Mpogoro
JF-Expert Member
- Dec 7, 2008
- 386
- 58
Nimesoma habari yenye kichwa cha "Serikali yatangaza Sh 58bn kila wilaya za Kilimo Kwanza" kwenye gazeti la Mwananchi leo na inasema kiasi hiko cha pesa kitatumika kwa ununuzi wa magari,pikipiki na baiskeli zitakazotumika katika utendaji wa kazi za maofisa wa kilimo mashambani.
Napata kigugumizi kidogo maana kiasi hiko cha pesa ni kikubwa sana na najaribu kuangalia programu hii ambayo imekuja hivi karibuni inapata msukumo huu mkubwa na kuacha programu nyingine zikiwa zimelala....serikali hii inayomwaga pesa hizi kwenye kilimo kwanza mbona imeshindwa kuweka pesa katika ujenzi wa maktaba na maabara katika kila shule ya sekondari iliyojengwa kwa nguvu za wananchi.
Nashawishika kuona kuwa pesa katika nchi inapatika ku-finance programu ya kiserikali kama kunakuwa na msukumo fulani wa kisiasa...sioni kwa nini tuna kawaida ya kufanya vitu nusu nusu na tunachukuliwa na upepo kitu kipya!
Je,ni kweli hizi pesa zitatumika kununua hivi vitu wanavyosema?Na,je kuwepo kwa magari,pikipiki na baiskeli kwa ajili ya wataalamu wa kilimo kutaleta mapinduzi ya kilimo?Tunaponunua hivi vitu na maslahi ya mtaalamu wa kilimo yakabaki kuwa ya chini na wataalamu wangapi watakubali kuendelea kufanya mashambani tu kwasababu kuna magari?
Nielewesheni jamani ila kwangu mimi naona hili suala la kilimo kwanza mmh....I am skeptical!
Napata kigugumizi kidogo maana kiasi hiko cha pesa ni kikubwa sana na najaribu kuangalia programu hii ambayo imekuja hivi karibuni inapata msukumo huu mkubwa na kuacha programu nyingine zikiwa zimelala....serikali hii inayomwaga pesa hizi kwenye kilimo kwanza mbona imeshindwa kuweka pesa katika ujenzi wa maktaba na maabara katika kila shule ya sekondari iliyojengwa kwa nguvu za wananchi.
Nashawishika kuona kuwa pesa katika nchi inapatika ku-finance programu ya kiserikali kama kunakuwa na msukumo fulani wa kisiasa...sioni kwa nini tuna kawaida ya kufanya vitu nusu nusu na tunachukuliwa na upepo kitu kipya!
Je,ni kweli hizi pesa zitatumika kununua hivi vitu wanavyosema?Na,je kuwepo kwa magari,pikipiki na baiskeli kwa ajili ya wataalamu wa kilimo kutaleta mapinduzi ya kilimo?Tunaponunua hivi vitu na maslahi ya mtaalamu wa kilimo yakabaki kuwa ya chini na wataalamu wangapi watakubali kuendelea kufanya mashambani tu kwasababu kuna magari?
Nielewesheni jamani ila kwangu mimi naona hili suala la kilimo kwanza mmh....I am skeptical!