Serikali yatangaza kiama kwa wanaouza dawa kwa wasio na vyeti kutoka kwa Daktari

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,191
4,104
Mwanza, Mganga mkuu wa Serikali, Profesa Abel Makubi amewaagiza wakaguzi wa dawa, wataalam na watumishi wote wa sekta ya afya nchini kudhibiti uuzaji, ununuzi na matumizi holela ya dawa bila cheti wala maelekezo ya daktari.

Akifungua mafunzo kwa wakaguzi wa maduka ya dawa kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa jijini Mwanza leo Alhamisi Desemba 10, 2020 Profesa Makubi amesema matumizi holela ya dawa bila ushauri wa daktari siyo tu inahatarisha maisha ya wananchi, bali husababisha usugu wa dawa.

“Tudhibiti matumizi holela ya dawa zinazohitaji cheti cha daktari kuokoa maisha ya wananchi na kuepuka athari za usugu wa dawa,” ameagiza Profesa Makubi.

Mganga mkuu huyo wa Serikali pia ameliagiza baraza la Famasi kukagua maduka yote ya dawa kubaini kama yamefunguliwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu na iwapo watoa huduma wana sifa za kitaaluma.

Kuhusu utendaji na uwajibikaji, Profesa Makubi ameagiza wataalam na watumishi wote wa sekta ya afya kushirikiana katika majukumu yao bila kujali wizara wanazotoka kwa sababu sekta ya afya ni moja.

“Baadhi ya watumishi wa sekta ya afya ngazi ya halmashauri wanatumia vibaya dhana ya ugatuaji wa madaraka kwa kudhani hawawajibiki kwa viongozi wa Wizara ya Afya; hii siyo sahihi kwa sababu sekta ya afya ni moja na Wizara ya Afya ndiyo msimamizi mkuu,” amesema Profesa Makubi

Akizungumzia mafunzo hayo ya siku mbili kwa wakaguzi kutoka mikoa ya Mwanza, Mara, Geita, Simiyu, Sinyanga na Kagera, Msajili wa Baraza la Famasi, Elizabeth Shekalaghe amesema yanalenga kukumbushana maadili, majukumu na uwajibikaji kazini.

Washiriki wa mafunzo hayo pia wataelimishwa kuhusu kanuni mpya sita za ukaguzi, uhakiki na usimamizi wa masuala ya dawa.

Chanzo: Mwananchi
 
Kwa hiyo mm Nina mafua nikose cetirizen mpk nimuone Doctor ndio nipate labda waseme baadhi ya dawa lakn sio kila dawa
Acheni kutunyanyasa kumuona Doctor mwenyewe kunahitaji hela
Yaan nimuone Doctor kisa mafua sifanyi upuuzi huo
Hapana, kuna dawa unaweza kununua tu bila cheti cha daktari , kama hiyo cetirizine ila kuna zingine mpaka upate cheti. Antibiotic zote zinahitaji cheti. Ni utaratibu mzuri na upo duniani kote sema kwa mazingira yetu ni tatizo. Magonjwa ya kuambukiza ambayo huhitaji dawa zilizoandikwa na daktari yapo kwa wingi.
 
Serikali ya Tanzania wasanii sana, kwa nini huwa wanatangaza ? Kwa nini wasivamie tu ? Utasikia wanatangaza kiama kwa waliojiunganishia umeme au maji au sijui wasiolipa kodi, kwa nini ? Unawatangazia ili nini ? Kwa nini msifanye kazi zenu kimya kimya tu na kuwa endelevu?

Ndio maana matatizo hayaishi wala kupungua kila siku tunaongelea matatizo yale yale tu kwa maana watu siyo intellingent, ...
 
Hapana, kuna dawa unaweza kununua tu bila cheti cha daktari , kama hiyo cetirizine ila kuna zingine mpaka upate cheti. Antibiotic zote zinahitaji cheti. Ni utaratibu mzuri na upo duniani kote sema kwa mazingira yetu ni tatizo. Magonjwa ya kuambukiza ambayo huhitaji dawa zilizoandikwa na daktari yapo kwa wingi.
Hapo sawa
 
Serikali ya Tanzania wasanii sana, kwa nini huwa wanatangaza ? Kwa nini wasivamie tu ? Utasikia wanatangaza kiama kwa waliojiunganishia umeme au maji au sijui wasiolipa kodi, kwa nini ? Unawatangazia ili nini ? Kwa nini msifanye kazi zenu kimya kimya tu na kuwa endelevu ?
Ndio maana matatizo hayaishi wala kupungua kila siku tunaongelea matatizo yale yale tu kwa maana watu siyo intellingent, ...
Sema jiwe na serikali yake ni wasanii sana.
 
Kuna kitu kinaitwa.
Willing seller, willing buyer.
Ndio maana duniani kote biashara ya umalaya imekua ngumu kutokomezwa.
Utakuta mwenye duka hajauza tangu asubuhi, hajala hajanywa. Ataacha kukuuzia mseto?
 
Hili jambo limeongezwa huku yale madogo hawajamaliza , kwa mfano Pharmacy zinafunguliwa kihalali lakini viduka uchwara viko kibao na wala havikaguliwi
 
Badala ya kudili na upungufu wa madawa Kwenye vituo vya Afya ndiyo Kwanza wanaenda kuharibu!!!
hizi Kiki za kijinga zinakuja kuharibu sekta ya Afya
 
Nitarejea ktk matumizi ya miti shamba sasa maana huko hospitalin kwenyewe bei yake sio mchezo
 
Serikali ya Tanzania wasanii sana, kwa nini huwa wanatangaza ? Kwa nini wasivamie tu ? Utasikia wanatangaza kiama kwa waliojiunganishia umeme au maji au sijui wasiolipa kodi, kwa nini ? Unawatangazia ili nini ? Kwa nini msifanye kazi zenu kimya kimya tu na kuwa endelevu?

Ndio maana matatizo hayaishi wala kupungua kila siku tunaongelea matatizo yale yale tu kwa maana watu siyo intellingent, ...
Aisee umeanza kuona madudu ya serikali hii basi ule usemi wa yajayo yanafurahisha naanza kuuelewa
 
Back
Top Bottom