Serikali yatangaza kuvunjwa mkataba tata wa zaidi ya Tsh. Trilioni 1 uliowafyeka Andengenye, Lugola

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
586
1,697
DODOMA: SERIKALI imetangaza kuvunjwa kwa mkataba tata kati ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Kampuni ya ROM Solutions wa zaidi ya Sh.Trilioni moja na kusema kwa kufanya hivyo hakuna hasara au madai yeyote ambayo itadaiwa kutokana na pande zote mbili kuridhia kuvunjwa kwake.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya kupitia hati ya makubaliano iliyoingiwa baina ya aliyekuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Polisi na Ukoaji Thobias Andengenye kwa niaba ya Jeshi hilo na Kampuni ya Rom Solutions.

Akizungumza Machi 13 na waandishi wa habari Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi George Simbachawene amesema hatua hiyo ilitokana na maagizo ya Rais John Magufuli aliyoyatoa ya kupitiwa mkataba huo ambapo wamebaini kuwepo na mapungufu mengi ikiwemo Kamishna kutokuwa na sifa ya kuingia mkataba huo.

“Serikali baada ya kupitia Mkataba huo uliokuwa kwa ajili ya kununua vifaa vya jeshi hilo,iliona haina haja ya kuendelea na makubaliano husika kutokana na kutokuwa na tija kwa nchi hivyo Februari 12, mwaka huu iliamua kuvunja mkataba na hakuna hasara au madai yeyote ambayo itadaiwa kutokana na pande zote mbili kuridhia,”amesema.

Mkataba huo ulisababisha kutumbuliwa kwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola na aliyekuwa Kamishna wa Jeshi hilo, Thobias Andengenye.
 
Serikali baada ya kupitia Mkataba huo uliokuwa kwa ajili ya kununua vifaa vya jeshi hilo,iliona haina haja ya kuendelea na makubaliano husika kutokana na kutokuwa na tija kwa nchi hivyo Februari 12, mwaka huu iliamua kuvunja mkataba na hakuna hasara au madai yeyote ambayo itadaiwa kutokana na pande zote mbili kuridhia,”amesema.

Mmh.... Hili litakuja kuibuka subiri muda utasema

Jr
 
Imenibidi niingie Google nijifunze kidogo

A memorandum of understanding is anagreement between two or more parties outlining the terms and details of anunderstanding, The primary difference between the two is that a letter of intent is not binding, whereas a memorandum of understanding is considered binding and carries weight in a court of law.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baadae mtatuambia serikali haina mpango wa kuendelea na kesi imewaachia huru wahusika wote, mla rushwa Lugola ataachiwa kwenye kesi ya rushwa Kama kawaida yake
 
The primary difference between the two is that a letter of intent is not binding, whereas a memorandum of understanding is considered binding and carries weight in a court of law.
Ngoja tusubiri "mabeberu wale" wajibu mapigo. Sidhani kama Lugola na Andengeye ni peke yao tu waliohusika.
 
Baadae mtatuambia serikali haina mpango wa kuendelea na kesi imewaachia huru wahusika wote, mla rushwa Lugola ataachiwa kwenye kesi ya rushwa Kama kawaida yake
Mkuu, hakuna kesi hapo.
Huwezi kumkangaa Waziri umwache Katibu Mkuu wa wizara ambaye ni msimamizi wa kasma ya wizara.

Kwanza hapakuwa na mkataba zaidi ya MoU ambayo kisheria haimfungi mtu.

Ndiyo maana Kangi yupo mtaani hana wasiwasi wowote.
 
Tutafsirie mkuu
Imenibidi niingie Google nijifunze kidogo

A memorandum of understanding is anagreement between two or more parties outlining the terms and details of anunderstanding, The primary difference between the two is that a letter of intent is not binding, whereas a memorandum of understanding is considered binding and carries weight in a court of law.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali baada ya kupitia Mkataba huo uliokuwa kwa ajili ya kununua vifaa vya jeshi hilo,iliona haina haja ya kuendelea na makubaliano husika kutokana na kutokuwa na tija kwa nchi hivyo Februari 12, mwaka huu iliamua kuvunja mkataba na hakuna hasara au madai yeyote ambayo itadaiwa kutokana na pande zote mbili kuridhia,”amesema.

Mmh.... Hili litakuja kuibuka subiri muda utasema

Jr
Serikali haikaguliwi siku hizi huoni wanajichotea pesa wanavyotaka
serikali hii kila mtu anajichotea tu
Atakuja mwingine atasema walikosea tutaanza kudaiwa
 
Ilivyokuwa hapo August 22, 2019 wakati mkuu wa jeshi la zimamoto akitetea mkataba.



Leo Machi 13, 2020
Serikali imevunja mkataba baina ya jeshi la zimamoto na uokoaji na kampuni ya ROM Solutions Co Ltd baada ya kubaini mapungufu yaliyokuwepo kwenye mkataba huo ambao uliingiwa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya jeshi hilo vyenye thamani ya zaidi ya shilingi trillion moja za kitanzania.
 
Iyo mikataba mzee baba analala nayo uvunguni alafu mnatuletea habari za Amza kanuni hapa. Nani kashaiona iyo mikataba? Bungeni imeshajadiliwa? Mnatuletea story tu za uongo na kweli kwendraaaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
DODOMA: SERIKALI imetangaza kuvunjwa kwa mkataba tata kati ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Kampuni ya ROM Solutions wa zaidi ya Sh.Trilioni moja na kusema kwa kufanya hivyo hakuna hasara au madai yeyote ambayo itadaiwa kutokana na pande zote mbili kuridhia kuvunjwa kwake.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya kupitia hati ya makubaliano iliyoingiwa baina ya aliyekuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Polisi na Ukoaji Thobias Andengenye kwa niaba ya Jeshi hilo na Kampuni ya Rom Solutions.

Akizungumza Machi 13 na waandishi wa habari Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi George Simbachawene amesema hatua hiyo ilitokana na maagizo ya Rais John Magufuli aliyoyatoa ya kupitiwa mkataba huo ambapo wamebaini kuwepo na mapungufu mengi ikiwemo Kamishna kutokuwa na sifa ya kuingia mkataba huo.

“Serikali baada ya kupitia Mkataba huo uliokuwa kwa ajili ya kununua vifaa vya jeshi hilo,iliona haina haja ya kuendelea na makubaliano husika kutokana na kutokuwa na tija kwa nchi hivyo Februari 12, mwaka huu iliamua kuvunja mkataba na hakuna hasara au madai yeyote ambayo itadaiwa kutokana na pande zote mbili kuridhia,”amesema.

Mkataba huo ulisababisha kutumbuliwa kwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola na aliyekuwa Kamishna wa Jeshi hilo, Thobias Andengenye.
Huwezi kuvunja mkataba kizembe zembe hivyo Ccm msitufanye wajinga, hapo lazima kuna kukurupuka kwa maaumuzi
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom