Serikali yataka Watanzania kumpuuza Profesa Assad kuwa 60% ya Viongozi wa Umma nchini hawana uwezo

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Dar es Salaam. Katibu mkuu ofisi ya rais, menejimenti ya utumishi wa umma, Dk Laurean Ndumbaro amewataka Watanzania kumpuuza aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Profesa Mussa Assad kwa kutoa tuhuma kuwa maofisa na viongozi katika taasisi za umma wana uwezo mdogo wa utendaji.

Dk Ndumbaro ametoa wito huo kwa Watanzania leo Alhamisi Aprili 15, 2021 kupitia vyombo vya habari, akimponda Profesa Assad ambaye hivi karibuni katika mdahalo uliofanyika Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro (MUM), alidai asilimia 60 ya watumishi na viongozi wa umma nchini hawana uwezo wa kutekeleza majukumu yao na asilimia 40 wana uwezo kidogo.

Akifafanua kuhusu uwezo wa utendaji walionao watumishi, Dk Ndumbaro amesema tuhuma alizozitoa Profesa Assad zilijikita katika hisia na maoni yake binafsi kuliko uwezo wa kiakili na kitaaluma alionao na wala hakufanya tafiti.

Amesema watumishi na viongozi wanatekeleza majukumu yao vizuri na ndio maana nchi imepata maendeleo makubwa katika sekta za elimu, miundombinu pamoja na afya na hatimaye Taifa limeingia katika uchumi wa kati.

Amefafanua kuwa watumishi watendaji na viongozi wa umma hupanda au kuteuliwa kuwa viongozi katika utumishi wa umma kwa mujibu wa miongozo ya utumishi wa umma ambayo pamoja na mambo mengine huzingatia sifa mbalimbali za weledi na vigezo vya majukumu wanayopaswa kuyatekeleza.

Ametoa mfano wa namna Serikali inavyohakikisha inakuwa na rasilimali watu yenye sifa stahiki kwa kuzingatia ipasavyo sera ya menejimenti na ajira katika utumishi wa umma kifungu namba 4.3 (ii) ambayo imebainisha kuwa, vigezo vya uteuzi katika utumishi wa umma vizingatie uwiano kati ya taaluma na ujuzi wa kazi pamoja na sifa nyingine kama uzoefu kazini, rekodi kazini na uwezo wa kujifunza.

Dk Ndumbaro ameuthibitishia umma kuwa, watumishi wana uwezo kiutendaji kwani wanapoteuliwa kwa mara ya kwanza kushika nafasi za uongozi katika taasisi za Serikali, hupatiwa mafunzo elekezi ya utawala na uongozi ndani ya kipindi cha miezi mitatu hivyo kuondoa uwezekano wa kuwa na viongozi wasiokuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma > Prof. Mussa Assad: Asilimia 60 ya viongozi wana uwezo mdogo
 
Dar es Salaam. Katibu Mkuu ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dk Laurean Ndumbaro amewataka Watanzania kumpuuza aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Profesa Mussa Assad kwa kutoa tuhuma kuwa maofisa na viongozi katika taasisi za umma wana uwezo mdogo wa utendaji.

Dk Ndumbaro ametoa wito huo kwa Watanzania leo Alhamisi Aprili 15, 2021 kupitia vyombo vya habari, akimponda Profesa Assad ambaye hivi karibuni katika mdahalo uliofanyika Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro (MUM), alidai asilimia 60 ya watumishi na viongozi wa umma nchini hawana uwezo wa kutekeleza majukumu yao na asilimia 40 wana uwezo kidogo.

Akifafanua kuhusu uwezo wa utendaji walionao watumishi, Dkt. Ndumbaro amesema tuhuma alizozitoa Profesa Assad zilijikita katika hisia na maoni yake binafsi kuliko uwezo wa kiakili na kitaaluma alionao na wala hakufanya tafiti.

Amesema watumishi na viongozi wanatekeleza majukumu yao vizuri na ndio maana nchi imepata maendeleo makubwa katika sekta za elimu, miundombinu, afya n.k
 
Ni ukweli uliokuwa wazi, watendaji wengi tena kwa asilimia 75+ wana uwezo mdogo sana kiutendaji. Inafikia hatua huoni maana au unashindwa kiulewa nafasi na vyeti vya kielimu walivipata vipi.

Ukweli mchungu watendaji wengi ni uwezo mdogo. Poor mentality, poor creativity, poor policy na mengine mengi ni poor tu.
 
Nimeshangaa sana Assad kudharau watumishi wa umma kiasi hicho cha kusema 60% or more hawana uwezo.

Assad alikua mjumbe wa bodi ya NSSF, tena alikua mwenyekiti wa audit committee lakini kila mtu anajua NSSF ina hali gani na hata juzi Rais amesema NSSF ina hali mbaya inaelekea kufa kifo cha mende.

NSSF ndio ilikua inaongoza kwa ujinga, miradi ya hovyo, miradi isiyoqeza kurudisha gharama za uwekezaji na mambo kama hayo, yeye alikua mmoja wa wamiliki(director) aliisaidia nini NSSF zaidi ya kujigawia nyumba walizojenga bila kufuata utaratibu wa tendering huku akiwa na mgongano wa kimaslahi.

Assad alikua mmiliki(board chairman/director) wa NBC. Kipindi cha utawala wake ama umiliki wake yeye bank ilielekea kufa, ilikua very close ifilisike ama ifungwe.

Mbona hatukuona hiyo competence yake ama mbona hakutuonyesha jinsi yeye alivyo brainy saana.

Ukiacha ualimu wa chuo kikuu na u CAG, Assad amekua mkurugenzi/director wa taasisi nyingi sana, signature yake ni nini kwenye hizo taasisi ili kweli tujue yeye ni brainy sana.

Assad ni wa kupuuzwa.
 
Prof. Assad should be declared an enemy of state, an enemy of the people, ASAP.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom