Katika Maswali ya Papo kwa papo kwa Waziri Mkuu Asubuhi ya leo Mh. Chiku Abwao CDM kamuuliza Waziri Mkuu kwa nini katika Muungano huu Zanzibar wameendelea kupeperusha Bendera yao ya Awali na ile ya Tanzania...Yaani bendera ya Tanzania na ile ya Zanzibar wakati Tanzania tunapeperusha Bendera ya Tanzania na ya Tanganyika haipeperuki tena
PM: Jibu ni jepesi tu, hayo ndio yalikuwa makaubaliano ya pande mbili wakati huo
ABWAO: Swali la Nyongeza...Huoni kama upande wa pili haukutendewa Haki katika kuruhusu pia bendera ya Tanganyika kupeperushwa?
PM: Huo ni utashi wako na unavyopenda wewe lakini utaratibu wa Kikatiba hausemi hivyo
Suala la Mabomu ya Gongo la Mboto yamejitokeza tena ambapo waziri Mkuu kaulizwa Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha Wananchi waliopoteza maisha, Ulemavu na hasara za majengo wanapewa Fidia
PM: Tayari serikali imefanya Tathmini na inatambua hasara, uharibifu na kuanishwa wanaotakiwa kupewa Fidia na kujengewa majengo mapya. Matofali elfu ishirini na tano yameishafyatuliwa na kinachoandaliwa ni fungu la Fedha na utaratibu utakapokamilika Zoezi hilo litaanza baada ya muda si mrefu
KUB Mh. Mbowe. Mh. Waziri mkuu, sasa ni miezi kumi impita tangu kuisha kwa uchaguzi mkuu. Baada ya uchauguzi kuna kesi 37 ambazo zimefunguliwa kutokana uchaguzi huo. Mh. Waziri mkuu, Kwa kuwa, Kwa mujibu sheria ya uchaguzi ni lazima kesi hizi ziishe ndani ya mwaka moja. Na kwa kuwa, Jaji mkuu ameshasema hana fedha za kuendesha kesi hizo kutokana na serikali kutompa fedha husika. Na kwa kuwa hata kama fedha hizo zitapangwa ktk bajeti hii, haiwezi kuwahi muda uliowekwa ktk sheria ya uchaguzi zilizotungwa na Bunge hili. Je, Serikali ya inatoa Tamko gani?
Majibu, kwa kuwa hii utataratibu tuliojiwekea, serikali itafanya kila kila liwezekanalo kutimiza matakwa hayo.
Chiku abwao- Chadema Baada ya Muungano tulikubaliana kuungana na tukaamua kupeperusha bendera moja. Lakini baadaye wazanzibar wakaruhusiwa kupeperusha bendera yao na ya muungano. Mh. Waziri mkuu, kwa kuwa wazanzibar wamekubaliwa kupeperusha bendera yao, Kwanini Watanganyika wasipewe haki yao?
Waziri mkuu, Hivyo, ndivyo tulivyokubaliana.
Swali la Nyongeza; Je, wewe waziri mkuu huoni kama watanganyika hawajapewa haki yao?
Waziri mkuu, Inawezekana wewe ukaona hivyo, lakini si kila mtu anaona kama wewe unavyoona.
PM: Kabla Hajajibu
SPIKA: Bibi kiroboto anasimama na kusema jukumu hilo ni la Ofisi ya Bunge na kuwa Ramani na tathmini ya fanicha inafanyika ili kuhakikisha kuwa fanicha zinakuwa za mtindo na standard mojan kwa ofisi zote na kwamba bado lipo katika mchakato
Suala muhimu hapa ni kuhakikisha Bunge linaepukana na Ofisi Binafsi za Wabunge majumbani kwao (BRO MASHA UPO HAPO?)
Prudencia Kikwembe: Kamuuliza Waziri Mkuu Inakuwaje serikali inaendelea kujihusisha katika biashara ya kuuza wanyama nje ya nchi huku biashara hiyo haina tija na inaendeshwa kwa misingi ya sheria?
Kwa mpango huo tunakusudia kuzipitia sheria hizo upya kabla ya kuamua kujiridhisha kuruhusu biashara hiyo na pia kutazma ni aina gani ya wanyama ambao tutaruhusu sasa kuendelea kujumuishwa katiak Biashara hii ya usafirishwaji wa wanyama Nje ya Nchi
Na pia Tozo ambalo wanatoa ni dogo mno ambalo wao wanafaidi mara mbili huku sisi tunatapata hasara.
Uliahidi ujenzi wa barabara huko katika kata ambazo sikuzinasa majina kwa haraka kutokana na kidogo majina hayo ni ya kienyeji sana ...katika kipindi cha mwaka 2005 wewe mwenyewe na mpaka leo Ahadi hiyo haijatekelezeka je una majibu gani?
SPIKA: Bi kiroboto anaingilia kati, kwa kuwa swali hilo ni lako nan ulitoa ahadi mwenyewe basi waziri Mkuu jibu (Mhh sasa sijui alitaka kumjibia au vipi!!)
PM: ndugu yangu hili swali ungekuja hata kuninong'oneza ningekuelewa maana linatuhusu sote huko kwetu. Ila natambua umefanya hivyo ili wapiga kura nao wakuone na watambue kuwa unalifuatilia kwa ukaribu.
Nimeshafanya taratibu zote na nimeongea na TANROAD nao watusaidie baadhi ya maeneo maana ni sehemu ya barabara za serikali kuu, kwa hiyo Ahadi hiyo ipo na Itashughulikiwa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.