Marekani 2.1 milioni,” alisema Ngeleja.

Mbali na hayo, alizungumzia mjadala wa wabunge kuhusu kukataliwa kwa muswada wa umeme na kufafanua kwamba, lengo si kubinafsisha Shirika la Umeme, badala yake ni kubadilisha sheria ya umeme ya mwaka 1931 ambayo imepitwa na wakati.

Aidha, aliitaka jamii ifahamu kwamba kupita au kutopita kwa muswada huo hakuhalalishi ubinafsishwaji wa TANESCO, na kuongeza kwamba wizara yake inaendelea kuufanyia marekebisho muswada huo.

Kuhusu dhana kwamba ipo faida inayopatikana kwa baadhi ya watendaji wa serikali ama wafanyabiashara, Waziri Ngeleja alikanusha na kusema uharakishwaji wa muswada huo unatokana na masilahi yake kwa jamii na taifa kwa jumla.

“Wapo baadhi ya watu wanadhani kwamba, kuna jambo nyuma ya pazia, lakini hakuna kitu, tunaipenda nchi yetu na tunafanya hivi kwa manufaa ya taifa kutokana na muswada uliokuwapo wa mwaka 1931 kupitwa na wakati. Mara zote unafanyiwa marekebisho lakini hayatoshi,” alisema Ngeleja.

Alisema, hivi sasa TANESCO linajiendesha kibiashara zaidi, hali iliyosababisha serikali kukatisha ruzuku kwa shirika hilo. Hivyo hata sheria ikipitishwa halitabinafsishwa.

Alisema: “Wizara inazingatia mapendekezo ya wabunge na itayafanyia kazi, lakini napenda wananchi waelewe kuwa Shirika la Umeme halitabinafsishwa na wala hakuna chochote nyuma ya pazia kuhusu muswada huu.”

Source: Tanzania Daima
 
Ni Juzi Juzi Tulipata Msiba Mzito Na Hata Tanga Hatujaanua, Jamani Naomba Serikali Msitupeleke Puta Namna Hii Hata Mpirani Kuna Kipindi Cha Mapumziko, Tuoneeni Huruma Jamani Na Sisi Tumeumbwa Na Huyu Huyu Mungu!!
 
Back
Top Bottom