Serikali yamtetea Mrema wa TANROADS

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,447
39,857
Waziri wa Miundo Mbinu Bw. Shukuru Kawamba leo amemtetea Mkurugenzi Mtendaji wa TANROADS Bw. Ephraim Mrema na kusema kuwa Bw. Mrema ana sifa zote za kuwa mkuu wa taasisi hiyo. Maelezo hayo yanazima hoja iliyotolewa na Mbunge mmoja.

Kawambwa ameiambia TBC kuwa hata hivyo serikali inaendelea kufuatilia ajira za watumishi wengine.
 
Aache Uzindakii Aseme Na Hayo Mafao Yake Inakuwaje??????????????????
 
Waziri wa Miundo Mbinu Bw. Shukuru Kawamba leo amemtetea Mkurugenzi Mtendaji wa TANROADS Bw. Ephraim Mrema na kusema kuwa Bw. Mrema ana sifa zote za kuwa mkuu wa taasisi hiyo. Maelezo hayo yanazima hoja iliyotolewa na Mbunge mmoja.

Kawambwa ameiambia TBC kuwa hata hivyo serikali inaendelea kufuatilia ajira za watumishi wengine.

Kwani ana sifa gani hizo zilizolalamikiwa? Aliajiriwaje? Uteuzi, au nafasi ilitangazwa waka-apply??
 
Twatakakujua alipatikanaje?au ni Pres Appointment?maaana kweli short list hayumo na hakuwemo....au ndio kama ya Tanesco???Politik hata kwenye Proffessional?I like this Country.........Ngoja nami nitafute Channel...maana Channel ndio Sifa kuu tz siku hizii la sivyoo...potelea kwemuu.......ngoja nipekeu makabrasha yangu sina channel kweli ya musee Pindazzz??duu ilaa hadi linii...?itajenga nchi kwelii??akitoka jee??na wewe wasi tele............
 
Aache Uzindakii Aseme Na Hayo Mafao Yake Inakuwaje??????????????????

Mafao itakuwaje ishu ilhali anavyo vigezo vyote kama serikali ilivyosema?
Kama kazi ina package na waliotangulia walipata iweje huyu asipate? Is it bcoz ni mzawa?
Tuwe wakweli.... ingekuwa wewe umepata hiyo kazi ungewaambia waondoe remuneration kwa vile ni kubwa?..Hivi mtu unapotafuta kazi...ni kwa vile unataka bora ajira hata kama haikubadilishii maisha yako to the betterau ajira boraambayo itakufanya maisha yako yawe bora kuliko mwanzo?
Watanzania tubadilike na tuwe objective....tusipende kuona gere kwa vile mwenzetu kapata.Wengi watakavyopata ndivyo tutajikuta tunapiga hatua kama taifa.
 
Waziri wa Miundo Mbinu Bw. Shukuru Kawamba leo amemtetea Mkurugenzi Mtendaji wa TANROADS Bw. Ephraim Mrema na kusema kuwa Bw. Mrema ana sifa zote za kuwa mkuu wa taasisi hiyo. Maelezo hayo yanazima hoja iliyotolewa na Mbunge mmoja.

Kawambwa ameiambia TBC kuwa hata hivyo serikali inaendelea kufuatilia ajira za watumishi wengine.

Tuliambiwa pia takukuru wanachunguza kuona kama anakatwa kodi mshahara na marupurupu mengine.
Nadhani wamemaliza uchunguzi wao walau na huyu CEO.
 
niliandika ktangu mwanzo kuwa mrema ana sifa zote kushikilia nafasi ya ceo tanroads, kilichokuwa kinabishiwa hapa, ni wale waliokosa hiyo nafasi wanatengeneza majungu wanampelekea mbunge wao naye anaropoka hovyoo

ni vema mrema akamshtaki huyo mbunge kwa kumdhalilisha yeye na taaluma yake
 
Hawezi kumshtaki Mbunge kwa kilichosema Bungeni.. inaitwa parliamentary immunity... ndio imetoka hiyo.
 
niliandika ktangu mwanzo kuwa mrema ana sifa zote kushikilia nafasi ya ceo tanroads, kilichokuwa kinabishiwa hapa, ni wale waliokosa hiyo nafasi wanatengeneza majungu wanampelekea mbunge wao naye anaropoka hovyoo

ni vema mrema akamshtaki huyo mbunge kwa kumdhalilisha yeye na taaluma yake

Mwikimbi,
Hapa sijaelewa,nafikiri ajira ni haki kwa kila mtanzania akiwemo Mrema,lakini hapa niliposhtuka ni hili suala kwamba hakuwemo kwenye orodha ya usaili,na baada ya usaili hakuna tangazo jipya la ajira lilitangazwa kama inavyotakiwa lakini ghafla ameajiriwa mtu,sasa hapo sheria ya ajira ilifuatwa?.Hapa mimi nilitegemea kusikia kuwa utaratibu wa ajira ulifuatwa wakati anaajiriwa ikiwemo Tangazo,orodha ya kusailiwa na kuteuliwa miongoni mwa waliosailiwa.Kama hawa waliokuwa kwenye orodha hawakukidhi vigezo ingetakiwa nafasi itangazwe tena watu waombe.Kama utaratibu ulikuwa huo na akapata ndugu Mrema basi hata mimi nitawashangaa watakaolalamika.Ila kwa vile BoT tayari kuna mfano kuwa kazi inayolipa hutolewa kwa 'memo' basi hata kwa hili kabla sijaita hizi shutuma majungu nahitaji kutafuta ukweli kwanza,majibu ya serkali bado ni ya juu juu.
 
Last edited:
Hapa mimi naona tunapelekwa ili muda nao uende maana issue nazo zimekuwa ni nyingi mno, yaani kama akili yangu ilivyo mtindi hata naona inakuwa nzito. Mheshimiwa mwingine ajulikanaye kama Mch. Mtikila naye akaleta ubishi wake, ati kakopa pesa kwa Rostam na sasa anadai kachafuliwa jina. Wanajuana hawa wapumbavu wote lakini wanatuona sisi tunatumia nyuti za mgongo tu maana hizi ni gumzo za kutupotezea malengo. Tuwe na malengo na lazima yafikiwe, member mmoja alisema thread ikianzishwa isiachwa hewani, iwe finalized ikiwa na maamuzi kamili. Ni maoni yangu tu wana-JF, Akhsanteni.
 
Mbona Marmo alimwambia Slaa, Slaa unavunja sheria kutoa siri za Serikali?
Tena hawakuishia hapo Kuhani, Naibu spika akasema na ukikamatwa na nyara za serikali unashtakiwa. Yaani hizo makabrasha alizonazo Dr. Slaa zinazohusu uchafu wa ccm zikipatikana anashtakiwa.
 
This Governmet is hopeless. The president is hopeless, ministers are hopeless, Deputy ministers are hopeless then what do you expect? Waziri alitakiwa aombe radhi na kama taratibu hazikufuatwa amuwajibishe mhusika mara moja na atoa ripoti. Lakini kwa kuwa waziri ni hopeless na mkuda ni kutetea tu. Stupid minister.
 
Kama ni kweli inavyodaiwa.............Inakuwaje mtu ambaye hakuwemo katika shortlist...akaukwaa u-CEO??....................huu ndio upuuzi (UFISADI network) wenyewe tunaopigia kelele kila siku hapa.........yaani nikiangalia CEO TANROADS.....halafu nikaangalia CEO ATCL............Yes they have qualifications...........however, scandals walizofanya huko nyuma...........only in Tanzania hawa kupewa nafasi hizo.........inaudhi sana
 
.....Naomba Mbowe na jeshi lake (Zitto,Slaa),hawa nawaamini,fuatilieni hili.Wandishi wa habari fuatilieni na andikeni hili.......

Tarehe 13,Jan,2009 katika mzani wa Kihonda Morogoro,Ezekiel Paschal (incharge) aliruhusu gari lenye namba za usajili T395AMC/T387ASC mali ya ndugu Benedict John Mberesero lililozidi tani 19.1 na kustahili faini ya Tsh.5 million,ambazo ziliandikwa ktk kitabu cha faini (TFN No.5060489).Katika hali ya kutia shaka gari hilo liliruhusiwa kuondoka bila kulipa faini.Habari hizo zilifika kwa Manager Tanroads Morogoro (Mr.Madinda)ambaye aliwasiliana na Technician Kattani (mlokole) aliyekuwa msimamizi wa mizani ambaye aliamua kulifuatilia hilo gari hadi Dumila na kuliamuru lirudi,hata hivyo dereva alikataa na kutishia kumwua Kattani hali iliyopelekea kuagizwa mzani wa kuhamishika uletwe Dumila ili wapime upya.Habari zilipofika Kihonda,Ezekiel Paschal kwa kushirikiana na mhasibu waliharibu mzani na kuandoka na baadhi ya sehemu zake hadi Dumila.Hivyo zoezi la kurudia upimaji halikufanikiwa na gari likapelekwa polisi na usiku kwa hali ya kutia shaka tena mzigo (mbao) ulifaulishwa.Paschal anatuhuma nyingine ya rushwa kwa gari lililokuwa na Abnormal load lenye namba T476AHL/T261ADM liloandikwa kwenye kitabu TFN. No 5060489.Yeye alifuta na kuchukua rushwa kisha akaruhusu gari.

Baada ya hatua kadha wa kadha,tarehe 19 jan 2009,baraza husika liliamua kumsimamisha kazi KWA MASLAHI YA TAIFA.Waliohusika na na kikao hicho ni pamoja na:
HoE. Eng.Tano Massaba,
HoPl.Eng.Benedicto Kinjoli,
HoA & Adm. Athuman Kambi,
Tech.Musa Kattani.

Waliandaa barua ili wamkabidhi Paschal hata hivyo hakupatikana hata kwa simu.
Tarehe 23jan2009,siku 3 tu baada ya kufukuzwa Paschal ambaye ni kibarua,Chief Executive wa Tanroads Ndg.Ephraim Mrema aliandika barua yenye Kumb no.TRD/HQ/E/01 na kichwa cha barua STAFF TRANSFERS yenye kuhamisha baraza lote lililohusika na kumfukuza kazi Ezekiel Paschal.

Hapa kuna kila dariri za rushwa! Kati ya Paschal na CE. Mrema,Serikali imekosa mil 5 kwa mkono wao.Kwani hata hivyo Paschal kanunua magari mawili ya kutembelea ndani ya mwaka mmoja kitu kinachotia shaka kwani mshahara wake ni Tsh 160,000/= tu.
Na uhamisho huu nimeutazama kama ni wa adhabu kwa WAFANYAKAZI WAAMINIFU KWA MASLAHI YA WACHACHE WASIOWAMINIFU japo ni kawaida kwa mfanyakazi kuhamishwa.Nawaita waminifu kwa sababu hata mmoja wao Musa Katani alishapewa jina (nick name) Mlokole kwa sababu hataki rushwa...Haki iko wapi??

Haya sasa wale watu wangu "ANTUFISADI" shughulikieni hili.Na nyie wandishi nendeni ofisi za Tanroad Dar na Moro mpate habari muandike,tupigeni kelele hadi ufisadi utokomee.Na nyie PCCB fanyeni kazi hapo kwani nimewapa vielelezo.
 
Ndugu Konzogwe,

Data zako dhidi ya huyo kibarua hazina shaka yoyote kua ni fisadi,lakini kumuunganisha Mrema na Ufisadi kwa kua eti aliandika barua kuhamisha timu nzima tuhuma hii haina uzito wowote.

Haujafanya utafiti kujua chanzo cha uhamisho,pengine ni uhamisho wa kawaida tu na ikawa 'coincidence' tu.

Unatakiwa ufanye utafiti kwanza kama ulivyofanya kwa huyo kibarua vinginevyo inaonekana una chuki binafsi tu.

Kumuamrisha Mbowe na jeshi lake mi sikuelewi,kwani mbowe ni nani kuliko wewe.unaonesha usivyojiamini kwa kujielekeza kwa mtu au kundi la watu ambao kwayo unaamini ni alpha na omega.

Mbowe mwenyewe ni fisadi anatuhumiwa kwa ufuska,ubadhirifu wa fedha za chama na ukabila tuhuma ambazo katu hajazikanusha hadharani
 
Ndugu Konzogwe,

Data zako dhidi ya huyo kibarua hazina shaka yoyote kua ni fisadi,lakini kumuunganisha Mrema na Ufisadi kwa kua eti aliandika barua kuhamisha timu nzima tuhuma hii haina uzito wowote.

Haujafanya utafiti kujua chanzo cha uhamisho,pengine ni uhamisho wa kawaida tu na ikawa 'coincidence' tu.

Unatakiwa ufanye utafiti kwanza kama ulivyofanya kwa huyo kibarua vinginevyo inaonekana una chuki binafsi tu.

Kumuamrisha Mbowe na jeshi lake mi sikuelewi,kwani mbowe ni nani kuliko wewe.unaonesha usivyojiamini kwa kujielekeza kwa mtu au kundi la watu ambao kwayo unaamini ni alpha na omega.

Mbowe mwenyewe ni fisadi anatuhumiwa kwa ufuska,ubadhirifu wa fedha za chama na ukabila tuhuma ambazo katu hajazikanusha hadharani



Mkulu, tupo pamoja mtoa mada hapa anatakiwa kufanya utafiti wa kutosha kujustify ufisadi wa Mrema katika ishu hii. Juu ya huyo kija na kweli haina ubishi. Nadhani kama Mrema angewaadhibu kwa kumfukuza kazi huyo kijana na pengine kumrudisha kazini, hapo tungekuwa na mashaka na Mrema.
 
Mkulu, tupo pamoja mtoa mada hapa anatakiwa kufanya utafiti wa kutosha kujustify ufisadi wa Mrema katika ishu hii. Juu ya huyo kija na kweli haina ubishi. Nadhani kama Mrema angewaadhibu kwa kumfukuza kazi huyo kijana na pengine kumrudisha kazini, hapo tungekuwa na mashaka na Mrema.

MREMA namhusisha kwa sababu zifuatazo:
1.Baada ya kutimuliwa Paschal kule Moro,alikuja ofisini kwa Mrema na waliongea kwa muda wa zaidi ya saa moja hali inayoleta mashaka.
2.Baada ya hapo Mrema alichukua jukumu la kuhamisha lile jopo la Moro bila kushirikisha kamati yake husika juu ya uamuzi huo,hivyo huenda yapo waliyoyapanga na kuamua kwa maamuzi yake binafsi kinyume na taratibu za kazi.
3.Sio kawaida kuhamishwa kwa pamoja watu wote waliokaa,haijawahi tokea.Hivyo kuna harufu ya rushwa hapa na inamgusa Mrema ndo maana hakuita kamati yake ili kujadili na kupitisha maamuzi hayo.
4.Ni ukweli usiopingika kuwa alikuwa na mawasiliano na baadhi ya matajiri ili amuondoe yule Mlokole (Kattani)kwenye njia ambayo wao hupitisha sana magari yao maana ni kikwazo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom