Serikali yakutana na Mabalozi na Taasisi za kimataifa kuwafafanulia kinachoendelea Ngorongoro

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,845
141,767
Serikali ya JMT leo imekutana na Mabalozi na wakuu wa Taasisi za kimataifa kuwafafanulia kinachoendelea Ngorongoro

Serikali ikiongozwa na Waziri Mulamula, waziri Ndumbaro na Naibu waziri Masanja

Masanja amesema mifugo ya nchi Jirani ndio Ilikuwa inaletwa Ngorongoro kwa ajili ya kunenepeshwa kisha kurudishwa nchini kwao kwa ajili ya mauzo na Tanzania haikuwa ikifaidika kwa chochote

Chanzo: ITV habari
 
Wawaruhusu na wawakilishi wa wahanga wa kule Ngorongoro wakutane nao,wawape mabalozi ufafanuzi,tena wawakilishi ambao hawajapangwa na serikali.Sakata hilo linatakiwa lifafanunuliwe na pande zote ili kudraw justice conclusion.
 
Wawaruhusu na wawakilishi wa wahanga wa kule Ngorongoro wakutane nao,wawape mabalozi ufafanuzi,tena wawakilishi ambao hawajapangwa na serikali.Sakata hilo linatakiwa lifafanunuliwe na pande zote ili kudraw justice conclusion.
Unamaanisha wabunge walio wachagua?
 
Wawaruhusu na wawakilishi wa wahanga wa kule Ngorongoro wakutane nao,wawape mabalozi ufafanuzi,tena wawakilishi ambao hawajapangwa na serikali.Sakata hilo linatakiwa lifafanunuliwe na pande zote ili kudraw justice conclusion.
Hao si ndio walianza kuishitaki serikali kwa hizo balozi na taasisi kwa barua na Hashtag?
 
Serikali ya JMT leo imekutana na Mabalozi na wakuu wa Taasisi za kimataifa kuwafafanulia kinachoendelea Ngorongoro

Serikali ikiongozwa na Waziri Mulamula, waziri Ndumbaro na Naibu waziri Masanja

Masanja amesema mifugo ya nchi Jirani ndio Ilikuwa inaletwa Ngorongoro kwa ajili ya kunenepeshwa kisha kurudishwa nchini kwao kwa ajili ya mauzo na Tanzania haikuwa ikifaidika kwa chochote

Chanzo: ITV habari
Serikali imeelekea kukosa wanadiplomasia


Turudi kwenye drawing board kusuka wataalam upya
 
Hoja dhaifu sana,wao wanajua hao mabalozi hawajui uhalisia wa mambo ulivyo...
 
Sioni mantiki ya hizi kelele, ni upunguani mtupu.
Hao wamasai wameoteshwa hapo kwamba waking'olewa hawatastawi sehemu nyingine?
Wawe wanaondolewa kwa madhumuni ya uhifadhi au uwekezaji yote ni sawa. Wao ni raia wa kwanza kuhamisha kupisha uwekezaji?

Tena wamepata upendeleo na nyumba wanajengewa halafu bado kuna mbwa wanabweka ati wanaonewa.

Halafu baada ya kufikiri kisiasa na kiuanaharakati utambue bottom line Rais ndiye mwenye ardhi kwa mujibu wa sheria. Anafanya uamuzi juu ya matumizi ya ardhi kwa maslahi mapana ya nchi sio kwa kuangalia maslahi ya Watu fulani tu.
 
Back
Top Bottom