Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,499
- 9,279
Serikali imeombwa kuwekeza fedha katika utafiti wa mbegu za mafuta ikiwemo Alizeti na Ufuta, badala ya kuwategemea wafadhili ambao licha ya kugoma kuwekeza katika mazao hayo wamekuwa na masharti magumu.
Kauli hiyo imetolewa na mtafiti kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo Naliendele, HAPPY DAUDI ambaye amesema nchi haiwezi kuendelea bila ya kuwekeza katika utafiti.
Amesema mazao ya alizeti na ututa mara nyingi wafadhili wamekuwa wakigoma kufadhili utafiti wake, kwa madai mazao hayo ni ya biashara na hivyo watafiti kukosa bajeti ya kuyafanyia utafiti hasa pale yanapovamiwa na magonjwa.
Kufuatia hilo ameiomba serikali kuona umuhimu wa kuwekeza fedha katika mazao hayo badala ya kutegemea wafadhili pekee ambao licha ya kutoa fedha kwenye mazao mengine wanakuwa na malengo yao na hivyo wanalazimika kufuata masharti ya mfadhili.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugeunzi wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo Naliendele, Dakta. OMAR MPONDA amesema mkutano huo uliowakutanisha maafisa kilimo na wadau wa kilimo lengo lake ni kutoa mrejesho dhidi ya tafiti zilizofanyika mwaka 2016-2017 kupitia kituo hicho.
ITV
Kauli hiyo imetolewa na mtafiti kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo Naliendele, HAPPY DAUDI ambaye amesema nchi haiwezi kuendelea bila ya kuwekeza katika utafiti.
Amesema mazao ya alizeti na ututa mara nyingi wafadhili wamekuwa wakigoma kufadhili utafiti wake, kwa madai mazao hayo ni ya biashara na hivyo watafiti kukosa bajeti ya kuyafanyia utafiti hasa pale yanapovamiwa na magonjwa.
Kufuatia hilo ameiomba serikali kuona umuhimu wa kuwekeza fedha katika mazao hayo badala ya kutegemea wafadhili pekee ambao licha ya kutoa fedha kwenye mazao mengine wanakuwa na malengo yao na hivyo wanalazimika kufuata masharti ya mfadhili.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugeunzi wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo Naliendele, Dakta. OMAR MPONDA amesema mkutano huo uliowakutanisha maafisa kilimo na wadau wa kilimo lengo lake ni kutoa mrejesho dhidi ya tafiti zilizofanyika mwaka 2016-2017 kupitia kituo hicho.
ITV