Serikali yatoa tahadhari ya Virusi Corona, yasema hakuna mgonjwa Tanzania

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
1579851511911.png

Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto imetoa tahadhari ya mlipuko wa ugonjwa wa homa ya mafua makali unaosababishwa na kirusi aina ya Corona, uliozikumba nchi za China, Thailand, Japan, Korea Kusini na Marekani.

Wizara imesema kuanzia Desemba mwanzo mwaka jana wamekuwa wakiufuatilia ugonjwa huo tangu ulipotokea katika nchi ya China, Thailand, Japan, Korea ya Kusini na Marekani.

Imeeleza kuwa ugonjwa huo huambukizwa kwa njia ya hewa kwa kuingiwa na maji maji yenye virusi kutoka kwa mtu mmoja kwa njia ya kukohoa au kupiga chafya au kwa kugusana majimaji au makamasi kutoka kwa mgonjwa aliyethibitishwa kuwa na ugonjwa huo.

Takwimu za ugonjwa huo zinaonyesha kuwa hadi kufikia tarehe 23 Januari 2020 watu wapatao 560 wameathirika huku vifo vikiwa ni 17 ambapo China imethibitisha wagonjwa 550 na vifo 17, Thailand wagonjwa wanne hakuna vifo, Hongkong wagonjwa wawili na Marekani pamoja na Japan zimethibitika kuwa na mgonjwa mmoja mmoja.

Dalili za ugonjwa huo ni homa na mafua makali, kuumwa na kichwa, mwili kuchoka, kikohozi, kubanwa mbavu, maumivu ya misuli, vidonda vya koo, kuathiri mapafu, kupumua kwa shida na hata kifo.

Taarifa ya wizara imeeleza kuwa hadi sasa Tanzania haina mgonjwa , hivyo kutokana na mwingiliano mkubwa wa kibiashara na kijamii kati ya Tanzania na nchi za bara la Asia ikiwamo China na Tanzania inakuwa katika hatari ya ugonjwa huo.

“Wizara inapenda kutoa tahadhari kwa wananchi wote hususani ambao wanasafiri kwenda kwenye mataifa yaliyoathiriwa na mlipuko huo na wale ambao wanapokea wageni kutoka katika nchi hizo,” ilieleza taarifa hiyo.
 
Ingawa Shirika la afya duniani bado hawajasema kuwa ni janga la kimataifa. Hii haitufanyi kutokuchukua hatua.

-Ukisikia homa kali na mafua fika hospitali haraka sana,tena hasa kama ulitembelea China.

-Incubation period ni kuanzia siku mbili mpaka saba.

Afya yako,uhai wako,juu yako.
CHUKUA TAHADHARI.
 
Ingawa Shirika la afya duniani bado hawajasema kuwa ni janga la kimataifa. Hii haitufanyi kutokuchukua hatua.
-Ukisikia homa kali na mafua fika hospital haraka sana,tena hasa kama ulitembelea China.
-Incubation period ni kuanzia siku mbili mpaka saba.
Afya yako,uhai wako,juu yako.
CHUKUA TAHADHARI.
Ushauri mzuri sana ! Kuchukua tahadhari ni muhimu na gharama ndogo kuliko kujitibu.
 
Tatizo sio hakuna mgonjwa. Watu anakwenda China na Kurudi. Tunajipanga vipi kuzuia tusiletewe Corona nchini mwetu.
 
Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, imewatahadharisha wananchi kujilinda na tishio mpya la ugonjwa mpya unaosababishwa na kirusi Cha Corona(Novel Corona Virus 2019- nCoV) ambao umelikumba taifa la China na kuwepo kwa taarifa kusambaa katika Mataifa Mengine.

Akizungumza na Wanahabari leo Bungeni Jijini Dodoma, Waziri wa Afya maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Mhe.Ummy Mwalimu, kuhusu ugonjwa huo, amesema ingawa kwa hapa nchini hakuna mgonjwa wala mtu anayehisiwa kuwa na ugonjwa huo, lakini amewataka wananchi kuchukua hatua ya kujilinda na kirusi hicho hatari.

"Wizara ya Afya inaendelea kutoa tahadhari kwa umma kuhusu Maendeleo ya mlipuko wa ugonjwa wa homa Kali ya Mapafu inayosababishwa na kirusi aina ya Corona ulioikumba nchi ya China na nyingine na umekuwa ukisambaa kwa kasi sana ambapo kumekuwa na ongezeko la wagonjwa pamoja na vifo katika kipindi kifupi" amesema Waziri Ummy.

Amesema kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) tangu mlipuko wa ugonjwa huo uanze katika Mji wa Wuhan uliopo katika jimbo Hubel Nchini China mwezi Disemba, 2019 hadi 28, Januari 2020 na jumla ya watu 4593 wamethibitishwa na 4537 na vifo 106 kutoka China.

Aidha ameongeza kuwa "Ugonjwa huu umesambaa na Mataifa mengine 14 Duniani zikiwemo Japani, Jamhuri ya Korea, Vietnam, Sangapore, Australia, Malaysia,Nepal, Sri Lanka, Marekani, Canada, Ufaransa Ujerumani, Cambodia na Thailand," amesema.

Amesema Ugonjwa huo husababishwa na kirusi Cha Corona ambacho ni tofauti na virusi vingine vya Jamii hiyo ambavyo viliwahi kusababisha na kusababisha milipuko ya Magonjwa kama "SARS-CoV" na MERS-CoV Corona Virusi mwaka 2013.

Amesema kuwa "Dalili za ugonjwa huu ni pamoja Homa, mafua kuumwa kichwa, Mwili kuchoka, kikohoz, kubanwa mbavu, maumivu ya misuli, vidonda vya Koo, Mapafu kuathirika, kupumua kwa shida na hata kifo, ugonjwa huo hauna chanjo Wala tiba ya moja kwa moja" amesema.

Aidha amesema Kama Wizara wanafanya kila jitihada kuhakikisha wanazuia ugonjwa huo kuingia hapa nchini, kwa kufanya jitihada mbalimbali pia wanafanya maandalizi endapo ugonjwa huo utaingia namna ya kuukabili kwa kutenga maeneo maalumu.

Pia amewatahadharisha watu wanaotarajia kusafiri kwenda Mataifa hayo ambako ugonjwa huo upo au wanahisiwa kuwa na mlipuko huo, huku akibainisha hakuna mtanzania ambaye anaishi nchini China kaathirika na ugonjwa huo wote wapo salama mpaka Sasa.
 
Utamu wa supu ya popo wanywe wao tabu waipe Dunia hiyo Nchi ipangiwe chakula badala.
 
Baada ya hali kuwa mbaya nchini China Kufuatia mlipuko wa ugonjwa wa Corona, hadi kusababisha vifo vya watu 425 .

Wapo watanzania waliko huko ikiwemo wafanyabishara na wanafunzi.Hivi punde Milard Ayo kwenye ukarasa wake alituwasilishia taarifa ya Afisa habari Jumuiya ya Wanafunzi Watanzania walioko Wuhan(China) akisema kwamba wuhan ndio eneo lenye watanzania wengi zaidi na hali sio shwari hapo wuhan, japo kuwa hakuna mtanzania aliyepata maambukizi ikiwashauriwa wasitoka nje bila mask

Je huku nyumbani Tanzania Wizara ya mambo ya Nje na Afya zinachukua tahadhari zipi kuzuia kuingia ugonjwa huu?

Hawa ndugu zetu tunawasaidiaje wakihitaji kurudi au wakiwa huko?
 

Attachments

  • oJLXPyGquo1TdVBm.mp4
    6.8 MB
Baada ya hali kuwa mbaya nchini China Kufuatia mlipuko wa ugonjwa wa Corona, hadi kusababisha vifo vya watu 425.

Wapo watanzania waliko huko ikiwemo wafanyabishara na wanafunzi. Hivi punde Milard Ayo kwenye ukarasa wake alituwasilishia taarifa ya Afisa habari Jumuiya ya Wanafunzi Watanzania walioko Wuhan (China) akisema kwamba wuhan ndio eneo lenye Watanzania wengi zaidi na hali sio shwari hapo Wuhan, japo kuwa hakuna mtanzania aliyepata maambukizi ikiwashauriwa wasitoka nje bila mask.

Je, huku nyumbani Tanzania Wizara ya mambo ya Nje na Afya zinachukua tahadhari zipi kuzuia kuingia ugonjwa huu? Hawa ndugu zetu tunawasaidiaje wakihitaji kurudi au wakiwa huko?
 
Waaafrika wana kinga imara ya haya magonjwa ya watu weupe na wa njano.. Lakini kwa hali ilivyo ni vema wakabaki huko chini ya karantine kwakuwa kitendo cha kutoka Wuhan mpaka airport kitawaweka kwenye hatari ya maambukizi na kusambaza

Jr
 
ALERT! ALERT! coronovirus already spreaded to Mombasa a Chinese is undergoing treatment at mombasa Hospital. He has infected the Doctors and Nurses and whoever was handling him.

Kindly be aware of any handshakes. Or a crowded place where a person is coughing or sneezing... It's contagious. Drink lots of water ni keep yourself and children hydrated Avoid foods sold on the streets... Especially children whose immune system is low. Pass this message to others prevention is better than cure

Jr
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom