Serikali yatoa siku 4 kwa wafanyabiashara wa Korosho kusema tani wanazohitaji. Baada ya hapo hawataruhusiwa tena kununua

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
SERIKALI YATOA SIKU NNE KWA WANUNUZI WA KOROSHO

*Yawataka waandike barua wakionesha tani wanazohitaji na lini watazichukua

*Yasema zaidi ya hapo haitoruhusu kampuni yoyote kununua korosho tena

SERIKALI imetoa siku nne kwa wanunuzi wote 35 waliojiandikisha kununua korosho wawe wamepeleka barua katika Ofisi ya Waziri Mkuu wakionesha kiasi cha tani wanazohitaji na lini watazichukua.

“Hivyo wanunuzi waliojiandikisha wakiwemo na wale wote ambao wamekuwa wananunua kwenye minada lakini kwa kiasi kidogo, wahakikishe ndani ya siku hizo nne kuanzia leo Ijumaa hadi Jumatatu saa 10 alasiri wawe wameleta barua na ofisi yangu ipo wazi saa 24.”

Hayo yamesemwa leo (Ijumaa, Novemba 9, 2018) na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati akitoa tamko la Serikali kuhusu ununuzi wa zao la korosho, ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma.Baada ya kupita siku hizo Serikali italazimika kufuta usajili kwa wote waliojisajili kununua zao hilo kwa sababu walikubaliana kwenda kununua lakini hali inayoonekana sasa ni kama kumkomoa mkulima kitu ambacho imesema haitakubaliana nacho.

“Mwenye nia ahakikishe katika siku hizo nne iwe ndio mwisho wa kununua korosho na waandike barua kwani ofisi yangu ipo wazi saa 24 wana nafasi ya kuleta barua wakati wowote wakionesha nia yao na kiwango wanachokihitaji. Zaidi ya hapo Serikali haitoruhusu kampuni yoyote kununua korosho tena.”

Waziri Mkuu amesema kwenye msimu wa ununuzi wa korosho wa mwaka huu, walishuhudia kusuasua kwa minada, ambapo Serikali ilikutana na wanunuzi wa korosho katika kikao kilichoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli ambapo walikubaliana kununua kwa bei inayoanzia sh 3,000 na kuendelea.

“Mjadala ulikuwa wa wazi na wafanyabiashara wenyewe walipendekeza bei ambayo ilikuwa inaanzia sh. 3,000, hata hivyo baada ya kikao hicho ununuzi katika minada imeendelea kusuasua na hata tani zilizokuwa zikinunuliwa zilikuwa kidogo sana. Sisi tunaiona hali hii kama mgomo baridi ambao si sawa sawa sana kwani malengo yetu sisi na sekta binafsi ni kumfanya mkulima apate bei nzuri.

Hali hii haifurahishi kwa sababu Serikali imedhamiria kuboresha mazao yanayolimwa na wakulima kwa kuwasaidia kuanzia katika hatua za utayarishaji wa mashamba, upatikanaji wa pembejeo na masoko ili waweze kunufaika na kilimo na kupata tija katika mazao hayo.”Waziri Mkuu amesema baada ya kugundua bei imekuwa tatizo Serikali ilifanya jitihada za kupeleka wataalamu wake katika masoko makuu duniani na kupata bei halisi ambayo bado inatosha kumlipa mkulima sh 3,000.

Hatua hiyo imekuja baada ya zao la korosho kuendelea kununuliwa kwa bei ya chini na idadi ya wanunuzi kuwa ya chini licha ya uzalishaji wa mwaka huu kuwa mdogo ukilinganisha na msimu wa mwaka jana.Amesema msimu wa mwaka jana uzalishaji ulikuwa zaidi ya tani 300,000 na mwaka huu zinatarajiwa tani zaidi ya 200,000 hivyo wafanyabiashara wanao uwezo kununua korosho zilizopo.

Hata hivyo Serikali imewataka wananchi hususani wakulima wa korosho nchini kuendelea kuwa wavumilivu na watulivu wakati ikiendelea kushughulikia suala hilo.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980
41193 – Dodoma
IJUMAA, NOVEMBA 9, 2018.

IMG-20181109-WA0012.jpeg
IMG-20181109-WA0013.jpeg
 
Maajabu haya!

Yaani ufutie watu usajili kisa wameshindwa kununua bidhaa/korosho? Kama bei imeporomoka, wao wafanyaje?

Hata kwenye sukari kulikuwa na vitisho vya aina hii ila mwisho wa siku yakawashinda.

Hili zao ndio limeshakufa hapa chini na sidhani kama wakulima watalima tena hili zao.

Vitisho na ubabe ndio vimegeuka kuwa mtaji wa hii serikali badala ya maarifa!!
 
Waziri Mkuu yuko TBC Live akitoa tamko la Serikali.

Serikali imetoa muda wa siku nne pekee, kuanzia leo Ijumaa hadi Jumatatu kwa Kampuni zote 35 nchini zilizojiandikisha kununua korosho kuhakikisha zinajirodhesha katika Ofisi ya Waziri Mkuu, zikieleza kunuia kununua korosho na kueleza kiwango cha korosho zinazotarajiwa kununuliwa na kampuni hizo.

Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa amesema, watakaokuwa tayari waandike katika Ofisi ya Waziri Mkuu lakini watakaoshindwa kuomba kununua korosho, hawataruhusiwa kununua korosho.

Waziri Mkuu amesema korosho iliyozalishwa mwaka huu ni kiasi cha tani zipatazo 200,000 ambazo ni pungufu kulinganisha na za mwaka jana.
 
Nafurahi Sana nazidi kupata matumaini kuona serikali yangu haiyumbishwi
Safi Sana walizoea..na huu NI ujumbe tosha kwa vikundi vingine vinavyoamini vina nguvu kuliko ofisi ya Rais
Wawe wauza madawa ya kulevya,wawe Wala ruzuku,wawe wafadhili wa mashoga,wawe waaandishi mankanjanja wote wakae wakijua awamu hii iko on fire walete tu vichwa vyao uone Magufuli anavyovikata kwa shoka
 
SERIKALI YATOA SIKU NNE KWA WANUNUZI WA KOROSHO

*Yawataka waandike barua wakionesha tani wanazohitaji na lini watazichukua

*Yasema zaidi ya hapo haitoruhusu kampuni yoyote kununua korosho tena

SERIKALI imetoa siku nne kwa wanunuzi wote 35 waliojiandikisha kununua korosho wawe wamepeleka barua katika Ofisi ya Waziri Mkuu wakionesha kiasi cha tani wanazohitaji na lini watazichukua.

“Hivyo wanunuzi waliojiandikisha wakiwemo na wale wote ambao wamekuwa wananunua kwenye minada lakini kwa kiasi kidogo, wahakikishe ndani ya siku hizo nne kuanzia leo Ijumaa hadi Jumatatu saa 10 alasiri wawe wameleta barua na ofisi yangu ipo wazi saa 24.”

Hayo yamesemwa leo (Ijumaa, Novemba 9, 2018) na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati akitoa tamko la Serikali kuhusu ununuzi wa zao la korosho, ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma.Baada ya kupita siku hizo Serikali italazimika kufuta usajili kwa wote waliojisajili kununua zao hilo kwa sababu walikubaliana kwenda kununua lakini hali inayoonekana sasa ni kama kumkomoa mkulima kitu ambacho imesema haitakubaliana nacho.

“Mwenye nia ahakikishe katika siku hizo nne iwe ndio mwisho wa kununua korosho na waandike barua kwani ofisi yangu ipo wazi saa 24 wana nafasi ya kuleta barua wakati wowote wakionesha nia yao na kiwango wanachokihitaji. Zaidi ya hapo Serikali haitoruhusu kampuni yoyote kununua korosho tena.”

Waziri Mkuu amesema kwenye msimu wa ununuzi wa korosho wa mwaka huu, walishuhudia kusuasua kwa minada, ambapo Serikali ilikutana na wanunuzi wa korosho katika kikao kilichoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli ambapo walikubaliana kununua kwa bei inayoanzia sh 3,000 na kuendelea.

“Mjadala ulikuwa wa wazi na wafanyabiashara wenyewe walipendekeza bei ambayo ilikuwa inaanzia sh. 3,000, hata hivyo baada ya kikao hicho ununuzi katika minada imeendelea kusuasua na hata tani zilizokuwa zikinunuliwa zilikuwa kidogo sana. Sisi tunaiona hali hii kama mgomo baridi ambao si sawa sawa sana kwani malengo yetu sisi na sekta binafsi ni kumfanya mkulima apate bei nzuri.

Hali hii haifurahishi kwa sababu Serikali imedhamiria kuboresha mazao yanayolimwa na wakulima kwa kuwasaidia kuanzia katika hatua za utayarishaji wa mashamba, upatikanaji wa pembejeo na masoko ili waweze kunufaika na kilimo na kupata tija katika mazao hayo.”Waziri Mkuu amesema baada ya kugundua bei imekuwa tatizo Serikali ilifanya jitihada za kupeleka wataalamu wake katika masoko makuu duniani na kupata bei halisi ambayo bado inatosha kumlipa mkulima sh 3,000.

Hatua hiyo imekuja baada ya zao la korosho kuendelea kununuliwa kwa bei ya chini na idadi ya wanunuzi kuwa ya chini licha ya uzalishaji wa mwaka huu kuwa mdogo ukilinganisha na msimu wa mwaka jana.Amesema msimu wa mwaka jana uzalishaji ulikuwa zaidi ya tani 300,000 na mwaka huu zinatarajiwa tani zaidi ya 200,000 hivyo wafanyabiashara wanao uwezo kununua korosho zilizopo.

Hata hivyo Serikali imewataka wananchi hususani wakulima wa korosho nchini kuendelea kuwa wavumilivu na watulivu wakati ikiendelea kushughulikia suala hilo.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980
41193 – Dodoma
IJUMAA, NOVEMBA 9, 2018.

View attachment 927388View attachment 927389

Something is seriously wrong with this government! Time will tell
 
SERIKALI YATOA SIKU NNE KWA WANUNUZI WA KOROSHO

*Yawataka waandike barua wakionesha tani wanazohitaji na lini watazichukua

*Yasema zaidi ya hapo haitoruhusu kampuni yoyote kununua korosho tena

SERIKALI imetoa siku nne kwa wanunuzi wote 35 waliojiandikisha kununua korosho wawe wamepeleka barua katika Ofisi ya Waziri Mkuu wakionesha kiasi cha tani wanazohitaji na lini watazichukua.

“Hivyo wanunuzi waliojiandikisha wakiwemo na wale wote ambao wamekuwa wananunua kwenye minada lakini kwa kiasi kidogo, wahakikishe ndani ya siku hizo nne kuanzia leo Ijumaa hadi Jumatatu saa 10 alasiri wawe wameleta barua na ofisi yangu ipo wazi saa 24.”

Hayo yamesemwa leo (Ijumaa, Novemba 9, 2018) na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati akitoa tamko la Serikali kuhusu ununuzi wa zao la korosho, ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma.Baada ya kupita siku hizo Serikali italazimika kufuta usajili kwa wote waliojisajili kununua zao hilo kwa sababu walikubaliana kwenda kununua lakini hali inayoonekana sasa ni kama kumkomoa mkulima kitu ambacho imesema haitakubaliana nacho.

“Mwenye nia ahakikishe katika siku hizo nne iwe ndio mwisho wa kununua korosho na waandike barua kwani ofisi yangu ipo wazi saa 24 wana nafasi ya kuleta barua wakati wowote wakionesha nia yao na kiwango wanachokihitaji. Zaidi ya hapo Serikali haitoruhusu kampuni yoyote kununua korosho tena.”

Waziri Mkuu amesema kwenye msimu wa ununuzi wa korosho wa mwaka huu, walishuhudia kusuasua kwa minada, ambapo Serikali ilikutana na wanunuzi wa korosho katika kikao kilichoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli ambapo walikubaliana kununua kwa bei inayoanzia sh 3,000 na kuendelea.

“Mjadala ulikuwa wa wazi na wafanyabiashara wenyewe walipendekeza bei ambayo ilikuwa inaanzia sh. 3,000, hata hivyo baada ya kikao hicho ununuzi katika minada imeendelea kusuasua na hata tani zilizokuwa zikinunuliwa zilikuwa kidogo sana. Sisi tunaiona hali hii kama mgomo baridi ambao si sawa sawa sana kwani malengo yetu sisi na sekta binafsi ni kumfanya mkulima apate bei nzuri.

Hali hii haifurahishi kwa sababu Serikali imedhamiria kuboresha mazao yanayolimwa na wakulima kwa kuwasaidia kuanzia katika hatua za utayarishaji wa mashamba, upatikanaji wa pembejeo na masoko ili waweze kunufaika na kilimo na kupata tija katika mazao hayo.”Waziri Mkuu amesema baada ya kugundua bei imekuwa tatizo Serikali ilifanya jitihada za kupeleka wataalamu wake katika masoko makuu duniani na kupata bei halisi ambayo bado inatosha kumlipa mkulima sh 3,000.

Hatua hiyo imekuja baada ya zao la korosho kuendelea kununuliwa kwa bei ya chini na idadi ya wanunuzi kuwa ya chini licha ya uzalishaji wa mwaka huu kuwa mdogo ukilinganisha na msimu wa mwaka jana.Amesema msimu wa mwaka jana uzalishaji ulikuwa zaidi ya tani 300,000 na mwaka huu zinatarajiwa tani zaidi ya 200,000 hivyo wafanyabiashara wanao uwezo kununua korosho zilizopo.

Hata hivyo Serikali imewataka wananchi hususani wakulima wa korosho nchini kuendelea kuwa wavumilivu na watulivu wakati ikiendelea kushughulikia suala hilo.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980
41193 – Dodoma
IJUMAA, NOVEMBA 9, 2018.

View attachment 927388View attachment 927389

kwa hisani ya Sikwangalasyene ..........

1. hali za wakulima zinatia simanzi. Masoko ya mazao ya wakulima yamevurugwa

2. wafanyakazi hawakopesheki kwa kuwa hawajaongezewa mishahara kwa miaka mitatu mfululizo hivyo kutokidhi vigezo vya makato

3. biashara zimevurugwa

4. kodi inakusanywa kwa vitisho

5. biashara kama enzi za ukoloni

6. hakuna uwazi kwenye manunuzi (Ndege zimenunuliwa pasipo kufuata taratibu)

7. kuna double standard kwenye kuwajibisha watumishi (Upendeleo)

8. vyombo vya habari havipo huru tena

9. wananchi wamenyimwa haki ya mijadala ya wazi

10. serikali haipo radhi kukosolewa

11. kila mwenye mamlaka ana kauli ya mwisho (Wakuu wa Wilaya na Mikoa wamekuwa kero)

12. upotoshaji kwenye hali ya uchumi wa nchi ni mkubwa

13. 1.5 trillion hazina maelezo (Kuna wizi na ufisadi mkubwa kuwahi kutokea)

14. polisi wanafanya kazi za CCM na si kwa maslahi ya wananchi

15. usalama wa viongozi ni kipaumbele na si usalama wa nchi

16. Traffic police wanakusanya kodi badala ya kuimarisha usalama barabarani
 
HaKuna mtu asiyependa faida na HaKuna mwenye hela kuliko serikali..huu NI bonge la mtego..watazinunua tu na wasipozununua wasubiri kuona uwezo wa serikali
 
  • Thanks
Reactions: UCD
Soko la dunia sasa hivi korosho ghafi ni $1.5 kwa kilo. Hawa jamaa tunawalazimisha wanunue kwa $1.4 kwa kilo minimum. Sasa huko wanako enda kuuza sijui watauza kwa bei gani. Maana hapo bado usafiri, storage na gharama zingine kabla ya kumfikia mlaji. Plu kuna uwezekano bei ikashuka zaidi!
 
Hizi movie hata za Kihindi siyo za kiwango hizi!
Kiuchumi na kibishara huo si mwendo sahihi. Serikali inunue at list hata Nusu ya Korosho iliyopo kwa sasa bila hizi mikwara. Hatua ambayo itasaidia kuamsha bei kwenye soko la ndani na kuwapa nafuu wakulima. Wabunge saidieni Serikali kwa ushauri hasa Kipindi kama hiki cha kikao cha Bunge ni muda muafaka.

Cc Zitto
 
Nafurahi Sana nazidi kupata matumaini kuona serikali yangu haiyumbishwi
Safi Sana walizoea..na huu NI ujumbe tosha kwa vikundi vingine vinavyoamini vina nguvu kuliko ofisi ya Rais
Wawe wauza madawa ya kulevya,wawe Wala ruzuku,wawe wafadhili wa mashoga,wawe waaandishi mankanjanja wote wakae wakijua awamu hii iko on fire walete tu vichwa vyao uone Magufuli anavyovikata kwa shoka
Elimu Elimu Elimu.
 
Back
Top Bottom