Serikali yamtaka Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho aeleze sababu ya wakulima kucheleweshewa malipo yao

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
471c3afa2e5e51283ccec912e53095e3.jpg
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema atamuita Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho, Bw. Hassan Jarufo ili aje amueleze ni kwa nini wakulima wa zao hilo wanacheleweshewa malipo yao kinyume na maagizo ya Serikali

Ametoa kauli hiyo leo mchana wakati akizungumza na viongozi na watendaji wa mkoa wa Lindi mara baada ya kupokea taarifa ya mkoa huo kwenye Ikulu ndogo wilayani Nachingwea. Waziri mkuu amewasili wilayani Nachingwea akiwa njiani kuelekea Ruangwa kwa mapumziko ya mwisho wa mwaka

Oktoba 16. 2016 wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Sokoine wilayani Nachingwea, mkoani Lindi, Waziri Mkuu alisema alishatoa maelekezo tangu Aprili, mwaka huu kwamba wanunuzi wa Korosho ni lazima watoe asilimia 25 ya malipo wanayotaka ili kuepuka tatizo la madalali kuingilia kati biashara hiyo

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bw. Godfrey Zambi na Wakuu wote wa wilaya za mkoa huo wawahimize wakulima wapande miche mipya ya korosho kwa sababu mikorosho iliyopo imezeeka na haitoi mazao ya kutosha

Amesema kigezo kikuu cha ununuzi wa korosho hivi sasa ni idadi ya punje na kwa Ruangwa na Nachingwea, idadi inakuwa kubwa kwasababu punje zake ni ndogo

"Wenzetu wa Tandahimba walipanda miche mipya tangu miaka minne iliyopita kwa hiyo sasa hivi wanavuna korosho zenye ubora", ameongeza

Amempongeza Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk. Charles Tizeba kwa uamuzi wake wa kuvunja mfuko wa wakfu wa korosho (CIDTF) na akamtaka afute mifuko kama hiyo kwenye mazao mengine kama Katani, Chai na Kahawa kwani inafanya kazi ambazo zinaweza kufanywa na bodi za mazao hayo.

Chanzo : ITV channel
 
Tena atoe majibu ya kuridhisha vinginevyo awajibishwe tu ,wakulima miezi miwili sasa wanalalamika jasho lao
 
Afadhali wametusumbua sana sisi wakulima,tunahangaika halafu tunacheleweshewa malipo.
 
.... hawa wakurugenzi bado tu wanafanya kazi kwa mazoea..!?.kama naiona dalili ya kutumbuliwa hapa.
 
Hapo kuna mchezo wa kuwaibia wakulima ,ili kuwachanganya wakulima .minada ya Korosho ina bei tofauti tofauti.minada ya octoba bei ilikuwa @3700+.lakini Luna baadhi ya vyama vinamlipa mkulima mpaka @2600/-Na ukienda chama kikuu unakuta documents za ware house zimeshabadilishwa .ili kufanikiwa kunahitaji ucheleweshaji.wakulima hajui bei za kila mnada .minada ya katika ya novemba Na kuendelea bei ilishuka ,kwa hiyo wanaanza kulipa hii ili iwe wazoee bei pungufu kisha wanawachapa za octoba
 
Hapo kuna mchezo wa kuwaibia wakulima ,ili kuwachanganya wakulima .minada ya Korosho ina bei tofauti tofauti.minada ya octoba bei ilikuwa @3700+.lakini Luna baadhi ya vyama vinamlipa mkulima mpaka @2600/-Na ukienda chama kikuu unakuta documents za ware house zimeshabadilishwa .ili kufanikiwa kunahitaji ucheleweshaji.wakulima hajui bei za kila mnada .minada ya katika ya novemba Na kuendelea bei ilishuka ,kwa hiyo wanaanza kulipa hii ili iwe wazoee bei pungufu kisha wanawachapa za octoba
Kwakweli mtaalamu anahitajika atoe ufafanuzi inakuwaje minada ni tofauti kiasi hiki

Kuna sehemu Shs 4,000 na Shs 3810, na Shs 3700 mpaka 2600 sababu yake ni ipi ilhali ubora wa zao hilo kwa sasa ni mmoja tu.
 
Apite na RUNALI aone kuna figisu nyingi sana.

471c3afa2e5e51283ccec912e53095e3.jpg
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema atamuita Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho, Bw. Hassan Jarufo ili aje amueleze ni kwa nini wakulima wa zao hilo wanacheleweshewa malipo yao kinyume na maagizo ya Serikali

Ametoa kauli hiyo leo mchana wakati akizungumza na viongozi na watendaji wa mkoa wa Lindi mara baada ya kupokea taarifa ya mkoa huo kwenye Ikulu ndogo wilayani Nachingwea. Waziri mkuu amewasili wilayani Nachingwea akiwa njiani kuelekea Ruangwa kwa mapumziko ya mwisho wa mwaka

Oktoba 16. 2016 wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Sokoine wilayani Nachingwea, mkoani Lindi, Waziri Mkuu alisema alishatoa maelekezo tangu Aprili, mwaka huu kwamba wanunuzi wa Korosho ni lazima watoe asilimia 25 ya malipo wanayotaka ili kuepuka tatizo la madalali kuingilia kati biashara hiyo

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bw. Godfrey Zambi na Wakuu wote wa wilaya za mkoa huo wawahimize wakulima wapande miche mipya ya korosho kwa sababu mikorosho iliyopo imezeeka na haitoi mazao ya kutosha

Amesema kigezo kikuu cha ununuzi wa korosho hivi sasa ni idadi ya punje na kwa Ruangwa na Nachingwea, idadi inakuwa kubwa kwasababu punje zake ni ndogo

"Wenzetu wa Tandahimba walipanda miche mipya tangu miaka minne iliyopita kwa hiyo sasa hivi wanavuna korosho zenye ubora", ameongeza

Amempongeza Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk. Charles Tizeba kwa uamuzi wake wa kuvunja mfuko wa wakfu wa korosho (CIDTF) na akamtaka afute mifuko kama hiyo kwenye mazao mengine kama Katani, Chai na Kahawa kwani inafanya kazi ambazo zinaweza kufanywa na bodi za mazao hayo.

Chanzo : ITV channel
 
Wao wanalalamika wakurima kucheleweshewa lkn mbona serikar hiyohiyo imeshindwa kuwalipa wastaafu kwa wakati?,wasikimbilie kuwaonea wengine wkt wao ndo waonezi wa kwanza
 
Wakulima walikuwa wanafanyiwa uhakiki. Labda pia swali kwa mukulu PM, ni lini serikali itatulipa malimbikizo yetu ya mishahara kwa miaka zaidi ya mitatu sasa?
 
Wao wanalalamika wakurima kucheleweshewa lkn mbona serikar hiyohiyo imeshindwa kuwalipa wastaafu kwa wakati?,wasikimbilie kuwaonea wengine wkt wao ndo waonezi wa kwanza
Tofauti mkuu.. Serikali wao watasema kwa sasa hawana uwezo ila itawalipa hao wastaafu

Lakini wakulima pesa wametoa wafanyabiashara, Serikali inasimama kati yake ndio maana kama utasoma vizuri thread ni kuwa Waziri mkuu alitoa maelekezo kwa wanunuzi wa Korosho
 
Back
Top Bottom