Serikali yatoa ripoti ya hali ya uchumi na hali ya chakula nchini

comrade igwe

JF-Expert Member
Jan 12, 2015
7,295
3,939
Waziri wa fedha na mipango Dr Philip Mpango amesema matarajio ya ukuaji wa uchumi hayakufikiwa kwa baadhi ya maeneo kadhaa,ukuaji wa uchumi kwa sekta ya kilimo ulitegemewa kukua kwa 2.2% hivyo ukuaji huo umeshuka mpaka 2.1%, wakati katika sekta zenye watumishi wengi hazijafikia malengo ya ukuaji uchumi kama ilivyotegemewa, Aidha,amesema deni la Taifa limeongezeka kutoka dola mil 18 mpaka dola milioni 19, Wakati huo huo Waziri wa kilimo Mh Charles tizeba amesema kuna upungufu wa chakula katika baadhi ya maeneo nchini hivyo vyakula kupanda bei mara dufu mfano debe moja la mahindi sasa limefikia shilingi 20000 kutokana na ukame ulioikumba nchi

Chanzo: ITV
 
Tueleweje huyu uchumi wakilimo umekua mwingine njaa acheni kutuchanganya

Mkuu uchumi wa kilimo uliotegemewa umeshuka yaani Agriculture Revenue projection dropped vinahusiana sana na hali ya chakula kwani chakula kwaajili ya biashara hakuna ni wazi mapato kwenye kodi hiyo yatashuka
 
Back
Top Bottom